Nilifunga ndoa na mtu nisie mpenda

Nilifunga ndoa na mtu nisie mpenda

SEHEMU YA 08



Baada ya kuingia Uwanja wa ndege wa Mwanza, Baba Robson akaingia kwenye Tax akaelekea kituo cha polisi ambacho Robson alikuwa ameshikiliwa, kwanza akakumbuka kumpigia Mkuu wa polisi wa Jiji la Mwanza akampa taarifa kuwa Kijana wake anashikiliwa, Mkuu huyo akapiga simu kituo cha polisi ili

Robson aachiwe, hadi Baba yake Robson anafika kituo cha polisi simu ilikuwa imeshapigwa na maelekezo maalum yalikuwa yametolewa, alipofika palikuwa panaanza kupambazuka, akamkuta Robson akiwa ameketi mahali na Mark maana wote waliachiwa kwa pamoja baada ya maelekezo kutolewa.

“Shikamoo Baba” Wote walisalimia kwa pamoja maana walimjuwa Mzee huyo jinsi alivyo mkali

“Hebu kaeni” alisema kisha wote wakaketi ili Robson aeleze kilichotokea hadi wakashikiliwa kituoni hapo

“Hebu nieleze umefikaje huku na kwanini ulikamatwa Robson?” Alihoji akiwa katika hali ya umakini, Robson akamtazama Mark kisha akapewa ishara na Mark kuwa ni bora aeleze kilichotokea. Robson alimsimulia Baba yake kila kitu hadi wao kukamatwa kwa kosa la kumtishia kifo Mage

Robson akajikuta anapigwa kibao cha nguvu na Baba yake, Mark akashtuka sana japo anamjuwa Mzeee huyo kuwa ni mtata lakini hakutegemea kama angelimpiga kibao Robson tena mbele ya askari pale kituoni

“Sijawahi kuona Mtu mdhaifu kama wewe Robson, kulikuwa na sababu gani ya kuomba wakili kwenye mambo ya kipuuzi kama haya?” Alihoji Baba yake Robson

“Lakini Baba….” Mark akataka kusema jambo akakatishwa

“Mark huu upuuzi mnaoufanya, yaani mmetoka Dar hadi Mwanza kisa mapenzi? Robson wewe ni msomi, Baba yako nina hela, kitu gani kinachokutia wazimu wakati una uwezo wa kuwa na yeyote?

Mke gani mpuuzi yule…. Sasa unajuwa alichokifanya huyo Sylivia?”

“Amefanya nini Baba?” Aliuliza Robson

“Amemgonga na gari Baba yake na kumsababishia maumivu hadi sasa yupo Hospitali?” Alisema Baba yake Robson, Robson akashtuka sana akauliza kwa mshangao

“Sylvia amewezaje kufanya hivyo Baba?”

“Hebu turudi Dar sasa hivi yote utayasikia huko, lakini nakwambia ukweli Robson huu ni upumbavu, unanidharirisha Mimi na familia kwa ujumla” Alisema Baba yake Robson kisha alisogea akazungumza machache na Askari aliyekuwa zamu

“Nini kimetokea, Ina maana mambo yamefikia hatua hii?”

Aliuliza Mark, Robson hakujibu chochote huku moyoni akizidi kuumia, alifikiria kufanya hivyo kungeituliza ndoa yake kumbe ndiyo kwanza ndoa inazidi kuparaganyika.Dakika chache Baba Robson akawa amerudi, wakaondoka kuelekea Uwanja wa ndege tayari kurudi Dar.



Wazazi wa Sylivia walijaribu kumpigia sana simu Sylvia lakini simu haikuita, ilionesha ilikuwa imezimwa, Mama yake Sylvia ndiye aliyekuwa akihangaika zaidi sababu Baba alikuwa katika hali ya kuuguza jeraha la Mguu, alipiga sana simu bila mafanikio yoyote

“Baba Sylvia, tumekosea katika hili tunapaswa kuwajibika” Akasema Mama Sylvia wakiwa wodini

“Nilisimama Kama Baba, ukasimama kama Mama, huu ni ujinga wake Mke wangu.,Kijana aliyemuowa mbona walikuwa marafiki wazuri sana, kuna nini hapa kati?”

“Baba Sylvia moyo wangu unaniuma sana yaani, sijui hata nifanye nini kwasasa, naomba nikamwangalie Sylivia nyumbanikwake” Akasema Mama Sylvia, alishindwa kuvumilia akiwa kama Mama kwa kile kilichokuwa kinaendelea

“Sawa nitabaki salama” alisema Baba Sylvia japo kwa shingo upande sana, palikuwa pameshapambazuka kabisa, Mama Sylvia akachukua Bajaji hadi nyumbani kwa Robson ili kujuwa kinachoendelea kwa Sylivia.

Geti lilikuwa limefungwa, haikuonekana dalili kuwa Sylvia alilala hapo, Mama Sylvia aliumia sana akakaa hapo maana hata ile nguvu ya kutoka hakuwa nayo, alikaa hapo huku nawazo yakimtafuna, alijiuliza na kujijibu mwenyewe hadi jua lilipokuwa kali, hapakuonekana na dalili ya Sylvia kurejea, akaamuwa kunyanyuka aondoke, Mara aliona Tax ikifika hapo, akashuka Robson na Baba yake….Naaam! Walikuwa wameshafika Dar kutokea Mwanza

“Mama mbona upo nje?” Alihoji Robson

“Nimegonga sana bila mafanikio, nimepiga simu ya Sylvia bila mafanikio pia” Akajibu Mama Sylvia huku akionekana kukata tamaa kabisa, Robson akajipapasa akachukua funguo, akafungua geti kisha akawakaribisha ndani Baba yake na Mama Sylvia

“Hivi ni nini kinaendelea Robson, maana wewe ndiye Mtu wakaribu wa Sylvia” aliuliza Mama yake Sylvia

“Kusema ukweli Mama ukiniuliza kinachoendelea nitashindwakukupa jibu linaloeleweka kwasababu hata Mimi nipo njia panda kwa yanayoendelea” alisema Robson

“Sasa atakua yupo wapi?” Alihoji Mama Sylvia

“Mama ngoja niangalie vizuri” alisema Robson kisha akaingia chumbani, ndipo alipogundua kuwa siyo tu Sylvia hayupo bali hata mabegi yake na nguo zake zote hazipo, Robson akatoka mbio hadi Sebleni

“Kuna nnini?” Akauliza Baba Robson kwa mshangao mkubwa sana

“Baba….Sylvia ameondoka hapa, ameondoa nguo zake zote sijui hata ameenda wapi aaah” alisema Robson huku akiwa amejishika kichwa chake

“Unasemaje?” Aliuliza Baba Robson

“Sylvia ameondoka?” Akadakia Mama Sylvia kuuliza

“Ndiyo Mama hakuna chochote chake humu ameondoka hapa au atakuwa amerudi kwenu?” Aliuliza Robson,,Haraka Mama Sylvia akapiga simu kwa msichana wa kazi, akajibiwa kuwa Sylvia hakwenda huko kabisa

“Oooh Mungu wangu huyu Mtoto sasa ameenda wapi?” Aliuliza Mama Sylvia

“Ukituuliza sisi utakuwa unakosa majibu sababu hakuna anayejuwa alipo Binti yako” alijibu Baba Robson, likawa limeibuka jambo jipya nalo ni kutoweka kwa Sylvia ambaye hakujulikana alikuwa wapi

“Baba….Sylvia anawasiliana na Mtu anaitwa Brahama, hapana shaka wapo pamoja hivi sasa” Aliesema Robson akiwa amechoka, akatua kitini akiwa hoi kabisa, mwili na akili vilichoka kufanya maamuzi, aliumia mno

“Brahama ndiyo Nani?” Aliuliza Baba Robson

“Ndiye Mwanaume anayekisumbua sana kichwa cha Sylvia, ndiye anayeharibu ndoa yangu” Chozi likambubujika Robson

“Ndiyo sababu ya nyie kwenda Mwanza?” Alihoji Baba Robson

“Ndiyo Baba!!”

“Uuupsss!! Hili jipya sasa, au watakuwa wameenda Mwanza?”

Aliuliza Baba Robson, hakuna aliyekuwa na jibu la moja kwa moja kuwa Sylvia alikuwa ameenda wapi na huyo Brahama kama hisia zao zilivyowatuma.

Mama Sylvia akaondoka hapo bila hata kuaga alikuwa amechanganikiwa sana kama ambavyo Robson alikuwa amechanganyikiwa, Baba Robson akamtuliza kijana wake akamwambia

“Popote alipo kama wapo ndani ya Nchi hii, tutawapata. Huyo Brahama ni mshenzi sana” Alisema Baba Robson, alijuwa siyo vizuri Robson akakaa mwenyewe kutokana na kilichotokea, akahofia angeweza kujidhuru, akamchukua akaenda naye nyumbani kwao.

Taarifa ya kutoweka kwa Sylvia ikatikisa vichwani mwa wanafamilia na walioyafahamu mahusiano kati ya Robson na Sylvia, Baba Robson akaenda kutoa taarifa polisi ili wamsaidie kumtafuta Sylvia kila kona ya jiji la Dar-es-salam

“Robson Mwanangu sikujuwa kama una moyo mdogo kiasi hiki, hizi ni changamoto za kawaida sana katika Maisha ya Mwanadamu….naamini atarudi kwako siku moja” Alisema Baba yake Robson wakiwa wameketi kwenye Bustani

“Aah Baba ni ngumu kuamini hivyo kwasababu Brahama ni ufunguo wa moyo wa Sylvia, kabla yangu alikuwa na huyo. Nilifanya jitihada kubwa sana kuhakikisha nakuwa naye lakini mara zote amekuwa Mtu ambaye ananiumiza na kurudisha mawazo yake nyuma” Alisema Robson kwa sauti ya upole sana

“Hakuna kizuri kinachopatikana kirahisi, kama kweli unamhitaji Sylvia ni lazima upambane kuhakikisha anarejea kwako, pigana vita ya kiume” Akasema Baba Robson akiwa anampiga bega Kijana wake

“Nimepigana sana Baba hadi nikamuowa Sylvia, naona naanza kukata tamaa, inakuwa ngumu sana kumrejesha mikononi mwangu….nianzie wapi na sijui alipo Baba” alisema Robson

“Yule Binti wa Mwanza ambaye alitoa taarifa za Sylvia na huyo Kijana anayesumbua akili yake anaweza kuwa ufunguo wa kujua Sylvia yupo wapi” Alisema Baba yake Robson kisha akatabasamu

ili kumtia moyo Mwanaye

“Una maanisha nirudi tena Mwanza?”

“Ndiyo lakini unapaswa kutumia akili zaidi ya nguvu zako, tukijua alipo itakuwa rahisi sana…jiandae urudi Mwanza, Kwa upande wangu nitashirikiana na familia ya Binti kujuwa alipo”

Alisema Baba yake Robson kwa sauti ambayo Robson hakuitegemea kabisa, yaani Baba yke alipoa kabisa kutokana na unyonge ambao Robson alikuwa nao, mara akaingia Mama Robson akiwa amebeba Juisi, akampatia Mwanaye kisha kamtazama kwa sekunde kadhaa alafu akauliza

“Mna mpango gani?”

“Nimemshauri Robson arudi Mwanza kwa yule Binti aliyetoa taarifa Mwanzo, pengine atakuwa anajuwa walipo akina Sylivia kama kweli yupo na huyo Kijana”

“Robson, kuwa makini sana hatuna Mtoto mwingine zaidi yako, Tunakutegemea sana” Aliongezea Mama Robson kisha aliondoka zake, Robson akamtazma Baba yake kwa uchungu sana huku Mzee huyo akimpa ishara ya kumtia moyo Kijana wake.

Sylvia alikuwa zake Hotelini na Brahama wakipanga mpango wa kuondoka Nchini ili wakaishi Maisha ya uhuru zaidi maana waliamini wanatafutwa

“Ni lazima tuondoke Sylvia kama kweli tunataka kuishi Maisha ya uhuru na kufurahia penzi letu, Robson atatutafuta Kila kona ya Nchi hii” Alisema Brahama akiwa anatabasamu mbele ya Sylvia ambaye moyo wake ulikuwa na furaha sana, hakujali maumivu aliyomsababishia Baba yake

“Mimi naona tusikilizie hili jambo kwanza hadi lipoe ndipo tuondoke maana bila kufanya hivi itakuwa vita kubwa, Namjuwa Robson na ukichaa wake” Alisema Sylvia

“Kwahiyo tuendelee kuishi hapa Hotelini?”

“Ndiyo hatuna mahali pengine pa kwenda Mpenzi wangu”

“Haya, usemacho ni sheria Sylvia, siwezi kukupinga kwa lolote lile..”



“Lakini namuonea huruma sana Mama yangu, sababu huko alipo atakuwa analia kwa kufikiria kama nipo salama, hajui nilipo lakini najuwa atahuzunika ila atasahau. Wao ndiyo sababu ya Mimi kuolewa na Robson”

“Usijali, Mama yako atakuwa sawa Sylivia” akasema Brahama, Waliamua kuishi hapo ili kuwakwepa akina Robson

Mchana mmoja Robson alimpigia Mark wakapanga kuonana, wakakutana Baa moja iliyopo Mikocheni A, wakaagiza kwanza Bia ili kuondoa uzito mwilini, kisha maongezi yakaanza

“Kilichonifanya nikupigie ni kwa ajili ya kukueleza kuhusu Alichokisema Baba, wakati polisi wanafanya upelelezi wao na sisi tunatakiwa kufanya jitihada binafsi” Alisema Robson kisha akapiga funda la Bia

“Amesemaje?”

“Turudi Mwanza kwa ajili ya kumfuatilia Mage, huwenda anajuwa mahali alipo Brahama, ni lazima atakuwa pamoja na Sylvia

“Si unakumbuka kilichotukuta tukakamatwa na polisi, safari hii tunaenda na mpango gani?”

“Ndiyo maana nimehitaji kuongea nawe Mark ili tupeane Mawazo ya namna ya kuingia Mwanza na kutekeleza jambo letu”

“Kwenda Mwanza siyo tatizo kabisa, ila hofu yangu tunawezarudia kile kile, safari hii itakuwa mbaya zaidi” alisema Mark huku Bia zikizidi kunyweka

“Mimi nina wazo moja, tumteke Mage ili tumlazimishe aseme ni wapi alipo Brahama”

“Unasemaje?” Alihoji kwa mshituko Mark

“Ndiyo…kwasababu bila hivyo itakuwa ndiyo vilevile, nafikiria kwa kufanya hivyo Mage atasema kwa haraka na hatutomwachia hadi tumpate Brahama sababu naamini wanawasiliana” Alisema Robson huku akimwangalia Mark ambaye alikuwa ameduwaa

“Mh! Baba yako analijuwa hili wazo?”

“Hapana na hawezi kukubali hili wazo, ila niamini Mimi itakuwa ni rahisi zaidi kumpata Brahama, unafikiria ni rahisi kumpata kwenye Nchi hii kubwa?”

“Ok sawa! Kama ni hivyo basi ni lazima turudi Dar na Mage hakuna njia nyingine”

“Sawa tutaondoka na Prado ya Mzee ili iwe rahisi kurudi na Mage hapa Dar” Yakawa ndiyo makubaliano warudi Mwanza wamchukue Mage ili aseme ni wapi alipo Brahama.

Wakanywa pombe hadi wakalewa, Mapenzi ni rahisi kuyasikia na kuyaelewa kwa Mtu mwingine ila yanapokukuta ndipo unapokuja kutambua si jambo la kawaida, wivu ukawa umemjaa sana Robson

kila alipofikiria kuwa Brahama yupo na Mke wake, aliporudi kwao alimueleza Baba yake kuwa Mchana wa siku inayofuata watafanya safari kwa kutumia Prado

“Hivi ni akili yako au pombe? Kuna sababu gani ya kutumia gari kwa safari ndefu? Robson kama huna pesa niambie nikupe upande ndege na siyo gari” Alisema Baba yake Robson hukuakiwa anamtazama Mwanaye ambaye alikuwa tungi sana.

“Baba si unanipenda Mwanao, si unanijali na kunithamini? Basi niache niondoke na Prado nina mipango nimeipanga” Akasema Robson akiwa anasinzia kochini, mwisho akalala hapo hapo,

Baba yake alisikitika sana

“Oooh Mapenzi haya, Mwanangu umekuwa kichaa kwasababu ya Mwanamke, upo sahihi sijui unapitia maumivu kiasi gani” alisema

xxx



Asubuhi mapema taarifa ambayo ilisambaa kwenye familia zote mbili ni kupatikana kwa Mage ambaye alikuwa akifahamu walipo, pia maamuzi ya Brahama ya kukubali kumrudisha Sylvia

“Mume wangu hizi ni habari njema sana hatimaye Binti yako anarejea” Alisema Mama Sylvia mbele ya Baba Sylvia

“Anarudi kufanya nini hapa? nimekuwa kilema kwasababu yake, sitaki kusikia tena kuhusu Sylvia, tena Mungu angempa laana akafa kifo kibaya sana” Alisema kwa hasira sana Baba Sylvia

“Usiseme hivyo Baba Sylvia, Binti yako amejifunza vya kutosha hupaswi kumwadhibu kiasi hiki” Alisema Mama Sylvia lakini haikubadilisha msimamo wa Baba. Sylvia

Nako upande wa pili, Baba Robson alikuwa ameketi sofani akitafakari taarifa ya kupatikana kwa Mage huku akifikiria maamuzi ya Brahama kuhusu kubadilishana Mage na Sylvia

“Mume wangu kwanini hauna raha?” aliuliza Mke wake akiwa anamuandalia chai.

“Mke wangu, Robson na mapenzi yake kwa huyu Binti yanaweza yakaharibu kabisa Maisha yake, Mimi nina wazo?” alisema kwa sauti iliyojaa umakini wa hali ya Juu sana

“Wazo lipi hilo?”

“Tumuuwe huyu Binti ili asirudi kwenye Maisha ya Robson, sababu kama ataendelea kuwa hai atamsumbua sana Kijana wetu, sasa ni Bora afe ili Robson alie asahau kabisa” Kauli ya Kumuuwa Sylvia ilimtisha sana Mama Sylvia

“Unasemaaje? umeyafanya hayo ukiwa Jeshini kwasasa sitaki utende dhambi za Kinyama Baba Robson, Kumbuka yule Binti ana wazazi wake. Najuwa unataka kumlinda Robson lakini njia hii siyo sahihi” Alisema Mama Robson akiwa anamtazama kwa makini Mume wake anbaye alionekana kudhamiria kutenda tukio hilo

“Hakuna njia nyingine zaidi ya kumpoteza tu, Mark na Robson wapo Barabarani wanarudi, napaswa kuifanya hii kazi. Brahama na Sylvia wapo Ocean View ambako mabadilishano yatafanyika, napaswa kuwahi” Alisema Baba Robson kisha aliingia chumbani akachukua Bastola

“Mume wangu hebu acha hili jambo kuna namna ya kulimaliza bila kuathiri chochote kile”

“Nimesema hakuna njia nyingine, tuna Mtoto mmoja tu Mama Robson alafu tuje kumpoteza kisa mpuuzi ambaye hana msimamo?yule Binti anastahili kifo” alisema kwa hasira sana na kumfanya Mama Robson ashindwe kumzuia Baba Robson, akamuacha akatoka.

Masaa matano yalipita, ndani ya Hoteli ya Ocean view hakukuwa na maelewano mazuri kwa Sylvia na Brahama, Msimamo wa Brahama wa kutaka kuacha kila kitu ulimfanya Sylvia ajawe na hasira sana akawa anamlaumu Brahama

“Hiki ndicho ulichoniahidi na kunitia hasara ya Maisha Brahama?” Alisema Sylvia akiwa mbele ya Brahama

“Sylvia nakupenda lakini siwezi ruhusu kibaya kimkute Mage, ana thamani kubwa ni rafiki wa muda mrefu kwangu” Alisema

“Sasa kama ulijuwa itakuja kuwa hivi kwanini uliniaminisha, kwanini uliniongopea? nakuuliza Brahama nijibu” AliSema kwa hasira sana Sylvia huku chozi likimvuja

“Nimelazimika Sylvia, nimefanya jitihada nyingi za kumficha Mage lakini imeshindikana, ilipofikia hapa hakuna njia nyingine zaidi ya kukubaliana na hali halisi kuwa mpango wetu umefeli. Sikutaka kumaliza namna hii kwanini hautaki kunielelewa?” akalalama Brahama

“Ok sawa!! lakini kaa ukijuwa kuwa nitakuchukia katika Maisha yangu yote endapo hatutoondoka Nchini Brahama, utakuwa adui yangu kuanzia siku ambayo utanikabidhisha kwa Robson”

“Sylvia….Rob ni Mumeo sikupeleki kwa adui yako bali kwa Mtu ambaye amekuowa kwa ndoa…..” Alisema Brahama kisha akaingia Bafuni, akawa anajimwagia maji ili kuondoa hofu iliyokuwa imemtawala.

Muda huo Baba Robson alikuwa ameshafika katika Hoteli hiyo kwa ajili ya Kumuuwa Sylvia kama ambavyo alikuwa amepangilia, hakutaka kujiuliza mara mbili akaisoma meseji ya Robson iliyokuwa inaonesha chumba ambacho Sylvia na Brahama walikuwepo, akapandisha ngazi taratibu akiwa ameficha Bastola yake kiunoni, alitembea akiwa na uhakika sana wa kutekeleza mauwaji hayo

Chumba Namba 404 ndicho ambacho Sylvia na Brahama walikuwepo,

Mzee huyo alifika hadi mbele ya mlango huo, akatafakari kidogo kisha akagonga mlango, Sylvia akashtuka kisha akauliza

“Nani wewe?” Muda huo bado Brahama alikuwa akijimwagia maji hivyo hakusikia kelele za kugongwa kwa mlango wala sauti ya Sylvia, Baba Robson alikaa kimya.

Sylvia akanyanyuka taratibu na kuuelekea Mlangoni ili aangalie ni nani alikuwa akigonga, laiti kama angelijuwa asingeliinuka akaenda mlangoni, Baba yake Robson alitumia maelekezo ya Robson kupajuwa walipo na alikuwa amesimama kuhakikisha anamuuwa Sylvia. Alipofungua mlango kwa kufikiria

huwenda ni Mhudumu wa Hoteli alikutana na sura ya Baba Robson ikiwa kavu sana.
 
SEHEMU YA TISA-09

“Babaaaa!!!” Aliita Sylvia, Muda huo huo Baba Robson akafyatua Risasi mbili eneo la moyo wa Sylvia, alihitaji kummaliza ili kijana wake asiteseke tena na Mapenzi. Baada ya kumpiga risasi akakimbiaRobson akatoka haraka bafuni akamuona Sylvia akiwa anatapatapa Sakafuni, muda huo huo Walinzi wa Hoteli wakafika pale na kumsaidia Brahama kumpeleka Hospitalini Sylvia, akakimbizwa Muhimbili haraka ili kuona kama wanaweza kuokoa uhai wake.

Hakuna aliyekuwa akilifahamu hilo zaidi ya Brahama na Baba yake Sylvia

Damu zilikuwa zimetapakaa kwenye shati la Brahama, alikuwa akitetemeka na kujialaumu sana, akiwa hapo Robson alipiga simu. Ikawa ngumu kwa Brahama kuipokea sababu hakujuwa atamueleza nini akaeleweka.

Akaamuwa kuwapigia simu familia ya Sylvia kuwa Binti yao yupo mahututi Muhimbili,, haraka sana Mama Sylvia alifika hapo kumjulia hali Binti yake ambaye alikuwa akipigania uhai chumba cha wagonjwa Mahututi baada ya kupigwa risasi na Baba Robson

“Kimemkuta nini Binti yangu?” Aliuliza akiwa anahema juu juu, ilikuwa ndiyo mara ya kwanza anamuona Brahama ambaye aliifanya ndoa ya Sylvia kuwa Shaghalabaghala kwa siku chache tu

“Mama…Sylvia amepigwa risasi nikiwa Bafuni nikasikia akisema Baba” Mama Sylvia alishtuka sana akamwambia Brahama

“Siwezi kukuamini Mtu ambaye umevuruga kabisa Maisha ya Binti yangu, sikujui hunijui wewe Kijana hebu sema ukweli nini kimetokea kabla sijapiga simu polisi” Alisema, Bahati nzuri pembeni kulikuwa na mlinzi mmoja wa ile hoteli akadakia

“Mama anachokisema ni kweli japo kumjuwa mpigaji ni ngumu sana kwasababu hatukumwona Mtu yeyote pale zaidi ya huyu na Binti yako,” pale pale Mama Sylvia akamshika mishiko Brahama

“Umeniulia Mwanangu si ndiyo? Nakuuliza uneniulia Mwanangu…wewe ni shetani wewe Kijana” Alisema akaanza kumpiga Brahama kama Mtu aliyepandwa na kichaa, Mlinzi akaokoa

“Mama hauna haja ya kushuku kwa sasa kikubwa ni kuangalia afya ya Binti yako namna inavyoendelea vinginevyo utajikuta unapata presha, baada ya hapa kesi itafika kwenye dawati la jeshi la polisi, wao watafanya uchunguzi wao.” Alisema Mlinzi huyo ,

Mama Sylvia akakaa chini na kujiinamiaMuda huo Baba yake Robson alifika nyumbani kwake akiwa

anatokwa na jasho kama Mtu anayekimbizwa, damu kidogo ilimrukia kwenye Shati. Alikutana na Mke wake mlangoni akiwa anataka kuingia ndani

“Baba Robson hiyo damu ya nini?” aliuliza kwa mshtuko mkubwa sana

“Hebu pisha kwanza” AliSema akaingia ndani kwa kumsukuma Mama yake Robson

“Unachokijuwa kibakie kuwa siri yako, sitaki yeyote alijuwe hili tumeelewana? si Robson wala Mtu mwingine” Alisema kwa sauti iliyojaa msistizo sana huku Mama Robson akiwa katika hali ya kushangaa akamuuliza

“Ina maana umemuuwa kweli Sylvia?”

“Ishia hapo hapo, sitaki urudie tena. Sitaki kukusikia ukisema chochote hata Robson atakapofika. Nimefanya hivi ili kumlinda yeye asiharibu Maisha yake” Alisema Baba Robson.

“Umemkosea sana Kijana wako sababu anahangaika kuipata furaha ambayo uneiondoa kwa urahisi sana Baba Robson, Hujaacha Maisha ya kikatili uliyoyapata jeshini?”

“Mama Robson huu uamuzi una faida kubwa sana, hatutosumbuka hata sisi kwa ajili ya Robson tena, atapata Mwanamke mzuri mwenye mapenzi na Kijana wangu…”Alisema kisha akataka kupandisha ngazi kuelekea chumbani

“Itakuwaje kama Robson atapata Mwanamke kama Sylvia, naye utamuuwa?” aliuliza swali ambalo lilimfanya Baba Robson amtazame Mama Robson bila kutoa jibu lolote lile, akapandisha ngazi

Mama Robson akampigia simu Robson muda huo huo akamuuliza yupo wapi kisha akataka kujuwa kama amefanikiwa kujuwa alipo Sylvia, alifanya hivyo ili tu kudadisi kwa kina Kama Kijana wake amepata taarifa ya kutisha kuhusu Sylvia, majibu ya Robson yalimuonesha Mama huyo Robson hajui chochote.

Muda huo huo akampigia simu Mama Sylvia, hakutaka Robson azipate taarifa hizo wakati yupo Njiani kurudi Dar, akajifanya hajui lolote lakini kilio cha Mama Sylvia kilimfanya amuulize tatizo nini, akapewa taarifa hiyo nzito lakini bado hakukuwa na taarifa ya kifo cha Sylvia

“Nakuja lakini naomba Robson asilijuwe hili tafadhali, atachanganikiwa sana maana yupo Njiani anarudi Dar” Alisema Kisha haraka haraka akatoka akaelekea Muhimbili, akasimuliwa vizuri kilichotokea.

Moyoni alijuwa aliyefanya jaribio hilo ni Mume wake kwa ajili ya kumlinda Robson kama alivyosema

“Pole sana Mama Sylvia, laiti kama ningelijuwa haya yote yatatokea ningezuia ndoa ya Sylvia na Robson isifanyike, imeleta uchungu mwingi kwenye familia” Alisema Mama Robson.

Huku akizidi kuumia, akifikiria namna Robson atakavyo changanikiwa hakupata jibu

“Huyu Kijana ni Nani?” Alimuulizia Brahama ambaye alikuwa ameloa damu

“Huyo ndiye aliyekuwa na Sylvia kwa muda wote”

“Ina maana huyu ndiye akiyekuwa kizingiti cha mambo yote?”

“Ndiyo!!” Alisema Mama Sylvia akiwa anazidi kulia. Mama Robson alimtazama Brahama akatikisa kichwa chake sababu alishajuwa endapo Robson atakapokuwa amefika Dar balaa zito linaenda kuibuka

Brahama alikuwa ameketi kama Mtu aliyetengwa na kila Mtu,

Mara daktari alfika na kufanya wote wawe katika hali ya Kumsikiliza

“Tumefanya Upasuaji wa kuondoa risasi mbili ambazo zilikuwa upande wa kushoto, Bado yupo hai ila hajarudisha fahamu zake. Kwasasa jambo la Msingi ni Dua na sala” Alisema Daktari

“Tunaweza kumwona?” Aliuliza Mama Sylvia

“Kwasasa hapana mnaweza kurudi nyumbani sababu yupo katika chumba maalum kwa ajili ya uangalizi hadi pale hali yake itakavyoanza kuimarika” Alisema alafu akaondoka zake haraka.

Brahama akainamia chini maana alijuwa baada ya mazungumzo hayo atakatakaye fuatia ni yeye

“Utasema nini kimemkuta Binti yangu Kijana, haiwezi kwisha katika hali kama unayoifikiria” Alisema Mama Sylvia, Ukweli alikuwa akiujuwa Mama Robson sababu Baba Robson ndiye aliyetaka Kumuua Sylvia

“Mama Sylvia!!” aliita Mama Robson

“Ndiyo ni lazima atasema, tena atasema mbele ya sheria” Mara wakaingia polisi wakamkamata Brahama, akawa anawaambia polisi kuwa hakumpiga risasi Sylvia

“Kama hukumpiga basi utakuwa unamjuwa aliyempiga risasi si mlikuwa wote, alafu kwanini ukae na Mke wa Mtu Hotelini? hilo ni kosa namba moja na ndiyo Mzizi wa hili linaloendelea” Alisema Askari polisi akiwa amemshikilia Brahama

“Tutakutana kituoni” Alisema Askari huyo kisha wakaondoka na Brahama kuelekea kituo cha polisi



“Una uhakika kuwa yule Kijana ndiye aliyemdhuru Binti yako Mama Sylvia?” alihoji Mama Robson huku akitamani sana amueleze ukweli Mama Sylvia ili Brahama asihukumiwe kwa kosa ambalo hakutenda lakini alijikuta akiwa mzito sana kusema chochote anachokijuwa

“Amekaa na Binti yangu Hotelini kwa siku zote hizo, amesababisha madhara kwenye familia yangu….na

yako…unawezaje kukosa kumhisi yeye?”

“Sina maana asihisiwe lakini mbona alishazungumza na Robson kuwa akirudi atamuacha Sylvia, inawezekana vipi ampige risasi alafu amlete Hospitali na akupigie simu wewe? aliweza kufanya unyama akamuacha Sylvia Hotelini” Alisema Mama Robson akiwa anaumia ndani ya moyo wake. Angalau Mama Sylvia maneno yalimuingia akakaa kimya

  • ••••••••••
Saa tano Usiku, Jiji la Dar liliwapokea Mark na Robson wakiwa wamemshikilia Mage. Hakuna hata mmoja kati yao ambaye alikuwa na taarifa ya kilichomfika Sylvia, walienda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Baba Robson, wakaingiza gari ndani.

Baba Robson alikuwa ameketi Sebleni akiwasubiria, Mara Mama Robson naye akaongezeka pale Sebleni baada ya kusikia ngurumo ya gari na purukushani za kufunga na kufungua geti, alitazamana na Mume wake, Kisha akamkimbilia Robson na kumkumbatia kwa uchungu.

“Mama Usijali kila kitu kitakaa sawa hivi karibuni, nimekuja na Mage” Alisema Robson, akaketi Usawa wa Baba yake

“Baba na Mama, poleni kwa kuwaingiza katika hili najuwa hamkustahili usumbufu huu” Alisema Robson, akamtazama Mark kidogo akaendelea

“Kesho ni siku ya kutamatisha kila kitu kwasababu Brahama yupo tayari kufanya makabidhiano, anipatie Sylvia ili nimpe Mage. Naamini kila jambo linaenda kukaa sawa” Alisema, Baba

yake akakohoa kidogo, alikuwa hana taarifa kuwa Sylvia bado anaishi kwani hata Mke wake hakunweleza chochote sababu alijuwa kufanya hivyo kunaweza kuzua taharuki zaidi.

“Hilo ni jambo ambalo tulikuwa tukilisubiria Mimi na Mama yako, tunaamini kesho itakuwa ni siku bora sana kwako Mwanangu” Alisema Baba Robson kama hakuna kilichotokea vile,

alifanya hivyo ili asiwe sehemu ya mshukiwa wa moja kwa moja, wakalala hadi kulipo pambazuka



Robson akampigia simu Mama yake Sylvia ili waambatane pamoja kuelekea Ocean view, lakini Mama Sylvia alianza kulia kama unavyojuwa Mwanamke hasa Mama ni ngumu kuvumilia maumivu ya Binti yake

“Mama unalia nini wakati leo tunaenda kumpata Binti yako?” aliuliza Robson, Mark akaingia akakuta Robson anaongea na simu

“Kwani Mama yako hajakwambia chochote Robson, Sylvia yupo Hospitalini tokea jana. hali yake siyo nzuri” Robson alishtuka sana, kwanza kujuwa kuwa Mama yake alimficha jambo pili alitaka kujuwa nini kimemsibu Sylvia Mwanamke ambaye anampenda sana.

“Sylvia amepigwa risasi akiwa Hotelini” Macho yakamtoka Robson, akadondosha saa aliyokuwa anataka kuivaa

“Amepigwa risasi? yupo hai kweli?” Alihoji akiwa na wasiwasi huwenda Sylvia akawa amekufa. Chozi likawa linamvuja taratibuu

“Robson! nimechanganikiwa sana sijui nifanye nini, Sylvia yupo hai lakini mahututi hajitambui”

“Brahama ndiye aliyempiga risasi, Okay!! yupo Hospitali gani?” Aliuliza Robson, akaambiwa ni Muhimbili, akakata simu akataka kutoka lakini Mark alimzuia

“Kuna nini Robson?”

“Sylvia amepigwa risasi na Brahama yupo Hospitalini” Alisema Robson

“Unamaanisha?..”

“Hivyo ndivyo ilivyo amekiuka makubaliano, nakwapia Mark kama Sylvia kitamkuta kibaya namuuwa Brahama” Alisema kisha akamsukuma Mark akatoka, akapita sebleni akamkuta Mage akiwa hapo

Robson akasimama na Kumtazama kwa hasira huku akiwa anavuja mchozi, Mara Mama yake Robson akaingia Sebleni na kumkuta Robson akimtazama Mage kwa hasira huku akivuja mchozi

“Robson!” akaita Mama

“Unataka kusema nini Mama?” Aliuliza Robson

“Kuna nini? si mmekubaliana kila kitu kwanini unalia sasa…”

“Nalia kwasababu Mama yangu ni mnafiki, Muongo na mficha siri…Hivi Mama ulikaa kimya wakati Sylivia yupo Hoi Muhimbili akipigania uhai wake, kulikuwa na sababu gani kunificha jambo lenye maana kubwa kwangu?”

Mama Robson akainamia chini huku Robson akizidi kuzungumza kwa hisia kali sana, ndipo Mage aliposhtuka na kumuuliza Robson

“Sylvia yupo Muhimbili? kimemkuta nini?” alihoji kwa Mshangao mkubwa akiwa anasimama

“Unashamgaa nini, unafikiria naweza nikakuamini tena Mage? Wewe na Brahama ni kitu kimoja alafu unajifanya hujui si ndiyo….Brahama amempiga risasi Mke wangu wakati tulikubaliana, kama Sylvia kitamkuta kibaya Nakuuwa wewe”

Alisema Robson kisha alitoka kwa hasira akaingia kwenye prado akaondoka hapo akaelekea Muhimbili ambako Sylvia alikuwa akipigania uhai wake.

Akampigia simu Mama yake Sylvia kisha akaelekezwa mahali ambapo Mama huyo alikuwepo, Kwa mwendo wa Haraka sana Alisogea hapo akaonana na Mama Sylvia

“Mama,, Sylvia anaendeleaje?” alihoji

“Hali yake bado haijakaa sawa hatuwezi hata kumuona tangu jana Robson” Alisema Mama sylvia kisha chozi likamdondoka

“Brahama yupo wapi?”

“Amekamatwa na Polisi jana, yupo kituoni”

“Kwanini amempiga risasi Sylvia wakati tulikubaliana kilakitu kiishe leo?”

“Hata Mimi nimeshindwa kupata jibu Robson, nimejiuliza kwa muda mrefu hadi akili imechoka. Brahama anasema hakumpiga risasi Sylvia bali alisikia Sylvia akiita Baba kabla ya kusikia mlio wa Risasi, inakuwa ngumu kumwamini sababu yeye ndiye chanzo cha matatizo yote haya” Alieleza Mama Sylvia

Akamshika Robson ili waketi wazungumze

“Ilipofikia Robson sioni kama unaweza ukamfurahia Binti yangu, Baba yake pia hataki kumwona Sylvia. Hata alivyosikia alisema ni bora afe tu” Alisema Mama Sylvia wakiwa wameketi

“Mama Mimi naamini Sylvia alitereza mahali, bado ananipenda sababu Mimi ni Mume wake hawezi kulisahau hilo….na kuhusu Baba yake nafikiri ni hasira tu sababu ya maumivu ya Mguu”

“Sidhani Robson, Hata familia yako haiwezi kumpenda tena Sylvia. Nikushauri tu achana na Sylvia..” Alieleza kwa uchungu sanaa Mama Sylvia, Robson akamwambia Mama Sylvia

“Wakati nafanya maamuzi ya kuwa na Binti yako ilikuwa ni Mimi na moyo wangu, sitajali hata kama Familia itanisusia” Alisema Robson, Mara akaingia Daktari ambaye tangia jana alikuwa akimtibia Sylvia

Wote walisimama kumsikiliza, akavua Gloves kisha akawaambia.

“Poleni sana, Bahati mbaya muda mchache uliopita Sylvia amefariki” Alisema Daktari huyo, Mama Sylvia akaanguka palepale. Robson akamdaka huku chozi likiwa linambubujika

“Dokta Sylvia amekufa?” alliuliza akiwa anatokwa na mchozi

“Pole sana Kaka kazi ya Mungu haina makosa” Alisema Daktari huyo kisha aliwaita manesi kwa ajili ya kumsaidia Mama Sylvia ambaye alikuwa ameishiwa nguvu, Manesi walimchukua MamaSylvia hadi kwenye wodi kwa ajili ya matibabu

Mlango wa chumba alichotokea Daktari ulikuwa wazi, macho ya Robson yalikita huko, akajkuta ananyanyuka hadi ndani ya wodi hiyo ya uangalizi maalum, akakuta mwili ukiwa umefunikwa juu ya kitanda, akaufunua taratibu akamuona Sylvia akiwa amelala hapo, nguvu zilimuisha Robson hakuamini kama kweli Sylvia alikuwa amekufa, chozi la maumivu lilimbubujika akasema

“Haikuwa njia nzuri ya kuniaga Sylvia, nilipambana kukurudisha, nimefanya vyote…..Nawe umenilipa Kifo si ndiyo!” Maneno haya yaliwaumiza hadi manesi waliopo kwenye chumba hicho, pete ya ndoa ilikuwa kidoleni kwa Sylvia

Wale manesi walimuondoa Robson kwa nguvu pale wodini sababu maumivu aliyokuwa nayo yasingeliweza kupoa haraka na pengine yangemletea maumivu zaidi.

“Niacheni nikakae na Mke wangu Mimi” Alisema Robson kwa uchungu lakini Manesi walihakikisha wanamtoa kabisa hadi nje, wakamuacha akiwa emekaa kwenye korido

Kama kuna siku Robson aliumia, alilia basi ni siku hiyo. Alilia sana kama Mtoto mdogo akitokwa na makamasi, kila alivyokumbuka namna alivyohangaikaa Mwanza kwa ajili ya Sylvia alizidi kulia, dakika chache baadaye kilio kilikoma, hasira zikajaa kwenye kifua cha Robson, Kichwani akawa na jina moja tu la kulifanyia kazi, si lingine bali Brahama, aliamini Brahama alikuwa amempiga risasi na kusababisha kifo cha Sylvia.

Akanyanyuka na kukimbilia kwenye gari, akawasha kisha akaelekea nyumbani kwao. Akamkuta Mama yake akiwa nje, akampita mbio hadi chumbani kwa Baba yake, akavuta droo na kutoa Bastola ya Baba yake ambayo laiti kama angelijuwa kuwa ndiyo iliyotumika kuondoa uhai wa Sylvia sijui ingekuwaje?

Mama yake akamzuia Robson akamuulzia

“Una kichaa Robson, unaenda wapi?” alihoji Mama Robson, kwakuwa alikuwa mwanaye tu ndiyo maana aliweza kukaa karibu naye lakini jinsi alivyo na hasira ilikuwa inatisha sana.

“Ndiyo nina kichaa kwasababu ua langu limenyauka mbele yamacho yangu, aliye nifanya nikakosa raha katika Maisha yangu ndiye atakayelipa gharama ya maumivu yangu” Alisema Robson

“Robsson kuna nini hasa?”

“Sylvia amekufa Mama, nina raha gani kwasasa, nina thamani gani? siwezi kumwacha Brahama”

“Una hakika ndiye aliyempiga risasi Sylvia, Robson mbona unataka kuniacha na Mimi? nilikwambia mwisho utakuwa mbaya”

“Brahama atalipa gharama ya damu aliyoimwaga kwa Sylvia Mama nipishe….” Maneno haya yalimfanya Mama Robson ashindwe kuvumilia, alifikiria anachoenda kukofanya Robson kinaweza kuleta matatizo zaidi sababu Brahama yupo polisi, na kama ataenda polisi basi atauawa na polisi kabla ya kumfikia Brahama

“Robson Mimi namjuwa aliyempiga risasi Sylvia lakini siyo Brahama” Ilibidi aseme Mama Robson huku akimwaga chozi la haja

Robson alijawa na mshangao kumsikia Mama yake akisema kuwa anamjuwa aliyemuuwa Sylvia, alishusha munkari kisha akamuuliza Mama yake kwa utaratibu sana

“Unamjuwa aliyempiga risasi Sylvia?”

“Ndiyo Namjuwa, Robson Naona aibu siku nikifa na siri hii ambayo inaweza kuleta taharuki kubwa kwako Mwanangu” Alisema kwa sauti iliyojaa kilio

“Nani aliyempiga risasi Mke wangu?” Aliuliza Robson

“Nakuomba Robson nikikutajia kaa chini ufikirie nini ufanye lakini usikurupuke na hasira utafanya maamuzi magumu, nakuomba weka Bastola chini” Alisema

“Mama huwezi kuniondoa katika njia yangu, najuwa aliyempiga risasi Sylvia ni Brahama sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mke wangu, hakuna Mwenye uadui na Mke wangu” Alisema

“Si Brahama….” Alisema Mama Robson akafuta chozi akamwambia Robson
 
Ilipoishia “

Robson alijawa na mshangao kumsikia Mama yake akisema kuwa anamjuwa aliyemuuwa Sylvia, alishusha munkari kisha akamuuliza Mama yake kwa utaratibu sana

“Unamjuwa aliyempiga risasi Sylvia?”

“Ndiyo Namjuwa, Robson Naona aibu siku nikifa na siri hii ambayo inaweza kuleta taharuki kubwa kwako Mwanangu” Alisema kwa sauti iliyojaa kilio

“Nani aliyempiga risasi Mke wangu?” Aliuliza Robson

“Nakuomba Robson nikikutajia kaa chini ufikirie nini ufanye lakini usikurupuke na hasira utafanya maamuzi magumu, nakuomba weka Bastola chini” Alisema

“Mama huwezi kuniondoa katika njia yangu, najuwa aliyempiga risasi Sylvia ni Brahama sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mke wangu, hakuna Mwenye uadui na Mke wangu” Alisema

“Si Brahama….” Alisema Mama Robson akafuta chozi akamwambia Robson

Tuendelee:

SEHEMU YA KUMI -10 (SEHEMU YA MWISHO)


“Ni Baba yako…!!” Macho yalimtoka pima Robson, kusikia ni Baba yake kulizidi kumshangaza Robson

“Baba yangu?”

“Ndiyo Baba yako ndiye aliyesababisha kifo cha Mke wako na alifanya hivyo akiamini anakulinda wewe Robson” Alisema Mama yake, Robson alijikuta akikaa chini, nguvu zikamuisha, jinsiBaba yake aliavyokuwa mstari wa mbele kuhakikisha Sylivia anapatikana, alijiuliza ilikuwaje akamuuwa

“Robson! Baba yako aliona unateseka kwa ajili ya Sylvia akaona ni bora amuuwe ili upate kuwa salama, hakufanya kwa nia mbaya naomba unielewe”

“Kwahiyo Baba yangu ndiye aliyemuuwa Mke wangu, ndiye aliyenifanya namwaga chozi sasa hivi? Mama unajuwa nimeumia kiasi gani ndani ya moyo wangu? Furaha yangu imetoweka, nina thamani gani Mimi?” Aliuliza Robson.

“Thamani unayo Mwanangu, hebu tuifiche hii siri ili Baba yako awe salama” Alisema Mama Robson, kadiri alivyomuona Robson aliona ni wazi alikuwa amepowa sakafuni, akamsogelea akamwambia

“Sahau yote, muache yule Kijana aubebe mzigo wote ili Baba yako abakie kuwa salama” Aliongezea Mama Robson

“Vipi familia ya Brahama, umeifikiria? wakati unataka Baba awe salama umepima ni maumivu kiasi gani anayasikia Brahama? atafungwa kifungo cha Maisha kwa kosa ambalo hakutenda, siwezi kuendelea kuitazama Dunia ambayo kila kitu kimebadilika” AliSema Robson kisha akasimama kama mzimu.

Akamnyooshea Bastola Mama yake, akamuamrisha atulie kisha akamfungia ndani ya chumba hicho, akakimbilia nje akaingia kwenye gari akaondoka

Mama Robson alihangaika sana pale chumbani lakini hakuweza kufanikiwa kufungua, akaitafuta simu yake ili amwambie Mume wake kuwa Robson ameujuwa ukweli lakini bahati mbaya simu aliiacha jikoni. Brahama alikanyaga Mafuta kuelekea ofisini kwa Baba yake

Akaiacha gari nje ya ofisi akaingia haraka na kumkuta Baba yake akiwa anazunguka katika kiti, akashtuka kumwona Robson

“Robson kuna nini?” aliuliza Baba Robson

“Sylvia amekufa” Alijibu Robson

“Masikini pole sana Kijana wangu, sasa kwanini Mungu ameamua kukupa adhabu kali namna hii?” alisema Baba yake Robson, lakini akaiona Bastola kwenye kiuno cha Robson akajuwa tu Robson ameshajuwa kuwa yeye ndiye aliyempiga risasi Sylvia, akaitumia njia ya Kijeshi kutaka kuichukua Bastola kwa Robson, akawa anamsogelea taratibu huku akimsemesha Robson akashtuka lakini Baba yake alikuwa ameshamfikia lakini kabla hajachukua Bastola Robson aliiwahi akamnyooshea Baba yake

“Kwanini Umemuuwa Sylvia?” aliuliza Robson, Baba yake akaanza kutetemeka huku akisema

“Robson nimefanya kwa ajili ya kukuweka salama, nakuomba Mwanangu weka Bastola pembeni tuongee sisi ni familia moja”

Alisema Baba Robson akiwa anajaribu kusogea tena ili aichukue Bastola, Robson hakutaka maswali wala majibu kutoka kwa Baba yake

Akamtungua Baba yake Risasi ya kichwa, Baba yake akaangukia mezani kisha chini, harakaa Robson akakimbia, akaingia kwenye gari, akaondoa gari kwa kasi sana ili aondoke hapo lakini haraka yake haikuwa na Baraka, wakati anaingia Barabarani akakutana na roli lililobeba simenti, akagongwa ubavu ambao alikuwepo. Robson alifia pale pale.

Vilio vikatanda kwenye familia mbili ambazo ziliwapoteza wapendwa wao, Sylvia, Robson na Baba Robson wakazikwa siku iliyofuata. Mama Robson akasimama kizimbani kutoa ushahidi, Brahama akaachiwa kwasababu hakuwa na kesi ya kujibu.

MWISHO
 
Ilipoishia “

Robson alijawa na mshangao kumsikia Mama yake akisema kuwa anamjuwa aliyemuuwa Sylvia, alishusha munkari kisha akamuuliza Mama yake kwa utaratibu sana

“Unamjuwa aliyempiga risasi Sylvia?”

“Ndiyo Namjuwa, Robson Naona aibu siku nikifa na siri hii ambayo inaweza kuleta taharuki kubwa kwako Mwanangu” Alisema kwa sauti iliyojaa kilio

“Nani aliyempiga risasi Mke wangu?” Aliuliza Robson

“Nakuomba Robson nikikutajia kaa chini ufikirie nini ufanye lakini usikurupuke na hasira utafanya maamuzi magumu, nakuomba weka Bastola chini” Alisema

“Mama huwezi kuniondoa katika njia yangu, najuwa aliyempiga risasi Sylvia ni Brahama sababu yeye ndiye aliyekuwa na Mke wangu, hakuna Mwenye uadui na Mke wangu” Alisema

“Si Brahama….” Alisema Mama Robson akafuta chozi akamwambia Robson

Tuendelee:

SEHEMU YA KUMI -10 (SEHEMU YA MWISHO)


“Ni Baba yako…!!” Macho yalimtoka pima Robson, kusikia ni Baba yake kulizidi kumshangaza Robson

“Baba yangu?”

“Ndiyo Baba yako ndiye aliyesababisha kifo cha Mke wako na alifanya hivyo akiamini anakulinda wewe Robson” Alisema Mama yake, Robson alijikuta akikaa chini, nguvu zikamuisha, jinsiBaba yake aliavyokuwa mstari wa mbele kuhakikisha Sylivia anapatikana, alijiuliza ilikuwaje akamuuwa

“Robson! Baba yako aliona unateseka kwa ajili ya Sylvia akaona ni bora amuuwe ili upate kuwa salama, hakufanya kwa nia mbaya naomba unielewe”

“Kwahiyo Baba yangu ndiye aliyemuuwa Mke wangu, ndiye aliyenifanya namwaga chozi sasa hivi? Mama unajuwa nimeumia kiasi gani ndani ya moyo wangu? Furaha yangu imetoweka, nina thamani gani Mimi?” Aliuliza Robson.

“Thamani unayo Mwanangu, hebu tuifiche hii siri ili Baba yako awe salama” Alisema Mama Robson, kadiri alivyomuona Robson aliona ni wazi alikuwa amepowa sakafuni, akamsogelea akamwambia

“Sahau yote, muache yule Kijana aubebe mzigo wote ili Baba yako abakie kuwa salama” Aliongezea Mama Robson

“Vipi familia ya Brahama, umeifikiria? wakati unataka Baba awe salama umepima ni maumivu kiasi gani anayasikia Brahama? atafungwa kifungo cha Maisha kwa kosa ambalo hakutenda, siwezi kuendelea kuitazama Dunia ambayo kila kitu kimebadilika” AliSema Robson kisha akasimama kama mzimu.

Akamnyooshea Bastola Mama yake, akamuamrisha atulie kisha akamfungia ndani ya chumba hicho, akakimbilia nje akaingia kwenye gari akaondoka

Mama Robson alihangaika sana pale chumbani lakini hakuweza kufanikiwa kufungua, akaitafuta simu yake ili amwambie Mume wake kuwa Robson ameujuwa ukweli lakini bahati mbaya simu aliiacha jikoni. Brahama alikanyaga Mafuta kuelekea ofisini kwa Baba yake

Akaiacha gari nje ya ofisi akaingia haraka na kumkuta Baba yake akiwa anazunguka katika kiti, akashtuka kumwona Robson

“Robson kuna nini?” aliuliza Baba Robson

“Sylvia amekufa” Alijibu Robson

“Masikini pole sana Kijana wangu, sasa kwanini Mungu ameamua kukupa adhabu kali namna hii?” alisema Baba yake Robson, lakini akaiona Bastola kwenye kiuno cha Robson akajuwa tu Robson ameshajuwa kuwa yeye ndiye aliyempiga risasi Sylvia, akaitumia njia ya Kijeshi kutaka kuichukua Bastola kwa Robson, akawa anamsogelea taratibu huku akimsemesha Robson akashtuka lakini Baba yake alikuwa ameshamfikia lakini kabla hajachukua Bastola Robson aliiwahi akamnyooshea Baba yake

“Kwanini Umemuuwa Sylvia?” aliuliza Robson, Baba yake akaanza kutetemeka huku akisema

“Robson nimefanya kwa ajili ya kukuweka salama, nakuomba Mwanangu weka Bastola pembeni tuongee sisi ni familia moja”

Alisema Baba Robson akiwa anajaribu kusogea tena ili aichukue Bastola, Robson hakutaka maswali wala majibu kutoka kwa Baba yake

Akamtungua Baba yake Risasi ya kichwa, Baba yake akaangukia mezani kisha chini, harakaa Robson akakimbia, akaingia kwenye gari, akaondoa gari kwa kasi sana ili aondoke hapo lakini haraka yake haikuwa na Baraka, wakati anaingia Barabarani akakutana na roli lililobeba simenti, akagongwa ubavu ambao alikuwepo. Robson alifia pale pale.

Vilio vikatanda kwenye familia mbili ambazo ziliwapoteza wapendwa wao, Sylvia, Robson na Baba Robson wakazikwa siku iliyofuata. Mama Robson akasimama kizimbani kutoa ushahidi, Brahama akaachiwa kwasababu hakuwa na kesi ya kujibu.

MWISHO
Asantee mkuu
 
Aseeeeh tisha sana mkuu japo uyo mama robson kazingua sanaaa kwan angekaa kmy angepungukiw nn qmmk
 
Aseeeh tisha sana mkuu asante, sema uyo mama kazingua asa angekaa kmy angepungukiw nn ameniudhi kwelikweli qmmk
 
Back
Top Bottom