Nikija kuwa na familia kuna vitu sintoruhusu

Naandika nafuta, naandika nafuta, kua na kwako kwanza ntakwambia
Asante
 
Mtoa post utakuwa na ubinafsi wa Hali ya juu' Sasa majirani utawakwepea wapi? Utakwepa ndugu na marafiki lakini jirani humchagui na hana mpango wa kuhama pale ni kwake , wewe kama hauwataki majirani siku kitakukuta kitu na wao watakuachq hivyohivyo utateseka sana . Hakuna mtu muhimu kama jirani Yako katika maisha kikubwa ni kuwekeana mipaka , kama humtaki hata ndugu Yako basi huwezi kufanya KAZI ofisi yeyote na ni Bora ukaondoka duniani , hakuna namna utaishi humu duniani bila interaction
 
Acha utoto fam, majirani ndo watakao kuja kukusaidia, ndugu waje ila wasipazoee sana home
 
Wanawake wamekua fantasized na maisha ya wazungu wanayoyaona kwenye tamthilia hawajui jinsi maisha ya upweke yanavyowasababishia sonona hao wazungu.
 
Wakati wa kukua kama ulitaman kuwa mtu fulani na sasa ndivyo ulivyo. Basi hayo unayoyasema sasa yatawezekana. Lakini maisha yana sarakasi nyingi. Unavyotaka huwa haiwi kwa 100%.
 
Jata huyo mchumba wako ni hajitambui unawezaje kuwa na mahusiano na mtu asiyetaka kuwa na mahusiano hata na ndg zake wakuzaliwa nae, hilo ni tatizo tena kubwa sana,
Hataki sasa wanini kwetu?? Wala hatuendagi kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…