Niliahidi kuja na 'Exclusives' Saba (7) Saa 3 hii sasa naweka Mambo yote hadharani...

Niliahidi kuja na 'Exclusives' Saba (7) Saa 3 hii sasa naweka Mambo yote hadharani...

Wewe ulikuwa wa kwanza kutuambia Barbra ana uhusiano na Mo, leo tena umehamia kwa Hersi, sijui kesho utaenda kwa nani...
Level yako ya kujua ninayoyajua kuhusu Masuala ( Issues ) Mtambuka ni mdogo sana hivyo acha Kunipotezea muda na kwa taarifa tena kwa Kujiamini niliyoyaandika hapa ni sahihi ( kweli ) 100% zote.
 
Mengine yoote ni utopolo ila hilo la bakhresa kupewa timu ikiwezekana itapendeza.
 
Nakubaliana na Gentamycine 100%, ishu ya Morrison ni mipango tu ya hao jamaa
Mkuu hapa GENTAMYCINE nimepiga Bomu la Mwisho Vitani na sasa huko Msimbazi ( SSC ) wanatafutana.

MImi ni mwana Simba SC ila sijazoea Unafiki na huwa ninanyoosha tu Maelezo yangu bila Uwoga wowote.

Hakuna Uwongo juu ya niliyoandika!!!
 
Tuleteeeeeni Bakhressa tuleteeeee Bakhressa....!!

Ila kiukweli Mimi sijawahi mkubali Mo sio kwamba hajaisaidia Simba Ila sio MTU sahihi wa kuifikisha Simba level za Al Ahly na wengine.... Mpira unahitaji uwekezaji endelevu na kujitoa sio wa kulambwa miguu.
"Siba guvu moya" by mo
 
Ajiajiri wapi mkuu wakati kwao ni Colombia kwenye biashara ya ngada & utekaji
Muulize sina Ajira ( Kazi ) nakula Kwake au Bata ninazokula ananipa chochote au hizi Safari mbalimbali za Tanzania za kutumia Barabara ( Uso wa Kima ) au Anga ( Bung'o ) au Hela za Kununua 'Bando' za 'Internet' ananipa Yeye?

Cc: Matola / change formula
 
Nilikua nakuheshimu Sana, Ila hii habari uliyoandika haihitaji akili kujua Kua ni riwaya tu Kama hekaya za abunuwasi.

6. Kutokana na huu utumbo wako ulioandika inaonyesha Haji Hana ugomvi na Mo, sasa mbona kila kukicha anamtukana mo?

7. Haji alivokua Simba alisema Simba itachukua ubingwa mara kumi mfululizo, so hakuna jipya kwenye hizi habari.

Sanasana umejishushia heshima yako kwa kutuletea huu utumbo.
 
CEO wa Simba SC anatuzuga tu wana Simba SC ila ukweli ni kwamba ana Mahusiano ya 'Kibaiolojia' na Rais ajaye wa Yanga SC Injinia Hersi Said
Hii imewezekanaje mkubwa wakati wanasimba malijari na wenye $$$ za kutosha &kutisha mpo?
 
Wewe ulikuwa wa kwanza kutuambia Barbra ana uhusiano na Mo, leo tena umehamia kwa Hersi, sijui kesho utaenda kwa nani, unamgeuza binti wa watu kitenesi cha wanaume.

Tatizo hauna kumbukumbu, ulishatuambia sababu ya ugomvi kati ya Manara na Barbra ilikuwa ni u-snitch wa Manara aliowafanyia Simba SC kwa GSM na Hersi kule Kigamboni, Avic Town, naona leo umekurupuka tena kuja na ngonjera zako za uongo.

Kuhusu ile Press Conference iliyoahirishwa, tatizo lilikuwa ni Barbra hakutaka kuendelea kufanya kazi na Dewji aliyerudishwa Simba SC, huyu Dewji alimsema vibaya Barbra kwenye kituo kimoja cha radio, na yale yalikuwa majungu tu, nothing else.

Kama kweli Mo alikuwa anataka kuondoka Simba SC asingewaachia mapesa ya usajili akaenda zake Sudan, Dewji yuko poa na Simba, tatizo kidogo lilikuwepo kwa Barbra na Dewji ambalo nalo limeshamalizwa.

Kama umetumwa kuja kuzima ule ujinga aliofanya Manara juzi pale Sheikh Amri Abeid Stadium mwambie aliekutuma huku hakuna mapopoma wa sampuli yako.
Hata Mimi nadahamu hivo,
Huyu bwana hizi ngonjera sijui katoa wapi.
 
Hii imewezekanaje mkubwa wakati wanasimba malijari na wenye $$$ za kutosha &kutisha mpo?
Nishukuru kwa hii Taarifa vinginevyo Simba SC yako ingeendelea 'Kuhujumiwa' na Watu mnaowaamini 100% wakati kumbe ndiyo Wanawaharibia.

Hapa nimeshawazibua Akili zenu wana Simba SC wote kuwa amkeni kwani mnahujumiwa na mliowapa Dhamana hivyo fanyeni upesi itisheni Kikao cha Dharula mlikabili hili kabla hata Ligi Kuu ya Msimu ujao haijaanza.

Nastahili tu Tuzo ya Heshima si Kejeli.
 
Back
Top Bottom