Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Kuna restaurant moja kigamboni marneo ya kibada tuliuziwa bei tofauti ya chakula kinachofanana mimi na jmaaa fulani hadi nilibaki nashangaa nilitaman nimwambie ila nikaamua kukausha sababu alivyotajiwa akalipa akasepa
 
Do not bite off more than you can chew.Maisha ya kuiga na kujifaragua matokeo yake ndio haya.Ungekufa na tai shingoni baada ya kuamua ulichoamua.Kulalama na kutafuta walioingia cha kike kama wewe haitakusaidia lolote.
mkuu sijataka msaada…nimejifunza tu jambo muhimu na somo la msingi sana.

heshima kwa wajomba nimepata lakini,ndio cha muhimu
 
Kama mlienjoy hakuna shida yeyote,
Hela zinatafutwa ila huo mtoko na wajomba zako utabaki kua ni memory,

Watoto wataulizwa na shemeji,mlienda wapi? Watataje mlipoenda,bila shaka shemeji anajua kua hiyo sehemu vyakula ni gharama,

So,kwa upande mwingine umejijengea heshima fulani mkuu.
 
Kuna mitaa hapo mlimani city chakula cha watu watatu bill ilisoma 665,000/=
 
Siku hiyo nimefuata mwenyewe gari langu Dar (wakati huo nimeajiriwa mikoani). Nilikuwa sina uzoefu wa kuendesha umbari mrefu. Ile nakunja kona ya Morogoro naifuata mbuga ya mikumi usingizi ukaanza. Niliamua kuendesha usiku kukwepa matrafiki kwasababu sikuwa vizuri mfukoni ukizingatia ndo nimenunua ndinga na wese la kunifikisha. Basi, ile naianza mbuga ya mikumi usingizi kama woote! (Kama mnavyojua mbuga za wanyama huruhusiwi kusimama! ni sehemu ambayo ni hatari kusimama, au kuegesha gari sijui upige usingizi kidogo). Basi nilipata shida saana ukizingatia ni usiku na nilikuwa peke yangu! Sijui huo usingizi ulitoka wapi maana si kwa kuyumba huko wakati spidi ilikuwa haizidi 40km/h. Mikumi ina urefu kama kilometer 50 - 60 kuivuka na ukiongeza kama kilometer 20 (buffer zone) inafika kama 70km hivi I guess! Nakwambia nilitumia kama masaa 2 kumaliza mbuga na kufika sehemu ya mahoteri. Kipindi hicho ilikuwa mwaka 2014. Basi nikaendesha na kufunguliwa Gate ya hoteli na kuingiza gari ndani ili angalau nikalale pia kwa usalama wa gari. Eeebwaanah wee! Kufika reception naambiwa for a night 🌙 ni 80,000/=. Nilichoka! Kuondoka siwezi! Nikaingiwa na akili ya kujifanya kuna kitu nimesahahu kwenye gari nilivyoingia kwenye gari nikashusha vioo vya nyuma kidogo na kupiga mbonji mpaka asubuhi saa 2. Nashukuru Mungu hakuna aliyenibughudhi na nadhani sijui walinistahi au vipi maana sikuona nikifwatwa au kuuliza nilivyawasha gari asubuhi na kuondoka! Mlinzi alinifungulia Gate kwa tabasamu na kunitakia safari njema na kusema "Karibu tena". Kwakweli bei za uduma sehemu za washua tuwaachie wenyewe!
 
Siku na jamaa mmoja tumetoka kwenda kupiga mdudu tuendelee na mambo ingine, si akaagiza janamke lake lije? Ni ile mikurumbembe ya kuimba taarabu kko huko au migo.
Nikajua hizo ni issue zake hainihusu, e bana likaja na menzie matano.
Ni vibonge aisee wana stamina hatari.
Waligonga menyu , bia kilo 3 ikakata pale mshkaji hana senti kumi.
Kasema kesho narudisha.
Duh tukatoka ikabidi niingie kutoa ulinzi kilo 3 ingine.maana ndo kwanza tunaenda club
Ziliisha zote usiku ule.
Jamaa hajarudisha hata senti.
Kubandeki zake yule fwala
 
Hi Hizo bei za kawaida sana. Halafu bia 4000? Hicho kiwanja cha uswazi sana labda ingekuwa 8000 ndo cha kidoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…