Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Apa labda ufungue duka la beer tu uwakala ni pesa ndefu asee ila duka inaweza kutosha japo bdo n ndogo naongea hvyo kwa experience sibahatishi
Mkuu, napendaga sana biashara kama hii ambayo capital haiathiriki kabisa, unakuwa unahesabu net profit tu kwa kiasi chochote tu. Nipe mauzoefu katika eneo hili mkuu, inbox please!!
 
Mkuu me naomba kuuliza hivi ni gharama ngapi inahitajika kupata eneo ndani ya chuo kufanya biashara

NB: eneo la kujenga kama frem[emoji120]
Kwema mkuu, nilichokua namshauri sio kupata fremu Bali ni kufungua chuo. Kwa shilingi million 12 nimemshauri afungue chuo kitakachosajiliwa chini ya nacte. Na kwavile ndio anaanza itambidi akodi jengo ikiwezekana akodi floor moja au mbili katika ghorofa, afanye renovation afanye marketing. Usajili sio tatizo siku hizi wako faster Sana ukiwa umejiandaa kwa jengo na vifaa vidogo vidogo. Kumbuka hiyo 12mil ni kwa ajili ya mwanzoni tu. Ukikamilisha Ada itafanya mambo mengine
 
Kwema mkuu, nilichokua namshauri sio kupata fremu Bali ni kufungua chuo. Kwa shilingi million 12 nimemshauri afungue chuo kitakachosajiliwa chini ya nacte. Na kwavile ndio anaanza itambidi akodi jengo ikiwezekana akodi floor moja au mbili katika ghorofa, afanye renovation afanye marketing. Usajili sio tatizo siku hizi wako faster Sana ukiwa umejiandaa kwa jengo na vifaa vidogo vidogo. Kumbuka hiyo 12mil ni kwa ajili ya mwanzoni tu. Ukikamilisha Ada itafanya mambo mengine
Hujanielewa mkuu me nauliza labda kwa experience yako kupata eneo ndani ya chuo kufanya biashara kama ni kwa njia ya kujenga frem au kuweka container huwa ni bei gani???.....
 
Salaam Alleykhum,

Wadau kwa kutumia uzoefu wenu, nishaurini nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa million 12 nilionao ili kila mwisho wa mwezi at least nipate Net profit ya milioni mbili.

Nipo tayari kufanya biashara ktk mkoa wowote Tanzania au hata kama ni importation business kama mtaji unatosha nipo tayari.

Nipeni ushauri ili nami nitoboe.
mimi nawazo la biashara tukikubaliana nakuuzia kwa ela yako inatosha kabisa kuliendeleza mimi ninamambo kibao nayoyafanya kwa sasa alafu wazo tu lipo silifanyi kazi
 
Hujanielewa mkuu me nauliza labda kwa experience yako kupata eneo ndani ya chuo kufanya biashara kama ni kwa njia ya kujenga frem au kuweka container huwa ni bei gani???.....
Ok nimeelewa mkuu, hiyo inategemea na makubaliano kati yako na uongozi wa chuo. Kwa vyuo vya serikali hua kuna utaratibu wa kutoa tender kwa suppliers. Kwa mfano unataka ufungue canteen ili staff na wanafunzi wapate huduma ya chakula, kwa kawaida chuo husika kinatakiwa kutangaza tender na supplier wanaomba tender, bodi ya manunuzi ya chuo itashindanisha suppliers wote ili kuchagua supplier alie bora. Akishapatikana supplier bora kinachofuata ni mikataba kwa ajili ya kuanza kazi. Process hii ni standard procedure, vyuo vingi vya serikali havifati bali wanatoa tender kwa kujuana. Tena wakati mwingine biashara zinazowekwa chuoni zinamilikiwa na watumishi wa vyuo hivyo. Kwa vyuo binafsi ni maelewano tu na uongozi wa chuo husika japo huko pia hali sio tofauti Sana.
 
Itabidi nikutafute unipe shule kwanza coz forex business kibongo bongo inaonekana ni biashara ya bahati nasibu, yaani badala ya kukosa faida inasemekana forex unaweza kupoteza mpaka mtaji wote. Wengi tumezoea biashara yenye mtaji fixed then unaingiza faida au unakosa faida ila mtaji always unakuwa salama.
Mkuu nakushauri hizo pesa uziache bank itakuwa unakula polepole...katika dunia hii hakuna biashara yenye risk free kwamba kama unavyosema wewe always mtaji utakuwa salama ...narudia tena acha kabisa kufanya biashara yoyote endelea kula mshahara tu biashara hutoiweza.
 
Ok nimeelewa mkuu, hiyo inategemea na makubaliano kati yako na uongozi wa chuo. Kwa vyuo vya serikali hua kuna utaratibu wa kutoa tender kwa suppliers. Kwa mfano unataka ufungue canteen ili staff na wanafunzi wapate huduma ya chakula, kwa kawaida chuo husika kinatakiwa kutangaza tender na supplier wanaomba tender, bodi ya manunuzi ya chuo itashindanisha suppliers wote ili kuchagua supplier alie bora. Akishapatikana supplier bora kinachofuata ni mikataba kwa ajili ya kuanza kazi. Process hii ni standard procedure, vyuo vingi vya serikali havifati bali wanatoa tender kwa kujuana. Tena wakati mwingine biashara zinazowekwa chuoni zinamilikiwa na watumishi wa vyuo hivyo. Kwa vyuo binafsi ni maelewano tu na uongozi wa chuo husika japo huko pia hali sio tofauti Sana.
Makadilio ya kwenye vyuo vya private uliwah kuckia unisaidie
 
Biashara mpya kwa mtaji huo mkubwa is too much risk kama hautasimamia mwenyewe mkuu

Ila kuna option ya kununua mazao ya chakula hasa Mpunga gunia zako za kutosha na kuziweka store na inapofika kipindi cha Masika unafanya kuzikoboa gunia zako na kupata mchele wako swafi tayari kwa kuingiza sokoni kwani kipindi hicho uhitaji wa mchele unakuwa mkubwa sana hapa Dar es Salaam na Zanzibar

Minimum profit calculation

Katika centre nyingi ninazo zifahamu kwa muda huu gunia moja la Mpunga lina range kwenye TSH. 50,000/=
Hivyo basi kwa Pesa uliyonayo yaani TSH. 12,000,000, utaweza kupata gunia zenye debe sita sita 240 za mpunga na kuzihifadhi.

Kipindi ambacho Masika imechanganya hasa mwezi wa kwanza au wa pili, wewe ndo unafanya kukoboa mpunga wako ili upate mchele na gunia 1 la mpunga la debe sita linatoa debe tatu za mchele na debe moja la chenga za mchele

Hivyo basi katika zile gunia 240 unazidisha mara 3 na utapata debe 720 za mchele clear na debe 240 za chenga za mchele

Ukija sokoni debe moja la mchele lina range kwenye 35,000/= kwahyo unazidisha mara debe zako 720 za mchele na utapata kiasi cha TSH. 25,200,000/=, pia debe moja la chenga za mchele ina range kwenye TSH 10,000/= ukizidisha na debe 240 utapata kiasi cha 2,400,000/=

Total itakuwa ni Tsh. 27,600,000/= na ukitoa mtaji wako wa 12,000,000/= utapata net profit ya TSH. 15,600,000/= katika kipindi cha miezi mitano cha kuhifadhi mpunga wako

Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu.

Centre zenye mpunga mzuri ni kama zifuatazo Kyela, Kamsamba na kilyatundu, Usangu, Kahama ila kwa Morogoro sizifahamu vizuri

Naomba kuwasilisha na ninakaribisha maswali
Gharama za viroba vya kuwekea,

Gharama za kukusanyia (kuubeba toka majumbani mwa watu hadi center ya kukusanyia) huo mpunga huko vijijini.

Gharama ya usafirishaji kuuleta mjini.

Gharama za kupakia na kushusha.
 
You are a such best mathematician bro, japo wadau wanasema hesabu za kwenye makaratasi huwa zinatofautiana ukienda kwenye field
Hajaweka :
Gharama za viroba vya kuwekea,

Gharama za kukusanyia (kuubeba toka majumbani mwa watu hadi center ya kukusanyia) huo mpunga huko vijijini.

Gharama ya usafirishaji kuuleta mjini.

Gharama za kupakia na kushusha.

Quote
 
Gharama za viroba vya kuwekea,

Gharama za kukusanyia (kuubeba toka majumbani mwa watu hadi center ya kukusanyia) huo mpunga huko vijijini.

Gharama ya usafirishaji kuuleta mjini.

Gharama za kupakia na kushusha.
Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu

Sexless hiyo 5,000,000/= hapo juu inamaliza kitu, nikitulia nitakupa mchanganuo wa wa hizo gharama zake za kupakia na kushusha
 
Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu

Sexless hiyo 5,000,000/= hapo juu inamaliza kitu, nikitulia nitakupa mchanganuo wa wa hizo gharama zake za kupakia na kushusha
Asante mkuu. Nimekusoma. Shukurani kwa ufafanuzi mzuri
 
Biashara mpya kwa mtaji huo mkubwa is too much risk kama hautasimamia mwenyewe mkuu

Ila kuna option ya kununua mazao ya chakula hasa Mpunga gunia zako za kutosha na kuziweka store na inapofika kipindi cha Masika unafanya kuzikoboa gunia zako na kupata mchele wako swafi tayari kwa kuingiza sokoni kwani kipindi hicho uhitaji wa mchele unakuwa mkubwa sana hapa Dar es Salaam na Zanzibar

Minimum profit calculation

Katika centre nyingi ninazo zifahamu kwa muda huu gunia moja la Mpunga lina range kwenye TSH. 50,000/=
Hivyo basi kwa Pesa uliyonayo yaani TSH. 12,000,000, utaweza kupata gunia zenye debe sita sita 240 za mpunga na kuzihifadhi.

Kipindi ambacho Masika imechanganya hasa mwezi wa kwanza au wa pili, wewe ndo unafanya kukoboa mpunga wako ili upate mchele na gunia 1 la mpunga la debe sita linatoa debe tatu za mchele na debe moja la chenga za mchele

Hivyo basi katika zile gunia 240 unazidisha mara 3 na utapata debe 720 za mchele clear na debe 240 za chenga za mchele

Ukija sokoni debe moja la mchele lina range kwenye 35,000/= kwahyo unazidisha mara debe zako 720 za mchele na utapata kiasi cha TSH. 25,200,000/=, pia debe moja la chenga za mchele ina range kwenye TSH 10,000/= ukizidisha na debe 240 utapata kiasi cha 2,400,000/=

Total itakuwa ni Tsh. 27,600,000/= na ukitoa mtaji wako wa 12,000,000/= utapata net profit ya TSH. 15,600,000/= katika kipindi cha miezi mitano cha kuhifadhi mpunga wako

Ila ukija kutoa gharama za kuhifadhi mpunga na kukoboa haizidi TSH. 5,000,000/=,hivyo bado net profit itabaki kama 10,000,000/= katika miezi mitano yako ya uvumilivu.

Centre zenye mpunga mzuri ni kama zifuatazo Kyela, Kamsamba na kilyatundu, Usangu, Kahama ila kwa Morogoro sizifahamu vizuri

Naomba kuwasilisha na ninakaribisha maswali
Umemaliza mtaji (tshs 12,000,000/=) kununua gunia 240 za mpunga . Atapataje hiyo tshs m5/= za kukoboa nk!?
 
Umemaliza mtaji (tshs 12,000,000/=) kununua gunia 240 za mpunga . Atapataje hiyo tshs m5/= za kukoboa nk!?
Mkuu kwenye mchakato wa kukoboa mpunga, kwanza Magunia unaweza kuhifadhi kwenye store ya mwenye mashine kwasababu ana uhakika wa kupata hiyo kazi na hivyo ndio huwa tunafanya.

Kuanzia siku ambayo umehifadhi mpunga wao kwake, huwa kuna wanunuzi wa mchele kutoka nje ya nchi wanafika kwenye hizi mashine kwa lengo la kujipatia mzigo na kwasababu ww umehifadhi pale mpunga wako utapigiwa simu kwamba mnunuzi amepatikana na kama hauupo tayari utasema na utaendelea kusubiri hadi kipindi ambacho unaona upo tayar kukoboa

Mpunga ukisha kobolewa kuna chenga za mchele huwa zinapatikana kwa kila gunia moja la mpunga linatoa debe moja la chenga za mchele na linauzwa minimum ni 15,000 hadi 20,000/= kabisa na wanunuzi wa hizo chenga ni kina mama huwa wapo nje ya mashine kwa ajili ya kuzikusanya hizo chenga na huwa wanaweka oda hata kabla haujaanza kukoboa, kwahyo automatic pesa ya kukobolea huwa inatoka kwenye chenga za mchele

Na kama utakuwa tayari kuuza kwa jumla mchele wako, basi wanunuzi huwa wanafika palepale kwenye zile mashine

Hii biashara pesa huwa inajitengeneza yenyewe ila ukiwa umekaa kwenye kiyoyozi huwezi kuelewa ninachokieleza hapa coz utaona kama napiga hesabu rahisi.
 
Da
Salaam Alleykhum,

Wadau kwa kutumia uzoefu wenu, nishaurini nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa million 12 nilionao ili kila mwisho wa mwezi at least nipate Net profit ya milioni mbili.

Nipo tayari kufanya biashara ktk mkoa wowote Tanzania au hata kama ni importation business kama mtaji unatosha nipo tayari.

Nipeni ushauri ili nami nitoboe.
Dah... Najaribu kushare link nashindwa.... Ila kuna uzi mmoja hum kuhusu biashara ya mbuzi ni mzuri sana.... Ndo hivi sasa nipo naupambania (ukiwa interested karibu Pm)
🚶🚶🚶🚶🚶🚶
 
mimi nawazo la biashara tukikubaliana nakuuzia kwa ela yako inatosha kabisa kuliendeleza mimi ninamambo kibao nayoyafanya kwa sasa alafu wazo tu lipo silifanyi kazi
kama unahisii hilo wazo litatemesha mkwanja wa uhakika...nami naomba unishirikishe mkuu, nione kama linatekelezeka kwa upande wangu...mimi nipo Zanzibar, kama wazo lako ni useful nipo tayari kulinunua pia km ambavyo umepropose
 
Mkuu kwenye mchakato wa kukoboa mpunga, kwanza Magunia unaweza kuhifadhi kwenye store ya mwenye mashine kwasababu ana uhakika wa kupata hiyo kazi na hivyo ndio huwa tunafanya.

Kuanzia siku ambayo umehifadhi mpunga wao kwake, huwa kuna wanunuzi wa mchele kutoka nje ya nchi wanafika kwenye hizi mashine kwa lengo la kujipatia mzigo na kwasababu ww umehifadhi pale mpunga wako utapigiwa simu kwamba mnunuzi amepatikana na kama hauupo tayari utasema na utaendelea kusubiri hadi kipindi ambacho unaona upo tayar kukoboa

Mpunga ukisha kobolewa kuna chenga za mchele huwa zinapatikana kwa kila gunia moja la mpunga linatoa debe moja la chenga za mchele na linauzwa minimum ni 15,000 hadi 20,000/= kabisa na wanunuzi wa hizo chenga ni kina mama huwa wapo nje ya mashine kwa ajili ya kuzikusanya hizo chenga na huwa wanaweka oda hata kabla haujaanza kukoboa, kwahyo automatic pesa ya kukobolea huwa inatoka kwenye chenga za mchele

Na kama utakuwa tayari kuuza kwa jumla mchele wako, basi wanunuzi huwa wanafika palepale kwenye zile mashine

Hii biashara pesa huwa inajitengeneza yenyewe ila ukiwa umekaa kwenye kiyoyozi huwezi kuelewa ninachokieleza hapa coz utaona kama napiga hesabu rahisi.
Mkuu kwenye mchanganuo wako wa wa hii biashara ulisema mchele sokoni bei yake unarange kwenye 35000/ kwa debe..hii ni bei ya soko la wapi? Au wanunuzi ndo huwa wanakuja hapo hapo mashineni kuja kuununua kwa bei hiyo?
 
Mkuu kwenye mchanganuo wako wa wa hii biashara ulisema mchele sokoni bei yake unarange kwenye 35000/ kwa debe..hii ni bei ya soko la wapi? Au wanunuzi ndo huwa wanakuja hapo hapo mashineni kuja kuununua kwa bei hiyo?
Yaah mkuu, hiyo ni bei ya kuuzia mashineni ambapo wanunuzi ndio hufika hapo, hasa kwa mpunga kutoka Bonde la kamsamba upo vizuri sana, na watu wengi kwa ukanda ule wanaenda kukobolea Tunduma

Mchele huu ndio kilo yake huwa inafika minimum kwa kilo ni Tsh. 1800/=

Ila kuna wenye uwezo wa kuleta mchele hadi Dar es Salaam hadi Zanzibar hawa ndio wanapata faida kubwa sana

Pia unaweza kufungua store yako kwa ajili ya kuuza mchele wako kidogo kidogo, pia kunakuwa na maharage (mchele hauozi wala maharage haya haribiki kirahisi)

Kwahyo unakuwa una kusanya mpunga wako kwa ajili ya kukoboa na kuuza kwenye store yako mwenyewe ya nafaka

Wali maharage ukishajua ni namna gani hiki ni chakula pendwa basi utajua ni namna gani pesa inapatikana hapo.
 
Back
Top Bottom