Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa milion 12

Kama kweli hii pesa unayo ukipewa mchongo wa kuingiza 10M ndani ya wiki mbili ama mwezi, utakubali kutoa 40% ya Faida utakayopata?
Mkuu, ninataka tuwasiliane zaidi kwa ajili ya hizo fursa ulizonazo.
 
Kama ungekua na walau 20M
Ningekushauri nenda mgodini kahama/geita au Tarime
[emoji117]Nunua crusher machine(karasha) 7M
[emoji117]kodi eneo bei 60k per month(though inategemea na makubaliano yenu)
[emoji117]ingia share/agreement na wamiliki wa duara nzuri
[emoji117]nunua mawe usage na kuosha
In the next two or three months unaenda leaching plant kwa ajili ya kuozesha trust me faida utaipata nzuri tu kama ulipata mtu mzuri wa kusort mawe kwenye duara
Mkuu nimetamani sana kujua zaidi kuhusu hii biashara na niko na maswali yafuatayo.
1.Hayo mawe unanunua kwa bei gani kutoka kwenye hilo duara?
2.Je hao wamiliki wa duara mikataba yao ikoje je huwa wanahitaji walipwe kodi kila mwezi au ukinunua tu mawe kutoka kwao inatosha?
3.Hiyo kuozesha mawe ndio inakuwaje na lengo ni nini?
4.Processes zote zikishakamilika ni wapi soko la kuuzia hayo mawe au wateja wanayafuata hapo hapo kwenye duara?
 
Mchanganuo mzuri lakini ungejaribu kuainisha na changamoto nyingi zilizo mbele yake.
Maana ukiangalia juu juu inavutia ila mpaka kufikia kuipata hiyo faida ya 10M, shughuli pevu, na huenda asiipate.
Moja ya changamoto kubwa ni kuuziwa pumba badala ya mpunga, matokeo yake hizo gunia 240, akaambulia 200 au pungufu ya hapo.
Na huu ndio mtego uliopo kwenye biashara ya mpunga ni kuuziwa pumba/chuya so ukiwa mgeni kwenye hii biashara lazima wakupige.
Watu wasiojua wanarahisisha tu kwenye hesabu za makaratasi.
Wazoefu wa kwenye hii biashara wakiushika tu mpunga kiganjani kama ndani hauna kitu wanajua ila wewe kama ni mgeni utaibiwa.
 
Kaka km una kwako au kwenu eneo kubwa tuu, anza kufuga kuku wa layers kuku wale wa mayai, niamini utapiga zaidi ya hiyo milion 2 kwa mwezi ila yakupasa tu uvumilie ndan ya miez mitano hutovuna kitu ila baada ya hapo adi miaka 3 ijayo ww unavuna mamilioni.

1. Toa 2,500,000 nunua vifaranga 1000
2.Toa mil 2 uje ufungiwe cage ya kuingiza kuku 1000
3.Gharama za chanjo za siku 28 kwa vifaranga.
4.Vyakula vya kuku kuanzia starter Mash na kuendelea. Mfuko wa kilo 50 @49000 ila hapa wakishafikisha wiki tatu unaweza kuwachanganyia pumba+layers premix+layers mash
5. Vyombo vya chakula na maji.
6. Chumba maalum cha joto kwa vifaranga kwa miez 2

Yani inshort utatumia milion 7 tu mpaka kuku wanafika miezi 5 kuanza kutaga, na wakianza kutaga it means una uhakika wa kukusanya mayai 1000 kila siku iendayo kwa Mungu na hapo kuna kuku wengine wakishiba vizur wanaweza kukuangushia mayai 2 kwa siku.

Sasa chukua unakusanya mayai 1000 tu kwa siku, haya mayai 1000 ni sawa na trey 33 na mayai 10.

Trey kwa sasa ni sh 8000
Kwahiyo kwa siku 33x8000=264,000

Kwa mwezi sasa 264,000x30=7,920,000.

NB: Kwahiyo ukiwatunza vizur vifaranga kwenye chanjo, chakula braza wewe ni milionea unapiga zako Milion 7,920,000/= kwa mwezi kama faida haina tax hyo wala VAT. Na ukumbuke kuwa hawa kuku watakuwa wana uwezo wa kukutagia ndani ya miaka 3 wakichoka unawatoa unawauza nako unapiga hela kuku 1 sokoni 8000. 8000x1000= 8000,000/= baada ya miaka 3 utavuna Mil 8 km pesa yakuwauza nyama hapo umekosa nn kaka!!.


Yan ungejua mm nina shida ya milion 2 tu nitanue nitoke hapa kwny kuku 55 ambapo kwa mwez wanaingiza 440K tu.
Je soko ni uhakika??
 
Pia mwulize ni aina gani hiyo ya kuku ambapo ukiwa nao kuku 1,000 kila siku utaokota mayai idadi sawa na kuku waliopo na pia kuku kutaga mayai mawili kwa siku eti kisa tu kala kashiba. Mwisho kuku wa mayai atage kila siku na kwa miaka mitatu mfululizo?! Ni mahesabu yasiyo na uhalisia.
Mkuu mm ni mfugaji wa hao layers..!hakuna mahesabu kama hayo..!hiyo pesa akinunua cage na vifaranga akajenga banda imeisha
 
Salaam Alleykhum,

Wadau kwa kutumia uzoefu wenu, nishaurini nifungue project/biashara gani kwa mtaji wa million 12 nilionao ili kila mwisho wa mwezi at least nipate Net profit ya milioni mbili.

Nipo tayari kufanya biashara ktk mkoa wowote Tanzania au hata kama ni importation business kama mtaji unatosha nipo tayari.

Nipeni ushauri ili nami nitoboe.
hyo hela kwenye nafaka inaingiza ml 4 kwa mwez, mfano dengu mwez wa nane, kuna choroko
 
Biashara ndogo ndogo ziko nyingi sana mkuu kwa mfano restaurant,banda la kuuza chips,balo nguo za mtumba,duka la chakula rejareja nk kutegemea na hobby yako
Yaani "restaurant" ni biashara ndogo au ni jina tu ullikuwa una maanisha biashara ya "baba/mama ntilie"!? Banda la kuuza chips sawa, hata hivyo, location yake ni muhimu sana; nguo za mitumba na duka la chakula la rejareja - KWA KWELI SIJUI, Hapa tunazungumzia pia mtaji na miundo mbinu yake ikiwa ni pamoja na sehemu ya kuuzia na kufanyia hizo biashara. Na hapa ni lazima tuelewane biashara ndogo, mtaji wake ni UPI?
 
Nauza mchele kwa bei ya jumla mkuu(Ifakara -Dar),kila wiki nasafiri mara mbili na kila safari napata faida 250K,kwa huo mtaji wa 5M,piga hesabu 250,000 X 8 = 2,000,000.
Kaka uko wapi na je nawez Nika ku pm , naitaj data zaid nataman hii biashara
 
Kopesha milioni 10 bot kwa mda wa miaka 20 au 25 inakua kama hazina yako ambapo kila mwaka wanakupa milioni 1 lakitano na kitu ukitaka kwa pamoja iyo 1.5 au kila baada ya miez 6 wanakupa laki 7 baada ya miaka 20 au 25 inakuja kucheza kwenye milioni 35+ na ile milioni 10 yako unapewa kama ilivo unakua kama umejitengenezea ki biashara chako mbadala au pesa za ada kwa watoto na kujikimu ki maisha incase main plan ikisumbua inatambulika kama treasure bonds (hatifunganii)
Hii sio biashara Bali ni upumbavu, yaan uweke 12m utemgemee 1m kwa mwaka alafu faida uje upewe baad ya 20yrs huo si umri wa mtu mzee maisha yenyew mafup hatun guarantee ata ya kuish miak miak 10.
 
Mkuu nimetamani sana kujua zaidi kuhusu hii biashara na niko na maswali yafuatayo.
1.Hayo mawe unanunua kwa bei gani kutoka kwenye hilo duara?
2.Je hao wamiliki wa duara mikataba yao ikoje je huwa wanahitaji walipwe kodi kila mwezi au ukinunua tu mawe kutoka kwao inatosha?
3.Hiyo kuozesha mawe ndio inakuwaje na lengo ni nini?
4.Processes zote zikishakamilika ni wapi soko la kuuzia hayo mawe au wateja wanayafuata hapo hapo kwenye duara?
Dah nimejikuta nacheka asee.

Mkuu alichoeleza huyo jamaa ni process nzima ya kuitafuta dhahabu.

Sio rahisi kama inavyosomeka kwenye maandishi yake hasa ukiwa hujui chochote kuhusu dhahabu. Ni biashara ambayo kuchoma mtaji wa 500million ndani ya week ni kawaida tu.
 
Hiyo pesa nenda nayo pale dodoma nunua mashine za kukamua alizeti, jenga kiwanda kidogo... Unanunua mbegu zaalizeti toka kwa wakulima pia unakamua mafuta unayapack kwenye galon na kuuza mikoa mbalimbali... Pia unaweza kukamua mbegu za watu binafsi wanaokuja wakiwa na mbegu zao.
 
Hiyo pesa nenda nayo pale dodoma nunua mashine za kukamua alizeti, jenga kiwanda kidogo... Unanunua mbegu zaalizeti toka kwa wakulima pia unakamua mafuta unayapack kwenye galon na kuuza mikoa mbalimbali... Pia unaweza kukamua mbegu za watu binafsi wanaokuja wakiwa na mbegu zao.
Mashine ya Alizeti milioni 12??
 
Back
Top Bottom