Nikitaka kujiunga UTT Amis ni lazima niende ofisini kwao?

Nikitaka kujiunga UTT Amis ni lazima niende ofisini kwao?

xi maha

Member
Joined
Dec 26, 2022
Posts
22
Reaction score
28
Hivi nikitaka kujiunga UTT amis ni lazma niende ofisini kwao?? Na je, mfuko gani una return nzuri?
 
Ndio ni lazima Kuna fomu za kujaza pale japo unaweza kujisajili kupitia *150*82# au app Yao but utaweza kuweka pesa tu ila ishu za kumfatilia maendleo ya vipande vyako na ukitaka kutoa itakua ngumu
 
Hivi nikitaka kujiunga UTT amis ni lazma niende ofisini kwao?? Na je, mfuko gani una return nzuri?
Download app, jisajili na anza kuweka michango yako humo. Baada ya hapo utahitaji kudownload form yao unajaza particular zako na kuituma kwa email au ende physically ofisini kwao. Maelezo yote haya yapo kwenye website yao
 
Download app, jisajili na anza kuweka michango yako humo. Baada ya hapo utahitaji kudownload form yao unajaza particular zako na kuituma kwa email au ende physically ofisini kwao. Maelezo yote haya yapo kwenye website yao

Mkuu kama una maelezo ya hizo scheme ipi ni nzuri zaidi
 
Mkuu kama una maelezo ya hizo scheme ipi ni nzuri zaidi
Idadi ya mifuko hadi sasa ni 6:
Ukwasi| Jikimu| Wekeza Maisha | Umoja | Hatifungani | Watoto.

1. Sasa unaweza kuuza vipande vyako kwa njia ya menu ya simu, siminvest *150*82#. Nenda eneo wameandika "Kuuza Vipande". Ukomo ni milioni 2 kwa siku.

2. Ukishafanya zoezi la kuuza au kutoa hela basi utatumia ndani ya muda usiozidi siku 3 kupata hela yako katika akaunti ya benki ulojaza wakati unafungua au kukamilisha usajili wako. Ndani ya siku 3 za kazi ni kwa mfuko wa Ukwasi/Liquid Fund huku mifuko mingine ni ndani ya siku 10 za kazi. #Siku za kazi ni J3 hadi Ijumaa#.

3. Unaweza kufungua akaunti yako kwa njia karibu 6 ( kwa njia ya simu *150*82#, Utt amis app, kujaza fomu mtandaoni, CRDB benki au kutembelea ofisi za UTT AMIS ). Kwa njia ya simu na app utaweza kuendelea kununua vipande/kuweka hela ila itakusumbua kutoa endapo hutakamilisha usajili wako.

4. Unaweza kutumia njia mbalimbali kuchangia/kuweka hela yako UTT AMIS. Kuanzia kuweka kwa njia ya benki ( CRDB, NMB, NBC), njia ya benki mtandaoni ( CRDB simbanking, NMB mkononi), mawakala ( CRDB), Utt amis app na mitandao ya simu yote nchini hadi Azam Pesa.

5. Unapoweka pesa yako unaweza kufuatilia salio ndani ya siku 3 za kazi kwa njia hizi: kwa siminvest menu *150*82# ( uliza salio), UTT AMIS app na tatu kuomba statement yako kupitia uwekezaji@uttamis.co.tz

6. Unaweza kufungua akaunti ya mtu mmoja ( individual account) au akaunti ya pamoja ( Joint account) kwa mtu zaidi ya mmoja ( wenza), vikundi, taasisi na asasi mbalimbali

7. Unaruhusiwa kufungua mfuko zaidi ya mmoja kulingana na malengo yako wewe yalivyo. Unaruhusiwa kuwekeza kusikokuwa na ukomo.

8. Unaruhusiwa kurithisha vipande kwa wanufaika wako ulojaza katika fomu ya kujiunga. Vipande ni mali kama mali zingine kama ardhi katika kurithisha au kuwapa wale watu wetu wa karibu.

9. Viambatanisho muhimu unapofungua akaunti ya uwekezaji UTT AMIS. Uwe na baadhi ya hivi vitambulisho: Kadi ya kupigia kura, leseni ya udereva, NIDA, Hati ya kusafiria + passport picha ( blue background)

10. Vipande vya UTT AMIS vinaweza kutumika kama dhamana katika taasisi za kifedha

Haya ni vyema ukafahamu kama ulikuwa hujajua.
 
Idadi ya mifuko hadi sasa ni 6:
Ukwasi| Jikimu| Wekeza Maisha | Umoja | Hatifungani | Watoto.

1. Sasa unaweza kuuza vipande vyako kwa njia ya menu ya simu, siminvest *150*82#. Nenda eneo wameandika "Kuuza Vipande". Ukomo ni milioni 2 kwa siku.

2. Ukishafanya zoezi la kuuza au kutoa hela basi utatumia ndani ya muda usiozidi siku 3 kupata hela yako katika akaunti ya benki ulojaza wakati unafungua au kukamilisha usajili wako. Ndani ya siku 3 za kazi ni kwa mfuko wa Ukwasi/Liquid Fund huku mifuko mingine ni ndani ya siku 10 za kazi. #Siku za kazi ni J3 hadi Ijumaa#.

3. Unaweza kufungua akaunti yako kwa njia karibu 6 ( kwa njia ya simu *150*82#, Utt amis app, kujaza fomu mtandaoni, CRDB benki au kutembelea ofisi za UTT AMIS ). Kwa njia ya simu na app utaweza kuendelea kununua vipande/kuweka hela ila itakusumbua kutoa endapo hutakamilisha usajili wako.

4. Unaweza kutumia njia mbalimbali kuchangia/kuweka hela yako UTT AMIS. Kuanzia kuweka kwa njia ya benki ( CRDB, NMB, NBC), njia ya benki mtandaoni ( CRDB simbanking, NMB mkononi), mawakala ( CRDB), Utt amis app na mitandao ya simu yote nchini hadi Azam Pesa.

5. Unapoweka pesa yako unaweza kufuatilia salio ndani ya siku 3 za kazi kwa njia hizi: kwa siminvest menu *150*82# ( uliza salio), UTT AMIS app na tatu kuomba statement yako kupitia uwekezaji@uttamis.co.tz

6. Unaweza kufungua akaunti ya mtu mmoja ( individual account) au akaunti ya pamoja ( Joint account) kwa mtu zaidi ya mmoja ( wenza), vikundi, taasisi na asasi mbalimbali

7. Unaruhusiwa kufungua mfuko zaidi ya mmoja kulingana na malengo yako wewe yalivyo. Unaruhusiwa kuwekeza kusikokuwa na ukomo.

8. Unaruhusiwa kurithisha vipande kwa wanufaika wako ulojaza katika fomu ya kujiunga. Vipande ni mali kama mali zingine kama ardhi katika kurithisha au kuwapa wale watu wetu wa karibu.

9. Viambatanisho muhimu unapofungua akaunti ya uwekezaji UTT AMIS. Uwe na baadhi ya hivi vitambulisho: Kadi ya kupigia kura, leseni ya udereva, NIDA, Hati ya kusafiria + passport picha ( blue background)

10. Vipande vya UTT AMIS vinaweza kutumika kama dhamana katika taasisi za kifedha

Haya ni vyema ukafahamu kama ulikuwa hujajua.
Je ni mfuko gani mzuri wa kuwekeza UTT AMIS ?

Jibu: Mifuko yote mizuri kulingana na lengo anayewekeza anawekeza kwa malengo yepi. Hivyo mwekezaji inabidi ajue lengo lake la uwekezaji ni lipi na hili litampa mwanga wa aina ya mfuko wa kuwekeza.

Kabla hujawekeza pata elimu, jua malengo yako, kipato chako na pengine umri wako. Hivi vitakusaidia kujua wapi uweke hela yako.
 
Je ni mfuko gani mzuri wa kuwekeza UTT AMIS ?

Jibu: Mifuko yote mizuri kulingana na lengo anayewekeza anawekeza kwa malengo yepi. Hivyo mwekezaji inabidi ajue lengo lake la uwekezaji ni lipi na hili litampa mwanga wa aina ya mfuko wa kuwekeza.

Kabla hujawekeza pata elimu, jua malengo yako, kipato chako na pengine umri wako. Hivi vitakusaidia kujua wapi uweke hela yako.
Je unapofungua akaunti ya UTT AMIS kuna gharama za awali ?

Jibu: Hakuna gharama zozote unapofungua akaunti ya uwekezaji. Hakuna kiasi utahitaji kulipia kwa kufungua akaunti ya uwekezaji. Ila kama unataka uanze uwekezaji hapo ndo kuna kiasi cha kuanzia kulingana na mfuko unaowekeza

Mfano
Umoja Fund kianzio ni 10,000/=
Ukwasi Fund kianzio ni 100,000/=
Watoto Fund kianzio ni 10,000/=
 
Kwa bukoba ofisi ziko wapi?
Bukoba hawana ofisi
1736756869051.png
 
But siku za nyuma CRDB bank walikuwa wakala wao ila nasikia na wao wameanzisha mfuko kama huo wa UTT so not sure kama wana offer huo uwakala
 
But siku za nyuma CRDB bank walikuwa wakala wao ila nasikia na wao wameanzisha mfuko kama huo wa UTT so not sure kama wana offer huo uwakala
Nakumbuka siku naenda tawi la CRDB kujaza fomu ya kukamilisha USAJILI yule muhudumu alianza kunipanga kuwa niachane na UTT, niingie Kwao (Mama Samia Infrastructure Bond)
Jamaa alivyokuwa serious akaniachia Hadi namba yake ili anishawishi vizuri.
 
Je ni mfuko gani mzuri wa kuwekeza UTT AMIS ?

Jibu: Mifuko yote mizuri kulingana na lengo anayewekeza anawekeza kwa malengo yepi. Hivyo mwekezaji inabidi ajue lengo lake la uwekezaji ni lipi na hili litampa mwanga wa aina ya mfuko wa kuwekeza.

Kabla hujawekeza pata elimu, jua malengo yako, kipato chako na pengine umri wako. Hivi vitakusaidia kujua wapi uweke hela yako.
Hapa umetoa jibu General, kama ilivyo kwenye web yao

Sasa naomba ujibu wewe kama wewe, wote tunajua lengo wa kujiunga UTT ni kupata pesa,

Ngoja nigeuze swali, katika mifuko yote sita ni mfuko upi mostly huwa na percent kubwa mwisho wa mwaka?
 
Back
Top Bottom