Nilitaka kumuoa binti wa Dini tofauti na yangu vita kubwa ikaibuka. Kuna kitu gani kati ya hizi dini mbili?

Mkuu hizi dini zote zimemwaga damu za watu wasotajika idadi, ni vile hatuelezwi yaliyokuwa yakitokea hapo zamani tu.

Na sasa Uislamu sababu ni contemporary basi unapata attention yote ila kuna mishenzi iliua watu kifala ikatumia Ukristo manina zao kama ilivyo mishenzi ya sasa inayotumia Uislamu.
 
Binafc ninaamin kwe iman yangu kuoa au kuolew nje ya iman nyngne unaleta matatz. Kwe ndoa
 
Hapana, hauko sahihi kabisa.
Falsafa ya imani ya kiislamu ni tofauti kabisa na falsafa ya imani ya kikristo. Nitafafanua hapa kwa kifupi.

Waislamu na wakristo kusema wanaamini Mungu mmoja haina maana kuwa wanaamini katika Mungu yule yule. Mimi ninaweza kuwa ninaamini mungu mmoja ambaye ni mbuzi, na wewe unaamini mungu mmoja ambaye ni ng'ombe, je tunaamini mungu yule yule?

Kuhusu Ibrahimu, wakristo wanaamini katika Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo, Mungu huyo ambaye alimtoa Yesu afe msalabani kwa ajili ya dhambi za ulimwengu na kisha kumfufua siku ya tatu na kisha kupaa mbinguni. Habari za Mungu huyo wanazisoma kupitia Biblia. Wakati waislamu wanaamini katika Mungu wa Ibrahim na Ishimaili, ambaye alimpa utume Mohammad ili watu wamfuate, na habari za Mungu huyo wanazisoma kupitia Quran na hadithi za mtume.

MY TAKE
1. Mungu anayeaminiwa na wakristo ni tofauti na Mungu anayeaminiwa na waislamu.

2. Ibrahimu anayeaminiwa na wakristo habari zake ziko kwenye Biblia, na Ibrahimu anayeaminiwa na waislamu habari zake ziko kwenye Quran na hadithi za mtume, ni watu wawili tofauti ukiwasoma kiundani.

3. Misingi ya dini ya Kikristo (inayosimamia katika Yesu) ni tofauti kabisa na misingi ya kiislamu (inayosimama katika Mohammed). Yesu na Mohammad hawafanani na wala hawaelewani, mmoja anabeba sifa za uungu (Yesu) na mwingine anabeba sifa za utume (Muhammad) kwa mujibu wa imani husika.
 
Wacha ubishi, Allah na Yehova ni Miungu tofauti. Allah alihubiriwa na Mudi wakati Yehova alihubiriwa na Abra na Yesu. Kuna miungu mingi sana sheikh wangu wakiwemo Miungu ya wabudha na wahindu, Wewe baki na Mungu wako kama anakusaidia ila usilazimishe Alla wako ni sawa Budha au Yehova wa watu wengine, Sisi wabantu Mungu wetu anaishi kwenye milima, makaburini, mapangoni au kwenye miti mikubwa, tuache kama tulivyo,
 
kumbe ni wewe hadi huku upo. ww ulitaka umuoe au umchezee mdogo wangu[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Wewe Sema unapenda vishungi usiwasingizie wanaume wenzio.
 
Upendo, utii, nidhamu na uchaji Mungu
Haya mambo hakuna asiye yajua.

Kibaya ni vile mnayahubiri lakini ninyi we nyewe hamyaishi.

Kwenye ndoa zenu ni vurugu kila siku. Usaliti, dharau, kiburi,

Maisha ya kawaida mmejaa unafiki, uchawi, rushwa..hamana hata chembe ya upendo.. ila mnajificha kwenye kivuli cha dini.

Nakataa mwafrika na dini ni unafiki tu. .. Acheni watoto waoane kama wamependana .

...
 
Wewe Sema unapenda vishungi usiwasingizie wanaume wenzio.
Hapana siwasingizii ebu fungua uzi wa namba hii uone kura zitaenda wapi utaona kabisa wanawake wakislamu watapata kura nyingi na ukizingatia hizo kura utakuta zinatoka kwa Wanaume wakikristo hata tukiwa kwenye vikao vyetu vya Wanaume unakuta hili halikwepeki kwenye mjadala na unaona Watu waliopitia kwenye hiyo situation wanatoa ushuhuda wao
 
Tukio kama hili lilishamtokea Kaka yangu. Yeye alipendana sana na Binti ambaye ni Muislam, tena Baba yake ni Shehe kabisa. Bro aivyoenda kujitambulisha aliambiwa labda abadili Dini ndio itawezekana. Vinginevyo hawezi kupata mke pale.

Kwa kuwa walikuwa wanapendana basi Binti akashika ujauzito wa Bro. Wazazi wa Binti walivyogundua tu, walimfukuza kwao na wakawa wamempiga marufuku asirudi tena kwao na hata ndugu zake wengi nao ni kama vile nao walimtenga.

Bro aliamua kuishi tu na yule Mke wake bila kupata baraka za wazazi wa Binti. Walikuwa wakiishi vizuri tu na walibahatika kupata watoto wawili hadi mwaka jana Mke wa Bro alipopata ajali ya Gali kisha kufariki.

Wazazi wa Binti bado waligoma kuupokea mwili wa Binti yao hata alipofariki hata kwenye mazishi hawakuja. Bint alizikwa Kiislam kwa msaada wa majirani na waislam wenzake na sisi ndugu wa mwanaume.

(Rest In Peace Shem wangu, ulikuwa na upendo wa kweli, mcheshi na uliwahi kunijuza kuwa hukupenda kuwa kwenye ndoa za wake wengi kama ilivyokuwa kwa Baba yako, kuna vitu uliviona na ukavichukia).

Tukio hili la Bro lilinifanya nijifunze kitu, kila ninapopata Dem wa dini Tofauti na yangu najikuta nalikumbuka hili tukio.
 
Ingekuwa hivyo walioa waislamu ndoa zisingevunjika
 
Dah umenikumbusha kaka yangu alipomfata ex wangu eti niachane nae kisa ni dini tofauti tena alimfata na panga hiki kisa natamani niazishie uzi yale mahusiano nilipigwa mikanda sana home😬
Hebu leta kisa hicho huweza kikawa na mafundisho fulani
 
Mambo ya Imani magumu sana mkuuu...!! Unaweza kuishi maisha ya mawazo na utumwa hata ukipuuzia vipi bado kuna kitu kitakuwa hakipo sawaa
 
Unavyo kuwa mjinga, mimi najua mpaka babu yake babu yangu mimi alikuwa Muislamu. Kama nyinyi kwenu hamna elimu za nasabab zeni ni nyinyi, sisi tuko tofauti na nyiny
Mbona unapanic..
Hiyo siyo dini ya babu yako wala mama yako wala mjomba wako.
Dini yenyewe umeletewa mkuu no matter babu wa kizazi cha pili au vipi.

Binadamu anazaliwa hana dini na sio kila imani inafaa kwa watu wote.
 
Wanaume wakislamu wanamatatizo yao tungepewa hiyo nafasi sisi Wanaume wakikristo tungepunguza Hilo wimbi lakuachika shida Ndio hivyo Wazazi wao wanatubania kuwaoa watoto wao
Khaa..Una matatizo wewe tabia ya MTU Aina uhusiano na dini ndugu.
 
Nimewaza mengi mkuu..daah hizi dini hizi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…