Nakubaliana na wewe kabisaa.ukiona mishe unayofanya hufuatwi na TRA, au POLISI juwa dili lako si la utajiri.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nakubaliana na wewe kabisaa.ukiona mishe unayofanya hufuatwi na TRA, au POLISI juwa dili lako si la utajiri.
Pengine amemuachia noti feki [emoji23][emoji23]jokesUmeniwahi kuuliza mkuu[emoji28]
Ahahahaha hatar. SnaHako kabegi usijeenda nako mgodini [emoji1787]
Acha basi,kuna biashara tunazifanyia nyumban na TRA na Polis hawajui kama watu tunapiga pesa,ukiona mishe unayofanya hufuatwi na TRA, au POLISI juwa dili lako si la utajiri.
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 11.
Nililipa kiasi cha Ksh 50 kwenye Hiace(Shuttle) iliyokuwa ikielekea Kisumu na niliwaambia waniache Migori.Migori ni mji ambao ulikuwa ni mkubwa tu na hapo kabla sikuwahi kufika lakini katika stori za washikaji walikuwa wakidai ni mji ambao ulikuwa jirani sana na Isebania,nilichokua nimepanga ni kwamba nikifika hapo mji wa Migori nitajua cha kufanya,jambo la msingi ni kutoka kwanza hapo Sirari ambapo hali ya hewa ilikuwa imechafuka!.
Nikiwa kwenye gari nilikuwa nimekumbatia kile kibegi ambacho hakikuwa kizito na kiukweli nilikuwa kama nimepagawa na kuduwazwa na ile hali ya hofu niliyokuwa nayo!.Tulitumia takribani nusu saa mpaka dakika arobaini kufika hapo mjini Migori!.
Nilipofika nilishuka na nilitembea kuelekea juu kama narudi tena Sirari,sasa nilipofika kwa mbele nilikutana na jamaa nikamuuliza anielekeze ilipo Guest House ili niende nikapumzike,sasa kwa wale jamaa wao walikuwa wanaita Lodge,ulikuwa ukiuliza neno Guest House kidogo wanakushangaa,basi jamaa akawa amenionyesha Lodge moja ambayo haikuwa mbali na ile stage(stand).
Nilifika pale nikauliza vyumba nikaambiwa ni Ksh 350,nilichomoa hela nikawa nimempa kisha nikaonyeshwa chumba changu!.Kiukweli baada ya kuingia chumbani akili yangu ilitulia sasa!,niliingia bafuni kuoga na nilipomaliza nililala sana na nimekuja kushituka ikiwa mida ya 12 jioni!,basi nikaamua kuamka ili niende kutafuta mahali walipokuwa wanauza msosi ili nitwange nirudi ndani,sasa nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa pale mapokezi akawa amenionyesha kimgahawa ambacho hakikuwa mbali na lile eneo,sasa baadae nilikuja kufahamu kumbe mwenye ule mgahawa ndiye aliyekuwa mwenye ile Lodge!.
Nilipofika hapo Migori kiukweli kilichonichanganya ni namna ya kuitumia hela ya Kenya kiusahihi,kuna muda nadhani nilikuwa naibiwa kwasababu sikuwa na muda wa kuanza kuhesabu hesabu vichenji vilivyokuwa vinabaki!.
Sasa wakati natoka Sirari,kwenye lile begi nilikuwa na kiasi cha Tsh milioni 5,na sikufahamu nitazifanyia nini nikiwa hapo Migori!,Sasa asubuhi kulipokucha niliamka mida ya 4 asubuhi nikanawa uso na kupiga mswaki kisha nikaondoka kuelekea pale kwenye kile ki-mgahawa ili kupata chai!.Ule mgahawa ilionekana kwa lile eneo ulikuwa unauza sana kwasababu ile jioni na hata asubuhi nilipoingia nilikuta kuna watu wengi wakipata vyakula mbalimbali,sasa wakati nimeagiza chai na chapati nikiwa nasubiria,ghafla waliingia jamaa wawili wakiwa wamevaa makoti ya kijeshi na suruali za kijani huku wakiwa na bunduki!,nilipata hofu sana lakini nikawa mtulivu,sasa kumbe wale jamaa walikuwa ni askari wa Kikenya na ndivyo walivyokuwa wakivaa,haukupita muda waliongezeka na wengine wawili wakiwa na silaha kama wenzao!.Basi nao walikaa wakawa wameagiza chai wakaendelea kunywa!.
Muda huo nilijikausha kama sina habari na mtu,namshukuru Mungu pia na wao hawakuwa na habari na mtu!,walipomaliza walinyanyuka wakawa wameondoka,sasa nilikuja kugundua kumbe lile eneo nililokuwepo halikuwa mbali na kituo cha polisi hapo Migori na kituo chenyewe kilikuwa barabarani kabisa,niliona lile eneo si sahihi kwangu,hivyo nikapanga ikifika mchana niondoke lile eneo nikatafute Lodge nyingine ambayo itakuwa mafichoni kidogo!. Kiukweli ile hela niliyokuwa nimebadili ilimalizika siku hiyo baada ya kutafuta Lodge nyingine iliyokuwa pembeni ya mji kama unaelekea Kisumu,sasa hofu ilianza kunijaa namna nitakavyoweza kusavaivu kwa kipindi chote nitakachokuwa huko!.
Ilipofika mida ya jioni nilitoka nikaelekea pale stendi kwa mguu na nilipofika jamaa walidhani ni abiria wakaanza kunichangamkia na niliwaeleza mimi si abiria,nilikaa pembeni kujaribu kuangalia namna wanavyofanyakazi lakini kila nikijaribu kuangalia mdau angalau nilete mazoea lakini hola!,kiukweli sikufahamu nitaishije yale mazingira ambayo sikuyazoea!.Utofauti niliuona pale stendi ni kwamba jamaa walionekana kujitahidi kuchangamka lakini bado washikaji na wahuni niliokuwa nikifanya nao kazi pale Sirari walikuwa wamewazidi wale wajaluo kwa uchangamfu!.Basi siku hiyo niliamua kurudi zangu pale Lodge ambako nililala mpaka asubuhi,ilipofika mida ya saa 3 asubuhi nilitoka zangu nikarudi pale stendi kushangaa,sasa nikasogea zilipokuwa zinapaki gari za kuelekea Isebania,pale niliwakuta jamaa wanaongea kikurya hivyo nikajiona kabisa kama nipo Sirari,sasa kuna dogo alikuwa konda akiita abiria kwenye zile shuttle na alikuwa amevaa tisheti iliyokuwa na picha ya Chege na Temba huku ikiwa imeandikwa TMK WANAUME,sasa baada ya kumcheki kwa muda mrefu yule dogo ni kama alinivutia kwa namna alivyokuwa mchangamfu!,sasa baada ya kuitia ile shuttle na kujaza,nilimsogelea kutaka angalau mazoea nae ili ikiwezekana yeye ndiye aifanye ile kazi ya kubadili zile hela wakati nikiwa kule!.
Mimi "Mwanangu mambo niaje?"
Dogo "Ni bomba bro!"
Mimi "Una muda mrefu sana hapa eeh!"
Dogo "Yes bro tuko hapa kitambo!"
Sasa wakati naongea nae hakusita kuniuliza kama mimi ni Mtanzania maana ongea yangu na yake ilikuwa tofauti kabisa!.
Mimi "Unaitwa nani mwanangu?"
Dogo "Mimi naitwa Joe lakini wengi huniita Mkamilifu!"
Dogo "Na wewe bro majina yako nani?"
Mimi " Mimi naitwa Umughaka"
Dogo "Its your first time hapa Migori?"
Mimi "Hapana,huwa nakuja mara kibao tu!"
Dogo "Mi pia huwa nakwenda Sirare kwa jamaa zangu"
Sasa wao kwa kule badala ya kuita Sirari,wao walikuwa wakiita Sirare na hata shuttle zao zote za kuelekea Sirari zilikuwa zimeandikwa Sirare,nadhani ilikuwa ni lafudhi tu lakini walikuwa wakimaanisha Sirari!.Sasa dogo alionekana kupafahamu vizuri Sirari na hata maeneo baadhi niliyomtajia alionekana kuyafahamu!.Pia nilimdanganya kwamba hapo Migori mimi sikuwa mgeni ili isije akawa mkora akatafuta genge la kihalifu wakanifanya kitu mbaya!.
Sikutaka stori nyingi kwasababu sikuwa na hela ya kunivusha siku itakayofuata,nilitaka yeye ndiye akawe chambo wa kubadili zile hela na nilipanga endapo kikinuka basi ningechafua hapo Migori kuendelea kusonga mbele!.
Mimi "Hivi hapa ni maeneo gani wanabadili hela"
Dogo "Ooh kwani una haraka sana bro,huwezi subiri nimalize hii job then nikuonyeshe!"
Mimi "Sawa haina noma"
Basi dogo akaendelea kupambana na ile kazi ya kuita abiria mpaka akawa amejaza tena gari ya pili,hiyo ilikuwa mida ya saa 7 mchana!.
Dogo "Naweza kukuelekeza sasa"
Basi dogo akawa amenichukua mpaka kwenye jengo moja ambalo tukaingia ndani tukakuta maduka kibao,sasa mimi baada ya kuingia mle ndani kiukweli niliona siwezi kubadili zile hela kwenye mazingira yale kwasababu ningedakwa tu!.Sasa nilimchukua dogo nikatoka nae nje nikamwambia twende mpaka kwenye ile Lodge niliyofikia kisha nikamwambia nitamlipa hela ili kufidia muda wake!.Tulipofika kwenye ile Lodge nilimuacha dogo pale mapokezi nikamwambia anisubiri,nilifungua lile begi nikatoa laki moja kisha nikaitia mfukoni nikawa nimefunga kile chumba na kutoka nje!.
Mimi "Nakupa hizi hela naomba ukabadili sehemu nyingine tofauti na pale pa mwanzo kwasababu wale jamaa wanakata hela kubwa"
Dogo "Ok bro kuna jamaa mmoja yupo hapo ng'ambo nampelekea huwa ana-exchange pesa ya Tz,nikukute basi hapa"
Mimi "Nitakulipa vizuri ukifanya vizuri!"
Dogo "Sawa bro nikukute hapa,sa hii tu nakuja!"
Mimi "Uwe muaminifu"
Dogo "Ahahaha bro ndiyo maana nikaitwa Mkamilifu,we uliza watu wote kwa pale stage hakuna ambae hanijui!"
Mimi "Sawa nakusubiri".
Basi dogo alitoka akikimbia akielekea kwa huyo jamaa kubadili ile hela niliyompatia,ile hela kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,ulikuwa ukiiangalia kiukweli hakukuwa na shaka yeyote kwamba ilikuwa ni pesa halali kwa matumizi,uenda kama ungeiweka kwenye mashine au ungekuwa na utambuzi wa hela feki ndipo ungeifahamu!.Nilipompa dogo ile hela nilikuwa nina mambo niliyokuwa nayafikiria kichwani,kama angekimbia basi kwangu isingeniuma kwasababu nilikuwa nazo za kutosha,na kama angefanikiwa kubadili basi ndiye angekuwa rafiki yangu kwa kipindi ambacho ningekuwa hapo,lakini pia kama wangemdaka nilipanga kutoweka kama kipanga!.
Basi baada ya kama nusu saa nikiwa pale nje,nilimuona dogo kwa mbali akiwa anakuja!.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] dah ningemuona wa hovyo sanaPengine amemuachia noti feki [emoji23][emoji23]jokes
Maeneo mengi nayajua vizuri, hapo Bunda...Big upNilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 13.
Mimi "Mama nyakuru Mwita"
Mama "Tata sabhoke"
Ilikuwa ni heshima na salamu ambayo nilimpatia mama yangu baada ya kuwa nimefika hapo sokoni kwenye meza aliyokuwa akifanyia biashara!.
Mama "Ulienda wapi baba?"
Mimi "Nilikuwepo tu mama!"
Mama "Mbona umenenepa hivyo,au umepata kibarua huko baba!?"
Mimi "Nabangaiza tu hivyo hivyo!"
Mama "Nilimpigia mama yako mkubwa lakini akaniambia uliondoka na akajua labda ulirudi nyumbani"
Mimi "Mama nilienda kupambana na maisha yangu!".
Mama "Sasa baba utaendelea kuhangaika hivi hadi lini,rudi nyumbani mimi niliongea na baba yako na akasema hayo yameisha"
Mimi "Mama kwa umri huu siwezi kukaa tena pale nyumbani"
Mimi "Nilipita tu kuwasalimia"
Mama "Ulipita nyumbani?"
Mimi "Nimeanzia huko ndiyo nikaja hapa"
Mama "Dada yako alikuja na amemaliza kuondoka wiki iliyopita!"
Aliendelea "Chukua namba yake utawasiliana nae alisema ukirudi nikwambie umtafute"
Basi baada ya mazungumzo na mama nilichukua ile namba ya dada yangu mkubwa(Sarah)kisha nikaondoka zangu!.Mama yangu mara zote alikuwaga rafiki yangu kipenzi,pamoja na lile seke seke la mzee lakini bado alitaka nirudi pale nyumbani kitu ambacho kisingewezekana kwa wakati huo!.Sasa wakati naondoka nilimpigia dada yangu simu ili kumjulia hali maana tangu nilivyokuwa nimemaliza shule sikuwahi kuongea nae kwasababu yeye alikuwa ameolewa huko Mwanza!.
Baada ya kuongea na dada kwa dakika kadhaa alishangaa sana kwa kile kitendo ambacho mzee alinifanyia na alilaumu sana kwanini nilishindwa kumshirikisha kwa muda wote huo nikawa kimya!.
Da'Sarah "Sasa sikuhizi unafanya kazi gani hapo Tarime?"
Sikutaka kabisa kumficha kitu dada nilimwambia niliamua kuwa mpiga debe angalau maisha yaendeleee,alinishangaa sana ya kwamba nawezaje kuwa na elimu halafu niende kupiga debe!.
Da'sarah "Nilimwambia baba ukweli na kama ni kuchukia ngoja achukie,haiwezekani pesa anamalizia kwa mama yake Robina halafu sisi tunahangaika!"
Aliendelea "Kwahiyo sasa ulikuwa unakaa wapi?"
Mimi "Niliamua kupanga hapo Sirari!"
Da'Sarah "Ngoja nimwambie shemeji yako aje akutumie nauli uje huku"
Aliendelea "Na huyo mzee wala usimwambie chochote,muacheni na hela zake,yeye si anaona mama yetu hana maana!"
Mimi "Mimi nishamsahau na wala sihitaji hata kumi yake!"
Mimi " Halafu dada kama huko kuna sehemu ya kufikia hilo suala la nauli kwangu alinisumbui,we hata usimsumbue shem we kama inawezekana hata leo nianze safari"
Da'Sarah " Sasa hivi kweli kuna gari za kutoka hapo kuja Mwanza?"
Mimi "Hilo suala wewe niachie mimi,mimi nikifika nitakwambia"
Da'Sarah " Sawa wewe panda gari uje kama una nauli na ngoja nimpigie shemeji yako simu muda huo!"
Ile kauli ya Dada kunitaka niende Mwanza nikama ilinisaidia maana mpaka wakati huo nilikuwa sielewi hatma yangu!.Basi nilielekea mpaka stendi ambako nilikuwa nikitembea kwa umakini na tahadhari kubwa ili nisije kujikuta naangukia mkoni mwa mapongo,wakati huo begi langu lilikuwa na hela lipo mgongoni sikutaka kabisa kuliachia!.Basi nilipofika pale stendi nilidandia Hiace za Musoma ambako nilipanga nikifika pale Zero zero( Makutano) nisubiri gari zinazoenda Mwanza kutokea Musoma mjini!.Nilifika pale Makutano mida ya saa 9 alasiri na nikatelemka kusubiri gari za Mwanza.
Sikutaka kupandia gari za Mwanza pale Tarime mjini maana kulikuwa na wajuaji wengi hivyo nikawa naogopa kukamatishwa!.Basi haukupita muda nikawa nimepanda gari za Mwanza na nikawasiliana na dada nikawa nimemjulisha nishapanda gari!.,Kiukweli akili yangu mpaka wakati huo ilikuwa inawaza mambo mengi sana,sikujali ya kwamba Sirari nimeacha vitu vyangu wala nini,mimi nilichojali ni usalama wangu na kama ni vitu niliona ningevifata hali ambapo ingetulia!.
Wakati nikiwa kwenye gari nilimtafuta mshikaji wangu Mtatiro ambaye niliamini yupo Mwanza na nilipanga nikifika Mwanza tuonane!.
Mimi "Mwanangu vipi?"
Mtatiro "Mwanangu umekuwa adimu sana kama mate ya nyoka!"
Mimi "Ahahahaa ahahaaa,nambie mwanangu"
Mtatiro "Nimekutafuta juzi kati ulikuwa hupatikani!"
Mimi "Kuna mahali nilikuwepo mtandao ulikuwa haushiki kaka"
Mimi "Nipo njiani mwanangu nakuja M-Z-A"
Mtatiro "Unakuja lini,leo!?"
Mimi "Yeah nipo njiani"
Mtatiro "Umefika wapi?"
Mimi "Tunakaribia Kiabakari"
Mtatiro "Mimi sipo Mwanza mwanangu"
Mimi "Ulirudi Tarime?"
Mtatiro "Hapana,nipo hapa Bunda kuna ki mgodi kimetema ndiyo tupo na brother"
Mimi "Duuu!"
Mtatiro "Mwanza unaenda kwa nani?"
Mimi "Naenda kwa sista Sarah!"
Mtatiro "Mwanangu achana na habari za Mwanza kwanza,we kama vipi telemkia hapo Bunda mimi nitakufata uje tuone kama tutapata chochote"
Mtatiro alinishawishi hadi nikajikuta tena safari ya Mwanza kama imetoweka moyoni mwangu,nilichokuwa namshukuru Mshikaji wangu Mtatiro alikuwaga kila fursa haachi kunishirikisha kama rafiki yake,iwe haramu au iwe halali,kiukweli kwenye hilo sitamsahau jamaa yangu(Kwasasa anaishi Uganda).
Mtatiro "We mwambie Konda akushushe kituo kinaitwa Nyasura"
Aliendelea "Akikushusha hapo Nyasura ndiyo itakuwa jirani na huku nilipo!"
Mimi "Sawa"
Basi safari ikawa inaishia Bunda ingawa nilishalipa nauli ya Mwanza moja kwa moja,sikuona taabu kwasababu bado fungu nilikuwa nalo la kutosha.Ingawaje pesa niliyokuwa nayo ilikuwa haramu lakini ilikuwa inanipa kujiamini kwingi sana!.
Baada ya safari ya dakika kadhaa tukawa tumefika pale Bunda na mimi kushushwa hapo Nyasura kama Mtatiro alivyokuwa amenielekeza!.Basi nilimpigia simu Mtatiro nikamueleza ya kwamba nishafika hapo Nyasura,jamaa akawa amenitaka nipumzike sehemu aje kunifuata maana alipokuwepo yeye kulikuwa na umbali mrefu kidogo!.
Acha kukalili weweukiona mishe unayofanya hufuatwi na TRA, au POLISI juwa dili lako si la utajiri.
Muda kama ule hakupaswa kumwamini mtu tenaYaani jamaa kanishangaza sana yaani anajianika hadharani hivyo wakati ni the most wanted?
Kabisa ukizingatia huyo jamaa yake ndy aliwakutanisha na yule mketa fedha fakeMuda kama ule hakupaswa kumwamini mtu tena
Enewei ilikuwa lazima makosa yatoke ili kisa kisimuliwe.Kabisa ukizingatia huyo jamaa yake ndy aliwakutanisha na yule mketa fedha fake
Braza kuvuta bangi siyo ujinga wew ndo mjingaNisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane!.
Kwenye haya maisha kuna wakati huwa ninakaa chini na kusema "Kama sikufa kipindi kile,basi siwezi kufa mpaka Mungu atakaporuhusu".
Nadhani wengi mtakumbuka ni siku chache tu zimepita nimeandika kisa cha maisha ambayo nilikutana nayo wakati nikiwa nimekwenda kumsalimia baba yangu mdogo akiwa ni Headmaster, maisha yale yalikuwa ya kawaida ila washirikina walifanya tukakosa amani.
Sasa baada ya hapo nilifaulu vizuri tu kuelekea shule ya upili(advance)na nikapangiwa huko Tanga kwa mchepuo wa Sayansi wenye combination PCB. Hali yangu ya maisha ya shule kiukweli ilikuwa mbaya sana mpaka nikajuta kwanini nilichukua hiyo combination, siyo kwamba sikuwa na akili, la hasha!,akili ilikuwepo ya kutosha kwasababu nilifaulu kwenda advance kwa divisheni 2,ni combination iliyohitaji kupiga msuli kana kwamba umetumwa na kijiji, haikutaka mchezo wala kujisahau hata kidogo,sasa mimi nilipofika huko nikajikuta naungana na makundi na kujanjaruka kuwashinda hata niliyowakuta!.
Mkurya mimi kutoka wilayani Tarime kijiji cha Mogabiri nikajikuta nazamia kwenye dimbwi la mapenzi ya mtoto wa kitanga ambaye alifanya hata kusoma nikaacha nikawa namuwaza yeye na utamu wa papuchi yake!.
(Shamima popote ulipo ulaaniwe mbwa wewe kwa kuniharibia maisha[emoji23][emoji23]). All in all ni kwamba napambana na maisha yanasonga japo ni kibishi!. Sasa haya ya kwanini nilifeli nadhani kwa leo si mahala pake,nitawaeleza tu kilichofuata baada ya mimi kufeli shule!.
Kiasili mimi ni mkurya kutokea wilaya ya Tarime huko kijijini Mogabiri,ingawa hatukuishi sana hapo kijijini lakini ndipo chimbuko letu lilipo hapo, kwa pale Tarime mjini nyumbani kwetu ni Rebu.Pia tunao ndugu wengi tu waliotapakaa karibu kila kona ya hii nchi!, hapa Dar es salaam wamejaa ila wanajifanya kama hawanioni vile!(Maisha ya sikuhizi yamekuwa yakipumbavu sana).Kwakuwa wanajifanya kukausha na mimi pia napiga mikausho ya hatari!,sitaki kumgasi mtu!.
Basi bana, nakumbuka ile nimemaliza skonga nikawa nashangaa shangaa pale nyumbani kusubiri tokeo la kuelekea chuo, sasa nilifahamu kabisa siwezi kufaulu kwa kile nilichokifanya kule skonga, Mzee yeye aliamini toto lake limemaliza shule na anajivunia kwasababu nilikuwa nina akili,hakuelewa kabisa kwamba baada ya kufika shule nilijanjaruka kuwazidi hata niliowakuta!. Baada ya matokeo kutoka na ikaonekana nimepata divesheni zero, mimi kwa upande wangu sikushituka ila Mzee alihamaki sana na kushangaa nilipatwa na nini hadi nifeli!.
Tangu nimeanza darasa la kwanza hadi darasa la saba, sikuwahi kuvuka namba 5,ingawaje sikuwahi kuwa namba 1 lakini nilikuwa nacheza kwenye namba 2-4. Nilipofika form 1 hadi form 4 wembe ukawa uleule!,nashika namba 3 -5,sasa hadi nafaulu kuingia advance Mzee wangu hakushangaa maana alifahamu kabisa toto lake nilikuwa nina akili!.Mzee wangu kiukweli alikuwa mkali mno na ilikuwa ikitokea nimefanya kosa akanikamata,kiukweli nilikuwaga naimba Haleluya!.Yeye alikuwaga achapi kwa fimbo za miti ya kawaida,bali alikuwa anachapa kwa nyaya ya umeme!,Aisee usiombe kukutwa!.Kuna muda nilikuwa nikifahamu nimefanya kosa siku hiyo najiwahisha kuoga na kuingia kulala na kujifanya naumwa!,sasa akija akikushika shingoni kama anakupima joto akakuta huna joto,aisee utaomba ardhi ipasuke ikumeze ili ikuepushe na kipigo kisichokuua ila chenye kukufanya ukajuta kwanini ulizaliwa!.
Kutokana na kutokuridhika kwa mzee na yale matokeo, kuna siku kadhaa sikumuona pale nyumbani nikajua uenda atakuwa kwenye mambo yake, sasa kumbe mzee amesafiri hadi Tanga kwenda kuonana na Headmaster kufahamu mwanae ni kwanini nimefeli kiasi kile na wenzangu kufaulu!, Alichoamini mzee ni kwamba sikustahili kufeli na nilipaswa nifaulu!. Ule mpango wa yeye kwenda Tanga kumbe hadi Maza nae alikuwa akifahamu ila aliamua kula buyu ili ukweli ufahamike!, Mama yangu alikuwa rafiki yangu mkubwa sana na yeye peke yake ndiye shida zangu zote nilikuwaga nikimwambia!.Ila safari hii na yeye aliukaza uso wake na hakutaka kabisa kucheka na kima!.
Mwanaume niliendelea kujinafasi na kujimwayamwaya kwa kipindi kile kifupi ambacho mzee hakuwepo nikiamini atakuwa ameenda kwenye shughuli zake, akili yangu iliamini kwasababu mzee wangu alikuwa akinimini basi angenipatia mtaji ili nianze biashara!.
Baada ya kama siku 5 mzee alirejea, sasa tukiwa tunapata chakula usiku alikuwa akiniangalia kwa jazba sana, sikuwa na tatizo nae kwasababu niliamini yeye kuwaga na hasira za karibu ndiyo ilikuwa kawaida yake!. Sasa ile naendelea kula sijui ili wala lile,nilishitukia amenipiga kofi ambalo lilifanya kuanza kuona maluweluwe!.
Mama "Tamtigha omwana araghere!"(Muache mtoto ale)
Mzee "Amos hebu niletee waya hapo chumbani"
Sasa mdogo wangu aitwaye Amos akaagizwa waya akachukue waya ili viboko vichukue nafasi!.
Mzee "Leo nakuua mbwa wewe"
Kiukweli siku hiyo nilijua kabisa nakufa maana mzee wangu alikuwaga hana masikhara kabisa na maneno yake!. Basi mama alikuwa akijaribu kumtuliza mzee lakini bado ikashindikana, kwa wakati huo sikuelewa kabisa ni kitu gani kilimsibu mzee wangu ambaye alikuwa amerejea kutoka huko alikokuwa ameenda!.
Mzee alinyanyuka akatoka akaenda ndani ambako sikufahamu alikwenda kufanya nini,wakati huo kiukweli hata chakula sikuwa na hamu nacho tena kwasababu mabanzi na makwenzi niliyokuwa nimechezea yaliniharibia mudi kabisa!.Baada ya mzee kutoka chumbani alikuja na kamba ya katani akanisogelea akanifunga na kunibana miguu kana kwamba anataka kuchinja kuku!,sasa akauchukua ule waya uliyoletwa na dogo nikaanza kuchezea stiki!,kiukweli nilipigika sana!. Baada ya kuona ameniadhibu vya kutosha alinilaza kifudi fudi wakati huo kanifunga mikono kwa nyuma kama vile jambazi au mwizi amepigwa pingu.
Mzee "Leo nakuua, sali sala yako ya mwisho!"
Aliendelea "Siwezi kuharibu pesa yangu halafu wewe uende shule kuwa mtoro!"
Baada ya kusikia ile kauli basi nikajiongeza kiakili na nikafahamu kabisa atakuwa alikwenda shuleni kuutafuta ukweli wa mimi kufeli!.Kiukweli nilikiona kifo kiko karibu yangu!.
Mzee "Yaani nakulipia karo wewe unaenda kuvuta bangi shule?"
Aliendelea "Hizo bangi ulianza kuvuta lini?"
Sasa nikaanza kushangaa ni nani alimwambia nilikuwa navuta bangi? Kiukweli kitu ambacho sikuwahi kukifanya kwenye maisha yangu ni huo uvutaji wa bangi alionieleza!.
Mimi "Hapana baba sivuti bangi!"
Mzee "Leo utanitambua mshenzi wewe"
Kiukweli kujitetea ilikuwa ngumu sana maana kila nilipojaribu kujitetea nilionekana muongo na kuishia kukandamizwa viboko visivyokuwa na idadi!. Sasa kumbe alipokwenda kule shuleni, walimu walimwambia ya kwamba mimi nilijiingiza kwenye kundi la waliokuwa wameshindikana na kuanza kujihusisha na uvutaji wa bangi!,walimu pia hawakufahamu hicho hakikuwa chanzo cha mimi kufeli bali ilibidi wamwambie mzee kwasababu ya kuniona mimi kukaa na watu ambao pale shuleni walikuwa wameshindikana!.Na kwa kipindi kile walimu walikuwaga hawaangaiki na mtoto wa mtu,wao walikuwa wakituambia mwisho wa mambo yote ni pepa(mtihani)ndiyo utakaochuja nafaka halisi na magugu!.
Basi bana, baada ya kupigika sana na mzee kunishikia panga, ilibidi maza aingilie kati kwa kujifunga kibwebwe na kumkoromea mzee!.
Mama "Hivi baba Sarah unataka kumuua mtoto kisa kufeli shule!"
Aliendelea "Kama humtaki mtoto muache akatange tange huko!"
Basi baada ya mama kuingilia kati, mzee aliniacha na akanitaka nipotee pale nyumbani na nisije kumtambua kama baba yangu. Mama alinisogelea na kunifungua zile kamba mkononi na miguuni!. Kiukweli nilipigika sana.
Nilitoweka pale sebuleni nikaelekea chumbani kulala huku nikiendelea kulia kwa kwikwi, mwili wangu wakati huo ulikuwa umejaa alama ya nyaya za umeme zilizosababishwa na kile kipigo!.
Usiku huo kiukweli sikupata usingizi kabisa kutokana na maumivu ya viboko!.
Soma zaidi:
Mambo ya kutrak hua yako dar tuJamaa anamchomesha kizembe Sana, wacha tuone anadai mtatiro Ni mshikaji Sana huwa anampa deals kadhaa !
Vp hao police (mapongo) walishindwa kutrack ? Make hakuna mahali umesema ulitupa simu /laini na kutumia simu/namba nyingine !
Good story teller
Mkuu chillo clan conscious umefanya nimecheka kwa sauti sana [emoji23][emoji23][emoji23]Mapongo tukimsubiri Umughaka aingie kwenye 18 ze2View attachment 2399852