Nilichokikuta ukweni imebidi nimsamehe mume wangu

Nilichokikuta ukweni imebidi nimsamehe mume wangu

Kataeni baadhi ya majukumu saidieni yale yasiyozuilika kwa ndugu wa karibu wenye umri chini ya miaka 18. Vinginevyo mtu awe shule ahitaji support mara moja moja.

Nilichokipata miaka 4 baada yakuanza kazi hakifai kusimulia. Concentrate with your life regrets are ahead.
 
Kama hukumpenda na uliangalia mshahara wake,angalia njia ya kutokea. Lkn kama unampenda tulia nae,ndio maisha ipo siku atakua sawa. Kwa sasa mwache awasikilize wazazi ndio wamemfikisha hapo ulipomkuta.
 
Mwanahabari wa kituo cha runinga cha the citizen nchini kenya kufanyiwa uchunguzi wa akili.
 
Mbinu peekee hapo ni yy mumeo kutambua kwamba hata awasaidie vp ndugu zake shida hazito isha.

Tayar anafamilia asipo kua makini uzee utamkuta hajafanya chochotee.

Chamuhimu awasaidie nduguze chochote kiwe kinawaingizia kipato kama vile kihosk, au kijigenge, then aendelee n maisha Yake.

Ukisaidia kupita uwezo wako ni Dhambi.
 
hili suala linafanya watu wengi wawe maskini kwa kweli au kutokuwa maendeleo mazuri ila kiufupi naweza sema unapoishi na mwenza wako macho yenu yote ni juu ya familia yenu tu na si vinginevyo ili kupata maendeleo kwan hao dada zake,wajomba zake c watu wazima kabisa sasa kwanini wamtegemee zaidi mmeo huyo wewe cha kufanya pesa nyingi itumike katika kuleta maendeleo kwenye familia yenu usitazame zaidi eti ndugu watasema nini sometime lazima uwe na moyo mgumu katika kuleta maendeleo....! sijamaanisha usisaidie ndugu lakini kumbuka familia yako kwanza kuna misaada mingine tunayotoa kwa ndugu zetu siyo ya lazima sana jamani
 
Maisha yako hivi ukiwa unamsaidia mtu siku zote usiwe jibu LA matatizo yake Bali onyesha njia ya kutoka katika tatizo hapa namaanisha hivi kama kwenu wamekosa chakula usipende kununua chakula maana baada ya mda kitaisha.

Bali we nunua shamba na majembe wawe wanjilimia na kupata chakula maana shamba halitoisha. Haya mambo hayaitaji kusumbua sana akili.
 
Siku akistaafu, na huku hajajenga wala kiwanja hana, ndo akili itafunguka........ Na hapo mtakuwa mmechelewa sana. Hao hao ndugu anaowasapot ndo watakuwa wa kwanza kumcheka... Akili kichwani
 
Siku zote nimekua nikilalamika humu mme/mwenzangu kutohudumia nyumbani na kuhamishia nguvu kwao ila nilichokiona mpaka nimemuonea huruma

Iko hivi mi na mwenzangu tulikua tunaishi pamoja tangu mwaka Jana mwaka huu wazazi wakaamua wakamilishe taratibu zote ikabaki ndoa tu sasa katika maisha na mwenzangu wajibu wake ndani umekua mdogo maendeleo hakuna hafanyi

Nimeenda kwao likizo nimechoka mwili na roho nimepoteza ndoto za kua na maisha mazuri kabisa jamaa ukoo mzima iwe shangazi, mjomba,Dada zake hata walioolewa yeye ndio anawahudumia

Nimemuonea huruma maana sio ombi nilazima familia ile dada zake wavae aanunulie nguo kila siku ikifika mwisho wa mwezi hela zote zinaenda kwao ikifika tarehe 10 mshahara umeisha nilikua nachukia namuona hana akili za maendeleo lakini kwa hali nilivyoiona hata yeye hana jinsi

Jamani nishauri nifanyeje tue na maendeleo na sisi? sababu kipato changu ni lak 3 binafsi mwenzangu yeye anapokea mil 1.4_5 lakini majukumu ni mengi kwao hawezi kufanya chochote

Nifanyeje jamani?

Maishani ukiwaendekeza sana ndugu utateketea kwa umaskini wa kiwango cha chupi ikichanika upeleke kwa fundi ikashonwe...


Misaada lazima iwe na mipaka
 
bwana niokoeeeeeeee, ndugu walitutenga sana wana hali nzuri sana, wazee wangu walihangaika sana na sisi Mama alikua anapiga kelele kila siku mtegemea cha ndugu hufa masikini, wakatuzaa 3 tu, Mungu katujalia uzima sijui kama kuna ndugu atakuja kulamba hata 50 yangu
 
Maisha yako hivi ukiwa unamsaidia mtu siku zote usiwe jibu LA matatizo yake Bali onyesha njia ya kutoka katika tatizo hapa namaanisha hivi kama kwenu wamekosa chakula usipende kununua chakula maana baada ya mda kitaisha.

Bali we nunua shamba na majembe wawe wanjilimia na kupata chakula maana shamba halitoisha. Haya mambo hayaitaji kusumbua sana akili.
Mashamba yapo majembe yapo ikifika masika anatoa hela wanalimiwa wenyewe tangu mtoto wao apate kazi wanaweka wafanyakazi tu kuwalimia
 
Mbinu peekee hapo ni yy mumeo kutambua kwamba hata awasaidie vp ndugu zake shida hazito isha.

Tayar anafamilia asipo kua makini uzee utamkuta hajafanya chochotee.

Chamuhimu awasaidie nduguze chochote kiwe kinawaingizia kipato kama vile kihosk, au kijigenge, then aendelee n maisha Yake.

Ukisaidia kupita uwezo wako ni Dhambi.
Kuna kaka zake 2 wanakazi mmoja ni mwalimu mwingine ni hua anafanya biashara ya kusafirisha ng'ombe ila wanafanya maisha yao hawahangaiki na ndugu ila wakwangu na hisi anamoyo mzuri sana
 
Maisha sio km nilivyotarajia, nitawafundisha wanangu kupambana kila mmoja, yani km ni kusaidiwa itokee tuu!! My sons and daughter should work hard, so help God.

Mtoto wa kiume akishaoa sio wako tenaee!
 
Kusaidia watoto wa ndugu ambao wazazi wao wako hai huwa sitoi kipaumbele katu,kufanya familia yangu iwe ktk daraja la pili ktk maendeleo na kila kitu ni KOSA ambalo hata mbingu hazitanipokea kama zilivopanga.
 
Siku zote nimekua nikilalamika humu mme/mwenzangu kutohudumia nyumbani na kuhamishia nguvu kwao ila nilichokiona mpaka nimemuonea huruma

Iko hivi mi na mwenzangu tulikua tunaishi pamoja tangu mwaka Jana mwaka huu wazazi wakaamua wakamilishe taratibu zote ikabaki ndoa tu sasa katika maisha na mwenzangu wajibu wake ndani umekua mdogo maendeleo hakuna hafanyi

Nimeenda kwao likizo nimechoka mwili na roho nimepoteza ndoto za kua na maisha mazuri kabisa jamaa ukoo mzima iwe shangazi, mjomba,Dada zake hata walioolewa yeye ndio anawahudumia

Nimemuonea huruma maana sio ombi nilazima familia ile dada zake wavae aanunulie nguo kila siku ikifika mwisho wa mwezi hela zote zinaenda kwao ikifika tarehe 10 mshahara umeisha nilikua nachukia namuona hana akili za maendeleo lakini kwa hali nilivyoiona hata yeye hana jinsi

Jamani nishauri nifanyeje tue na maendeleo na sisi? sababu kipato changu ni lak 3 binafsi mwenzangu yeye anapokea mil 1.4_5 lakini majukumu ni mengi kwao hawezi kufanya chochote

Nifanyeje jamani?
Jamaa alisomeshwa na ukoo au? Hebu muhoji kuanzia hapo. Maana kuna wengine wanakuwa victimized kwa sababu tu walichangiwa na ukoo hivyo akifanikiwa inabidi arudishe fadhila zote kwenye ukoo. Hebu mdadisi kuanzia hapo kwanza. Ukipata majibu njoo tena tuangalie the way forward.
 
Mmeo yuko sawa tu,

hata mimi mke wangu hawezi kunipangia namna ya kutumia pesa yangu,

Ukiona mtu anatoa sana misaada ujue alisaidiwa.
 
Back
Top Bottom