Hivyo wazee wakiongopa, wakisema uongo au urongo wasiambiwe ?. Kama JK ameambiwa ukweli humu, JPM ameambiwa ukweli humu na Samia pia ataambiwa, who is he compared hata aje adanganye humu asiambiwe. Dawa pekee ya kutunza heshima kwa wakubwa zetu hawa, ni kwa wao kusema ukweli daima, uongo kwao mwiko!. Ni bahati mbaya sana, sisi wengine wenu sio watu wa kukopesha, ukisema uongo tunakurekebisha.
P
Leo hii wangejaa madaktari wa afya dunia nzima waliosomea Udaktari kupitia Quran. Allah kaweka wazi kila kitu kwenye Quran kulingana na Waumini. Isitoshe ma Engineer wa kila nyanja wangesomea fani zao kupitia Quran
CHUO GANI DUNIANI kinatoa mafunzo ya Udaktari kupitia Quran ??!!
Khamis ni mjukuu wa Mzee Sued Kagasheki. Khamis Kagasheki na Abdallah Kagasheki ni watu wawili tofauti. Abdallah Kagasheki ndie aliwahi kuwa Balozi. Huyu tunayemuita Balozi Khamis Kagasheki sina hakika kama alipata hadhi ya ubalozi bali alikuwa mkuu ya Idara fulani kule Geneva kwenye Shirika la Kazi Ulimwenguni.
Uongo ni mtu kusema kitu ambacho sii sahihi na anayesema uongo ni muongo au mrongo, na kumuita mtu muongo au mrongo, ni kumtukana na pia sio kumtukana.
Unapomuita mtu muongo, au mrongo, kama mtu huyo sio muongo, huko ndiko kumtukana, lakini kumuita mtu muongo, na ikatokea ni kweli huyo mtu ni mrongo, huko sio kumtukana bali ni kumwambia ukweli.
Kitendo cha kusema Daktari Mtanzania ndio dakitari wa kwanza Africa ni uongo !. Dakitari huyo ni dakitari wa kwanza Tanganyika but not Africa.
Kitendo cha mimi kukuambia ukweli wa urongo wako huo, japo umesema nimekutukana, kama kuambiwa ukweli ni kutukanwa, nimekuomba msamaha ila kiukweli nimesaidia wengi kujua ukweli kuwa kumbe ni dakitari wa kwanza Tanganyika na sio dakitari wa kwanza Africa.
Mkuu Maalim, Mohamed Said, naomba tuambizane ukweli bayana, sio mara moja wala mbili katika hoja zako ama unadanganywa na hao sources wako na kutuletea urongo humu, ama ni wewe ndio huongeza chumvi ili kunogesha hoja zako.
Kazi yangu mimi ni moja tuu, being critical kwenye urongo na chumvi chumvi.
Ameandika huyu Daktari ndiye Daktari wa kwanza Africa, nikakuomba substiate, umeshindwa!.
Jee unaukumbuka ule urongo wako wa kusema ndani ya Bunge letu, Waislamu ni asilimia 6%?, na uliwekwa hadi YouTube ?. Baada ya mimi kukukosoa kuwa huo ni urongo, ndipo kule YouTube ukaondolewa?. What was your motive kwa uongo kama ule ?.
Amini usiamini, angalizo hili
Wanabodi, mimi ni mshabiki na mfuasi wa simulizi za mwana Jf maarufu, mwenye powers fulani za ushawishi, Mkuu Maalim Mohamad said, nyingi ya simulizi zake zina some religious controversies zinazoibua very heated debates humu jukwaani, kwa baadhi ya watu kumsupport asemacho ni kweli, na wengine...
www.jamiiforums.com
lilisaidia ulitulia kidogo, sasa naona unaanza tena mdogo mdogo, kwa vichumvi chumvi vidogo vidogo, tukinyamaza utazidi kukoleza!.
Kama unaamini dakitari wa kwanza Bara zima lote la Africa alitoka Tanzania, thibitisha !. Kama mimi kukuambia hiyo ni chumvi na umeona neno hilo ni tusi, naomba radhi, naomba msamaha, nisamehe bure, mimi ni Mkristo wa type ya Tomaso, kazi yangu ni kuhoji tuu na sio kwako tuu, nimemuhoji hadi Magufuli !.
Samahani tena, endelea na mnakasha huu bila bughudha ya kuhojiwa hojiwa na sisi akina Tomaso wa humu JF.
P
Bwana Mohamed historia safi sema sina uhakika kama huyo Daktari Muta ni mswahili wa kwanza kuwa daktari. Kwa upande wa kusini mwa jangwa la Sahara nadhani mmojawapo wa madaktari wa mwanzo ni Dr William Anderson Soga wa Afrika Kusini aliyepata shahada yake ya utabibu mwaka q1883 ukiachia wengine waliofuatia toka Ghana, Nigeria na Siera Leone kama sikosei.
The Boss,
Kichekesho ni kuwa hakuna popote niliposema, "Daktari wa kwanza Afrika."
Kilichomchoma ni ule msisimko katika historia ya Abdul Sykes alivyokuja kuunda TANU 1954.
Kijana wa mjini Dar es Salaam 1950 akiwa na umri wa miaka 26 na akiwa kiongozi wa TAA anafanya mkutano wa siri na viongozi wa KAU ambao baadae walikuja kujulikana kama The Kapenguria Six, hili kwake ni zito sana.
Kijana huyu, Abdul Sykes si tu alikuwa kiongozi wa TAA baba yake ndiyo muasisi wa harakati hizi 1929.
Abdul Sykes atampokea Julius Nyerere 1952 na 1953 atafanya mkutano mwingine wa siri na Hamza Mwapachu nyumbani kwake Nansio Ukerewe kujadili ikiwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA awe President na mwaka wa 1954 waunde TANU.
Katika mkutano huu mwingine aliyekuwapo alikuwa Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) chama kilichotokana na African Association na kiliundwa 1933 na baba yake Abdul Syke Kleist Sykes na Mzee bin Sudi aliyekuwa President wa African Association.
Historia hii inamchoma Pascal kiasi inamvuruga akili.
Kalamu yangu katika historia hii ya TANU na uhuru wa Tanganyika na katika kumueleza Julius Nyerere hapo ndipo ilipobeba kikombe.
Hakuna aliyekuwa anayajua haya.
Vipi Pascal historia hii haimshughulishi anahangaishwa na jambo dogo lisilo na uhusiano wowote na historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?
Bwana Mohamed historia safi sema sina uhakika kama huyo Daktari Muta ni mswahili wa kwanza kuwa daktari. Kwa upande wa kusini mwa jangwa la Sahara nadhani mmojawapo wa madaktari wa mwanzo ni Dr William Anderson Soga wa Afrika Kusini aliyepata shahada yake ya utabibu mwaka q1883 ukiachia wengine waliofuatia toka Ghana, Nigeria na Siera Leone kama sikosei.
The Boss,
Kichekesho ni kuwa hakuna popote niliposema, "Daktari wa kwanza Afrika."
Kilichomchoma ni ule msisimko katika historia ya Abdul Sykes alivyokuja kuunda TANU 1954.
Kijana wa mjini Dar es Salaam 1950 akiwa na umri wa miaka 26 na akiwa kiongozi wa TAA anafanya mkutano wa siri na viongozi wa KAU ambao baadae walikuja kujulikana kama The Kapenguria Six, hili kwake ni zito sana.
Kijana huyu, Abdul Sykes si tu alikuwa kiongozi wa TAA baba yake ndiyo muasisi wa harakati hizi 1929.
Abdul Sykes atampokea Julius Nyerere 1952 na 1953 atafanya mkutano mwingine wa siri na Hamza Mwapachu nyumbani kwake Nansio Ukerewe kujadili ikiwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA awe President na mwaka wa 1954 waunde TANU.
Katika mkutano huu mwingine aliyekuwapo alikuwa Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) chama kilichotokana na African Association na kiliundwa 1933 na baba yake Abdul Syke Kleist Sykes na Mzee bin Sudi aliyekuwa President wa African Association.
Historia hii inamchoma Pascal kiasi inamvuruga akili.
Kalamu yangu katika historia hii ya TANU na uhuru wa Tanganyika na katika kumueleza Julius Nyerere hapo ndipo ilipobeba kikombe.
Hakuna aliyekuwa anayajua haya.
Vipi Pascal historia hii haimshughulishi anahangaishwa na jambo dogo lisilo na uhusiano wowote na historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?
Ukiandika maelezo yako uwe unayapitia pia kuyakumbuka. Ngoja nikunukuu kujibu swali lako "Dr Mutahangarwa alikuwa Mwafrika wa kwanza kufuzu udaktari." Wapi hayo unayosema kuwa hao niliotaja wanaingiaje. Kimsingi, linaweza kuwa kosa la kawaida katika uandishi. Hata hivyo, umefanya general assertion ambayo, kiuandishi wa kisomi, kama ningekuwa nakusahihisha, nisingekosa kuuliza swali, MWAFRIKA WA KWANZA KUFUZU UDAKTARI?!!!!! Seriously? Kwa vile wewe ni mwandishi na msomi, hapa utaelewa na kukubali kuwa ulikosea jambo ambalo ni la kawaida na kama binadamu lazima utakosea hata pale ambapo hukutegemea kwa msomi wa kiwango chako.
Bwana Mohamed historia safi sema sina uhakika kama huyo Daktari Muta ni mswahili wa kwanza kuwa daktari. Kwa upande wa kusini mwa jangwa la Sahara nadhani mmojawapo wa madaktari wa mwanzo ni Dr William Anderson Soga wa Afrika Kusini aliyepata shahada yake ya utabibu mwaka q1883 ukiachia wengine waliofuatia toka Ghana, Nigeria na Siera Leone kama sikosei.
Kuna watu humu, they are always right, wakileta hoja hata kama zina uongo na chumvi ndani yake, hawataki kukosolewa!. Mtu analeta uongo, anaambiwa huo ni uongo, anasema ametukanwa!.
P
Ukiandika maelezo yako uwe unayapitia pia kuyakumbuka. Ngoja nikunukuu kujibu swali lako "Dr Mutahangarwa alikuwa Mwafrika wa kwanza kufuzu udaktari." Wapi hayo unayosema kuwa hao niliotaja wanaingiaje. Kimsingi, linaweza kuwa kosa la kawaida katika uandishi. Hata hivyo, umefanya general assertion ambayo, kiuandishi wa kisomi, kama ningekuwa nakusahihisha, nisingekosa kuuliza swali, MWAFRIKA WA KWANZA KUFUZU UDAKTARI?!!!!! Seriously? Kwa vile wewe ni mwandishi na msomi, hapa utaelewa na kukubali kuwa ulikosea jambo ambalo ni la kawaida na kama binadamu lazima utakosea hata pale ambapo hukutegemea kwa msomi wa kiwango chako.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.