Nilidhani ukiingia mbuga ya wanyama Unaona wanyama kirahisi kumbe napo tabu tupu

Nilidhani ukiingia mbuga ya wanyama Unaona wanyama kirahisi kumbe napo tabu tupu

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Hivi majuzi nilibahatika kufika Ngorongoro National Park eneo la Crater; nikitarajia kuona wanyama wakubwa kwa ufasaha kama inavyosimuliwa kwenye movie mbalimbali za wanyama.

Niseme kwa dhati kabisa baada ya kuzungushwa muda mrefu niliambulia kuona nyati, kiboko, digidigi, punda na ndege flamingo. Lakini Tembo nilioneshwa miguu tu walipokanyaga sikuwaona, Simba nao nilioneshwa kwa mbaali sana tena wawili tu wadogo kama mbwa, nikaoneshwa kichaka cha Faru wanamopenda kukaa lakini sikuona!

Kiufupi roho yangu haikuridhika kabisa bora ningeangalia movie tu!

Matarajio yangu nilidhani nitaona Faru, chui, twiga, Tembo na wanyama wengine kirahisi kumbe sio kazi rahisi kama nilivyotarajia.

Nifanyeje Next time ili niwaone wanyama kiufasaha kama tusimiliwavyo?
 
Serikali sijui imefeli wapi kwa sasa zamani kwenye baadhi ya mikoa kulikuwa na zoo mfano Mwanza ple pasiasi ulikuwa ukienda unaona wanyama takribani wote wakiwa wamefungiwa kwenye mabanda, pale Tabora kulikuwa na zoo napo ulikuwa hivyo hivyo siku za sikuu au week end wazazi walitembelea na familia zao kwenda jionea wanyama na ndege wa aina mbali mbali

Kuna kipindi nilienda Dar zoo nikiwa na picha ile ile ya zile zoo nilizokuwa nikiziona udogoni mwangu ila nilipofika uko hakuna lolote niliona simba tu

Wito wangu wizara husika ebu fanyeni kitu watoto wapate kukifunza kwa kuona siyo lazima sote twende bugani ona mdau analalamika hapa kafika mbugani hakuna kitu

Tatizo waziri mwenye dhamana kageuka mwandishi wa story za Instagram sijui nje ya box baada kudeal na vitu vya msingi vilivyofanya tumjue yupo kutuadithia hadithia tu akitaka tuamini kakulia kwenye shida yeye ni mpambanaji tunasubilia ajichanganye tufukue makaburi
 
Ndugu yangu Dmkali, katika mji unakoishi ni rahisi wewe kupatikana? N wanyama ni hivyo hivyo.

Kule porini ni maskani yao lakini pia huwa na maficho yao humo humo.

Hivyo sio rahisi sana kuwaona mara tu uwapo ndani ya mbuga.

Pia wanyama huzunguka huku na kule kutafuta chakula na maji. Tena huko Crater ni rahisi zaidi kuwaona wanyama kwa kuwa wako ndani ya eneo ambalo hawahami kwenda mbali sana.

Mbuga zingine waweza kuzunguka siku nzima na usimuone Chui. Hata hivyo nikupongeze kwa kuendeleza utalii wa ndani.

Isiwe mara ya mwisho, fanya safari nyingi zaidi katika mbuga za wanyama ili ufaidi utukufu wa Mungu katika uumbaji.
 
mbuga gani?
Kila hifadhi inasifa zake na wanyama ambao waweza kuwaona kirahisi hivyo ni vyema ukafanya tafiti kabla ya kuamua ni hifadhi gani unataka kwenda kutembelea.

Kwa mfano kama unataka kuona jua likizama na makundi makubwa ya nyumbu nenda Serengeti na kama unataka kuona Tembo kwa wingi na wakubwa zaidi basi usisite kwenda Tarangire.
 
Ndugu yangu Dmkali, katika mji unakoishi ni rahisi wewe kupatikana? N wanyama ni hivyo hivyo. Kule porini ni maskani yao lakini pia huwa na maficho yao humo humo. Hivyo sio rahisi sana kuwaona mara tu uwapo ndani ya mbuga. Pia wanyama huzunguka huku na kule kutafuta chakula na maji. Tena huko Crater ni rahisi zaidi kuwaona wanyama kwa kuwa wako ndani ya eneo ambalo hawahami kwenda mbali sana. Mbuga zingine waweza kuzunguka siku nzima na usimuone Chui. Hata hivyo nikupongeze kwa kuendeleza utalii wa ndani. Isiwe mara ya mwisho, fanya safari nyingi zaidi katika mbuga za wanyama ili ufaidi utukufu wa Mungu katika uumbaji.
kwahiyo ili niwaone niende Mara ngapi? maana hata ile shughuli ya kutelemsha ule mteremko wa creta sina hamu nao tena; Mtelemko ule ni mkali na wa hatari sana sikutamani kurudi tena labda kwa elkopita
 
Serikali sijui imeferi wapi kwa sasa zamani kwenye baadhi ya mikoa kulikuwa na zoo mfano mwanza ple pasiasi ulikuwa ukienda unaona wanyama takribani wote wakiwa wamefungiwa kwenye mabanda, pale Tabora kulikuwa na zoo napo ulikuwa hivyo hivyo siku za sikuu au week end wazazi walitembelea na familia zao kwenda jionea wanyama na ndege wa aina mbali mbali

Kuna kipindi nilienda dar zoo nikiwa na picha ile ile ya zile zoo nilizokuwa nikiziona udogoni mwangu ila nilipofika uko hakuna lolote niliona simba tu

Wito wangu wizara husika ebu fanyeni kitu watoto wapate kukifunza kwa kuona siyo lazima site twende bugani on a mdau analalamika hapa kafika mbugani hakuna kitu

Tatizo wazili mwenye dhamana kageuka mwandishi wa story za Instagram sijui nje ya box baada kudeal na vitu vya mwingi vilivyofanya tumjue yupo kutuadithia hadithia tu akitaka tuamini kakulia kwenye shida yeye ni mpambanaji tunasubilia ajichanganye tufukue makaburi
Bajeti ya kuwalisha hao wanyama mkuu tuambie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwahiyo ili niwaone niende Mara ngapi? maana hata ile shughuli ya kutelemsha ule mteremko wa creta sina hamu nao tena; Mtelemko ule ni mkali na wa hatari sana sikutamani kurudi tena labda kwa elkopita
Idadi ya safari itategemea na uzito wa mfuko wako ndugu. Ila nakushauri utembelee mbuga zingine pia ili uwaone hao wanyama wengine ambao hukubahatika kuwaona crater.
 
Serikali sijui imeferi wapi kwa sasa zamani kwenye baadhi ya mikoa kulikuwa na zoo mfano mwanza ple pasiasi ulikuwa ukienda unaona wanyama takribani wote wakiwa wamefungiwa kwenye mabanda, pale Tabora kulikuwa na zoo napo ulikuwa hivyo hivyo siku za sikuu au week end wazazi walitembelea na familia zao kwenda jionea wanyama na ndege wa aina mbali mbali

Kuna kipindi nilienda dar zoo nikiwa na picha ile ile ya zile zoo nilizokuwa nikiziona udogoni mwangu ila nilipofika uko hakuna lolote niliona simba tu

Wito wangu wizara husika ebu fanyeni kitu watoto wapate kukifunza kwa kuona siyo lazima site twende bugani on a mdau analalamika hapa kafika mbugani hakuna kitu

Tatizo wazili mwenye dhamana kageuka mwandishi wa story za Instagram sijui nje ya box baada kudeal na vitu vya msingi vilivyofanya tumjue yupo kutuadithia hadithia tu akitaka tuamini kakulia kwenye shida yeye ni mpambanaji tunasubilia ajichanganye tufukue makaburi
Huyo jamaa nimemuona insta na story zake.. Nikapita tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom