mwanyaluke
JF-Expert Member
- Jan 22, 2015
- 704
- 2,435
Naandika hili hapa kwa moyo mkujufu, sina kinyongo na wala sijutii ila namhurumia sana.
Mwaka 2015 ilikuwa ni first appoitment yangu as mwalimu, nilimkuta huyu binti akiwa kidato cha tatu, baada ya miezi mitatu niligundua ni mtoto mwenye uwezo wa juu darasani.
Baadae nikaja kufahamu kama ni mtoto wa mazingira magumu, baba yake alifariki na mama yake yupo anaishi mazingira magumu sana na yupo Tabora kwao. So kwa kuzingatia uwezo wake na kukutana na bibi yake niliamua kumsaidia suala la shule as mdogo wangu na itabaki kuwa hivyo milele, i rate her as my young sister.
Mungu si Athuman form four alifaulu vizuri, nilifanya mchakato wa kumfanya achuguliwe shule za jirani na combination iwe PCB, nashukuru alichaguliwa shule na comb. hiyo, so nikawa namhudumia kama mdogo wangu na nilimshukuru Mungu kuwa umenipatia mtu ambaye ananipa experience ya kusomesha.
Na hata form six alifaulu bahati mbaya hakuchagulia course za afya, so ilibidi nikae nae tutafte course ambayo itampa ajira na akikosa ajira iwe rahisi kujishikiza, na ikawa hivyo.
Alichaguliwa chuo na akapata course ambayo tulitarget, alipokuwa chuo niliendelea kutake care asilimia zinaboki za bodi ya mikopo na kumpatia fedha za matumizi kama mtoto wa kike tena mwanachuo (nilifanya hivyo kwa moyo mkujufu as namsaidia mdogo wangu).
Alipokuwa chuo mwaka wa mwisho kabla ya semister ya pili alikuja rafiki yangu na kuniambia amekutana na mdogo wangu huyo na binti mmoja msagaji, tena kamuliza yule msagaji na msagaji kakili kuwa yule binti ni msagaji na ukizingatia ni tom boy ilinichanganya sana.
Sikuona shida nilimpigia kumuliza hilo na kweli kuwa hayupo chuo yupo mtaani, akajibu kuwa ni kweli yupo mtaani kuna likizo fupi na yeye sio msagaji wanamsema vibaya kwa sababu ya muenekano wake wa u Tom boy (nakumbuka hiyo simu ilikuwa ya mwisho kuonanana naye wala kuwasiliana, kila nikipiga simu hapokei na akipokea haongei.
Kinachoniuma ni pale nilipopiga hesabu kuwa amemaliza chuo na sasa yupo mtaani (hata kunijulisha nimemaliza chuo hakufanya hivyo, I said ni utoto unamsumbua), badaye niliamua kumtaftia kazi baada ya kumpigia na kuona hapokei niliamua kutuma sms hakujibu, na kila nikimuona yupo mtandaoni na anarusha video zake akicheza music.
Namhurumia kwa sababu sioni future kwa anachokifanya ila ndio hivyo sina njisi ya kukaa naye, najiwazia sasa kama ningesomesha mwanamke kwa hoja ya mapenzi ingekuwaje, si ningepanic mimi? All in all nashukuru Mungu atakachonipa kama kinaweza kugawanywa na kuwafikia wengine i will do it, sijakata tamaa.
Mwaka 2015 ilikuwa ni first appoitment yangu as mwalimu, nilimkuta huyu binti akiwa kidato cha tatu, baada ya miezi mitatu niligundua ni mtoto mwenye uwezo wa juu darasani.
Baadae nikaja kufahamu kama ni mtoto wa mazingira magumu, baba yake alifariki na mama yake yupo anaishi mazingira magumu sana na yupo Tabora kwao. So kwa kuzingatia uwezo wake na kukutana na bibi yake niliamua kumsaidia suala la shule as mdogo wangu na itabaki kuwa hivyo milele, i rate her as my young sister.
Mungu si Athuman form four alifaulu vizuri, nilifanya mchakato wa kumfanya achuguliwe shule za jirani na combination iwe PCB, nashukuru alichaguliwa shule na comb. hiyo, so nikawa namhudumia kama mdogo wangu na nilimshukuru Mungu kuwa umenipatia mtu ambaye ananipa experience ya kusomesha.
Na hata form six alifaulu bahati mbaya hakuchagulia course za afya, so ilibidi nikae nae tutafte course ambayo itampa ajira na akikosa ajira iwe rahisi kujishikiza, na ikawa hivyo.
Alichaguliwa chuo na akapata course ambayo tulitarget, alipokuwa chuo niliendelea kutake care asilimia zinaboki za bodi ya mikopo na kumpatia fedha za matumizi kama mtoto wa kike tena mwanachuo (nilifanya hivyo kwa moyo mkujufu as namsaidia mdogo wangu).
Alipokuwa chuo mwaka wa mwisho kabla ya semister ya pili alikuja rafiki yangu na kuniambia amekutana na mdogo wangu huyo na binti mmoja msagaji, tena kamuliza yule msagaji na msagaji kakili kuwa yule binti ni msagaji na ukizingatia ni tom boy ilinichanganya sana.
Sikuona shida nilimpigia kumuliza hilo na kweli kuwa hayupo chuo yupo mtaani, akajibu kuwa ni kweli yupo mtaani kuna likizo fupi na yeye sio msagaji wanamsema vibaya kwa sababu ya muenekano wake wa u Tom boy (nakumbuka hiyo simu ilikuwa ya mwisho kuonanana naye wala kuwasiliana, kila nikipiga simu hapokei na akipokea haongei.
Kinachoniuma ni pale nilipopiga hesabu kuwa amemaliza chuo na sasa yupo mtaani (hata kunijulisha nimemaliza chuo hakufanya hivyo, I said ni utoto unamsumbua), badaye niliamua kumtaftia kazi baada ya kumpigia na kuona hapokei niliamua kutuma sms hakujibu, na kila nikimuona yupo mtandaoni na anarusha video zake akicheza music.
Namhurumia kwa sababu sioni future kwa anachokifanya ila ndio hivyo sina njisi ya kukaa naye, najiwazia sasa kama ningesomesha mwanamke kwa hoja ya mapenzi ingekuwaje, si ningepanic mimi? All in all nashukuru Mungu atakachonipa kama kinaweza kugawanywa na kuwafikia wengine i will do it, sijakata tamaa.