Nilimsomesha binti akaishia kuwa mcheza show

Nilimsomesha binti akaishia kuwa mcheza show

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Naandika hili hapa kwa moyo mkujufu, sina kinyongo na wala sijutii ila namhurumia sana.

Mwaka 2015 ilikuwa ni first appoitment yangu as mwalimu, nilimkuta huyu binti akiwa kidato cha tatu, baada ya miezi mitatu niligundua ni mtoto mwenye uwezo wa juu darasani.

Baadae nikaja kufahamu kama ni mtoto wa mazingira magumu, baba yake alifariki na mama yake yupo anaishi mazingira magumu sana na yupo Tabora kwao. So kwa kuzingatia uwezo wake na kukutana na bibi yake niliamua kumsaidia suala la shule as mdogo wangu na itabaki kuwa hivyo milele, i rate her as my young sister.

Mungu si Athuman form four alifaulu vizuri, nilifanya mchakato wa kumfanya achuguliwe shule za jirani na combination iwe PCB, nashukuru alichaguliwa shule na comb. hiyo, so nikawa namhudumia kama mdogo wangu na nilimshukuru Mungu kuwa umenipatia mtu ambaye ananipa experience ya kusomesha.

Na hata form six alifaulu bahati mbaya hakuchagulia course za afya, so ilibidi nikae nae tutafte course ambayo itampa ajira na akikosa ajira iwe rahisi kujishikiza, na ikawa hivyo.

Alichaguliwa chuo na akapata course ambayo tulitarget, alipokuwa chuo niliendelea kutake care asilimia zinaboki za bodi ya mikopo na kumpatia fedha za matumizi kama mtoto wa kike tena mwanachuo (nilifanya hivyo kwa moyo mkujufu as namsaidia mdogo wangu).

Alipokuwa chuo mwaka wa mwisho kabla ya semister ya pili alikuja rafiki yangu na kuniambia amekutana na mdogo wangu huyo na binti mmoja msagaji, tena kamuliza yule msagaji na msagaji kakili kuwa yule binti ni msagaji na ukizingatia ni tom boy ilinichanganya sana.

Sikuona shida nilimpigia kumuliza hilo na kweli kuwa hayupo chuo yupo mtaani, akajibu kuwa ni kweli yupo mtaani kuna likizo fupi na yeye sio msagaji wanamsema vibaya kwa sababu ya muenekano wake wa u Tom boy (nakumbuka hiyo simu ilikuwa ya mwisho kuonanana naye wala kuwasiliana, kila nikipiga simu hapokei na akipokea haongei.

Kinachoniuma ni pale nilipopiga hesabu kuwa amemaliza chuo na sasa yupo mtaani (hata kunijulisha nimemaliza chuo hakufanya hivyo, I said ni utoto unamsumbua), badaye niliamua kumtaftia kazi baada ya kumpigia na kuona hapokei niliamua kutuma sms hakujibu, na kila nikimuona yupo mtandaoni na anarusha video zake akicheza music.

Namhurumia kwa sababu sioni future kwa anachokifanya ila ndio hivyo sina njisi ya kukaa naye, najiwazia sasa kama ningesomesha mwanamke kwa hoja ya mapenzi ingekuwaje, si ningepanic mimi? All in all nashukuru Mungu atakachonipa kama kinaweza kugawanywa na kuwafikia wengine i will do it, sijakata tamaa.
 
na hata form six alifaulu baahti mbaya hakuchagulia chuo degree, so ilobidi nikae nae tutafte course ambayo itampa ajira ama rahisi kujishikiza ,na ikawa hivyo , alichaguliwa chuo na akapata course ambayo tulitarget, alipokuwa chuo niliendelea kutake care asilimia zinaboka za bodi ya mikopo na kumpatia fedha za matumizi kama mtoto wa kike ten mwanachuo,
Kama hakuchaguliwa chuo degree alipataje mkopo?
 
nandika hili hapa kwa moyo mkujufu, sina kinyongo na wala sijutii ila namhurumia sana

Mwaka 2015 ilikuwa ni first appoitment yangu as mwalimu ,nilimkuta huyu binti akiwa kidato cha tatu, baad ya miezi mitatu niligundua ni mtoto mwenye uwezo wa juu darasani,...
Hamna anae saidia bila lengo, wewe lengo lako lilikua lipi? Wewe sio serikali
 
Hivi uwongo unawasaidia nini, nani anawalipa? Peleka haya mauwongo yako kwenye majukwaa ya kipuuzi. Mara nilifanya mchakato wa kumfanya achaguliwe shule za jirani.

Hapo yu ni uwongo, we ulikuwepo wakati wizara inawapngia shule za kwenda A level? Yote umeandika hayana mantiki, upoyoyo tu.
 
Sema ukweli hakuna vitisho ulimpa ulivyompigia simu baada ya kuambiwa ni msagaji?

Anyway, achana nae hana shukurani kuna watu ukiwafanyia roho nzuri wao huigeuza na kukuona wewe ni Zuzu,
Waliosema Umaskini ni Laana hawajakosea.
fair nilimhoji kwa ukali but sio kwa vitisho
 
Hivi uwongo unawasaidia nini, nani anawalipa? Peleka haya mauwongo yako kwenye majukwaa ya kipuuzi. Mara nilifanya mchakato wa kumfanya achaguliwe shule za jirani. Hapo yu ni uwongo, we ulikuwepo wakati wizara inawapngia shule za kwenda A level? Yote umeandika hayana mantiki, upoyoyo tu.
acha ujinga mwanafunzi akifaulu,mwalimu wa taluuma anakaa na kuwajazia wanafunzi combination zilizo balansi na shule wanazotaka, then majina yanatumwa wizari kuthibitisha, kuna kuwa na changes ndogo sana wizara kukupangia shule ambayo haikujazwa na masomo ambayo hukuchaguwa , muwe mnafaulu shule ili muwe na nafasi ya kujua vitu vidogo, sio kila ni kila kitu uwongo, nidanganye kwa gain ipi mzee
 
MUNGU si athuman form four alifaulu vizuri nilifanya mchakato wa kumfanya achuguliwe shule za jirani na combination iwe PCB,Kumbe unaweza kufanya mchakato wa kumfanya mtu achaguliwe shule za jirani na Combination pia.
 
Pole sana vyuoni kuna changamoto mnoo!!!huyo mtoto hajitambui km ni maskini
Mungu ampe ufahamu mapema
ni familia ya kimaskini sanaaa , huyo bibi aliyekuwa anamlea anasema since amemaliza chuo naye hajawahi pigiwa simu na huyo binti,
MUNGU si athuman form four alifaulu vizuri nilifanya mchakato wa kumfanya achuguliwe shule za jirani na combination iwe PCB,Kumbe unaweza kufanya mchakato wa kumfanya mtu achaguliwe shule za jirani na Combination pia.
mpigie mwalimu wa taluma wa shule yoyote ili akueleze mchakato upoje mwanafunzi akifaulu ili achuguliwe combi flan na shule flan
 
acha ujinga mwanafunzi akifaulu,mwalimu wa taluuma anakaa na kuwajazia wanafunzi combination zilizo balansi na shule wanazotaka , then majina yanatumwa wizari kuthibitisha , kuna kuwa na changes ndogo sana wizara kukupangia shule ambayo haikujazwa na masomo ambayo hukuchaguwa , muwe mnafaulu shule ili muwe na nafasi ya kujua vitu vidogo, sio kila ni kila kitu uwongo, nidanganye kwa gain ipi mzee
Nimekuuliza hujajibu...Kama hakuchaguliwa chuo degree alipataje mkopo?
 
expand...Kama hakuchaguliwa chuo degree alipataje mkopo?
Soma upya nilisema hakuchaguliwa cousre za afya na sikuwa na ujanja wa kumpeleka private asome afya kwa sababu ya kipato changu kipindi hicho, nilichokuwa nawez kuaford ni vyuo vya serikali na cutting point kwa vyuo vya serikali kwa course za afya ni kubwa
 
Back
Top Bottom