Nilichobaini kwa watu wa Njombe

Nilichobaini kwa watu wa Njombe

Wengi wanafanya biashara Soko la Kariakoo na wanaishi Ilala, hawapandi gari, wanatoka Ilala kwa mguu na kwenda Kariakoo na kurudi, kwa wafanyakazi wa wa kike huruhusiwi kusuka ni mwendo wa kunyoa tu, na wakiume ni kunyoa kipara, yaani ni wabahili (wachumi).
 
Mimi siyo mrefu wala mfupi, lakini naweza nikawa mrefu kwa watu wengi wa Njombe!

Kwa siku chache nilizokaa Njombe, nilibaini ukweli kuwa ukubwa wa mwili hauamui "ukubwa" wa mtu. Anaweza akawa na umbo dogo sana lakini akawa ni mtu "mkubwa" sana.

Watu wengi wa Njombe wana maumbo madogo, unaweza kusema ni watu wafupi. Lakini akili zao na utu wao si "mfupi".

Kwa niliyoyashuhudia, nilihitimisha kama ifuatavyo kuhusu watu wa Njombe:

1. Ni watu wanaojikubali! Wamerkdhikia na maumbo yao ya kuzaliwa. Hawahangaiki kuwa kama "wengine" kimwonekano.

2. Ni watu wastaarabu sana, na wakarimu pia. Hata ukimwuliza mtu njia, anakuelekeza kwa upendo utafikiri unamlipa.

3. Ni wajasiri sana. Si wanaume wala wanawake. Wanajua kusimamia kile wanachokiamini.

Nakumbuka, tukiwa stendi kuu ya mabasi tukiwa tunataka kwenda Ludewa, wamama fulani waligoma kulipa nauli kabla gari halijaanza safari. Walikuja kulipa baada ya gari kutoka stendi. Si kama wamama wa mikoa fulani ambao wakikoromewa tu kidogo na konda "wanahanya" utafikiri huo usafiri wamepewa msaada.

Hilo basi likiwa njiani kuelekea Ludewa, lilikwama na hivyo kondakta na dereva wakawaomba abiria msaada wa kusukumwa. Mbona waligoma kufanya hivyo!. Hata mimi ilinibidi "nijikaushe" japo nilitamani kuwasaidia.

Walitoa sababu mbili za kukataa kwao:
A). Wamelipa nauli hivyo ni jukumu la watoa huduma kutafuta namna ya kuwafikisha wanakoenda kama tiketi inavyoonesha

B). Pale kuna vijana wanaoweza kuifanya hiyo kazi hivyo kondakta awalipe vijana waliopo eneo hilo ili waitie hiyo huduma.

Walisimama na huo msimamo mpaka wahudumu wa basi walipojiongeza na hatimaye basi kukwamuliwa.

Lakini hao watu si wakatili. Wana upendo mno. Siku iyo hiyo, wakati tukiendelea na safari, mmoja wa abiria aliugua njiani. Abiria walionesha ushirikiano wa hali ya juu katika kumpatia huduma ya kwanza hadi alipofikishwa hospitalini kwa basi ilo hilo.

4. Ni wachapa kazi sana. Kule kuna wenyeji wenye mashamba makubwa ya parachichi na miti ya mbao na nguzo. Inaonekana kuna mabilionea japo hawapigi kelele.

5. Ni watunzaji wa mazingira. Hata stendi yao ya mabasi, ukiiangalia, inavutia sana. Ina ukijani mzuri ambao umetokana na kupata matunzo stahiki.

Kwa kifupi, watu wa Njombe ni wajasiri, wakarimu, wastaarabu, wanajikubali, wachapa kazi na matajiri wasio na makelele.

Aliyewahi kuwa Mbunge maarufu kipindi cha utawala wa Kikwete, marehemu Deo Filikonjombe alikuwa Mbunge wa Ludewa. Ni zao la Njombe.

Sishangai kwa nini alikuwa jasiri! Ni asili ya watu wa Njombe.

Hongereni watu wa Njombe[emoji122][emoji122][emoji122]

Keep it up!

Tanzania nzima hakuna watu wenye sifa zote hizo labda kama umeamua kuwa chawa wa watu wa njombe.

Ni sehemu gani watu wanahangaika na maumbo yao ya kuzaliwa iwe urefu, ufupi, uwebamba au unene. Kama ni wanawake kutafuta uweupe wa mchina, wanawake wa njombe nao ni mafundi.

Wangekua majasiri, wakarimu, wasitarabu na kujiamini mkoa huo usingeongoza kwa takwimu za HIV, wasingekuwa wanaburuzwa CCM na mkoa ungekua na maendeleo lakini badala yake wamejaa imani potofu za kishirikina.

Uchapakazi unaakisi maisha halisi ya watu, lakini uchapakazi wa watu wa njombe ni kizamani usiozingatia tija, wanawake kwa wanaume kutwa wako shamba lakini mwisho wa siku masilahi kisoda kama ilivyo sehemu zingine za nchi..

Njombe ukimtoa yule jamaa anayelima parachichi nyingi Nemes, mexison na mwenye hillside waliobaki wana hela za ugali na niliowataja nao sio mabillionea. Njombe hakuna mabillionea.

Ni kweli njombe watu wanajituma sana kazi za kilimo lakini efficiency ni ndogo sana kwa sababu wanafanya kilimo cha kizamani .

Namalizia kwa kusema watu wa njombe hawana hizo sifa zote ulizoandika,ni watanzania kama watanzia wengine waliojaa ujinga na umaskini mwing,mtu maskini na mjinga hawezikuwa mstaarabu,mjasiri wala kujiamini.
 
Tanzania nzima hakuna watu wenye sifa zote hizo labda kama umeamua kuwa chawa wa watu wa njombe.

Ni sehemu gani watu wanahangaika na maumbo yao ya kuzaliwa iwe urefu, ufupi, uwebamba au unene. Kama ni wanawake kutafuta uweupe wa mchina, wanawake wa njombe nao ni mafundi.

Wangekua majasiri, wakarimu, wasitarabu na kujiamini mkoa huo usingeongoza kwa takwimu za HIV, wasingekuwa wanaburuzwa CCM na mkoa ungekua na maendeleo lakini badala yake wamejaa imani potofu za kishirikina.

Uchapakazi unaakisi maisha halisi ya watu, lakini uchapakazi wa watu wa njombe ni kizamani usiozingatia tija, wanawake kwa wanaume kutwa wako shamba lakini mwisho wa siku masilahi kisoda kama ilivyo sehemu zingine za nchi..

Njombe ukimtoa yule jamaa anayelima parachichi nyingi Nemes, mexison na mwenye hillside waliobaki wana hela za ugali na niliowataja nao sio mabillionea. Njombe hakuna mabillionea.

Ni kweli njombe watu wanajituma sana kazi za kilimo lakini efficiency ni ndogo sana kwa sababu wanafanya kilimo cha kizamani .

Namalizia kwa kusema watu wa njombe hawana hizo sifa zote ulizoandika,ni watanzania kama watanzia wengine waliojaa ujinga na umaskini mwing,mtu maskini na mjinga hawezikuwa mstaarabu,mjasiri wala kujiamini.


Kama huijui njombe Kaa kimya
IMG-20240402-WA0057.jpg
 
Njombe ni moja ya mkoa ambao imejipambanua zaidi na utazidi kukua zaidi kutokana na nature ya watu wake ni wampambanaji na wanapenda maendeleo na kupitia miji yao miwili makambako na njombe wameteua mji wa makambako uwe wa viwanda na biashara hii ni kutokana na jiografia pia na utajiri wa rasilimali walizo nazo kama madini na mazao ya kibiashara nk ko utarajie kuona mkoa wa njombe utazidi kukua mno ndo kwanza wawekezaji wanazidi kwenda kuwekezana plan yao ni kukuza mji wa makambako ili wa host kibiashara kwa mikoa ya iringa na ruvuma na nchi jilan kwa kujenga bandari kavu, industrial park,masoko ya mazao nk makambako na kazi imeanza
1704432526050.jpg
Pic+1~2.jpg
FB_IMG_16767646601212987.jpg
1711339999667.jpg
FmfkrrFWQAE9n_s~2.jpg
1702914137702.jpg
IMG-20231124-WA0123.jpg
1708269600701.jpg
1700285478467.jpg
1696737622411.jpg
1711339180702-jpg.2965893
 

Attachments

  • 1711339180702.jpg
    1711339180702.jpg
    143.7 KB · Views: 51
Hilo basi likiwa njiani kuelekea Ludewa, lilikwama na hivyo kondakta na dereva wakawaomba abiria msaada wa kusukumwa. Mbona waligoma kufanya hivyo!

2. Ni watu wastaarabu sana, na wakarimu pia. Hata ukimwuliza mtu njia, anakuelekeza kwa upendo utafikiri unamlipa.
Hudhani unakinzana na point zako mwenyewe hapo kwenye ukarimu?
 
Nimeishi na kupita maeneo kadhaa huko njombe wilaya ya wanging'ombe kuelekea huko Ludewa Kuna mlima wanaita gangitololi asee ni balaa utatelemkia sehemu wanaita mkiu Kona ya kwenda lugalawa, nilipata na mke huko.
 
Back
Top Bottom