Kwa muonekano wa macho ungeweza kudhani vipo karibu (kama mita moja tu!). Ukweli ni kwamba ile ni sayari ya Venus (Zuhura) ambayo ni sayari ya pili toka kwa Jua (Solar). Ikumbukwe pia mwezi upo karbu zaidi ya Dunia kuliko sayari hiyo. Kilichotokea ni kwamba Dunia na Venus vilikuwa katika mfungamano/mfuatano (planetary alignment); na kwa vile mwezi huwa unaizunguka Dunia, nao ukajikuta katika mfuatano huo. Hii ilidumu saa kadhaa na baadaye vikaachana!
Aidha inatarajiwa tarehe 25 January, sayari sita zitakuwa katika mfuatano huo na katika hizo nne zitaweza kuonekana dhahiri; hizo ni Venus, Mars, Jupiter na Saturn.