Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.

Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.

Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.

Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.

Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.

Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.

Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.

…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa

chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5

kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.

Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.

Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…

Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.

Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.

Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.

basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.

Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
Hahaha....unabahati kwenye Account zilikuwemo. Ungevunja ndoa ya Dada yako kwa aibu.
 
Sifa zimekuponza mkiambiwa Dar jiji la biashara muwe mnaelewa 😹😹

Tena nyie kina Ngosha ndo wabishi na ujuaji mwingi.!!
Si vibaya ukaagiza Menu list uweze kuona bei.
Ni busara kununua chakula au huduma ambayo unajua bei kabla ya kuagiza ili urizike nayo.
Mwaka Fulani niliend Jerusalem Israeli.

Nilikuwa na bajeti inayobana sana. Na natakiwa kuishi nayo hivyo hivyo kwa miezi kadhaa.

Siku moja nililala nikaamka muda wa hotel chakula kimeshaisha.

Nilishuka ghorofani na kwenda mtaa wa Hillele angalau nipate mkate maana nilikuwa na njaa kali siwezi kulaka usiku.

Nikasome Menu kwenye Cofee room.

Nilisoma(whole bread) 15Shekeli. Kwa haraka haraka haraka nikadhani ni Mkate mzima.

Nikamwambia mhudumu aniletee. Kumbe bi Slice moja tu ya mkate wa ngano.
🤣🤣🤣
Nikalillpa Dola zangu tano sawa na 15 shekeli. Nikasepa
.
 
Pole mkuu, uwe unauliza next time
Hii Sh. Ngapi hii sh ngapi hauna hela nini?

Sasa wewe jifanye unazo uone.

Kuna jamaa yangu tukiwa chuo kapata hela za boom akabeba Pisi kali Bahari Beach.

Ile pisi ikawa inamkomoa nshikaji, ikaagiza kuku mzima.

Mshikaji alijua ni elfu 30 tu hii.

Kumbe ni 50k.

Akakosa nauli ya kurudi😅😅😅
 
Si vibaya ukaagiza Menu list uweze kuona bei.
Ni busara kununua chakula au huduma ambayo unajua bei kabla ya kuagiza ili urizike nayo.
Mwaka Fulani niliend Jerusalem Israeli.

Nilikuwa na bajeti inayobana sana. Na natakiwa kuishi nayo hivyo hivyo kwa miezi kadhaa.

Siku moja nililala nikaamka muda wa hotel chakula kimeshaisha.

Nilishuka ghorofani na kwenda mtaa wa Hillele angalau nipate mkate maana nilikuwa na njaa kali siwezi kulaka usiku.

Nikasome Menu kwenye Cofee room.

Nilisoma(whole bread) 15Shekeli. Kwa haraka haraka haraka nikadhani ni Mkate mzima.

Nikamwambia mhudumu aniletee. Kumbe bi Slice moja tu ya mkate wa ngano.
🤣🤣🤣
Nikalila Dola zangu tano sawa na 15 shekeli. Nikasepa
.
Ubahili ulikuzidi had Nchi za watu dr 😹😹

Mimi rafiki yangu tukiendaga wote kufunga mzigo, anashangaa nikimpa dollar 100 ale chakula na hainiumi…!!
Ila tukiwa bongo siwezi kumpa hiyo pesa kwa Tsh hata iweje🤣🤣

Hii kitu najiulizaga sipati jibu bongo pesa inaniuma.!
 
Mkuu Nimecheka kwamba kuna mmoja kiherehere aliagiza pizza. Mimi kipindi nipo chuo weekend na mama watoto tumeingia supermarket tunafanya shopping sasa kuna shelf la wine tukafika sasa ile nachukua chupa ya wine lahaula upande wa shelf wote upo chini wine kadhaa zimepasuka walinifwata spidi kama mama anavyosikia kishindo alafu mtoto wake Akalia huko nje. Wakawa wanafoka kweli kwa hasira nikasema nipeni bill nitalipia. Nakumbuka mmoja akaniambia utaweza wife akamjibu Unatuchukulia kama wewe mfanyakazi supermaket. Wakatupa bill inasoma 645000/-. Uzuri pembeni kulikuwa na ATM ya NBC wife akaenda kutoa maana mfukon nilikuwa na 180000/- Tukawalipa Tukawafyonza Tukaondoka Zetu Ila ile pesa inaniuma mpaka Leo nadhan lile shelf walikuwa wamelitegesha sikuapply nguvu kubwa kuchukua chupa ya wine kiasi cha kuuangusha ule upande wa shelf
We ungesema limeanguka lenyewe Watanzania waoga sana kubishana hapo angekua Mzungu asingekubali Wazungu wabishi sana tena ukute Wataliano au Warusi.
 
Niliwahi kunywa chai ya 25,000/= nashela hotel Morogoro.

Chai yenyewe Sasa:-
1. Kipande Cha kiazi Cha kienyeji kimoja.
2. Kikombe kidogo Cha Maziwa mixer kahawa.
3. Yai moja lililokaangwa
4. Slices mbili za mkate
Uzuri nilikuwa na pesa ya kutosha.
Bia moja 5000/=

Jumla fasta tu 50,000/=
Hii ilinitokea ledger plaza kule bahari beach. Breakfast ya tuvitu vitu tu halafu sasa bei... Sema sikomi kwenda huwa kuna mazingira mazuri ya kupunguza stress ila sithubutu kwenda na nyomi hata mara moja.
 
Kuna restaurant moja kigamboni marneo ya kibada tuliuziwa bei tofauti ya chakula kinachofanana mimi na jmaaa fulani hadi nilibaki nashangaa nilitaman nimwambie ila nikaamua kukausha sababu alivyotajiwa akalipa akasepa
Mkuu itakua viungo vilivyotuka ni tofauti
 
Ubahili ulikuzidi had Nchi za watu dr 😹😹

Mimi rafiki yangu tukiendaga wote kufunga mzigo, anashangaa nikimpa dollar 100 ale chakula na hainiumi…!!
Ila tukiwa bongo siwezi kumpa hiyo pesa kwa Tsh hata iweje🤣🤣

Hii kitu najiulizaga sipati jibu bongo pesa inaniuma.!
Hahahaha Mkuu Hela inauma kutokananna jinsi ulivyoipata.
Ndio maana kwenye vibanda vya chips wanawake woote wanaagiza chips Kuku.

Mamen wanangiza chips kavu akijitahidi na soseji moja🤣🤣
 
Niliwahi kunywa chai ya 25,000/= nashela hotel Morogoro.

Chai yenyewe Sasa:-
1. Kipande Cha kiazi Cha kienyeji kimoja.
2. Kikombe kidogo Cha Maziwa mixer kahawa.
3. Yai moja lililokaangwa
4. Slices mbili za mkate
Uzuri nilikuwa na pesa ya kutosha.
Bia moja 5000/=

Jumla fasta tu 50,000/=
Hela hata kama unayo ni vema ukawa umeridhika na kile unachoenda kula.
 
Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.

Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.

Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.

Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.

Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.

Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.

Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.

…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa

chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5

kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.

Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.

Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…

Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.

Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.

Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.

basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.

Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
Uulize mkuu kabla ya yote. Mm sili msosi bila kuulizq maana kuna maeneo nilikula wali tu na nyama ya ngombe afu bill inakuja 12elf iliniuma sana
 
Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.

Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.

Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.

Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.

Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.

Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.

Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.

…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa

chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5

kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.

Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.

Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…

Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.

Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.

Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.

basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.

Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
Bahati yako ungeumbuka.
 
Mafundi gareji wanafikiri kumiliki gari ni utajiri. Nilienda gereji nikamueleza tatizo akasema andaa kama 60,000. Nikasema fanya kazi. Wakafungua kwenye miguu baadaye anasema wamekuta matatizo mengine. Jumla ikaja 380,000. Ilikuwa balaa. Kuacha gari gereji siwezi maana wizi mwingi. Mpangaji akaniokoa. kodi ilikuwa inaisha siku hiyo, kumpigia akatuma muamala chap😃. Nikalipa na kusepa. Sijarudi gereji hiyo tena.
Wengine matapeli.....na hukupaswa kulipa maana hukupewa hizo taarifa za matengenezo mengine.
 
Hapo ulitakiwa uondoke kama upo wale watoto ndo dhamana yako wahudumu wakiwaona wanajua upo around, bahati nzuri mabasi siku hizi yapo hadi usiku, zile nguo ulizoacha kwa shemeji yako unaachana nazo.

Unapanda katarama lux ukifika manyoni ndo unampigia simu dada yako unamwambia akafate watoto wake huko ulipowaacha.
 
Hapo ulitakiwa uondoke kama upo wale watoto ndo dhamana yako wahudumu wakiwaona wanajua upo around, bahati nzuri mabasi siku hizi yapo hadi usiku, zile nguo ulizoacha kwa shemeji yako unaachana nazo.

Unapanda katarama lux ukifika manyoni ndo unampigia simu dada yako unamwambia akafate watoto ulipowaacha.
Hahaha
 
Back
Top Bottom