Nilitaka kumuoa binti wa Dini tofauti na yangu vita kubwa ikaibuka. Kuna kitu gani kati ya hizi dini mbili?

Weeehhh!! Sasa si ubadili dini tu kaka, Wote tunamwabudu Mwenyezi Mungu na kikubwa amani ya moyo
 
Kama unampenda badili wewe dini.
 
Ukitaka kuharibu jamii basi ruhusu mahusiano ya kimapenzi baina ya imani mbili tofauti.

Ukiona mtu ana uhusiano wa kimapenzi na mtu wa imani nyingine huyo hajitambui au anajiendekeza. Huu ukweli mchungu.
 
Mimi nilibadili dini kitambo kidogo nikiwa na miaka 17 Ukristo kwenda Uislamu. Lakini nilichokiona huko ni tofauti kabisa na nilichokuwa naamini. Hizi dini zipo tu tuzifuate lakini siyo kila unachoambiwa ukichukulie kuwa ni kweli.
 
Dah umenikumbusha kaka yangu alipomfata ex wangu eti niachane nae kisa ni dini tofauti tena alimfata na panga hiki kisa natamani niazishie uzi yale mahusiano nilipigwa mikanda sana home😬
Sasa bibie ilikuwaje ukawa na mahusiano na mtu wa imani tofauti na yako ? Au ndiyo huwa mnasema Mapenzi ni upofu ?
 
Lakini zote zinatambulika kama Ibrahimism, zina vinasaba vya pamoja na ndio maana mitume karibu wote wanatajwa na vitabu vya dini hizi mbili kwa pamoja na matendo yale yale.
Hiyo siyo kweli hili jina wanalitumia kimakosa. Nabii Ibrahimu alikuwa Muislamu, Uyahudi na Ukristo ni Dini zilizo kuja kuzuliwa, ukiziangalia zote zimewakana mitume walio fata baadae.
 
Umeandika vya maana sana, ndiyo maana nasema watu wanajiendekeza na kuzembea.

Watu waende na watu wa imani zao, mbona wako wengi sana.
 
Ni hatari mimi marehemu baba alisema nikioa mwanamke wa kiislamu hatakaa aingie kwenye kizingiti cha mlango wake hata akiwa kaburini naogopa kweli kweli. ingawa nilipataga toto moja inajua kunidekeza hatari nikaona simfanyii poa nikamuacha nisimpotezee mda.Hizi dini bana.
 
Watoto zetu wa kike mna ujinga mwingi sana huwa mnaona hakuna maisha baada ya huba . Allah awasitiri na awape msimamo thabiti, kuna sehemu ulikosea bibie.
kila kitu ni mipango ya Mungu upendo sioni na siwezi kuushika ila nahisi upo kama imetokea nimependa sehemu nawezaje kujizuia maana kwa hakika hakitokei kitu bila Allah kubariki basi asingenipa upendo kwa Mwanaume dini tofauti hata hivyo tuliachana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…