Nilichokikuta ukweni imebidi nimsamehe mume wangu

Nilichokikuta ukweni imebidi nimsamehe mume wangu

Siku zote nimekua nikilalamika humu mme/mwenzangu kutohudumia nyumbani na kuhamishia nguvu kwao ila nilichokiona mpaka nimemuonea huruma.

Iko hivi mimi na mwenzangu tulikua tunaishi pamoja tangu mwaka Jana mwaka huu wazazi wakaamua wakamilishe taratibu zote ikabaki ndoa tu sasa katika maisha na mwenzangu wajibu wake ndani umekua mdogo maendeleo hakuna hafanyi.

Nimeenda kwao likizo nimechoka mwili na roho nimepoteza ndoto za kua na maisha mazuri kabisa jamaa ukoo mzima iwe shangazi, mjomba,Dada zake hata walioolewa yeye ndio anawahudumia.

Nimemuonea huruma maana sio ombi nilazima familia ile dada zake wavae aanunulie nguo kila siku ikifika mwisho wa mwezi hela zote zinaenda kwao ikifika tarehe 10 mshahara umeisha nilikua nachukia namuona hana akili za maendeleo lakini kwa hali nilivyoiona hata yeye hana jinsi.

Jamani nishauri nifanyeje tue na maendeleo na sisi? Sababu kipato changu ni lak 3 binafsi mwenzangu yeye anapokea mil 1.4_5 lakini majukumu ni mengi kwao hawezi kufanya chochote.

Nifanyeje jamani?
Afumbe macho kwa mwezi mmoja tu asipahudumie huko kwao then 1.4m akiongeza na 300k yako mfanye kuongeza nguvu ya pamoja

1.4M akiitunza ww unatumia 300k yako kuhudumia chakula na mahitaji yako na yake kwa mwezi huo pamoja na chakula kama mko wawili tu naamini itatosha hivyo hapo mnabaki na akiba ya 1.4M

Mwezi unaofuatia anatoa 1M anaongezea pale unanunua bodaboda mmnapatia kijana muaminifu akutetee 10k per day kwa mkataba wa mwaka mmoja

Utabakiwa na 300k yako na yeye 400k itakuwepo, mwezi huo mnatuma nyumbani kwao 200k na 200k kwenu 300k inabaki kuwahudumia tena ninyi ukiongeza na 10k za kila siku hamtashindwa kuishi

Mshahara wa mwezi wa tatu ukija unakua ni wenu sasa ile pikipiki itatosha kuhudumia kwao huko maana 10k per day kwa mwezi ni 300k mkuu

Maisha inasonga mdogo mdogo tu lakini
 
Nimerudia tena kukomenti baada ya kushauriana na wadau huku mtaani:

Kwanza kabisa hii itafaa endapo mumeo akiwa anapokea ushauri, kama hapokei ushauri ni bomu tayari

1. Mumeo aanze kutoa misaada vile vile ila apunguze kidogo kidogo, mfano alikuwa anatoa 200000 kwa kila mtu basi aanze kutoa 100000 ili isilete chuki kwako kuwa umemzuia kaka yao kutoa kwao, kwa wazazi anaweza endelea kutoa vile vile dau la kawaida ila lisizidi laki mbili kwa mwezi

2. Baada ya miezi minne hivi aache kabisa kutoa kwa ndugu zake isipokuwa wazazi wake aendelee vile vile

3. Hao ndugu anaweza kuwasaidia kutafuta ajira ama biashara ndogo ndogo (akijaaliwa mbeleni)

4. Wewe na yeye mkae pange maendeleo ya familia, ila msisahau wazazi wanazeeka na wanahitaji sapoti yenu, ila ndugu achaneni nao taratiiiibu mpaka watazoea tu na hautapata lawama kuwa umembadili kaka yao

Kila la heri mkuu
 
Happy ndoa kwako ni kama zigo la misumari inabidi uachane nayo ufanye mambo mengine..... Ndoa haikuachi upumue hata sekunde sio ndoa hiyo.
 
Unachotakiwa kujua ni kwamba hata kama utakua unawapa 1.5 yote kila mwezi, ndugu wako sijui 8 huwezi maliza matatizo yao! Ila wao watakua maskini na wewe utakua maskini.

weka budget limit then nyingine aishi maisha yenu.
Kabla ya kuanza kuwahudumia walikua wanaishi vipi? Au yeye alikuta wamekufa ndo akawafufua?
 
Ukiendelea naye jiandae kuchukiwa na UKOO mzima.
 
Back
Top Bottom