Nikija kuwa na familia kuna vitu sintoruhusu

Nikija kuwa na familia kuna vitu sintoruhusu

Kwa kweli mpaka sasa mimi si mtu wa kutembelea watu sana.

Na ingawa nambana mtoa mada, naelewa sana anavyofikiri, kwa sababu hata mimi nimepitia huko.

Sasa hivi kuna mambo mengi sana, na hata tunapombana mtoa mada ajifikirie zaidi, inatubidi tumuelewe. Maneno mengine hayasemwi bure, inawezekana kapitia, kaona au kasikia kitu cha kumpa sababu nzuri za kupanga anavyopanga.

Kuhusu mimi, kuna wakati nilikuwa na focus sana kwenye mambo yangu, kusoma, kuji establish katika kazi, kula bata mwenyewe, kuanzisha famikia yangu.

Halafu, baada ya kuji establish mwenyewe, kuweka himaya yangu, kuanzisha familia yangu, nikaona umuhimu wa kuwa na mahusiano na jamii, familia. Hata kama si kila mtu, kuwa na watu wangu wachache ambao nakuwa nao karibu. Nikawa hata kama sihitaji ku interact na kila mtu, kuna key focal points za jamii, wale viongizi, nakutana nao, nawatembelea. Na wao wananitembelea.

Najivunia sana uwezo wa kuwa na kwangu na ndugu zangu, jamaa na marafiki wakifika Marekani wawe na sehemu ya kufikia.

Mathalani mwaka juzi kuna vijana wawili wa familia (extended) wamekuja kuanza chuo Marekani, wadogo sana, mara yao ya kwanza kuja Marekani, hawamjui mtu. Nikaenda JFK Airport hapa New York kuwapokea, wakakaa nyumbani kwangu siku chache, nikawapeleka mpaka chuoni kuwaandikisha, sasa wanakaribia kumaliza chuo. Wanajua kuwa Marekani kina nyumba ni kwao, wana sehemu ya kufikia.

Kuna kijana kaja mwaka jana kutoka Tanzania kama scholar hapa Marekani, nimekaa naye sikunkadhaa, kafurahi sana kukutana na Mtanzania Marekani.

Kuna mtoto alikimbia kwao Houston akija New York City, kitu cha hatari sana kwa kuwa kuna watu wanateka watu. Nikapigiwa simu na famikia kutoka Dar kumtafuta na kumchukua, akakaa kwangu mpaka alivyopata kutukia na kurudi kwao.

Sasa kaka mkubwa balozi asiye rasmi wa famikia moja ya function yangu ni kuwa na sehemu ambayo ndugu zangu wanaweza kufikia. Nikisema nifunge vioo hata sababu ya mimi kuwa nililo inaondoka.

Ila pia, naelewa matatizo mengi ya kijamii yanayoweza kusababisha watu wafunge vioo.

Issue si kufunga vioo au kutofunga vioo, issue ni kuwa na chujio la kujua unamruhusu nani awe karibu nawe na nani humruhusu.

Naelewa ukifungua madirisha ili hewa safi iingie, unaweza kuruhusu nzi waingie ndani. Lakininunaweza kuweka wavu hewa safi iingie na nzi wasiingie.

Ukiwafungia sana watu vioo, unaweza hata kujifungia wewe mwenyewe advantages fulani.
Mtoa mada ni tofauti na wewe, na mazingira ya nchi uliyopo, Labda kama yupo ughaibuni, anataka abakie yeye na mumewe tu hataki ndg wa upande wowote, jirani, wachungaji nk kibongo bongo hiyo ni haiwezekani hata uwe unajiweza vipi kiuchumi

Ndio maana nikamwambia anaota, sababu yeye binafsi anaweza kuishi hivyo ila sio kwa mwenzi au watoto nk

Mi pia si mpenda muingiliano hivyo lakini sio kama mtoa mada
 
Mtoa mada ni tofauti na wewe, na mazingira ya nchi uliyopo, Labda kama yupo ughaibuni, anataka abakie yeye na mumewe tu hataki ndg wa upande wowote, jirani, wachungaji nk kibongo bongo hiyo ni haiwezekani hata uwe unajiweza vipi kiuchumi

Ndio maana nikamwambia anaota, sababu yeye binafsi anaweza kuishi hivyo ila sio kwa mwenzi au watoto nk

Mi pia si mpenda muingiliano hivyo lakini sio kama mtoa mada
Wanakuwinda tu wakishakupatia utakuja toa post unaomba ushauri hujielewi
 
Moja ni kuwaalika ndugu zangu nyumbani kwangu ambapo watoto wangu wanaishi na sio ndugu zangu tu hata ndugu wa mume.

Kingine marafiki , wachungaji ,mazoea sitaki.
Majirani wote siwataki kabisaa .

Na mawatu tu ambao hawajui kwanini wanakuja .

Kwangu pawe kwangu tu hawa watu hawana wema ni wanakuja tu kuharibu maisha ya watoto wako. Kabisa ..... hauoni leo ila baadaye wakitaka kuoa , kupata kazi , kuoelewa, kutafuta riziki hapo sasa mnaanza usumbufu usio hitajika.

Labda huyo mtu awe anajitambua . Aisee maana watu ni wanafiki sana.
Tangu nakua mpaka sasa nazeeka nimekua nikiamini na nitaendelea kuamini kuwa wakubwa wanakutana baa/BAR sio majumbani.
 
Mtoa mada ni tofauti na wewe, na mazingira ya nchi uliyopo, Labda kama yupo ughaibuni, anataka abakie yeye na mumewe tu hataki ndg wa upande wowote, jirani, wachungaji nk kibongo bongo hiyo ni haiwezekani hata uwe unajiweza vipi kiuchumi

Ndio maana nikamwambia anaota, sababu yeye binafsi anaweza kuishi hivyo ila sio kwa mwenzi au watoto nk

Mi pia si mpenda muingiliano hivyo lakini sio kama mtoa mada
Lakini kasema hatajifungia kabisa watu fulani wanaojielewa atawafungulia.

Kufungulia mnaanza kidogo kidogo, halafu mkishatuamini mnatupa yote 🤣🤣🤣
 
Lakini kasema hatajifungia kabisa watu fulaninwanaojielewa atawafungulia.

Kufungulia mnaanza kidogo kidogo, halafu mkishatuamini mnatupa yote 🤣🤣🤣
Unaona hapo eti ananipa tahadhari😅😅😅hili kweli debe tupu
 
Unaona hapo eti ananipa tahadhari😅😅😅hili kweli debe tupu
Ujue kujinafasi ni haki ya kikatiba.

Mimi huwa najiapiza kuna nchi fulani sitakwenda daima kwa sababu za kifalsafa, kupingana na misimamo yao.

"Huku Russia huku, sitakaa nikanyage daima, Putin mshenzi sana kavamia Ukraine, siendi ng'o".

Wakati nilikuwa siendi Russia, hata kabla Russia haijavamia Ukraine.
 
Ukiwa single mother utafanikiwa hilo. Ila ukienda kuishi kwenye maisha ya mwanaume, nyumbani kwake kakuoa wewe umekuta anatembelewa na ndugu zake wanaishi bila shida, wewe ndo uende ukaweke sheria zako......aisee labda kama jamaa hawezi kuinua mdomo kwako.
Na hilo ukifanikiwa basi hiyo ndoa umejioa
 
Moja ni kuwaalika ndugu zangu nyumbani kwangu ambapo watoto wangu wanaishi na sio ndugu zangu tu hata ndugu wa mume.

Kingine marafiki , wachungaji ,mazoea sitaki.
Majirani wote siwataki kabisaa .

Na mawatu tu ambao hawajui kwanini wanakuja .

Kwangu pawe kwangu tu hawa watu hawana wema ni wanakuja tu kuharibu maisha ya watoto wako. Kabisa ..... hauoni leo ila baadaye wakitaka kuoa , kupata kazi , kuoelewa, kutafuta riziki hapo sasa mnaanza usumbufu usio hitajika.

Labda huyo mtu awe anajitambua . Aisee maana watu ni wanafiki sana.
Na wala huu sio ubinafsi.

Watu wana mazoea ya ajabu sana na nyumba za watu. Unamkaribisha mtu na yeye anakaribisha watu
 
Kuna kaka yetu katika ukoo. Ameoa na watoto wa2. Kuna kipindi mke wake kalibia anaelekea kujifungua mtoto wa3 alianguka na pikiliki akateguka mguu kiasi akawa imobile kwa miezi3.

Mume wake akiwa anarudi kutoka mkoani alipo lazwa mkewe, akapata ajali na kuvunjika miguu na mkono nae akawekewa hogo na kua immobile.

Wote walipotoka hospitali wakaenda kuishi kwa kaka yake na mumd kwa miezi2.

Tunza akiba ya maneno binti
 
Mimi nakuelewa mleta mada, naomba tuijenge family nzuri nitakupenda,kukuheshimu na kukujali daima.
 
Back
Top Bottom