Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Vipi graduation ya mshua iliendaje?

Leta mambo sasa mkuu.
 
Boss achana nae uyo tupo wengi tu ambao tunaishi SA kila mtu ana jinsi alvopamban kutoka kimaisha.

Tuangushie EPISODE zlizobak [emoji120]
 
Akili za konda msafi za kimanzi chana...
Wivu kuzila hata kwenye ule uzi wake ilifikia sehemu akawachangisha Raia wema.....
 
Jf kweli changamoto.
Ilianza kila mtu kwao mambo safi,kila mtu ana drive na anaishi kwenye apartment kali halafu anafanya ofisi yenye maslahi mazuri. (Ndio maana tunaolalamika maisha magumu,hakuna ajira serikali ikipita humu inadhani sisi wahamiaji toka somalia).
Ukitoka hapo kila mtu anaenda mkoani kikazi. Sawa. Ukienda kwenye uzi wa rikkiboy kila mtu amekula kimasihara demu mkali mwenye msambwanda mkali na kalamba hadi mtaro mchafu hadi demu ana squirt (ku squirt sio kazi rahisi hivyo tena toka kwa school boys)
Sasa kwenye uzi wa Keagan inaonekana kila mtu kashaenda sauzi na anajua majanga ya uhamiaji na mitaa ya johanesburg na midrand.
Ndio maana mzozo umekuwa mkubwa sababu hakuna anayetaka kushindwa.
 
Mkuu achana nae ww endelea na story hawa wengine tuachie sisi mbona tunawamudi wakija kihun tutaenda kihun wakija kistrabu nasi ni wasitrabu kwahy mkuu ondoa Shaka tupo kwa ajil kuhakikisha Uzi unaisha mm na team yangu tumejipanga kupambana na wakosoaji na madanga tupo vizur kwa hili shusha mambo boss
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]Mkuu kwenye huu uzi sikutaka kutia comment zaidi ya kusoma ila duh!!!

Umetisha kaka.
 
Umesahau lingine jf wote ni TISS na wote awapendi CCM na wote wana magari na wote wana degree hakuna la saba.
 
Mkuu mie unafiki huwa siuwezi, wewe unge-clear tu doubts zetu then ukaendelea kuleta stori. Haya mambo ya watu kuogopa kuuliza maswali ndio sababu hata nchi yetu imefikia hapa ilipo. Watanzania tulio wengi hatujiamini ndio maana viongozi wetu wanatuendesha wanavyotaka, yaani tuna taifa la ndio mzee hata kama kunahitajika maelezo. Kitu kama hakijakaa sawa wewe kitolee ufafanuzi. Kuna vitu hatuwezi kukubishia kwa sababu kweli kila mtu ana experience yake ila mkuu kuna vitu very technical huwezi kusema kila mtu ana experience yake pia, kuna baadhi vitu lazima viwe common kwa kila mtu. Mfano ni hili la kuoverstay haliwezi kumalizwa kwa rushwa ya rand 300 na likaisha completely kwa sababu ni issue ya usalama wa nchi na system iko linked nchi nzima kuanzia makao makuu ya immigration hadi idara zote zinazohusika na maswala ya uhamiaji. So wakiscan tu passport yako hapo boarder au sehemu yoyote inayohusika na mfumo wa passport control taarifa zako zinaonekana hadi makao makuu ya immigration kuwa kuna mtu kaoverstay anahitajika kukamatwa au kulipa fine whatever the case may be. Sasa huyo immigration officer atakusaidiaje hapo? Hiyo fine atakulipia? maana hiyo fine ni zaidi ya rand 4,000. Na hiyo fine inakuwa registered kwenye system mpaka uilipe ndio iwe cleared la sivyo unakuwa black listed kukanyaga nchini kwao for the next five years. Kwa hiyo hoja kama hii unatakiwa uitolee maelezo ili twende sawa. Kuna watu humu wanafurahia tu stori na vitu kama hivi wanavioverlook kwa sababu either hawavijui kama vipo au wameamua kufunika kombe mwanaharamu apite. Halafu hata issue ya kupewa hifadhi na kanisa na yenyewe kuna utata kidogo kama hutajali pia itolee maelezo. South africa inajulikana kwa ujambazi na mauaji hivyo kwa mtazamo wangu sio rahisi viongozi wa dini wakupe hifadhi bila kujiridhisha kama wewe ni mtu salama au la. As a reasonable person nilikuwa nategemea wangekuhoji kwa kina kuhusu uhalali wako wa kuwepo nchini kabla ya kukupa hifadhi, lazima wangekuulizia documents zako kama upo nchini kihalali. Kumbuka hilo ni kanisa na linatakiwa kuheshimu sheria za nchi, hivyo hawawezi kurisk kumhifadhi mtu ambaye anavunja sheria maana ungekamatwa wangeonekana wanahifadhi wahalifu hivyo ingepelekea kanisa kuingia mgogoro na mamlaka za kiserikali na ingepelekea hatari ya kufutiwa usajili wa kanisa lao, mind you Midrands ni makazi ya watu wenye hela kwa hiyo ni watu wenye uelewa mpana. Samahani wasomaji kama nawaharibia stori yenu ila nimeamua kutokuwa mnafiki kwa kuuliza haya maswali critical.
 
Mkuu wacha kuu najisi uzi wa mwenzio.. Sio peke yako uliishi South Africa... Point's raia wanaona una wivu na huu uzi! Hata kama kuna kasoro zipotezee tuu...
 
nimefika south mara moja tu ila nilichokinote ni mitizamo tofauti kutoka watu wawili tofauti....na kila mtu kakaza
 
Konda msafi ablokiwe ili jamaa amalize stroy aachiweee ....nikupongeza sanaaa konda msaf kwa kuuuliza maswali critical ili isije kuwa jamaa anatulisha chai kavu nakuaminisha watu oungo niseme tu kuwa nakupongeza Sana kwelikweli au nasema uongo ndugu zanguu..@konda msafi oyeeee
 
OG dingi sorry sio kwa ubaya ila ulishasema hutabishana tena. Kila unayosema ni kweli lakini experience yako haiwezi kuwa sawa na yangu.

Tumuache jamaa kama ataendelea na story sawa. Ila hizi kelele nyingi ndio zimemfanya atukache.

Hata ningekuwa mimi nisingemalizia hii story kwasababu ya ujuaji wa mambanga hapa.
 
Niko najitahidi kupitia comment ya kila mmoja wa jf Kuna baadhi ya raia wana nanga Sana juu ya story ya jamaa na baadhi kuvutiwa na kutaka muendelezo.
Bytheway stry iko vzr na japo mapungufu huwa yapo kila sehemu, ukiona Kuna sehem kdgo inakupatia utata jarbu kuuliza pasipo kuweka machafuko.
Hii thread kwa vijana ambao bado tunachangamoto ya ajila na wale wa hustle za hapa na pale Kuna funzo la kujifunza Sana kwan kadri navyo zidi kuisoma najikuta nagain baadhi ya hatua za kujifunza.


Mkuu nitarudi hiv punde baada ya muendelez "notification on."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…