Uchaguzi 2020 Nilishawaambia muengueni Tundu Lissu, hamkusikia. Oneni!

Uchaguzi 2020 Nilishawaambia muengueni Tundu Lissu, hamkusikia. Oneni!

Je hatuwezi kuandaa mpango wa kuifanya Zanzibar kuwa sehemu ya Mkoa wa nchi hii. Kiukweli mimi sio muumini wa kuiondoa Zanzibar, tena nilikuwa naiwazia Burundi na Rwanda(utaona naota)
Kama mtachagua upinzani kodi zenu nitazikusanya kwa nguvu ila barabara siwajengei ng'o! Zanzibar kama wana akili si heri wajinasue mapema, kuliko huu upumbavu wetu huku bara!
 
Haya yote- Muulize Warioba na tume yake-
Kumbuka kwamba Hata wakijiondoa kwenye Muungani bado ni ndugu zetu.
Ndoa sio Ndoana , samaki akimeza hatemi...

Bado tunaweza kuuvunja na tukabki wamoja kama nchi zote ulimwenguni zinazofanya
Mfano:
UK na EU
Czechia na Slovakia
na nyingine zote...

Baba na mama wanaweza kutengana na kupeana talaka na watoto wakabaki bila kuwa na upande...
ukijua hivyo , edit bandiko lako...
 
Hivi wanzanzibar hawataki muungano mbona mnawalazimishia muungano? Kuna nini nyuma yake?
 
Mleta mada unapaswa kutambua haya kuhusu Zanzibar.
-Muungano ni jambo la hiari, hivyo wazanzibar hatupaswi kulazimishwa kuwepo kwenye muungano huu.

-Zanzibar ilikuwa ni taifa huru kabla ya muungano, hivyo muungano hauna haki ya kupora uhuru wa Zanzibar.

-Malengo ya muungano yalikuwa ni kushirikiana na sio nchi moja kuitawala nchi nyingine na wala sio muungano kuimeza Zanzibar.

-Muungano ni jambo la ziada tu kwa mzanzibar, maisha ya mzanzibar hayategemei uwepo wa huu muungano.

-Muungano kwa mzanzibar ni kama koti tu, ambalo ukilichoka unaweza kulivua mara moja. Zanzibar kwanza muungano baadaye.
 
Alichokisema Lissu nikuwa kwa Zanzibar achaguliwe Maalim Seif na kwa Rais wa muungano kichaguliwe chama chenye nguvu ya kuiondoa CCM madarakani.. na kwa pamoja wanzanzibar wameitikia kuwa ni CHADEMA.
 
Ameigawaje ??? Yeye kasema Anamuunga Maalim ashinde...nao wamuunge ashinde.

Baada ya hapo wakae waangalie aina ya muungano wenye faida .
 
binafsi nimekuelewa sana,huyu jamaa kuna kitu anataka.
 
Kura yangu nilimpa 2015 hiyo imenitesa mpaka saizi nirudie tena kosa ? Noooooo bora nife nitoweke kwenye sura ya dunia Ila siwezi rudia kosa wanao neemeka ni ccm peke yao wananchi wa kawaida sisi tumesahaulika nooo kura yangu bora iende upinzani tu hakuna namna
Usisahau Ibara ya 41 kifungu kidogo cha 7 kwenye katiba ya JMT
 
Unataka asipotangazwa awachekee? Acha awakazie mmezidi wizi
Umegundua mabango ya ccm hayasemi chagua ccm bali yanasema chagua magufuli.
Nahisi kuna chama kipya cha siasa kinaitwa magufuli
 
We kiazi sana yaani unalazimisha imani uliyorithishwa ndiyo uwe ukweli.
Tuambie Tanzania ilitokana na muungano wa nchi mbili ni ipi na ipi?
Hil neno "kiazi" huwa linachekesha sana anapo batizwa mtu na akil zake 😂😂😂. Ni kama dharau flan hiv .
 
Mtu anasema asipotangazwa mshindi safari anakinukisha.

Nashangaa hata Magufuli wanayesema ana roho mbaya anamuacha anaongea pumba, ningekuwa mimi saa hizi angekuwa jela kwa matamshi ya kichochezi.
Risasi 16,hiyo ndo karma.ccm oyee
 
Sorry to say weye ni kiazi mbatata maana hujuwi how system work and react. Nyie ndio mmemshauri vibaya mkuu na uwenda mmetufikisha hapa. Kaa kimya wenye akili wafanye kazi. Znz sio Leo wala Jana kuna upinzani na wanajuwa nn Lisu? Usilolijuwa usiku wa kiza.
 
Siamini kama TL anaweza kuwa rafiki matope kiasi hiki. Kosa la TL kuunga mkono katiba ya Warioba ya serikali 3 ambayo ni mapendekezo ya wananchi?
 
Zanzibar ilikuwa nchi kabla ya 1964 na Muungano tuliokuwa nao ni "marriage of convenience" kwa wakati ule kwenye kipindi cha vita baridi (NATO/ Warsaw Pact).
Ni USA kupitia kachero wao Frank Carlucci aliyekuwa Balozi wao Tanganyika kisha Congo na baadaye akaja kuwa CEO wa CIA. Huyu Carlucci alianza kumshawishi kwanza Jomo Kenyatta kutaka kuiunganisha Zanzibar na Kenya. Jomo Kenyyatta atakataa ndipo akamu approach J K Nyerere ambaye alikubali.

Nyerere aliweka muundo wa Serikali 2 ili kutoimeza Zanzibar kama nchi. Alikataa kabisa kuifanya Zanzibar kuwa Mkoa. Hata hivyo vita baridi ilikwisha mwaka 1989 baada ya kuanguka ukuta wa Berlin. Ushahidi upo kwenye Rasimu ya Katiba ya Warioba uliotaka Serikali 3.

Yeyote anayetaka ridhaaa ya kura za Wazanzibari lazima aongelee "sovereignty ya Zanzibar" as a country.

Zanzibar ilikuwa tajiri sana kuliko Oman kabla ya mwaka 1960 na ndiyo sababu Sultan Seyyid Said alihamisha Makao makuu ya Sultanate of Oman kwenda Zanzibar mmamo 1840. Mwaka 1960 kwa mfano Zanzibar ilikuwa na kilometres 22 za barabara ya lami wakati Oman ilikuwa haina. Leo hii Oman ni nchi tajiri sana baada ya kugundua raslimali za mafuta mpaka imekuwa nchi mfadhili.

Mimi ni Mtanganyika naamini kuwa muda wa kuendelea kuishikilia Zanzibar umekwisha. Tuwaache wapate maendeleo kipitia OIC na waanzishe bandari huru kama ulivyo Singapore au Dubai.
 
Mimi sijawahi kumdhulumu Mtu Mkuu.

Kuhusu Ajira, nimeshamwambia Magufuli sitamchagua hata alie, kama hanipi kula kwa nini nimpe kura. Aniombe nimuajiri alafu yeye hata kuniajiri. Nilishamuandikia.

Mimi sina ufuasi wa kipuuzi
Ongeza sauti[emoji441][emoji441]
 
Back
Top Bottom