Nifute kwenye kitabu cha kuzimu, niandike kwenye kitabu cha uzima" Hivi vitabu vikoje na uhalisia wake?

Nifute kwenye kitabu cha kuzimu, niandike kwenye kitabu cha uzima" Hivi vitabu vikoje na uhalisia wake?

Inatafakarisha sana, Kwa hiyo mtu akizaliwa tu automatically unakua umeandikwa kwenye kitabu cha kuzimu?????,🤔
Haya shetani alikua malaika mkuu wa sifa huko mbinguni, Hivi hiyo roho ya uasi ya kujiinua kutaka kumzidi Mungu ilitoka wapi???? hapo kabla hiaikuepo??
Hakuna kitu kama hiko kuwa ukizaliea tu umeandikwa kwenye kitabu cha kuzimu. Huyo Ibilisi hajaumba kiumbe chochote na hawezi kuwa mahali pote kwa wakati mmoja ili ajue nani kazamiwa kwa wakati gani.

Kinachotokea, Yeye aliyekuumba anakujua na ameandika jina lako kwenye kitabu cha uzima wa Milele cha mwana kondoo. Biblia inaeleza wazi mbinguni kuna vitabu viwili. Kitabu cha Uzima na kitabu cha hukumu. Kitabu cha Uzima huandikwa kila mwanadamu azaliwapo ila atendapo dhambi na kumuasi Mungu hufutwa kwenye kitabu cha Uzima na kuandikwa kwenye kitabu cha hukumu.

Kwa kuwa mwanadamu amepewa neema ya upatanisho kama ambavyo Kristo alikuja katika mwili na kutupatanisha naye kwa mwili wake. Ndivyo wanadamu tumepewa huduma ya upatanishi kati ya Mungu na wanadamu. Pale tumuombeapo mtu sala ya toba ndio tunampatanisha na Mungu wake na tunamuomba Mungu afute jina lake kwenye kitabu cha hukumu na aliandika kwenye kitabu cha Uzima wa Milele. Vitabu hivi vitatumika kwenye siku ile ya kukutania njia panda. Wale watendao uovu watafufuliwa kwanza kwa ajili ya hukumu na wema kwa ajili ya Uzima wa Milele.

Ndugu yangu mpendwa, Baba, kaka,Mama, Dada na mwana JF mwenzangu. Wapi pa kuishi katika umilele wako huandaliwa sasa ukiwa hai. Ni vyema.sasa uchague wapi utakapoishi katika umilele wako. Kumbuka kuwa, kesho yako ji fumbo ila umilele wako umekaribia.
 
Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote kwanza kabisa hahitaji kuandika majina kwenye vitabu wala kuombwa kitu.

Huyo Mungu hayupo katika uhalisia zaidi ni udanganyifu tu
Thibitisha uwepo wa ndoto kama zipo au umewahi ota.
Ukiweza thibitisha ndoto zipo unashindwa vipi kuthibitisha Mungu yupo
 
ni myth tu kila kitu imetengenezwa na ubongo wa mwanadamu mwenyewe
Fear
Hope
Kwa umri wangu mkuu, naweza kusimama kwa ujasiri mbele za watu hata wanadamu wote wakikataa mimi nitasimama na kukiri kuwa Mungu yupo na Mungu ni kweli na amini kabisa. Ulimwengu wa Roho upo, ni halisi, una nguvu na unatenda kazi katika Roho kunako kujidhihirisha katika mwili. Hii ya kusema hakuna Mungi sijui.myth and so on ni janja ya adui tu ambayo anazuga na kuwapumbaza wanadamu ila.Mungu ni kweli, Shetani ni kweli, shimo lile refu lisilo na maji ni kweli lipo, Mbingu ni kweli na halisia. Malaika na mapepo ni kweli na halisia. Kiburi cha uzima kisikudanganye. Nami nilikuwa hivyo ila sasa nasimama na kukiri hayo yore kuwa yapo, ni kweli na halisia.
 
Unajua kimantiki ni rahisi tu ku prove Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu huu hawezekani kuwepo?
Hitimisha nini chanzo cha Binadamu na ulimwengu.
Ukitoa ushahidi usioacha shaka.
Pengine unaweza kuwa na hoja
 
Kwanza huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Pili Mungu huyo, kimantiki, akiwapo, huhitaji kumuomba chochote, atakupa kizuri na kukuepusha na kibaya kutokana na sifa zake hizo.

Ukijikuta unamuomba Mungu huyo chochote, hicho kitendo cha kuomba ni kitendo cha kukubali huyo Mungu hayupo.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote utamuomba nini?

Kwani yeye hajui unachohitaji?
Kumekucha..😂😂
 
Hitimisha nini chanzo cha Binadamu na ulimwengu.
Ukitoa ushahidi usioacha shaka.
Pengine unaweza kuwa na hoja
Hapana.

Kuna logical fallacy inaitwa "non sequitur".

Yani, kuunganisha mambo mawili ambayo hayana uhusiano.

Naweza kujua Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo, hata kama sijui chanzo cha binadamu ni nini.

Naweza kujua jibu fulani si la kweli, hata kabla sijajua jibu la kweli ni lipi.

Nitakupa mfano rahisi wa kuelewa hoja hii.

Mfano, tukijua kwamba, ili mtu awe mama yako mzazi, inabidi awe mkubwa kuliko wewe. Kwa sababu, akiwa mdogo zaidi yako haitawezekane awe alikuzaa.

Halafu tukajua kwamba wewe leo una miaka 30.

Halafu tukaletewa binti mchanga mwenye umri wa miezi 6 leo, tukaambiwa kuwa huyu binti mwenye miezi 6 leo ndiye mama yako mzazi aliyekuzaa, tunaweza kukataa, na kusema huyo binti wa miezi 6 si mama yako mzazi. Kwa sababu ulivyozaliwa weee, huyo binti mchanga alikuwa hajazaliwa, amezakiwa miaka 29 baadaye.

Sasa, hapo tumejua binti huyo si mama yako mzazi, kwa kuangakia mantiki ya timeline na kuona cintradiction tu.

Sasa, hapo, ukichouliza wewe, habari za kuuliza chanzo cha binadamu, ni sawa na mtu aniulize, sasa kama huyu binti wa miezi sita leo si mama yako mzazi wewe mwanamme mwenye miaka 30 leo, mama yako mzazi ni nani?

Mimi nakwambia haijalishi mama yako mzazi ni nani, hata kama sijui mama yako mzazi ni nani, huyu binti wa miezi 6 leo si mama yako mzazi.

Yani ni hivi, naweza kujua kanuni fulani za kimantiki, halafu kutokana na kanuni hizo, nikipewa jibu lisilo sahihi, nikalijua hili jibu si sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi.

Wewe unachofanya ni kulazimisha kuwa siwezi kujua jibu lisilo sahihi mpaka n8jue jibu sahihi.

Hoja yako ina makosa ya kimantiki.

Unaniambia kwamba siwezi kujua kuwa binti mdogo mwenye umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama yako aliyekuzaa wewe mwanamme mwenye miaka 30 leo, mpaka nimjue mama yako mzazi ni nani.

This is rubbish.
 
Kumekucha..😂😂
Mkuu,

Wewe unaelewa mantiki ya kumuomba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kweli?

Kama Mungu huyo yupo na ana sifa hizo zote, maana yake anajua mahitaji yako kabla wewe hujayajua, sasa kwa nini hajakupa mpaka umuombe? Anasubiri nini kukupa mpaka unafikia stage ya kujisikia umuombe?

Kwa nini asifanye kwa uwezo wake mkuu, ujuzi wake mkuu na upendo wake mkuu upate tu unachotaka, bila kuomba, na kama kingine si kizuri kukipata, asikupe hata tamaa ya kukijua na kukiomba?

Kwa nini huyo Mungu hakufanya hivyo?
 
Mimi ni mkatoliki japo mara ya mwisho kwenda kanisani ni almost two years ago,haimaanishi nimepoteza imani la hasha niko vzuri,
Japo sio mzuri sana wa vifungu vya biblia km tulivyo wakatoliki wengi.
Kwa kumbukumbu zangu zilizosahihi enzi za ukuaji wangu enzi hizo niko primary mpk mitaa ya form one nimewahi kuokoka km mara kumi,ni vile mtoto ukisikia mikutano ya injili unatia timu hujakaa sawa unasikia km hunaokoka pita mbele,hata kabla hujavuta pumzi unasikia fumben macho na mrudie maneno nitakayoongea,anasema Mh Mchungaji..

Utasikia "nifute kwny kitabu cha kuzimu na moto wa milele niandike kwny kitabu cha uzima"

Sasa naomba kuuliza hili swala la kufutwa na kuandikwa kwny hivi vitabu liko kwny maandiko kwmb mpk sasa kuna watu wako top ten ya kwny kitabu cha motoni ama ni lugha ya picha inayotumiwa na wachungaji kumcomfort anaeombewa kumpa zile hisia za kuandikwa kwny kitabu cha uzima

Karibuni watu wa mataifa mnipe muongozo
Ukimwuzia Shetani yaani Ibirisi Lusifer roho yako. Inaandikwa kwenye kitabu cha Kuzimu.
Ikimpokea Roho Mtakatifu katika Nafsi yako unaandikwa kwenye kitabu cha uzima.

Ukiaandikwa katika kimojawapo ya hivyo vitabu unakuwa Mwanachama na Mfuasi na unamilikiwa nao uliye mchagua.
 
Mkuu tatizo mafundisho yamejaa vitisho, watu tumejengewa woga wa kupingana nayo kwa kuamini tutapata hukumu kali
Mkuu,

Wewe unaelewa mantiki ya kumuomba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kweli?

Kama Mungu huyo yupo na ana sifa hizo zote, maana yake anajua mahitaji yako kabla wewe hujayajua, sasa kwa nini hajakupa mpaka umuombe? Anasubiri nini kukupa mpaka unafikia stage ya kujisikia umuombe?

Kwa nini asifanye kwa uwezo wake mkuu, ujuzi wake mkuu na upendo wake mkuu upate tu unachotaka, bila kuomba, na kama kingine si kizuri kukipata, asikupe hata tamaa ya kukijua na kukiomba?

Kwa nini huyo Mungu hakufanya hivyo?
 
Atakupotezea muda tu na logic za kitoto kutaka umeonesha Mungu kama unavyomuonesha miti au milima. Ukimwambia nionyeshe atom au Oxygen au ufahamu kama kunionesha milima na miti hawezi anaanza kuzunguka zunguka tu.
Jibu lako hili linanionesha ulivyo na uwezo mdogo wa kuelewa, na jinsi kuendesha mazungumzo ya kimantiki na Watanzania wengi ilivyo kazi ngumu.

Hoja zangu za kupinga uwepo wa Mungu ni za kimantiki. Sijawahi kutaka kumuona Mungu ili kuhakikisha yupo. Hivyo kashfa yako kuhusu mimi kutaka kuuona Mungu imejengwa kwenye hoja ya uongo, sijawahi kutaka kumuona Mungu kama sehemu ya kuthibitisha uwepo wake.

Mara nyingi natumia the problem of evil na Epicurean Paradox.

Hizi ni hoja za kimantiki. Hazihoji uwepo wa Mungu kwa sababu haonekani.

Zinahoji uwepo wa Mungu kwa sababu dhana ya kuwepo kwake haina logical consistency.

Sasa wewe mpaka leo huelewi the problem of evil ni nini, huelewi Epicurean Paradox ni nini.

Of course huwezi kujibizana nami kimantiki.

Unatoa nonnsequitur objection kuhusu Oxygen.

Unaelewa kuwa uwepo wa Oxygen na wa atom hauna internal logical inconsistency?

Unaelewa hata internal logical inconsistency ni nini?
 
Mkuu tatizo mafundisho yamejaa vitisho, watu tumejengewa woga wa kupingana nayo kwa kuamini tutapata hukumu kali
Yani mtu anaamini kabisa kwamba.

1. Kuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

2. Huyu Mungu aliweza kuumba ulimwengu anavyotaka mwenyewe, ukiwamo ulimwengu ambao mabaya hayawezi kutokea kwa sababu yoyote.

3. Lakini, Mungu huyu, mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote, akaamua kuumba ulimwengu huu ambao ubaya unaweza kufanyika.

4. Baada ya kuumba ulimwengu huu ambao mabaya yanaweza kufanyika, viumbe wake wakafanya mabaya (kwa sababu Mungu aliachia yaweze kufanyika)

5. Halafu Mungu huyo huyo, ambaye aliruhusu mabaya yaweze kufanyika, na watu wakaweza kufanya mabaya (kwa sababu Mungu aliruhusu mabaya yaweze kufanyika) atahesabu mabaya yote wanayofanya watu.

6. Kisha, Mungu huyu, mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, atawahukumu mabilioni na mabilioni ya watu, kwa kuwachoma moto wa milele, watu waliofanya mabaya, mabaya ambayo yameruhusiwa kuwezekana na Mungu mwenyewe!

7. Zaidi, watu hawa watachomwa moto wa milele, kama adhabu ya mabaya ambayo wameyafanya kwa miaka michache sana!

Yani watu hawaoni matatizo mengi ya kimantiki kwenye imani hii?
 
Hapana.

Kuna logical fallacy inaitwa "non sequitur".

Yani, kuunganisha mambo mawili ambayo hayana uhusiano.

Naweza kujua Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo, hata kama sijui chanzo cha binadamu ni nini.

Naweza kujua jibu fulani si la kweli, hata kabla sijajua jibu la kweli ni lipi.

Nitakupa mfano rahisi wa kuelewa hoja hii.

Mfano, tukijua kwamba, ili mtu awe mama yako mzazi, inabidi awe mkubwa kuliko wewe. Kwa sababu, akiwa mdogo zaidi yako haitawezekane awe alikuzaa.

Halafu tukajua kwamba wewe leo una miaka 30.

Halafu tukaletewa binti mchanga mwenye umri wa miezi 6 leo, tukaambiwa kuwa huyu binti mwenye miezi 6 leo ndiye mama yako mzazi aliyekuzaa, tunaweza kukataa, na kusema huyo binti wa miezi 6 si mama yako mzazi. Kwa sababu ulivyozaliwa weee, huyo binti mchanga alikuwa hajazaliwa, amezakiwa miaka 29 baadaye.

Sasa, hapo tumejua binti huyo si mama yako mzazi, kwa kuangakia mantiki ya timeline na kuona cintradiction tu.

Sasa, hapo, ukichouliza wewe, habari za kuuliza chanzo cha binadamu, ni sawa na mtu aniulize, sasa kama huyu binti wa miezi sita leo si mama yako mzazi wewe mwanamme mwenye miaka 30 leo, mama yako mzazi ni nani?

Mimi nakwambia haijalishi mama yako mzazi ni nani, hata kama sijui mama yako mzazi ni nani, huyu binti wa miezi 6 leo si mama yako mzazi.

Yani ni hivi, naweza kujua kanuni fulani za kimantiki, halafu kutokana na kanuni hizo, nikipewa jibu lisilo sahihi, nikalijua hili jibu si sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi.

Wewe unachofanya ni kulazimisha kuwa siwezi kujua jibu lisilo sahihi mpaka n8jue jibu sahihi.

Hoja yako ina makosa ya kimantiki.

Unaniambia kwamba siwezi kujua kuwa binti mdogo mwenye umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama yako aliyekuzaa wewe mwanamme mwenye miaka 30 leo, mpaka nimjue mama yako mzazi ni nani.

This is rubbish.
Unajikanganya kupitia mfano wako
Tunaweza kumjua mama yako kupitia shuhuda za watu. Jirani, ndugu, marafiki, na jamii

Kuhusu umri na kuzaa umetoa mfano usio na ulinganifu kwa mantiki hiyo mfano wako ni Mufu.

Nimesha sema Mungu ni roho anathibitika na kudhihirika katika roho na sio mwili.
Na ili uprove lazima uwe kiroho zaidi, tunajuaje haya mambo?
kupitia maandiko( marejeleo) matakatifu.
Shuhuda na maumbile ya asili ya ulimwengu.
 
Unajikanganya kupitia mfano wako
Tunaweza kumjua mama yako kupitia shuhuda za watu. Jirani, ndugu, marafiki, na jamii

Kuhusu umri na kuzaa umetoa mfano usio na ulinganifu kwa mantiki hiyo mfano wako ni Mufu.

Nimesha sema Mungu ni roho anathibitika na kudhihirika katika roho na sio mwili.
Na ili uprove lazima uwe kiroho zaidi, tunajuaje haya mambo?
kupitia maandiko( marejeleo) matakatifu.
Shuhuda na maumbile ya asili ya ulimwengu.
Naona mnashushiana vinu vya maana
 
Unajikanganya kupitia mfano wako
Tunaweza kumjua mama yako kupitia shuhuda za watu. Jirani, ndugu, marafiki, na jamii

Kuhusu umri na kuzaa umetoa mfano usio na ulinganifu kwa mantiki hiyo mfano wako ni Mufu.

Nimesha sema Mungu ni roho anathibitika na kudhihirika katika roho na sio mwili.
Na ili uprove lazima uwe kiroho zaidi, tunajuaje haya mambo?
kupitia maandiko( marejeleo) matakatifu.
Shuhuda na maumbile ya asili ya ulimwengu.
Mkuu,

Mbona hatuelewani?

Kwani wapi nimesema hatuwezi kumjua mama yako?

Nimekambia hivi, naweza kujua jibu fulani si sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi.

Naweza kujua binti wa umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama yako mzazi, hata kabla sijamjua mama yako mzazi ni nani.

Naweza kujua 10 si square root ya 2, hata kabla sijajua square root ya 2 ni ipi.

Naweza kujua mji wa Washington DC ambao upo Marekani si mji mkuu wa Tanzania, hata kabla sijajua mji mkuu wa Tanzania ni mji gani.

Naweza kujua kwamba mimi si wewe, hata kabla sijakujua wewe ni nani.

Je, unakubali kwamba, nikijua kanuni fulani za msingi, naweza kujua jibu fulani si jibu sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi?
 
Mimi ni mkatoliki japo mara ya mwisho kwenda kanisani ni almost two years ago,
Sasa naomba kuuliza hili swala la kufutwa na kuandikwa kwny hivi vitabu liko kwny maandiko kwmb mpk sasa kuna watu wako top ten ya kwny kitabu cha motoni ama ni lugha ya picha inayotumiwa na wachungaji kumcomfort anaeombewa kumpa zile hisia za kuandikwa kwny kitabu cha uzima
Sasa ndugu, swali lako unalielekeza kwa Wakatoliki au wachungaji wa madhehebu wanaoongea hayo maneno? Maana katika utaratibu wa maombi ya Kikatoliki, hiyo phrase huwa haipo
 
Naona mnashushiana vinu vya maana
Hajaelewa kwamba mtu anaweza kujua jibu fulani si sahihi, hata kabla hajajua jibu sahihi.

Mimi nikimwambia "jibu hili naweza kuliona si sahihi, kwa sababu hii na hii', anashindwa kuchambua sababu zangu, analazimisha nimletee jibu la suala lingine ambalo halina hata uhusiano.

Nikimwambia kwamba, kwa kuwa najua square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2, ukiniambia 10 ni square root ya 2 nitakupinga, kwa sababu 10 ni kubwa kuliko 2, haelewi hiyo logic, analazimisha umpe square root ya 2.

Mimi namwambia hata kabla sijajua square root ya 2 ni nini, nishajua 10 si square root ya 2, kwa sababu square root ya 2 ni ndogo kuliko 2, tuitafute kwenye namba zilizo chini ya 2, si kwenye namba zilizo juu ya 2.

Na sijawahi kusema najua square root ya 2 ni nini, mimi nasema tu kwamba 10 si square root ya 2.

Haelewi hiyo "elimination method" ya kutafuta jibu sahihi kwa kuyaondoa yale yasiyo sahihi.

Anafikiri unahitaji kujua jibu sahihi ili ujue jibu fulani si sahihi.
 
Naona mnashushiana vinu vya maana
Kupitia hawa watu tunajifunza pia
Kuna mambo kwa akili zetu hatuwezi kuyang'amua yote.

Unaweza kuta anapinga hapa ili apate kitu fulani cha kujifunza. Lakini pia anaweza kuwa ni muumini mzuri sana tena mtiifu kwa Mungu kuliko wale wanaooneka kusali sana kumbe ni wanafiki wakubwa
 
Mkuu,

Mbona hatuelewani?

Kwani wapi nimesema hatuwezi kumjua mama yako?

Nimekambia hivi, naweza kujua jibu fulani si sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi.

Naweza kujua binti wa umri wa miezi 6 leo hawezi kuwa mama yako mzazi, hata kabla sijamjua mama yako mzazi ni nani.

Naweza kujua 10 si square root ya 2, hata kabla sijajua square root ya 2 ni ipi.

Naweza kujua mji wa Washington DC ambao upo Marekani si mji mkuu wa Tanzania, hata kabla sijajua mji mkuu wa Tanzania ni mji gani.

Naweza kujua kwamba mimi si wewe, hata kabla sijakujua wewe ni nani.

Je, unakubali kwamba, nikijua kanuni fulani za msingi, naweza kujua jibu fulani si jibu sahihi, hata kabla sijajua jibu sahihi ni lipi?
Rudi nyuma kidogo.
Kupitia hizo kanuni ndizo tunazozitumia kumuelezea Mungu
Kama ambavyo unazozitumia kumpinga Mungu.
 
Back
Top Bottom