Niko hapa kanisani kwa sasa wasabato nimevaa jeans, waumini wenzangu wananiona Kama Antichrist.

Jeans si vazi la kuendea kanisani, ni vazi la kihuni mitaani. Haipendezi, hebu fikiria mhubiri kavaa jeans alafu yuko mbele madhabahuni anahubiri ataonekana ni muhuni fulani hivi. Kila sehemu ina mavazi na mitindo yake inayofaa huko
 
Itakuwa ndio wewe niliyekuona hapa Ibadani... Wacha tumalizie ibada nitarudi tena
 
😂 Kama vile wengine wamevaa nguo zilizotengenezwa na Yesu mwenyewe kumbe inawezekana hata ya mchungaji wao imetoka kiwanda kimoja. ja na hiyo jeans yako. Imani ikikuingia vibaya ni uwendawazimu kabisaa
 
Badili mtizamo na ufuate kilichokupeleka kanisani. Sidhani ikiwa macho ya watu na kukuona kwao kutakifikisha kwenye malengo yako

Halafu wamekuambia jinsi wanavyokuona au ni fikra zako na hilo jona ulilojiita wamekutajia wao au wewe ndiye umejibatiza kisha ukawasingizia wao kuwa wanakuona vile. Acha uongo na uzushi na utubu

Wewe umewaonaje kuwa wanakuona ikiwa wewe huwaoni? Ulitaka wapite kwako wakiwa wamefumba macho?

Mpaka hapo nahisi utakuwa unajua jinzi sio nguo ya kanisani. Vinginevyo usingejihisi. Ikiwa wao hapo ulipo sio utamaduni wao kuingia na kanzu au jinzi lazima wakukodolee macho lakini ikiwa wewe unajikubali na hauoni ubaya wa jinzi mbele za Mungu, nafsi yako iko sawa endelea kupigilia jinzi na uabudu katika Roho na Kweli
 
Hakika
Kazi ipo mkuu. Basi fresh tukutane mbinguni tu, maana wengi tumeficha ya kwetu tunakuonaga mdhambi wewe tu. Ila kila ukilala usisahau kutubu.

Hakika Mkuu Kila mtu ana madhambi yake , tofauti sisi wengine tunaweza yaweka HADHARANI mkayaona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…