Umenikumbusha mbali sana,nakumbuka wakati naanza kazi mwaka 2011 nilikua na rafiki yangu mmoja ambaye yeye alikua na duka LA ....... ambalo lilikua ni Dogo sana kiasi kwamba wakati Mwingine ilinilazimu nimkopeshe mshahara wangu ili aweze kuongeza mataji
Baada ya miaka minne,nikashangaa jamaa amejenga,amenunua gari na anamtaji wa kutosha ambao bidhaa alikua anaagazia moja kwa moja toka. China,wakati huo Mimi bado tuu nasaga lami tena kazini hata cheo sijapata
Kibao kikageuka nikawa sasa Mimi ndo omba omba kwakwe ikifika tu kati kati ya mwezi Mimi hoi madeni kibao hahahaha nikaona isiwe tabu na Mimi mwaka Jana kama Utani tu tena kwa kuomba ushahuri himu humu jf nikajiongeza kudadadeki kazi tupa kule nikafaiti kama unavyojua mwanaume ni mwanaume
Sasa ivi na Mimi kila mwezi China mara mbili nilichogundua kwa maisha haya usipojiongeza hahahaha umekwishaa