Nilichoamua kufanya baada ya kugundua sina uwezo wa kipesa wala akili za kiubunifu za kuikomboa jamii

Nilichoamua kufanya baada ya kugundua sina uwezo wa kipesa wala akili za kiubunifu za kuikomboa jamii

NIMEONA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2019
Posts
3,862
Reaction score
5,693
Naipenda sana jamii yangu

Nilitamani sana kuwa mwenye mchango katika jamii lakini bahati mbaya mpaka naingia utu uzima sikufanikiwa kutoka kimaisha na kuweza kuifanyia jambo la maana. Niliangalia shughuli niifanyayo, kwa mifano hai ya waliotangulia kuifanya kabla yangu, HAKUNA KUTOKA.

Nilijipima uwezo wangu wa kiakili na ubunifu, nako huko pia sijabarikiwa kiasi cha pekee. Ni uwezo wa kawaida tu kama walionao watu wengi, sina maajabu.

Baada ya kuona hivyo basi nikajikubali na nikaona nifanye jambo lolote hata dogo tu ili mradi awepo wa kufaidika nalo katika jamii. Kwa msaada wa imani yangu ya dini, nikapa la kufanya....kupanda miti ya matunda sehemu ya wazi itakayofikika na yeyote yule.

Ilinigharimu kokwa za embe kumi tu kuweza kufanikisha ukuzaji wa miembe mitatu katika eneo la taasisi fulani hivi ya umma ninayofanyia kazi. Mwaka jana zimeanza kuzaa na vitoto vimeanza kupata chimbo jingine la kuzamia, furaha ilioje! Ahsante Mungu.

Nimehama huko na sasa nipo sehemu nyingine na dhamira yangu ni ileile na ninahusudu sana miembe sababu haina usumbufu sana na inafaidisha wengi zaidi na inadumu sana. Niliwahi kuwapandia mipapai lakini walikula kwa muda mfupi kabla ya haijamaliza maisha. Eneo lina changamoto ya ardhi yenye mawe na chumvi na uoteshaji ni mgumu lakini nitajitahidi tu.

*jamii yangu = pale ninapoishi na kufanyia shughuli zangu.
 
woman-holding-a-huge-cup-of-coffee-illustration-id165517310-6.jpg
 
Iwe chai or iwe real, hili ni jambo zuri sana la kupongezwa. Actually kila mtu angefanya nyumbani kwake na mtaa anaoishi in 20 yrs tutakua nchi yenye afya bora sana.

Tunakula matunda at keast every week, ukinaliza ukachukua mbegu ukakausha, ukaipanda hata kwenye chupa ya maji iliokatwa nusu na ikaota tayar ni mche ambao kipindi cha masika unawza kuuhamishia kwenye shimo na ukajua in 3 yrs watu wakala matunda matam bila gharama.

Hongera mkuu
 
No.hiyo ni akili kubwa ililoo jaa MAALIFA, MAONI na HURUMA kwa jamii inayokuzunguka. Jambo jema na ni mfano kwa wengine. Kupanda miti, miti inafaida kuu tatu.

KIVULI.
MATUNDA
TIBA.

ONGERA SANA.mimi ni muumini katika HILO.

JPEG_20220819_075750_1342888947.jpg
JPEG_20220819_075832_1158286789.jpg
 
Naipenda sana jamii yangu

Nilitamani sana kuwa mwenye mchango katika jamii lakini bahati mbaya mpaka naingia utu uzima sikufanikiwa kutoka kimaisha na kuweza kuifanyia jambo la maana. Niliangalia shughuli niifanyayo, kwa mifano hai ya waliotangulia kuifanya kabla yangu, HAKUNA KUTOKA.

Nilijipima uwezo wangu wa kiakili na ubunifu, nako huko pia sijabarikiwa kiasi cha pekee. Ni uwezo wa kawaida tu kama walionao watu wengi, sina maajabu.

Baada ya kuona hivyo basi nikajikubali na nikaona nifanye jambo lolote hata dogo tu ili mradi awepo wa kufaidika nalo katika jamii. Kwa msaada wa imani yangu ya dini, nikapa la kufanya....kupanda miti ya matunda sehemu ya wazi itakayofikika na yeyote yule.

Ilinigharimu kokwa za embe kumi tu kuweza kufanikisha ukuzaji wa miembe mitatu katika eneo la taasisi fulani hivi ya umma ninayofanyia kazi. Mwaka jana zimeanza kuzaa na vitoto vimeanza kupata chimbo jingine la kuzamia, furaha ilioje! Ahsante Mungu.

Nimehama huko na sasa nipo sehemu nyingine na dhamira yangu ni ileile na ninahusudu sana miembe sababu haina usumbufu sana na inafaidisha wengi zaidi na inadumu sana. Niliwahi kuwapandia mipapai lakini walikula kwa muda mfupi kabla ya haijamaliza maisha. Eneo lina changamoto ya ardhi yenye mawe na chumvi na uoteshaji ni mgumu lakini nitajitahidi tu.

*jamii yangu = pale ninapoishi na kufanyia shughuli zangu.
Hongera chief
 
Back
Top Bottom