Nilivyokula kuber mara ya kwanza

Nilivyokula kuber mara ya kwanza

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2015
Posts
2,395
Reaction score
2,391
IMG_20230523_202800.jpg

Ilikuwa mwaka 2004 nikiwa darasa la 6. Alikuja ndugu yangu toka mjini na kuja na kuber. Ilikuwa jioni flan kijijini wakatii huo kumetulia watu tunasubiri ugali wa usiku, kipindi hicho hakuna milo miwili wala mitatu, asubuhi uji,mchana matunda shambani usiku ndio chakula.

Nimekaa njaa inanisokota kweli, ndugu yangu akaja na mjomba wake ambaye nae alizimwa mchana kwa zaga hilo hilo. Kwa ushamba nikaomba nionje,nilivyonusa tu, nikahisi harufu kaali sana,yan zaidi ya ugoro,nikauliza hii si kama ugoro(sababu ugoro naujua na siupendi)wajamaa huu tofauti onja uone utakayokuwa kama huyu jamaa kwenye picha hapa.

Nikapewa nikaweka mdomoni, akaniambia usimeze, nikajichanganya nikachuka mate nikameza. Niliambaa na ukuta mpaka chumbani, nilikuja kushtuka asubuhi saa 12 asubuhi pamoja na njaa yangu sikuweza kula chakula tena. Sitosahau tukio hili la kuber.

Je unakumbuka nini?
 
Haha tunajiandaa kwenda prepo baada ya kutoka kwenye msosi wa jioni form two hiyo. Mwana sijui kaipata wapi akaja room akatugawia kidogo kidogo, nikajichanganya na kumeza mate mamaweeee😫😫😫 🙌
Hakika vitu vingine si vya kugeza😂😂
 
Haha tunajiandaa kwenda prepo baada ya kutoka kwenye msosi wa jioni form two hiyo. Mwana sijui kaipata wapi akaja room akatugawia kidogo kidogo, nikajichanganya na kumeza mate mamaweeee😫😫😫 🙌
Hakika vitu vingine si vya kugeza😂😂
Kabisa mkuu,hii kama ingekuwepo tz tusingekuwa mil 60
 
Toka siku hiyo niliiogopa sana hata watu walioitumia, nashukuru serikali ilikuja kuiharamisha miaka ya 2007 ikawa dawa za kulevya, mim naaamini kaabisa kuberi ilichanganywa na dawa za kulevya
Hivi uhindini bado inatumika kama kilevi? Nilikuwa na rafiki zangu toka India, kiingereza kwao ni cha kuokota, ndugu yao ndio alikuwa akisimama Kama mkalimani walikuwa wanatafuna aina nyingine ya kilevi kifafanacho na kuber toka huko kwao India juzi juzi tu hapa. Nadhani watakuwa wameirudisha katika package na brand tofauti
 
Pole sana, uraibu ni noma good thing hiyo kitu haikukuteka akili,...halafu siku hizi ukiachana na uraibu wa kunusa gundi, spirit na kemikali nyingine, kuna huu urahibu wa kunusa nguo za ndani za wenza wao naona unakuja kwa kasi ya 5G
 
Hivi uhindini bado inatumika kama kilevi? Nilikuwa na rafiki zangu toka India, kiingereza kwao ni cha kuokota, ndugu yao ndio alikuwa akisimama Kama mkalimani walikuwa wanatafuna aina nyingine ya kilevi kifafanacho na kuber toka huko kwao India juzi juzi tu hapa. Nadhani watakuwa wameirudisha katika package na brand tofauti
Kuber haitafunwi hiyo itakuwa Pariki
 
Dah serikali izirudishe tu…maana vijana saivi wametumbukia kwenye bangi tu
 
Pole sana, uraibu ni noma good thing hiyo kitu haikukuteka akili,...halafu siku hizi ukiachana na uraibu wa kunusa gundi, spirit na kemikali nyingine, kuna huu urahibu wa kunusa nguo za ndani za wenza wao naona unakuja kwa kasi ya 5G
jitusue unuse nguo ya ndani ya mwenye gono au chlamydia uone kama hutoacha huo uraibu kwa vundo utakalokutana nalo.
 
Back
Top Bottom