Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

We ndugu acha kijiona msafi sana, watu wanapiga story zao kusogeza uzi, hao unaowaita madanga hawajawahi kukudangia, na hao malaya hujawahi kuwafukunyua, acha umbea mtoto wa kiume relax tusubiri story iendelee
We ngine una wapisha, huna haja kujibzana nao...
 
@Noelia unajua huwa tunakosea sana sisi wabongo...

Passport ni hati au kibali cha kusafiria na tena kukutambulisha wewe kwa taifa jingine kama ni Mtanzania...

Sasa tujiulize wote tu, kama hauna mpango wa kwenda nchi nyingine, kwa nini uhitaji passport?

Halafu pia restrictions zinakuwa nyingi sababu kuna watu wanatumia passport kufanikisha shughuli zao za kiharamia kama kupitisha madawa ya kulevya n.k, sasa kama taifa huwezi tu kuwa unatoa passport ili kufanikisha mauharamia...

Mfano kipindi tulipokuwa na passport ya zamani (ile ya gamba la kijani), passport ya bongo ilikuwa shamba la bibi, watu wa mataifa mengine waliitumia sana kufanya mambo yao especially kwa zile nchi ambazo mbongo anaingia kwa kupata entry visa airport...
Ni visingizio visivyo na msingi, futailia hata kitambulisho cha nida utaelewa Mkuu
 
Wanaijeria nchi yao inaruhusu uraia pacha. Ukiwa na uraia pacha inasaidia kuwekeza nyumbani. Tanzania uraia pacha hawajaruhusu. Tanzania kila kitu kinyume nyuma tu. Nchi nyingi za Africa wameruhusu uraia pacha
Viongozi wetu wazee walio kwenye system wamejwa na uoga wa kufanya mabadiliko sana...
Hata hududma kama PayPal tu hadi leo wameshindwa iruhusu BOT kutoa kibali , wa Tz tuwe tunapokea pesa
 
Hahahaaa sisi maTrucker hao tushawazoea hawalambi hata chuma

Halafu we mdada unajipenda sana wewe ukaamua ukajipumzishe tu na Pajama lako[emoji23][emoji23]

Wasalimie bahi huko. Naona yule rafiki yako mmoja kachongewa na CAG mpaka anasababisha msee kaambiwa anademka
mkuu i wish me ningekuw pamaja nikainjoy uumbaji wa mungu
 
SEHEMU YA KUMI NA MOJA

Kwa hiyo Mimi kujileta mwenyewe kwenye huu mtandao wao, jamaa alifurahi sana kuwa amepata mtu wa kumuuzia Dawa zake bila shida.

Siku ile ni kama hatukulala kabisa, Wale jamaa wameshazoea kuchelewa kulala na kuwahi kuamka. Tulilala Saa Kumi na Kuamka Saa Moja. Yan Saa moja asubuhi tukawa macho. Jamaa wakaanza kujiandaa kwa ajili ya kwenda kuzungusha biashara yao hiyo. Na Mimi wakaniambia nijiandae ili tutoke wote wataniacha kwa yule Bosi wao, Jamaa Y. Nadhan kwa kuwa nilikuwa mgeni walishindwa kuniacha peke angu pale gheto. Walikuwa kama hawaniamini hivi.

Tukajiandaa tukatoka wote, Niliacha pale Gheto Begi langu ambalo lina vyeti vyangu ndani. Ukweli muda wote nilikuwa nawaza vile vyeti tu. Hao Hao mpaka kwa yule jamaa Y, wakaniacha pale, wao hawakuchukua muda wakasepa. Pale ghetto tukabaki Mimi na Jamaa Y. Jamaa Y akatengeneza chai pale tukanywa, tulivyomaliza kunywa tukashuka mpaka chini kuna mtaa Fulani tukaelekea huko.

Wakati tunatembea ndo nilipata muda mzuri wa kuuona mjini wao. Ebana nchi ya wenzetu nzuri jamani. Warembo kama wote, wote wamejazia hatari. Nikajisema moyoni ndo mana wabongo wengi wakija huku hawarudi Bongo mpaka baada ya miaka mingi. Ukweli kwa wenzetu mademu wanajua kuvaa, kila stail yan. Warembo wanavaa na kupendeza haswa. Nilikuwa natoa macho mpaka najishtukia.

Mimi na Jamaa Y tulifika mpaka sehemu Fulani karibu na Barabara tukasimama hapo. Tulikuta majamaa wengine wengi kama Tisa hivi nao wamesimama. Pale nilikuja kugundua kuwa ni Kijiwe chao cha kuuzia dawa za Kulevya. Jamaa wanakuwa na Kete ndogo ndogo wanaficha mdomoni, mteja akifika tu, wanatoa mdomoni wanampatia. Jamaa wamevaa Kibrazameni huwezi kuzania kama wanapiga ishu hizo hapo.

Wateja wao wengi waliofika pale walifika na Magari yao. Unakuta gari inapaki pale halafu hawa jamaa mmoja wao anazama ndani ya hiyo Gari anauza mzigo.

Walikuwa wanaficha Dawa zao ndani ya Mdomo ili kama itatokea wamekamatwa na Askari inakuwa rahisi wao kuzimeza na kupoteza ushahidi. Ukweli Mimi sikuwa Comfortable kabisa kusimama nao pale. Unajua hapa Bongo ishu ya Madawa ni kubwa sana lakini sio kule. Kule wanaona kitu cha kawaida tu. Tena wanakushangaa wewe unayewashangaa.

Hawa jamaa wa Kibongo karibia wote walionekana kuwa na maisha mazuri. Wao pia walikuwa wamepaki magari yao pembeni ya Barabara. Kila mmoja ukimuuliza pale atakwambia ana miaka kibao hajarudi Bongo. Hata wanunuzi wao pale walikuwa wanafika washua kweli kweli kuja kununua mizigo.

Maelezo yote hayo alikuwa ananipa kidogo kidogo jamaa Y, Ni Kama vile alikuwa ananifundisha Kazi kiaina. Ukweli kwa siku ile ya kwanza Wabongo wengi niliokutana nao walikuwa wanapiga hizi ishu, wachache sana walikuwa wanafanya Kazi kwenye Masaloon na maeneo mengine. Hata hawa ambao walikuwa wanafanya kwenye Masaloon, nyuma ya pazia walifanya dili hizi. Hata ambao walikuwa na Maduka makubwa nyuma ya biashara zao, Jamaa Y aliniambia nao wanauza unga.

Jamaa Y taratibu aliendelea kunifundisha Kazi na kunionesha Mitaa mbalimbali. Nilimweleza jamaa kuwa Mimi natamani kufanya michogo ya halali. Nakumbuka jamaa alinikatisha sana moyo. Kwamba Kazi za Halali ni ngumu sana kupata. Jamaa aliniuliza "Una Kibali cha kufanyia Kazi? (Work Permit)" Nikamjibu Hapana sina. Akasema kama ni hivyo itakuwa ngumu sana kupata mchongo wa halali.

Kwa asiyefahamu, kwa mujibu wa sheria mtu inabidi uombe Kibali cha Kazi kabla ya kuanza Safari. Yan unaombea ukiwa Bongo. Unakwenda pale Ubalozi wa South Africa uko pale Posta unaomba kabisa Kibali kabla ya kuanza safari. Ukifika pale utapewa taratibu zote za kuomba Kibali. Changamoto sio kuomba Kibali, Changamoto ni hayo Masharti yao.

Kwa hiyo Jamaa Y aliniambia kama sina Kibali nisahau kupata Mchongo wa Halali. Aisee nilichoka. Mchongo pekee uliopo mbele yangu ni wa Dawa za Kulevya.
Nitarudi
 
Kwa sasa nina ofisi mbili. Moja ipo Smit Street na Clein na nyingine ipo Edenvile hapa hapa J'burg. Mtaji wa mtu ni akili yake mwenyew, sio kila aishie kaburu ni muuza bangi au unga. Karibuni mapocho pocho wakubwa


View attachment 1757913


Huwa nacheka sana jinsi watu wanavyodanganyana humu kuhusu kaburu,eti kila mbongo mwizi,kila mbongo muuza unga nk,wakati kuna wabongo kibao kaburu wanakwenda kihalali kabisa na maisha yao yapo poa kabisaa.
Me mitaa yangu ni plain & clein karibu na MTN Tax Rank
 
SEHEMU YA KUMI NA TANO

Kuna Mdau mmoja amenikumbusha jambo la Msingi sana, ameniuliza niliwezaje kuongeza siku za kuishi South Africa wakati pale Boda BeitBridge nilipewa Mwezi mmoja tu wa kuishi. Ukweli siku zangu za kuishi ziliisha nikiwa bado nipo kule kwa Jamaa Y Pretoria. Kule nilikuta kuna utaratibu wa aina mbili, wapo watu ambao wenyewe toka wafike South Africa hawajawai kwenda kuongeza siku zao za kuishi mule. Wao wanaishi tu kama raia wengine, lakini inabidi usiwe umefanya Kosa, kama utafanya Kosa ukifikishwa kwenye vyombo vya sheria ndo mambo ya Passport yako iko wapi na Mambo mengine yataibuka.

Na wapo ambao wenyewe kila Passport zao zikiisha siku za kuishi (Visa Expired) wanakwenda kuongeza muda (Renew ). Kuongeza muda ni gharama kwa sababu inabidi uende mwenyewe mpaka Boda au Ofisi za Uhamiaji ukaongeze muda au umtume mtu akakugongee, kuna watu walikuwa wanapita mtaani kwetu, ni wabongo wenzetu tunawachangia nauli wanakwenda kutugongea Boda au kwenye Ofisi za Uhamiaji (Hii njia ya kutumia watu sio salama sana).

Changamoto ya kwenda kuongeza siku za kuishi kila zitakapoisha ni kwamba Je utakuwa unakwenda kuongeza mara ngapi? Maana Kila ukienda unaweza ongezewa mwezi mmoja au wiki au Miezi 3. Sasa Je utamudu gharama za kila mara kuwa unakwenda kuongeza siku? Unakuta inakuwa ngumu. Kwa hiyo mimi nilichagua kuishi bila kuongeza muda, Nilikuwa naomba tu lisitokee la kutokea. Ndo nilikuwa naishi hivyo, nilivunja sheria. Mambo ya siku ya kuondoka kwenye nchi hiyo nilifanyaje, Mimi Nilirudi kwa njia za panya. Nitaeleza huko mbele. Lakini wengine huwa wanaenda kule Pretoria kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania wanasema Passport zao wameibiwa kisha kuna Karatasi wanapewa wanarudi zao Bongo. Nadhan nimejibu hilo.

Tuendelee, Basi Kanya alikuwa ananiganda sana mpaka nikasema hapa nitapewa lawama Tu. Nitamla halafu baadae aje kukasirika akijua natoka na demu mwengine. Roho yangu ilikuwa inasita sana Kumla kwa kuogopa mitafaruku nchi za watu halafu mimi pale ni mgeni nimekwenda kutafuta maisha.

Kuna siku nikasema hapana, niliamka vibaya, Wanaume wenzangu najua nikisema niliamka vibaya mnanielewa, Nikasema iwe mvua, iwe jua Kanya lazima aliwe maana ndoto za kujichafua Usiku zilishaanza kuwa nyingi, nikamcheki Kanya akakubali kuja ghetto. Yan siku zote Kanya ni kama alikuwa ananisikilizia Mimi tu.

Kanya wakati anafika Thomas alikuwa hayupo, tukapiga zetu story kidogo nikamsogelea mpaka alipokaa. Wala hakuzingua tukaanza kufanya yetu. Hao tukavua nguo tukahamia Kitandani. Nilikuwa nimeshanunua kabisa Condom, nikavaa. Ebana Kanya ana bonge moja la Tako. Sijawai kupiga demu ana tako kama lile la Kanya maisha yangu yote mpaka leo. Halafu Kitu Laini OG, Unajua wale wanamakalio makubwa ya Asili. Ile naingiza Cha ajabu eti Kanya alikuwa Bikra. Nikasema dah nilishangaa kinoma. Moyoni nikajisemea huyu anataka kuniibia huyu. Hii Bikra kweli au Bandia? Lakini sikujali sana wala nini, nililazimisha hivyo hivyo tulihamia Chooni ili tusichafue mashuka ya Thomas . Nilimpiga hivyo hivyo huku analia kama Mtoto.

Kwa kuwa ilikuwa siku ya kwanza sikuinjoi sana, halafu ukizingatia natumia ghetto ambalo Thomas amejimilikisha kama lake basi nilikuwa na hofu Fulani hivi endapo Thomas angerudi. Kwa hiyo tuliwai kumaliza kabla Thomas hajarudi. Tulivyomaliza nilimsindikiza hadi kwenye nyumba waliyokuwa wanaishi.

Kile Kitendo kilizidisha ukaribu na mazoea sana na Kanya, Japo sikuwai kumtongoza lakini ndo ashakuwa demu wangu kilazima. Kanisani muda wote macho kwangu, akaanza mpaka kuwaambia rafiki zake kuwa Mimi ni mtu wake. Thomas nae kuzipata hizo habari nae akawa anasema ni kweli, Kanya kila siku anakuja kwetu. Thomas alikuwaga mmbea mmbea sna. Mimi najitahidi kumkwepa Kanya pale Kanisani lakini yeye hana habari muda wote anapenda kukaa karibu yangu. Hiyo hali ilikuwa inanivuruga sana akili.

Tatizo lilikuja kutokea siku moja kwenye Birthday Party ya Mchungaji wetu ilifanyika usiku nyumbani kwake. Tulifika waumini kama wote.Kulikuwa na Nyama choma kama zote. Sasa yule demu mrembo mwenye ndinga lake nae alikuwepo. Nikasema leo lazima nitumie nafasi vizuri. Party ilifanyika nje halafu kulikuwa na kigiza giza fulani hivi, Nikasema Leo natumia hii nafasi vzr, Nikawa napiga piga nae story pale, mara tunapiga piga picha pale, sikufanya makosa hadi tukabadilishana namba. Kosa nililolifanya ni kwamba baada ya kutoka pale zile Picha nakumbuka nilipost Facebook. Halafu Kanya sijawai hata siku moja kumpost. Ugomvi kati yangu na Kanya ulikuwa mzito. Ishu ya namna hii kwa Wanawake ni kubwa sana.
 
Back
Top Bottom