Niliahidi kuja na 'Exclusives' Saba (7) Saa 3 hii sasa naweka Mambo yote hadharani...

Niliahidi kuja na 'Exclusives' Saba (7) Saa 3 hii sasa naweka Mambo yote hadharani...

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
1. CEO wa Simba SC anatuzuga tu wana Simba SC ila ukweli ni kwamba ana Mahusiano ya 'Kibaiolojia' na Rais ajaye wa Yanga SC Injinia Hersi Said na mara nyingi ndiyo humvujishia Siri zote za Simba SC ambazo ziligeuka kuwa Sumu kwa Mafanikio ya Simba SC kwa Msimu Mzima.

2. Mwekezaji wa Simba SC Mo Dewji na CEO Barbara Gonzalez muda wowote Watajiuzuru Nyadhifa zao ndani ya Klabu.

3. Press Conference ya Simba SC iliyoahirishwa hivi Majuzi ilikuwa ni ya Mwekezaji Mo Dewji na CEO Barbara Gonzalez kuachia Ngazi Simba SC ila ilitumika Nguvu Kubwa kuzuia hilo ili Kuepuka Mpasuko mkubwa ndani ya Wanachama, Wapenzi na Mashabiki.

4. Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu kwa Kushirikiana na Mdogo wake Mwana Yanga SC lialia wametumika 'Kuihujumu' Simba SC katika Mashindano yote ili Kuinufaisha Yanga SC kwa Ahadi Kubwa aliyopewa na Kiongozi Mstaafu Mmoja Tanzania (mwana Yanga SC) na mwenye Ushawishi katika Serikali hii ya Rais Samia kuwa atamuombea ili ateuliwe kuwa Mbunge au apewe Wadhifa mwingine Mkubwa.

5. Baada ya Siri za Mwekezaji Mo Dewji kutaka Kujiuzuru kuwa Mwekezaji ndani ya Klabu ya Simba SC Tajiri wa Azam na Tajiri Mkubwa Tanzania Mzee Bakhressa ambaye hakuna asiyejua Mapenzi yake yasiyo na Kifani kwa Simba SC kuwa tayari kutaka Kuwekeza ndani ya Simba SC tena kwa Fedha mara Tatu ya aliyoweka Mo Dewji.

6. Sababu kubwa ya Ugomvi wa Haji Manara na CEO wa Simba SC Barbara Gonzalez ni Kitendo cha CEO Barbara kujua kuwa tayari Siri yake ya Yeye kuwa na huo ukaribu wa 'Kibaiolojia' na Injinia Hersi Said imeshajulikana na Haji Manara na kuwa kilichokuja Kumuuma zaidi Haji Manara ni Kitendo cha CEO Barbara Gonzalez kumchafua kwa akina Mo Dewji ( Mwekezaji ) na wana Simba SC Wote ili Wamchukie Haji Manara ili Kinachoendelea Kisijulikane.

7. Sababu kubwa ya Watu wa Yanga SC kuanzia Haji Manara, Rais ajaye Injinia Hersi Said na Mbunge Tarimba Abbas hadi Wana Yanga SC wote Waandamizi kusema kuwa Yanga SC itakuwa Bingwa mfululizo kwa Miaka 7 au 8 ijayo ni kutokana na huo Ukaribu wa 'Kibaiolojia' alionao Mkuu wao Rais ajaye Injinia Hersi Said na CEO wa Simba SC Barbara Gonzalez ambaye inasemekana akiwa amenogewa na 'Mavituz' ya Msomali Mswahili Injinia huwa tayari kutoa ( kuvujisha ) Kwake Siri zote za Klabu ( hasa hasa ) pale ikiwa inapambana na Simba SC.

Nimeshatimiza Ahadi yangu Leo hii!!!!
 
Nawaza tu kwa shule aliyonayo na sehemu alizosoma Gonzalez kwanini anafanya kazi zenye kelele kelele hivi....

Jiajiri achana na hizi kazi zenye kelele nyingi...utaona raha ya kujiajiri na exposure uliyonayo naamini utafanya vizuri.

Ni maoni binafsi Wakuu.
 
1. CEO wa Simba SC anatuzuga tu wana Simba SC ila ukweli ni kwamba ana Mahusiano ya 'Kibaiolojia' na Rais ajaye wa Yanga SC Injinia Hersi Said na mara nyingi ndiyo humvujishia Siri zote za Simba SC ambazo ziligeuka kuwa Sumu kwa Mafanikio ya Simba SC kwa Msimu Mzima...
pamparamba mlango wa chuma ukiufungua hauna huruma paapapapaaaaa
 
Tuleteeeeeni Bakhressa tuleteeeee Bakhressa....!!

Ila kiukweli Mimi sijawahi mkubali Mo sio kwamba hajaisaidia Simba Ila sio MTU sahihi wa kuifikisha Simba level za Al Ahly na wengine.

Mpira unahitaji uwekezaji endelevu na kujitoa sio wa kulambwa miguu.
 
Wewe ulikuwa wa kwanza kutuambia Barbra ana uhusiano na Mo, leo tena umehamia kwa Hersi, sijui kesho utaenda kwa nani, unamgeuza binti wa watu kitenesi cha wanaume.

Tatizo hauna kumbukumbu, ulishatuambia sababu ya ugomvi kati ya Manara na Barbra ilikuwa ni u-snitch wa Manara aliowafanyia Simba SC kwa GSM na Hersi kule Kigamboni, Avic Town, naona leo umekurupuka tena kuja na ngonjera zako za uongo.

Kuhusu ile Press Conference iliyoahirishwa, tatizo lilikuwa ni Barbra hakutaka kuendelea kufanya kazi na Dewji aliyerudishwa Simba SC, huyu Dewji alimsema vibaya Barbra kwenye kituo kimoja cha radio, na yale yalikuwa ni majungu tu, nothing else.

Kama kweli Mo alikuwa anataka kuondoka Simba SC asingewaachia mapesa ya usajili akaenda zake Sudan, Mo yuko poa na Simba, tatizo kidogo lilikuwepo kwa Barbra na Dewji ambalo nalo limeshamalizwa.

Kama umetumwa kuja kuzima ule ujinga aliofanya Manara juzi pale Sheikh Amri Abeid Stadium - Arusha, mwambie huyo aliekutuma huku hakuna mapopoma wa sampuli yako.
 
Wewe ulikuwa wa kwanza kutuambia Barbra ana uhusiano na Mo, leo tena umehamia kwa Hersi, sijui kesho utaenda kwa nani, unamgeuza binti wa watu kitenesi cha wanaume...
Kuhusu Manara nadhani wasafi wamechambua vizuri tusikilize na upande wa pili tusimhukumu Mtu kwa matukio yake ya Nyuma.
 
1. CEO wa Simba SC anatuzuga tu wana Simba SC ila ukweli ni kwamba ana Mahusiano ya 'Kibaiolojia' na Rais ajaye wa Yanga SC Injinia Hersi Said na mara nyingi ndiyo humvujishia Siri zote za Simba SC ambazo ziligeuka kuwa Sumu kwa Mafanikio ya Simba SC kwa Msimu Mzima...
Hapa wivu tu wa CEO kubanduliwa na Rais ajaye..!! full stop. Maana yote hao juu yanazunguka hapo hapo..!!

Makolo mmefika pabaya..!! Yaani kuyakosa makombe mnataka, mnataka kila upande wawe na wapenzi wao kwa wao wasiingie kwa wengine..!! Mmeisha
 
Kama kawaida yake Mtutsi huyu anaendeleza chuki yake kwa "Mstaafu". Yaani bifu la msataafu na Kagame bado mnataka kulipa kisasi tu?. Usiwaaminishe watu kuwa nyie huwa hamsamehi!
Hana utusi wowote uyu ni jobless tu,ambae amefanikiwa kumiliki simu,huoni mada zake ni za vijiwe vya kahawa ambazo ni za kujifurahisha tu!! ni lini haliwai kuleta mada yeyote ya maana hapa zaidi ya uzushi na uzandiki? Uyu ni Musiba wa JF ni wendawazimu tu na majobles ambao wanaweza kumuamini tu!! Uyu tunamfurahia maana ni kama akina bambo,senga,mpoki wa jamii forums,kazi yake ni kutuburudisha tu na kutufanya tuingie JF kusoma comedy zake.

Sent from my TECNO CC7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom