Nilichokiona leo Dodoma hakina afya kwa mustakabali mzima wa ustawi Taifa letu, tujirekebishe kwa maslahi mapana ya Taifa

Anaishi ulimwengu wake wa pekee huyu nutcase.
Inawezekana hata ni wale wanaoamini dunia sio duara.
Yaani wewe kila upuuzi kuanzia conspiracy theories zako za kupumbavu juu ya Corona unawasingizia Wazungu, trash.
 
Be more diagnostic and exploratory mkuu.Mimi siangalii tukio moja,naangalia mtiririko wa matukio na kuanisha na taarifa mbali mbali .
Mzee hebu yataje hayo matukio.
1. Kwenye CC wanawake wapo watatu tu kati ya wajumbe 26+
2. Kwenye NEC wapo wajumbe 160+ waliochaguliwa ni 2 tu. Je, kwenye hao 160+ wanawake wapo wangapi!?
3. Katika kujieleza namba 2,3 na 5 walijikanyaga na kupoteza muda kutoa sifa ambazo hazina maana.
4. Dada namba 4 alieleza kwa kifupi na kueleweka. Dada namba 6 alieleza uzoefu wake alipokuwa akisoma Urus.

Sasa wewe ungeletewa hao ungemchagua nani!? Maana mwingine anajisifu kuwa amezaliwa maeneo makamu wa rais aliko zaliwa.
 
Ndugai: Tulikubaliana 50 - 50 lakini Wanawake wamepata 100

Wanaume wote wakapiga makofi pwa....pwa....pwa...!

Bawacha oyeeee!
Na Sheria kama ile ya kukonyezana naiona iko mbioni kutekelezwa Kama akina mama watu wazima hawatatumia busara ,
.
 
hakuna ubaya wowote,ingekuwa kubeba zege ungelalamika?
 
Slaa hakuwa hardcore?
 
Nimetembelea tovuti ya BBC swahili nikaona wameandika SSH ameshinda kwa asilimia 100 uwenyekiti. Nikajiuliza kwa karne hii yenye wasomi wengi wenye maarifa mengi kuna ushindi wa hizo asilimia dunia ya sasa unaweza kupatikani.

Nikakumbuka haya maajabu wa Africa ndio wanayaweza tuu hakuna wengine
 
Mkuu nikuambie nini,Mama Samia kusimikwa kuwa Rais amewasha moto,kama kuna mwanaume ambaye halioni hili,ni kipofu.Wanaume tujiandae yajayo yanafurahisha.

And then nashangaa,kuna mijianaume sijui mijianaume gani,inapigia makofi hatari!Ni ajabu sana.
Hatari gani jamani
 
Ushindi wa 100% ni ushindi wa aibu, watu watatilia shaka uthabiti wa mchakato uliotumika.

Kwanza suala zima la mtu mmoja kugombea uenyekiti linaonesha uchaguzi huu ni magumashi tu.
 
Mambo haya hayaeleweki kwa wengi.

Bahati mbaya sana tunafanya mambo lakini hatujui athari zake.

Labda ni kwa sababu ya mambo tulioingia au tuliyomo hatuwezi tena kujifunza.

Anaeamini au kufikiri kwamba mwanamke au wanawake hawawezi uongozi, siasa au kufanya vema, anafikiri kimakosa au imani yake ni potofu.

Mimi sitaki kujadili hilo kwa sababu ushahidi upo mwingi katika historia ya mtu popote duniani.

Muhimu si nani anaweza kufanya vema kati ya mwanaume na mwanamke, bali MAJUKUMU ya mwanaume na mwanamke ndio muhimu.

Hawa wawili: mwanamke na mwanaume, kila mmoja ana majukumu yake.

Asili imemweka mwanaume afanye majukumu haya na mwanamke afanye majukumu haya. Kinachotokea wakati wetu hiyo hali inaharibiwa.

Hapa kwenye majukumu ndipo kosa lilipo. Kimsingi ni kwamba sheria ya maumbile imeingiliwa.

Sijui kama ni suala la utafiti au namna gani.

Madhara ya hili jambo ni makubwa na hatari kwa ustawi.

Hapa wanawake wa kiafrika si wa kulaumiwa kwa sababu wanaume wa kiafrika wameshindwa kutimiza wajibu wao.

Sheria ya maumbile imemweka mwanaume kama ndiye mtengenezaji wa MFUMO kati ya majukumu yake mengi. Hili wanaume wa kiafrika hawatekelezi.

Kwa makosa haya ya kuingilia sheria ya maumbile inayoweka majukumu ya mwanamke na mwanaume, angalia familia zetu zilivyo, angalia jamii ilivyo!

Kwanini familia zimeharibika? Kwanini jamii imeharibika? Katika mazingira haya ni kweli kwamba kuna uchumi au maendeleo?

Mtafiti mmoja huko Ufaransa alifanya utafiti kwanini Marekani ni taifa kubwa duniani. Katika utafiti wake alihitimisha kuwa Marekani ni taifa kubwa kwa sababu lina "MAADILI."

Sheria ya maumbile ambayo kwayo tunapata majukumu ya mwanaume na mwanamke ni wakati huo huo maadili.

Kuingilia sheria ya maumbile ni kuingilia maadili.

Bila maadili hakuna malezi; wala ustawi wa watu.
 
Hadi sasa najaribu kuelewa huu uzi una ujumbe gani kwa sababu mleta mada akuandika kwa kudhani kila mtu katazama/fuatilia mkutano wa CCM.

1. Wanawake hawapaswi kuwa viongozi?

2. Kuna ajenda mpya imepitishwa na CCM kuweka mgawanyo sawa wa madaraka kati ya wanaume na wanawake?

3. Kuna maneno yasiyofaa yaliyotamkwa na wanawake kwenye vikao vya CCM?
 
Mwanamke ni mwanamke, hawezi sumbua mwanaume. Ndio iko hivyo ondo shaka
 
Kwahiyo tukubaliane kuwa JPM alitumika na mabeberu wa NWO ili kuteua wanawake kuwa second in command kwenye mhimili wa Bunge na Serikali kuu?

Ama nani aliowa teua hapo kma sio Mwenyekiti wa CCM?
 
Kwa hiyo wanaume we are like..
 
Mheshimiwa, umepigwa chini au! Hiyo minyukano ndani ya CCM inatuhusu Watanzania wote, hata sisi tusio na vyama, au ni nyinyi wenyewe tu makada wa CCM?

Pole sana kama umeangukia pua.
Huyu ni kati ya hawa wawili kama sio Polepole ni Bashiru
 
Acha kuwaonea donge wamamangwa weweee. Angelia mamio usingefurahi? Acha kukumbatia mfume dume. by the way hao wanaume halo awali maajab gani wamefanya?!!!
 
Mheshimiwa, umepigwa chini au! Hiyo minyukano ndani ya CCM inatuhusu Watanzania wote, hata sisi tusio na vyama, au ni nyinyi wenyewe tu makada wa CCM?

Pole sana kama umeangukia pua.
Kila mtanzania anaathirika/ataathirika chanya au hasi kwa matendo yoyote mabaya au mazuri ya CCM. kwa maana ya chama tawala...vivyo hivyo ingekuwa chama tawala Ni TADEA.... Iwe kwa mambo yanayoitwa ya ndani ya chama au nje ya chama. Hakuna namna ya kukwepa hilo.

Ni sawa na mtu akikwambia siasa hazimsaidii wala kumdhuru kwa namna yoyote ile.... Si sawa hata kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…