#COVID19 Nilivyojisikia baada ya kuchanjwa chanjo ya COVID-19

#COVID19 Nilivyojisikia baada ya kuchanjwa chanjo ya COVID-19

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Nilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na wasiwasi kuhusu kuchanja chanjo ya covid 19. Hofu yangu kubwa kuliko zote ilikuwa kuganda kwa damu yangu baada ya kuchanja. Lakini Mimi ni miongoni mwa watu waliochanjwa chanjo ya COVID-19 Johnson And Johnson siku ya pili tu baada ya zoezi la kuchanja kuzinduliwa na Rais

Nilijisikia yafuatayo:
1. Nilichanjwa kwenye bega la kushoto, sehemu niliyochanjwa nijisikia maumivu ya sindano kwa siku kama 3 hivi

2. Baada ya kuchanjwa nilijisikia kama kichwa kizito kidogo kwa siku kama 3 hivi

3. Nilijisikia kutaka kupumzika nyumbani nisifanye kazi kwa siku kama tatu hivi

4. Sikutamani kufanya tendo la ndoa kwa siku kama 5 hivi

5. Baada ya wiki moja kupita nikarudi kwenye hali yangu ya kawaida na zaidi

6. Nilijisikia hamu zaidi ya kutaka kujamiiana baada ya wiki hivi

7. Nguvu za kiume ziliongezeka mara tatu zaidi

8. Nilitoa mbegu nyingi kuliko kawaida wakati wa kujamiiana

9. Nikajisikia mtu mwenye nguvu kuliko kabla ya chanjo.

10. Tangu nichanjwe sijawahi kupata kikohozi, mafua

11. Kama Koo likinikereketa ilikuwa lazima nimung'unye lozenges au nimeze antibiotics ili nipone lakini juzi koo linikereketa likatulia lenyewe bila kutumia dawa yoyote.

12. Umakini (concentration yangu na busara zangu nahisi kama vimeongezeka kuliko awali.

Nadhani chanjo Iko poa, unaweza kuja kujutia kama chanjo zitaisha bila wewe kuchanjwa. Maana kwenye foleni tulikuwa na watu raia wa Ulaya na Asia wanahitaji kuchanjwa.
 
Mkuu usitumie nguvu nyingi sana kuwaaminisha watu kuhusu usalama Wa chanjo.

Kumbuka hata mababu zetu walipoletewa ustaarabu wa kujenga vyoo na kujisaidia chooni,
vita vya kupinga kujisaidia chooni ilikuwa kubwa kuliko hili la wapinga chanjo.

Maana walishazowea kujisaidia vichakani.

Mimi nimechoma Pfizer, hadi muda huu nipo okay...

Na hakuna tatizo lolote.

Waache waendelee kupinga,
huku wakiumwa wanakimbilia hospital kwenye dawa za kizungu

Badala ya kwenda kwa mganga wa kienyeji kutibiwa.
 
Dah kuna maswali mengi kuliko majibu yenu mepesi
Hakuna maswali yeyote, kinachosumbuwa watu kwa sasa ni utandawazi.

Hivi zile chanjo za surua, ndui, nk Nini walijadiliana na nani zikaletwa huku Afrika? Au zikakubalika na wengine?

Si tumeletewa tu? Au kulikuwa na mjadala kama huu wa chanjo ya uviko?

Kuna yeyote aliyehoji usalama wa chanjo zile?
 
Hakuna maswali yeyote,kinachosumbuwa watu kwa sasa ni utandawazi.

Hivi zile chanjo za surua,ndui,nk Nini walijadiliana na nani zikaletwa huku Africa? Au zikakubalika na wengine?
Si tumeletewa tu? Au kulikuwa na.mjadala kama huu wa chanjo ya uvico?
Kuna yeyote aliyehoji usalama wa chanjo

Hakuna maswali yeyote,kinachosumbuwa watu kwa sasa ni utandawazi.

Hivi zile chanjo za surua,ndui,nk Nini walijadiliana na nani zikaletwa huku Africa? Au zikakubalika na wengine?
Si tumeletewa tu? Au kulikuwa na.mjadala kama huu wa chanjo ya uvico?
Kuna yeyote aliyehoji usalama wa chanjo zile?
Mlinganisho huo na wa polio surua haviendani mkuu sababu ilichukua muda mrefu kupatikana chanjo yake ila hii imekuja very soon yaani testing yake inafanyika directly ndio maana hata uchanjwe bado uko hatarini na zinapingwa kwa sehemu kubwa sana
 
Mlinganisho huo na wa polio surua haviendani mkuu sababu ilichukua muda mrefu kupatikana chanjo yake ila hii imekuja very soon yaani testing yake inafanyika directly ndio maana hata uchanjwe bado uko hatarini na zinapingwa kwa sehemu kubwa sana
Sidhani kama chanjo ya covid ilifanywa directly bila tafiti.

Na kama ni majaribio? Wasingefanya kwa dunia nzima wote wachanjwe.

Pia sasa watu wapo more advanced ktk technology

Hivyo kuchukuwa muda mchache kufanya tafiti inawezekana sana.

Kuliko miaka ya 1970 na 1980.
 
Mimi nilisafiri kwenda vijijini kuhakikisha mimi na wapendwa wangu wa huko uswekeni tunachanjwa (bila mtu kupotoshwa) kama sehemu ya utalii wa ndani.

Tulijiandikisha kama ilivyohitajika siku kama ilivyotangazwa. Tukasubiri maelekezo hadi walipokuwa tayari nasi tukachanjwa.

Ilikuwa siku ya uzinduzi kwenye eneo husika. Wachanjwa tulikuwa wengi (kwenye 300).

Haya ndiyo yaliyonisibu:

Nilichanjwa bega la kushoto. Yafuatayo ni niliyoyaona au kuyahisi kwa siku 3 tokea nilipochanjwa.

1. Muda mfupi baada ya kuchanjwa nilianza kusikia kiu, kilichoendelea bila kukoma, pamoja na kuongeza kiwango cha maji ambacho hunywa kwa kawaida.
3. Sense ya balance ilikuwa compromised kwa kiasi cha kutosha kwa kipindi chote.
4. Nilipata maumivu makali ya kichwa yasiyopungua mfululizo tokea muda kidogo baada ya kuchanjwa.
5. Mwili ulikuwa si wangu. Viungo viliniuma na mwili kulegea.
6. Nilibakia ndani mgonjwa kitandani kwa muda wote.
7. Mwili ulikuwa ukihisi baridi kuliko kawaida.
8. Palikuwa na hali ya kichefu chefu.

Ningali ninajifanyia tathmini kuhusiana na hali yangu yote leo kujilinganisha na ile ya mapema.

Sina majuto yoyote kwa kupokea chanjo hii. Ninayo furaha kuwa hatimaye nilipata. Ninaamini kuwa faida za chanjo ni kubwa kuliko madhara.

Niko tayari kuendelea kuleta mrejesho wa wazi kuhusiana na muendelezo wote, kulingana na hali yangu yote.

Msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.

#COVID19 - Chanjo - Mrejesho: Wizara tambueni changamoto hizi

#COVID19 - Chanjo isiwe Siasa, Vigezo na Masharti vizingatiwe
 
Mimi sichanjwi ng'ooo maana rais wangu mwendazake tayari alishanihatarisha juu ya hizi chanjo, sasa mm ni nani nipingane naye!

IMG_20210801_174150.jpg
 
Mimi ni miongoni watu waliochanjwa chanjo ya covid-19 Jonson Johnson siku ya pili TU baada ya zoezi la kuchanja kuzinduliwa na Rais.
Nilijisikia yafuatayo:

1. Nilichanjwa kwenye bega la Lushoto, sehemu niliyochanjwa nijisikia maumivu ya sindano kwa siku kama 3 hivi...
Mimi nimechanja nakubaliana nawe Kwamba chanjo unachanjwa bega la kushoto. Ila Kwa side effects natofautiana na wewe. Mimi masaa matano baada ya kuchanja nilipata homa ambayo sijawahi kuhisi tangu kuzaliwa, baridi Kali na kichwa kuuma Sana. Hali hii iliendelea Kwa masaa zaidi ya kumi na mbili nikarudi Sawa.

Hayo ya nguvu za kiume sijajua huenda ni Kwa vile sijawahi kujua upungufu WA nguvu za kiume ni nini
 
Mimi ni miongoni watu waliochanjwa chanjo ya covid-19 Jonson Johnson siku ya pili TU baada ya zoezi la kuchanja kuzinduliwa na Rais.
Nilijisikia yafuatayo...
Mwenzio nimeishia kucheka baada ya kusoma hizi point 3 zinazofuatana🤣🤣🤣

7. Nguvu za kiume ziliongezeka mara tatu zaidi.

8. Nilitoa megu nyingi kuliko kawaida wakati wa kujamiana.

9. Nikajisikia mtu mwenye nguvu kuliko kabla ya chanjo.
 
Back
Top Bottom