Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

SEHEMU YA KUMI NA SITA

Ukweli niseme kitendo nilichokifanya cha kupost zile picha hata mimi nilikijutia sana. Unajua wakati mwengine ukimpenda mtu kuna vitu vingine unajikuta umefanya tu, hata ukiulizwa sababu kwa nini ulifanya hivyo huelewi. Malengo yangu yalikuwa yanamhitaji sana Yule demu mwengine kuliko Kanya. Siku iliyofuata nilienda mpaka alipokuwa anaishi Kanya, Nilijaribu kukaa nae kuzungumzia hii ishu, nilimuomba Msamaha mwishoe alinisamahe, maisha mengine yaliendelea.

Tuliyamaliza lakini Kichwani nilibaki na dukuduku Fulani hivi, nilikuwa nawaza sasa nitafanyaje? Maana Kanya kwangu nilimuona kama mzigo wakati mimi nilipanga kutafuta demu ambae atanisaidia kufikia safari yangu. Namtema vipi Kanya? Yule demu mwengine tukawa tukikutana Kanisani tunasalimiana fresh, kwenye simu tunawasiliana. Ukaribu uliongezeka kiasi chake, Alikuwa hajui chochote kilichokuwa kinaendelea, Baadae nilikuja kujua kuwa huyu demu anaitwa Tshepiso na anafanya kazi Capitec Bank.

Sasa kuna wakati Kanisa lilitangaza kuna Safari ya kwenda kutoa Huduma za Kiroho kwenye Tawi lake lililopo Nchini LESOTHO. Kanisa lilikuwa na Matawi mpaka Marekani na Baadhi ya nchi za Ulaya. Walisema anayetaka kwenda na kama una Passport basi ruksa mtu yeyote kwenda, Usafiri, Chakula, Kulala vyote ni gharama za Kanisa. Nikasema hii ni fursa kwangu ya kuwa karibu zaidi na Mchungaji na Washua zaidi. Mpaka hapa kwa kweli nilianza kukubalika pale Kanisani si kama Mwanzo. Nilikuwa sio mgeni tena kwenye macho yao.

Lesotho ni nchi ndogo, Mfano ni kama Mkoa tu wa Morogoro au Morogoro inaweza kuwa Kubwa pia. Ni nchi ambayo ipo ndani ya nchi ya South Africa. Nchi yote imezungukwa na South Africa. Kama mtu hufahamu unaweza ku google ukaona.

Sasa kwa wasiofahamu, Vijana wengi wazawa wa South Africa hawana Passport za kusafiria, Wengi sio sana watu wa kusafiri safiri, kwa hiyo kigezo cha watu kuwa na Passport kilipunguza waumini wengi sana akiwemo Kanya. Alikuwa hana Passport. Kwenye Upande wa watu wa Camera, Mimi na Max tu ndo tulikuwa na Passport. Nilichofurahi Tshepiso alikuwa na Passport kwa hiyo alikuwepo kwenye hii safari.

Utaratibu wa siku ya Safari tulikuwa tunapewa gari Fulani zina muundo kama wa Toyota Alfad, rangi nyeupe, Mnakuwa mnachaguana wenyewe waumini kama sita, kati yenu anapatikana pia dereva, kisha mnaanza safari. Mimi na Tshepiso tulipanda gari tofauti. Siku ya safari ilikuwa ni jumamosi ila Muda wa safari mnapanga wenyewe wana Kikundi, Mchungaji alisema anachotaka watu wote Jumapili tuwe tumefika Lesotho. Kwa hiyo Kanisa lilitoa gari kama 10 hivi. Watu tukaanza safari. Sisi tulianza safari jumamosi jioni.

Kwenye gari yetu mwanaume nilikuwa peke yangu, wengine wote madem. Wote kati yetu hakuna hata mmoja anaijua njia ya kutufikisha Lesotho. Yan wenzetu wana barabara nyingi kiasi kwamba unaweza kuzaliwa palepale na Baadhi ya barabara za kuelekea baadhi ya nchi huzijui. Na ukikosea tu barabara unaweza kutumia muda mwingi sana kurudi kwenye barabara uliyoikusudia kupita. Nakumbuka tulipotea sana. Mpaka ikabidi tutumie Navigator kwenye simu zetu. Wote ndani ya gari tuliwasha Navigator tunamwelekeza dereva wetu wapi pa kupita.

Tulifika Boda kati ya South Africa na Lesotho usiku wa kama saa Saba hivi. Kwa kuwa nilikuwa na mademu wote, mimi ndo niliwaongoza mpaka mle ndani kwenye Ofisi za Uhamiaji. Kwa kuwa kwenye Passport yangu nilikuwa nimezidisha siku za kuishi mle South Africa, Nilisoma mazingira pale kwenye Passport yangu nikaweka Rand 300, nikagongewa bila shida. Japo Lesotho tulikuwa tunakwenda kukaa siku Tatu tu lakini Uhamiaji upande wa Lesotho walinipa siku Thelathini za kukaa Lesotho. Nilikuwa tayari mzoefu wa kupita kwenye Maboda.

Wale mademu walikuwa wanazinguliwa pale, nikawaambia wekeni Rand 100 kwenye Passport zenu halafu nendeni tena, wakafanya hivyo kisha wakagongewa mihuri kasoro mmoja tu kati yetu ndo hakugongewa huyo demu alikuwa ni Mnaijeria, Kwanza Mnaijeria kuingia Lesotho inabidi alipie visa. Sio kama sisi wengine tunaingia free tu. Pili Yule demu kama mimi tu pale South Africa alikuwa amezidisha siku za kuishi (Ame Overstay). Kwa hiyo wale maafisa uhamiaji walikuwa wanataka pesa ndefu.

Nakumbuka alikuwa anasema “Mbona Mtanzania na yeye ametoka mbali lakini amegongewa bila shida”. Basi pale mmoja wetu akafanya mawasiliano na mchungaji, Mchungaji na baadhi ya waumini walikuwa wameshafika Lesotho tayari. Kwa kuwa sio mbali sana, ule ule usiku, mchungaji ikabidi aje mpaka pale boda. Akaongea nao wale Maafisa Uhamiaji, nadhani aliwapa pesa kidogo ila sina uhakika sana. Hatimae wakatuachia tukaendelea na safari yetu mpka Mji Mkuu wa Lesotho unaitwa Masseru. Masseru pa kawaida sana pengine hata Dodoma pazuri. Huwezi hata kulinganisha na Dar, Arusha au Mwanza. Basi tulienda moja kwa moja kwenye Hostel tulizopangiwa kufikia. Tulilala pale.

Asubuhi mapema sana tuliamka na kuanza kujiandaa kwa ajili ya kwenda kupanda Mlima kwa ajili ya Ibada, Ibada ya kwanza tulienda kufanyia milimani huko. Ibada ya Jioni ndo tulienda kwenye Kanisa lao. Kwa hiyo Hata kupanda huo Mlima nakumbuka ilikuwa ni tabu, Mlima ulikuwa mrefu kiasi chake. Wakati magari yetu yanakusanyika pale chini ya Mlima ndo nilikutana na Tshepiso.

Ukweli Lesotho tuliinjoi sana, kwanza tulikuwa wachache, kwa hiyo tulikuwa kama ndugu Fulani hivi, tulipiga picha kama zote mpka leo hii ninazo kwenye Email yangu. Nikiziangaliaga huwa zinanikumbusha matukio yote haya ninayoyaeleza. Kule Lesotho Mimi na Yule demu tulikuwa marafiki kinoma yan, ile Camera ya Kanisa niliyokuwa natumia kupiga picha, Picha nyingi nilimpiga Tshepiso. Wakuu zote hizo ni harakati za kutaka kutafuta Mchongo ndani ya nchi ya watu. Naomba nisieleweke kwamba mimi ni Marioo ila mazingira ndo yalikuwa yananilazimisha kufanya nilichokuwa nafanya. Nilijua hapa nikicheza tu Akiba yangu ya Pesa inaisha yote halafu kinachofuta ni maisha magumu na kurudi Bongo, halafu mpango wa Kurudi Bongo nilikuwa sina kabisa. Na huyu mwanamke naona kabisa kwa maisha yake anaweza kunifikisha Mahali.

Hivi hii story ni ya mwaka gani?? Yani ulikwenda huko miaka ipi?
 
Mkuu mtoto wa mstaafu, Keagan Paul, naomba uniruhusu nicomment kidogo. Kuna vitu kwenye stori yako havipo sawa kidogo, naelewa huenda labda umeamua kuvifanya visiwe sawa kwa maksudi na si kwa bahati mbaya. Kuna sehemu nimekusoma unasema wale jamaa wanaomuuzia "nyaupe" jamaa Y wanafanya kazi kama punda. Hapo mzee umepindisha ukweli, Dizonga hakuna wabongo wanaokula bata kama wauza nyaupe. Kufanya kazi kama punda kwako wewe labda kuna tafsiri gani? Maana hao jamaa kazi yao ni kupokea simu tu na kupeleka mzigo location unapohitajika na akifika pale ni kitendo cha sekunde mbili keshamaliza kazi, haina hata kuhesabu hela, hela itahesabiwa baada ya kuondoka eneo la tukio, na wale wanunuzi ni waamifu sana hawatoi hela pungufu japo hamuhesabiani eneo la tukio. Zaidi ya yote jamaa wana usafiri hawasambazi kwa miguu, hata kama mtu ameanza kuuza leo haiwezi kumchukua zaidi ya mwezi hajapata usafiri, sasa unaposema wanafanya kazi kama punda kidogo kama umepindisha uhalisia. Pia umesema huwa wanaweka hizo kete mdomoni na polisi wakivamia wanazimeza, mzee hii pia sio kaka. huwezi kumeza madawa kizembe hivyo. Donga ndio zinamezwa wakati wa kuzisafirisha intercontinental lakini sio mzigo umeshafika ndani ya nchi bado mtu ameze. Hiyo risk hakuna mtu wa kuitake, kwanza ufungaji wa hizo kete sio imara sana uimeze halafu ubaki salama. Ufungaji wa donga ndio imara unaweza kumeza na ukasurvive lakini sio kete mkuu. Halafu mademu wa Gauteng yaani Joburg na Pretoria wana attitude flani tofauti na uliyoielezea tena kama hapo Midrands ndio kabisa. Nimekaa Randburg kama miaka 6 au 7, 209 Bellairs Drive, Banbury Cross, North Riding. Randburg nadhani kwa Johannesburg ni sehemu wanayokaa matajiri wa South Africa ukitoa Sandton na Fourways. Ninachotaka kusema hapa mademu wa kishua wa Gauteng nazijua attitude zao maana nimeishi nao. Pia umesema permit (viza) yako iliexpire ukiwa bado kwa bwana Y, sasa uliwezaje kutafuta kazi wakati tayari ulikuwa unaishi kinyume cha sheria maana kitu cha kwanza lazima wakuulize ID yako. Mind you Johannesburg na Pretoria ni miji ambayo kama huna permit ni ngumu sana kusurvive. Joburg hata ukiwa unatembea barabarani unaweza kushitukia tu unasimamishwa na police na kuombwa ID tofauti na miji mingine kama Durban, sasa wewe uliwezaje kutafuta kazi wakati hata permit yenyewe huna? sijui kama umenielewa? Na kwa Johannesburg misako ya kutafuta wahamiaji haramu ipo kila uchwao.
sawa jamaa ake khumbu!! ngoja ajee
 
Konda makosa ya kiufundi hayo yanatokea....

[emoji117]May be kwa kuwa alikua mpya akawa anajua wanaficha mdomoni maana ndio alianza kujifunza.

[emoji117]May be ile kurudi usiku sana ndio maana akawa anasema wanafanya kazi kama punda. Kuna sehemu alisema walilala saa 11 alfajiri na kudamka saa 1 asubuhi.... Si mchezo...

[emoji117] Hadithi yake mpaka sasa haionyeshi kuwa ametimiza hata miezi mitatu hapo SA. Na inaonekana hakuwa na ABC za sheria za huko, na hata aliokutana nao hawakuwa wamempa tahadhari ya vibali. Inawezekana alianza kusambaza barua bila kujua anaweza kudakwa au tuseme kama alivyosema aliamua kujilipua tu maana ndio kilichompeleka. Inawezekana ilikua bahati yake kutodakwa mapema 40 hazikufika....

[emoji117]Kumbuka alijiingiza kwenye kanisa na elewa mara nyingi watu makanisani huwa wanaweka wahamiaji sana. Nenda hata makanisa yetu haya ya kilokole utakuta wakenya wanyarwanda kila taifa wapo wanaishi bila vibali....

MAPITO NI TOFAUTI EXPERIENCE YAKO SI YAKE.....
TUMPE MUDA AELEZEEE KWA NAMNA ALIVYOISHI....

Ila pia KUDOS kwako umempa hint pale palipokua sio sawa.....

Jamhuri ya JF.... story iendeleeeee
mkuu agiza pepsi kwa mangi . hapo nakuja kulipa
 
Wasomali wanashirikiana hata hapa kariakoo kwenye madjka ya vifaa vya stationery/ computer Laptop/dektop & Accessories

wapo wengi sana ...nahisi hata mzigo wanaagiza kwa pamoja maana kola duka product wanazouza ni zile zile hazina utofauti.
Wametake over sana hata wahindi wamepungua
Bado wale wasomali wa ka "Western union" ka mtaani wanajiita Daharshbil nadhani hivi bado wapo??? Au upepo wa JPM ulipita nao

Ilikua ndo mkombozi wetu tukiwa DXB na Qatar kutuma hela nyumbani kwa gharama nafuu
 
Basi tu wanawake wanahofu tu...ukiwa na misimamo yako utasumbuliwa mwanzoni tu....kuna mdada i met last yr kahama bar nakula akaja kaa moja kwa moja nilipokaa..anaonekana amechoka na hangover juu..mie kahama nikikua naenda wknd kula pilau..napenda pilau bas wknd najiendelea kula pilau na videsperado 4 narudi gheto kulala..
Yaan yule dada kashuka ijumaa toka dar ameambiwa kahama kuna madanga yanatoa hela[emoji1787]! Sikion alivaa hereni nzuri sana...nikamwambia ungekuja na hereni kama hizo ningekuungisha na hapa chillers ningewashawishi barmaids wanunue.. akaniangaliaaa.akasonya .akasema mie biashaea sina passion nayo..so akawa anauliza ni wap huko kwenye madanga..nikamwambia shoga mie sijui uliza alokuambia...ujinga balaa unapewa 50k then unakaa bar .kuna helanhapo itabaki? Alipojua nafanya nini alihamaki akaona namkata stimu akasepa
Kwa hiyo alifikiri wewe ni ....
 
SEHEMU YA SITA

Ile Asubuhi kabla ya Safari kuanza, Kuna wadogo zetu kama 4 wa umri kama wa Miaka 16/17/18 walipanda ndani ya Bus. Waliomba kwa Konda kuongea na Abiria. Walituambia kuwa na wao wanaelekea South Afrika ila nauli zao ziliishia pale Tunduma. Waliomba tuwachangie Nauli.

Wametokea Dar ila wamekaa pale Tunduma kwa muda wa wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Kwa hiyo walikuwa wanaomba tuwachangie nauli ili waweze kuendelea na safari. Tulianza kuwachangia, Mmoja wao alikuwa na simu akaiuza mle ndani ya Bus. Madogo walikuwa wamechangamka sana. Mpaka wanakwenda South kwa nauli za kuunga unga. Wenyewe kutumia Mwezi mzima njiani ni kawaida tu.

Akiba waliyokuwa nayo, pamoja na Michango yetu waliweza kupata nauli ya kuwafikisha mpaka Harare. Walisema wakifika Harare watakaa tena wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Hivyo tuliendelea nao na safari kwenye bus letu. Kwa kifupi mbele ya safari katika kupiga piga nao story tulikuja kujua kwamba kati ya wale madogo, mmoja wao ndio kiongozi wao, yeye alishawai kuishi sana South Afrika. Ilionekana kila akirudi kwao Manzese Tanzania, wakati wa kuondoka huwa anachukua Vijana wengine anaenda nao South. Yani kwa zile story za Madogo nilijiona kumbe ni mim tu ndo sijafika South Africa, Kwa maelezo yao ni kama vile Vijana wengi wapo huko tayari.

Ni kweli kwa pilikapilika za Vijana niliowaona pale Tunduma niliona ni kama Vijana wengi sana wanaikimbia hii nchi, kila mmoja akilalamika kuwa Bongo Maisha magumu.

Staili ya hawa madogo kusafiri ni ya kuunga unga nauli, hawa madogo walivyofika Tunduma walikaa hapo, sidhani kama Kuna namna nyengine walifanya ili kupata nauli zaidi ya wizi. Na wapo madogo wengine wengi wa staili hii.

Pia pale Tunduma sio Waburundi wote walifanikiwa kupita, kuna baadhi walikosa pesa ya kulipia Visa ya kuingia Zambia. Sisi watanzania tunaingia Zambia bila kulipia Visa. Hivyo waburundi ndani ya Bus walipungua

Kila tulivyokuwa tukiendelea na Safari ndivyo Lugha yetu pendwa ya Kiswahili ilivyokuwa ikipotea. Tulifika Lusaka Mji Mkuu wa Zambia saa tatu usiku. Tulilala hapo. Wengine tulishuka kwenda kupata Huduma za Chooni, Wengine ndo ilikuwa mwisho wa safari yao. Asubuhi kulivyokucha tuliendelea na safari yetu ya kuelekea boda ya Zambia na Zimbabwe inaitwa CHIRUNDU
Hao madogo wa manzese ulivyowataja moyo umelipuka paaaa!!!!! Nikiangalia mwaka napata majibu kadhaa. Hadithi ya kweli hii hakika. Twende sehemu ya 7
 
Back
Top Bottom