Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Niliagiza chakula, ilivyokuja bili nusura nikimbie niwaache watoto. Umewahi kukumbana na fedheha hii?

Hapo ulitakiwa uondoke kama upo wale watoto ndo dhamana yako wahudumu wakiwaona wanajua upo around, bahati nzuri mabasi siku hizi yapo hadi usiku, zile nguo ulizoacha kwa shemeji yako unaachana nazo.

Unapanda katarama lux ukifika manyoni ndo unampigia simu dada yako unamwambia akafate watoto wake huko ulipowaacha.
Nimecheka kifala
 
Siku nyingine uliza bei kabla ya huduma wala sio ushamba.
Ushauri wa busara sana huo.

Mi nshajifunza siku nyingi sana hayo mambo, tena kwa kitu kidogo tu, soda.

Nimefika sehemu,... 'tupe soda'.. tukanywa mbili mbili kwa maongezi zaidi tukiwa watatu.

Kila kona bei ya soda inajulikana ni 500/-, nikatoa noti ya Sh. 5,000/-nikitumaini kurejeshewa 2,000/-.

Mhudumu naye akawa anasubiri buku, hadi nilivyoidai kwa sauti, ndonikaelezwa niongeze buku, yaani soda 350ml inauzwa elfu, kwa lipi hasa!

Tangu siku hiyo ni mwiko kwangu kutumia huduma za watu bila kuuliza bei kwanza.
 
We ungesema limeanguka lenyewe Watanzania waoga sana kubishana hapo angekua Mzungu asingekubali Wazungu wabishi sana tena ukute Wataliano au Warusi.
Kuna rafiki yangu ana pub kigamboni, TBL walikuwa wamepiga rangi zao na kuweka Bei za vinyeaji. Kumbe vinywaji vimepanda Bei lakini wao hawajabadilisha Bei ya vinywaji. Wakaja wazungu wameagiza vinywaji wamekunywa wanaondoka wanapewa bili wanagoma, wanasema Bei tunayoijua ni ile iliyobandikwa na siyo hii mnayotupa. Aliyekuja kuamua ugomvi ni baba wa rafiki yangu Ila wazungu waliondoka washindi.
Kesho yake alimwita fundi rangi afute yake matangazo ya Bei.
Baada ya miezi miwili TBL wakaja Tena wanataka kubandika matangazo ilibidi awatoe nduki.
 
Nilienda kutembea Dar es Salaam kwa dada yangu wakati wa sherehe hizi za christimass.

Basi tarehe 25/12 kama kawaida tulikwenda ibadani na kurudi nyumbani,kilichofuata ni maongezi tu ya kifamilia huku tukichoma nyama jioni na kunywa pombe pamoja na shemeji na marafiki zake.

Tarehe 26/12 nikataka na mimi onyesha msuli wangu kwa shemeji ili asinichukulie poa…Basi bwana nikawaambia leo niachieni hawa vijana nitoke nao out nao waone raha ya kuwa na mjomba,wako watoto wanne na dada wa kazi. jumla watano.

Basi wao wenyewe wakataja mahala wanataka kwenda…ni beach fulani hivi wamejenga vizuri sana na kuna michezo mingi sana ya watoto,vyakula na vinywaji.

Basi tukaondoka tukafika…kiukweli mimi nilidhani ni mahala naweza afford kulipia kila kitu na nilitenga 100,000/= nzima kwa ajili ya kutumbua.

Sasa kufika nikaambia kwanza vijana wapate chakula.Wakaagiza kila mmoja chipsi kavu pamoja na kuku nusu.Pia waliagiza juice freshi na kuna kamoja kiherehere kakaagiza pizza moja ya kushare wote…yule dada wa kazi kwa aibu za kikubwa aliagiza chipsi na mshkaki mmoja tu na juice.

Mahesabu yangu yalikua pale itakata kama 50,000/= hivi pamoja na michezo yao ile…wakamaliza kula,mimi mwenyewe nikaagiza bia zangu 5 pamoja na nyama choma ya mbuzi.

…..sasa game ikaanza karibia wanamaliza kula yule dada ndio akaniletea ile “menu”,lahaulaaaa

chipsi kavu-inasoma 6000/= mara 5
kuku nusu-inasoma 21,000/= mara 4
fresh juice-inasoma glass moja 6000/= mara 5
pizza moja-inasoma 35,000/=
mshkaki mmoja(niligundua wameandika fillet)-3500/=
nyama choma mbuzi—inasoma 25,000/= per portion
bia moja local ni 4000/= mara 5

kwa haraka haraka ilisoma kama 227,500/= kinyume kabisa na matarajio yangu.

Kwanza nilihisi baridi sana imenichapa sababu vitu vyote vishaagizwa na vingine vishaanza kutumika,watoto wanaenjoy sana na huwezi waambia kitu wakakuelewa.

Hapo wanasubiri washibe nikawalipe kila mmoja 5000/= ya kwenda kwenye michezo yao ya watoto…

Mimi bhana nikajitetea nataka kulipa kwa kadi…walete mashine,lengo langu hapa kubahatisha sababu ndio zilikua tarehe bosi anaingiza chochote kwenye account.

Ile kugusa tu pyaaaaa….nakuta sms inaingia umefanikiwa kulipia 227,500/= kwenda Utulivu beach resort,ikaja na sms ya muamala wa makato ya muamala kama 4000/= hivi.

Kwa kweli mood yote ilikata…kwa mshahara wangu hiko kiwango kilikua ni zaidi ya nusu yake mimi nimetumia kulipia watoto kula sehemu ambayo siyo level zangu….ila nikakaza kiume,ile kulipia kwa kadi nikaonekana doni sana pale.

basi na ile laki mkononi nayo nikaibunya mjini…..sahivi niko zangu kwenye katarama narudi zangu mkoani na somo.

Umewahi kutana na dhahama kama hii?!😂
Pole sana lakini umefaidi kupata somo hapo. Kati ya mambo nachukia ni kutumia fedha nyingi bila kupata ile kitu wanaita value for money.

Hadi saa naamini si sawa kula mlo unaozidi TZS 7000/- Juzi kati hapo nimekunywa chai na mayai mawili ya kukaanga wananiambia TZS 6,000/- nusura fujo itokee.
 
😂😂😂atakuwa anatumia mkunde pori kama chai haiwezekani we kila tunavyopindua mwaka we una mtoto mng'aa...siku hizi unajikuta mstaarabu mwenyewe 😂😂😂
😹😹😹
Dada wewe si ndo umesema niache ugomvi jamani 🤣

Ila mwafula hapana.!! Kwani kaambiwa dunia aijaze peke yake??
Atamaliza chanjo wengine tukizaa watoto wapate polio bure 🤣
 
Hapo ulitakiwa uondoke kama upo wale watoto ndo dhamana yako wahudumu wakiwaona wanajua upo around, bahati nzuri mabasi siku hizi yapo hadi usiku, zile nguo ulizoacha kwa shemeji yako unaachana nazo.

Unapanda katarama lux ukifika manyoni ndo unampigia simu dada yako unamwambia akafate watoto wake huko ulipowaacha.
Wakati tupo watoto marehebu baba yetu mdogo alikuwa na tabia anatuchukua anatupeleka Oysterbay hotel anatununulia ice cream Sasa Kuna siku katuchukua akaagiza ice cream halafu akatuacha, alipoondoka sisi tukawa tunaendelea kuagiza ice cream.
Aliporudi kuomba bill anakuta bill kubwa kutaka maelezo akaambiwa watoto ndio waliagiza. Akawahoji kwanini waliwasikiliza watoto baada ya ubishi bill iligawanywa Kati yake na wahudumu na ndio ikawa mwisho kutuchukua kula ice cream.
 
Back
Top Bottom