Niliingia k.koo majuzi kati hapa kwenye duka la Haya makitu akaja m.tandale
anaulizia SEA PIANO ile yenye disco light,hilo duka wakawa hawana ila wakawa
wanamshauri achukue sabufa nyingine,yeye akawambia sitaki zaidi ya sea piano
yenye disco lights,mimi nikawa najiuliza hii sea piano yenye disco light ipoje na maajabu
yake ni yapi kwann ing'ang'aniwe hivyo? basi jamaa mmoja akamwambia yule mteja asubiri
akae chini akamletee store nyingine,Jamaa akaenda kama dk 5 akarudi na sea piano lenye disco light
Jamaa (mteja) akasema YEEEEES huyo ndio mnyama sasa,naomba nitestie kbsa,chukua na hela yako
seapiano likachomekwa likaekwa flash,Mziki ukaekwa Aseee mteja mwenye bufa lake nikamuona
anatikisa kichwa kwamba mziki umemgusa hadi kunako,ila huwezi amini Nilishkwa hasira nikatamani
nimzabue yule jamaa kofi nimuulizee,huu n mziki unanunua au unanunua tambara?!
Jamaa alipewa bufa lake akaondoka anachekelea ndio nmesoma comment yako nikamkumbuka jamaa.