GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
- Thread starter
-
- #41
Mara nyingi JB Mpiana hupenda Kuwataja Wanamuziki wake wote katika nyimbo Mbili tu za taratibu ( Rhumba ) za Omba na Jeanette.Kuna wimbo mmoja JB mpiana anawataja wanamuziki wote wa bendi yao ni nzuri sana,
Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
Na hakuna Wanamuziki ambao JB Mpiana huwa akiwataja kwa Kuwaimba hujikuta hata akitokwa na Machozi ya Kihisia kama aliyekuwa Mwanamuziki wake Kipenzi ndani ya Bendi Alain Mpela 'Afande' na Rapa ( Atalaku ) wake Kipenzi Tutu Calugi bila Kumsahau aliyekuwa Mpiga Gitaa wake wa Bass ( Besi ) na Mmoja wa Waanzilishi wa iliyokuwa Bendi Mama ya Wenge Musica BCBG 4 X 4 iliyokuwa imesheheni 'Mafundi' watupu kama JB Mpiana mwenyewe aliyebaki na Wenge BCBG, Ngiama Makanda Werrason aliyebaki na Wenge Maison Mere, Blaise Bula ( ambaye ni Msomi sana na Kitaaluma ni Injinia wa Ndege ) aliyebaki na Bendi ya Wenge Ponderation na Adolphe Dominguez aliyebaki na Wenge Affaire Tonya Tonya bila Kuwasahau akina Alain Mpela, Aimelia Byakodile, Suzuki na Ferre Gola ambaye amefundishwa Mziki na JB Mpiana japo Werrason baadae akampika zaidi Kimuziki na leo nae anajitegemea.