Mstoiki
JF-Expert Member
- Oct 9, 2020
- 4,365
- 8,384
Habari zenu wakuu, True story!!
Sikuwahi kufikiria kuwa siku moja ningeweza kujikuta katikati ya mchezo hatari uliopangwa kwa ustadi wa hali ya juu.
Ilianza kama jambo la kawaida tu — ofa ya kuvutia na ahadi za mafanikio ya haraka.
Lakini kadri nilivyozidi kujihusisha, nilitambua kuwa nilikuwa nikiingia kwenye mtego wa kundi la matapeli wenye ujuzi wa hatari.
Huu ni ushuhuda wa jinsi nilivyokabiliana na hofu, kuchukua hatua ya ujasiri, na hatimaye kujinasua kutoka mikononi mwa kikundi hiki hatari.
Mimi Ibn Unuq baada ya kumaliza chuo cha NIT, Dar-es-salaam nilirudi nyumbani MBEYA, ili kutulia kusubiria ajira huku nikiangalia nifanye nini wakati huo.
Binafsi mimi ni kijana mtaratibu sana, ninafanya mambo yangu kwa utaratibu na utulivu, sina papara wala hofu, Sio muongeaji sana - mimi ni mkimya mno ila ninapenda kuandika - ni mchangamfu sana kwenye maandishi.
Ninavutiwa na matendo zaidi kuliko maneno - action oriented. Ukiniambia well done nakua proud sana kuliko ukiniambia Well said.
Sipendi sauti kubwa iwe mtu anazungumza kwa kelele ama mziki mkubwa unapigwa [kichwa hunigonga sana] hivyo huwezi kunikuta kwenye sherehe au club yeyote au vibanda umiza.
Hua nakua comfortable sana ninapokua pekee yangu - nikikaa na watu wawili au watatu baada ya muda kidogo najihisi siko comfortable kabisa - naondoka, Hata shemeji yenu anajua kuna muda hua nataka tu kua pekee yangu, ila sasa ukinikuta kwenye mood hua napiga story kama OKOT P' BITEK.
Kukaa tu pekee yangu ikawa inakua boring hivyo nikawa nautumia muda wa peke yangu kucheki movie [Napenda movie zinazotisha sana], pia kusikiliza muziki [Hiphop], kusoma vitabu na articles tofauti tofauti - na hapa ndipo niliijua "JF", Nikajifunza meditation toka kwa Mshana Jr, hivyo nikaongeza jingine la kufanya ninapokua pekee yangu pia hua ninatumia alone time kufanya mazoezi na huyu ni mimi kwasasa Ibn Unuq.
Kuna bro mmoja jirani yetu Jimmy alikua anavutiwa na mimi akaniomba tuwe tunakimbia wote asubuhi.
Tukawa marafiki sana, akanifundisha kuendesha pikipiki yake aliyokua akiitumia kutembelea tu , hii ikanifungulia fursa, nikajitoa mhanga nikachukua pikipiki ya kupeleka pesa kwa siku, shilingi elfu7 kipindi hicho "Deiwaka'.
Kutokana na muonekano pamoja na usafi nilikua napata wateja wengi sana kwa siku - watu mchanganyiko.
Siku moja nilimpakia jamaa mmoja pale Soweto alikua anaenda Uyole, bhasi kwakua mimi sio muongeaji tulitembea kimya kimya mpaka tunafika, nilichovutiwa na huyu jamaa, yeye pia hakuongea chochote - tofauti na wateja wengine wao huvunja ukimya.
Aliposhuka akaniuliza "dogo mbavu, unakula chuma?" Nkamwambia yaah!! Akaniuliza bodaboda inalipa nikamwambia kiasi chake, Akasema amependa Confidence yangu, kuna dili la pesa ndefu anataka kunipa, nkamwambia sawa nipe namba tutaongea, Tukaachana!!
Nikampotezea tu, ikapita kama miezi mitatu hivi boss wangu wa ile pikipiki sijui kilimkuta nini, akasema anataka kuiuza, ana Emergency, Sasa mimi sio mtu wa Ku-beg beg, nikairudisha muda huo huo, nikamshukuru tu kwa kunisaidia mana kwa muda huu nilishapanga hadi ghetto langu tayari, nikarudi ghetto.
Nikawa nawaza nitafute boss mwingine, katika kufikiri nikamkumbuka yule jamaa wa dili la pesa ndefu, nikajiambia "Liwalo na liwe, nikamchekii".
Nilidhani nitatumia nguvu kubwa kumkumbusha, lakini nilivyomwambia mimi fulani akasema nakukumbuka, uko tayari? Nkasema ndiyo, akasema ntakupigia simu muda wowote nikupe maelekezo.
Ikapita kama siku 2, Jamaa akanicheki akaniambia saa1 usiku atanicheki anipe maelekezo.
Hawa jamaa wanamanage time aisee, Saa1 kamili simu ikalia, jamaa akaniambia niende mtaa wa Isyesye karibu na uwanja unaojaa maji, nkakodi boda chap - ningeweza kumuomba mshkaji wangu yeyote anisogeze lakini angeanza kuniuliza uliza nataka nikafanye nini?
Nilivyofika nikampigia simu, akaniuliza, unaiona hiyo pikipiki uwanjani, ifuate. Nikamwambia naiona Boxer BM150 akasema ichukue, Ina mafuta full Tank, nipitie hapa Nane nane getini, tuna safari ya Igawa, Nilitamani kuuliza ila nilivuokumbuka tunaenda wote nikajikaza nikaiwasha.
Ilikua ni boxer gear4 Mpyaaah!! ina funguo na Chest cover yake na Groves za kuendeshea, nlishtuka.
Kweli nikamkuta, akapanda, Jamaa akaniambia nijitahidi kuitembeza kadiri niwezavyo.
Sikuwahi tembeza chuma kama siku ile, Niljitahidi kutembea ila niliishia kutumia saa1 na madakika kufika igawa- kila utaponikuta mimi Ibn Unuq lazima niwe na stop watch, sababu ninapenda sana kuhesabu muda.
Mfano niwaibie siri, Mimi hua ninatumia dakika 7 sec 32 kwa round ya kwanza 🛏️, mzabzab unaweza hii 🤣🤣.
Tufocus na Story sasa;
Tukaingia njia ya porini sana, jamaa akanipa code nikiona gari, niwashe na kuzima taa mara4, Na mwenye gari inatakiwa awashe na kuzima mara5, huyo ndiye mwenzetu.
Tukafika sehemu tukaona gari Landcruiser prado kama hii 👇
iko mbele nikafanya vilevile na jamaa naye akawasha mara5 , tukapaki kuifuata.
Akauliza huyu ni begginer,Yule jamaa nlieenda nae akasema, dogo ana roho ya paka.
Tukaingia mlango wa nyuma wa ile cruiser, Aisee kulikua na jamaa wanne kila mmoja yuko busy na laptop yake - jamaa wa IT.
Mle ndani ya gari mlikua mmetapakaa laini za mitandao tofauti tofauti bado mpya kabisa zaidi ya 600.
Jamaa mmoja wa IT akasema wa makambako wameshafanikisha mission, Hivyo tuwahi haraka tukutane nao njiani, Akaniuliza unaweza kutumia hii, akawa amemulika taa kichakani nikaiona Pikipiki baja, nikasema naweza kuonyesha tu ubabe ila ukweli sikuwahi kuendesha baja, ikabidi niulize nisije nikapuyanga, hii ni gia ngapi? yule IT akasema tano, unapanga kama zingine tu.
Nikaiwasha, jamaa akapanda kama kawaida, unajua mi mrefu 5ft8, Hivyo Nilikua nayo comfortable sana, Sema kazi ilikua kila pikipiki nayokutana naya kuwasha taa mara4, nijibiwe mara5, maana nao walikua wanakuja na pikipiki.
Tukafanikiwa kukutana nao hata sijui ni wapi pale, hapo ni arround saa6 usiku, wakatugei bag ya mgongoni tukageuka tena kurudi igawa porini, jamaa akaingia na ile bag kwenye gari, Mi nkaambiwa nitulie nje, jamaa wako na muda kama dakika 10, jamaa yule akatoka akasema niwashe ile boxer, Turudi Mbeya.
Safari hii nilikua sina hofu tena, nilishajua nimeingia kwenye mchezo gani, ndani ya lisaa tukawa mbeya, Jamaa akasema nimuache uyole, hapohapo tukafunga na plate number halali, Jamaa akanipa laki4 na Elfu30 halafu akasema ile pikipiki nibaki nayo, nisiogope, niendelee kuzugia kama ndio kazi yangu, ila nikae mkao wa kula muda wote.
Nilitoka kwa hamu ili niwahi nikazipigie hesabu zile pesa ghetto, nilijiona tayari nina pikipiki boxer mpya na Pesa ya kutosha mfukoni, nikajiambia nikipiga dili5 hivi, nawakimbia naenda kuishi Dizim 🤣.
Bhasi nikashinda zangu nalala mpaka mida ya mchana, then nkaenda kijiweni kuzugia, jamaa wakaisifia sifia sana chuma, wengine wakajaribu kuiendesha, kwa Mbeya zilikua chache sana time hii.
Mi nikawambia nilipata boss mpya hivyo yule nimemrudishia chuma lake, Tena nikawaambia safari hii nimechukua mkataba kabisa.
[Mana Yule jamaa aliniambia siri ikivuja ni kifo].
Nikaendelea kuzunguka na yule jamaa sehemu tofauti tofauti, tukapiga kazi kama4 hivi [Nitaelezea zaidi siku nyingine- nazikumbuka zote hatarii sana].
Mimi kazi yangu ni udereva wa chap tuu, jamaa kazi yake kupokea tu pesa na mali tofauti usiku kwa usiku, Maana asubuhi inatakiwa tuwe mbeya, hakuna anayetakiwa kujua tulikua wapi usiku.
Na kwa kazi yangu ya bodaboda hata nikirudi saa7 usiku majirani wanajua kawaida tu, mana bodaboda wanakesha mpaka asubuhi, ndio maana hawa jamaa wanapenda kutumia madereva bodaboda.
Ila usiku plate number inabadilishwa, tunaweka fake.
Wahenga walisema za mwizi arobaini, Siku hiyo tukaingia porini bhana kama kawaida, tukafika mpaka chimbo la kupangia mikakati.
Wakati nakaribia nikawasha taa mara4 kama kawaida, ajabu Ile cruiser ikawasha mara3 badala ya mara5 tuliyoizoea.
Jamaa akasema kimenuka, wawashie tena, nikawasha tena mara4, , round hii akajibu vilevile tena mara3, Jamaa akaniambia tumejaa, Akili ikacheza, nikageuza chuma U-turn haraka, yani almanusra tuanguke.
Nilichomoka na Accelelator mtoni mpaka tairi ya mbele ikataka kuinuka.
PAAAH!! PAAH!!
Sikuwahi kusikia mlio wa risasi kwa ukaribu vilee, Niliishiwa nguvu, nikapoteza Controll, mimi na yule jamaa tukaenda chini na pikipiki yetu 😭.
Nitakuja kuimalizia hapa hapa wakuu, Tutafute pesa za halali, Lakini pia Hawa polisi tusiwachukulie poaa mazee, Nilinyooshwa.
Imeendelea post no323.
Sikuwahi kufikiria kuwa siku moja ningeweza kujikuta katikati ya mchezo hatari uliopangwa kwa ustadi wa hali ya juu.
Ilianza kama jambo la kawaida tu — ofa ya kuvutia na ahadi za mafanikio ya haraka.
Lakini kadri nilivyozidi kujihusisha, nilitambua kuwa nilikuwa nikiingia kwenye mtego wa kundi la matapeli wenye ujuzi wa hatari.
Huu ni ushuhuda wa jinsi nilivyokabiliana na hofu, kuchukua hatua ya ujasiri, na hatimaye kujinasua kutoka mikononi mwa kikundi hiki hatari.
Mimi Ibn Unuq baada ya kumaliza chuo cha NIT, Dar-es-salaam nilirudi nyumbani MBEYA, ili kutulia kusubiria ajira huku nikiangalia nifanye nini wakati huo.
Binafsi mimi ni kijana mtaratibu sana, ninafanya mambo yangu kwa utaratibu na utulivu, sina papara wala hofu, Sio muongeaji sana - mimi ni mkimya mno ila ninapenda kuandika - ni mchangamfu sana kwenye maandishi.
Ninavutiwa na matendo zaidi kuliko maneno - action oriented. Ukiniambia well done nakua proud sana kuliko ukiniambia Well said.
Sipendi sauti kubwa iwe mtu anazungumza kwa kelele ama mziki mkubwa unapigwa [kichwa hunigonga sana] hivyo huwezi kunikuta kwenye sherehe au club yeyote au vibanda umiza.
Hua nakua comfortable sana ninapokua pekee yangu - nikikaa na watu wawili au watatu baada ya muda kidogo najihisi siko comfortable kabisa - naondoka, Hata shemeji yenu anajua kuna muda hua nataka tu kua pekee yangu, ila sasa ukinikuta kwenye mood hua napiga story kama OKOT P' BITEK.
Kukaa tu pekee yangu ikawa inakua boring hivyo nikawa nautumia muda wa peke yangu kucheki movie [Napenda movie zinazotisha sana], pia kusikiliza muziki [Hiphop], kusoma vitabu na articles tofauti tofauti - na hapa ndipo niliijua "JF", Nikajifunza meditation toka kwa Mshana Jr, hivyo nikaongeza jingine la kufanya ninapokua pekee yangu pia hua ninatumia alone time kufanya mazoezi na huyu ni mimi kwasasa Ibn Unuq.
Kuna bro mmoja jirani yetu Jimmy alikua anavutiwa na mimi akaniomba tuwe tunakimbia wote asubuhi.
Tukawa marafiki sana, akanifundisha kuendesha pikipiki yake aliyokua akiitumia kutembelea tu , hii ikanifungulia fursa, nikajitoa mhanga nikachukua pikipiki ya kupeleka pesa kwa siku, shilingi elfu7 kipindi hicho "Deiwaka'.
Kutokana na muonekano pamoja na usafi nilikua napata wateja wengi sana kwa siku - watu mchanganyiko.
Siku moja nilimpakia jamaa mmoja pale Soweto alikua anaenda Uyole, bhasi kwakua mimi sio muongeaji tulitembea kimya kimya mpaka tunafika, nilichovutiwa na huyu jamaa, yeye pia hakuongea chochote - tofauti na wateja wengine wao huvunja ukimya.
Aliposhuka akaniuliza "dogo mbavu, unakula chuma?" Nkamwambia yaah!! Akaniuliza bodaboda inalipa nikamwambia kiasi chake, Akasema amependa Confidence yangu, kuna dili la pesa ndefu anataka kunipa, nkamwambia sawa nipe namba tutaongea, Tukaachana!!
Nikampotezea tu, ikapita kama miezi mitatu hivi boss wangu wa ile pikipiki sijui kilimkuta nini, akasema anataka kuiuza, ana Emergency, Sasa mimi sio mtu wa Ku-beg beg, nikairudisha muda huo huo, nikamshukuru tu kwa kunisaidia mana kwa muda huu nilishapanga hadi ghetto langu tayari, nikarudi ghetto.
Nikawa nawaza nitafute boss mwingine, katika kufikiri nikamkumbuka yule jamaa wa dili la pesa ndefu, nikajiambia "Liwalo na liwe, nikamchekii".
Nilidhani nitatumia nguvu kubwa kumkumbusha, lakini nilivyomwambia mimi fulani akasema nakukumbuka, uko tayari? Nkasema ndiyo, akasema ntakupigia simu muda wowote nikupe maelekezo.
Ikapita kama siku 2, Jamaa akanicheki akaniambia saa1 usiku atanicheki anipe maelekezo.
Hawa jamaa wanamanage time aisee, Saa1 kamili simu ikalia, jamaa akaniambia niende mtaa wa Isyesye karibu na uwanja unaojaa maji, nkakodi boda chap - ningeweza kumuomba mshkaji wangu yeyote anisogeze lakini angeanza kuniuliza uliza nataka nikafanye nini?
Nilivyofika nikampigia simu, akaniuliza, unaiona hiyo pikipiki uwanjani, ifuate. Nikamwambia naiona Boxer BM150 akasema ichukue, Ina mafuta full Tank, nipitie hapa Nane nane getini, tuna safari ya Igawa, Nilitamani kuuliza ila nilivuokumbuka tunaenda wote nikajikaza nikaiwasha.
Ilikua ni boxer gear4 Mpyaaah!! ina funguo na Chest cover yake na Groves za kuendeshea, nlishtuka.
Kweli nikamkuta, akapanda, Jamaa akaniambia nijitahidi kuitembeza kadiri niwezavyo.
Sikuwahi tembeza chuma kama siku ile, Niljitahidi kutembea ila niliishia kutumia saa1 na madakika kufika igawa- kila utaponikuta mimi Ibn Unuq lazima niwe na stop watch, sababu ninapenda sana kuhesabu muda.
Mfano niwaibie siri, Mimi hua ninatumia dakika 7 sec 32 kwa round ya kwanza 🛏️, mzabzab unaweza hii 🤣🤣.
Tufocus na Story sasa;
Tukaingia njia ya porini sana, jamaa akanipa code nikiona gari, niwashe na kuzima taa mara4, Na mwenye gari inatakiwa awashe na kuzima mara5, huyo ndiye mwenzetu.
Tukafika sehemu tukaona gari Landcruiser prado kama hii 👇
iko mbele nikafanya vilevile na jamaa naye akawasha mara5 , tukapaki kuifuata.
Akauliza huyu ni begginer,Yule jamaa nlieenda nae akasema, dogo ana roho ya paka.
Tukaingia mlango wa nyuma wa ile cruiser, Aisee kulikua na jamaa wanne kila mmoja yuko busy na laptop yake - jamaa wa IT.
Mle ndani ya gari mlikua mmetapakaa laini za mitandao tofauti tofauti bado mpya kabisa zaidi ya 600.
Jamaa mmoja wa IT akasema wa makambako wameshafanikisha mission, Hivyo tuwahi haraka tukutane nao njiani, Akaniuliza unaweza kutumia hii, akawa amemulika taa kichakani nikaiona Pikipiki baja, nikasema naweza kuonyesha tu ubabe ila ukweli sikuwahi kuendesha baja, ikabidi niulize nisije nikapuyanga, hii ni gia ngapi? yule IT akasema tano, unapanga kama zingine tu.
Nikaiwasha, jamaa akapanda kama kawaida, unajua mi mrefu 5ft8, Hivyo Nilikua nayo comfortable sana, Sema kazi ilikua kila pikipiki nayokutana naya kuwasha taa mara4, nijibiwe mara5, maana nao walikua wanakuja na pikipiki.
Tukafanikiwa kukutana nao hata sijui ni wapi pale, hapo ni arround saa6 usiku, wakatugei bag ya mgongoni tukageuka tena kurudi igawa porini, jamaa akaingia na ile bag kwenye gari, Mi nkaambiwa nitulie nje, jamaa wako na muda kama dakika 10, jamaa yule akatoka akasema niwashe ile boxer, Turudi Mbeya.
Safari hii nilikua sina hofu tena, nilishajua nimeingia kwenye mchezo gani, ndani ya lisaa tukawa mbeya, Jamaa akasema nimuache uyole, hapohapo tukafunga na plate number halali, Jamaa akanipa laki4 na Elfu30 halafu akasema ile pikipiki nibaki nayo, nisiogope, niendelee kuzugia kama ndio kazi yangu, ila nikae mkao wa kula muda wote.
Nilitoka kwa hamu ili niwahi nikazipigie hesabu zile pesa ghetto, nilijiona tayari nina pikipiki boxer mpya na Pesa ya kutosha mfukoni, nikajiambia nikipiga dili5 hivi, nawakimbia naenda kuishi Dizim 🤣.
Bhasi nikashinda zangu nalala mpaka mida ya mchana, then nkaenda kijiweni kuzugia, jamaa wakaisifia sifia sana chuma, wengine wakajaribu kuiendesha, kwa Mbeya zilikua chache sana time hii.
Mi nikawambia nilipata boss mpya hivyo yule nimemrudishia chuma lake, Tena nikawaambia safari hii nimechukua mkataba kabisa.
[Mana Yule jamaa aliniambia siri ikivuja ni kifo].
Nikaendelea kuzunguka na yule jamaa sehemu tofauti tofauti, tukapiga kazi kama4 hivi [Nitaelezea zaidi siku nyingine- nazikumbuka zote hatarii sana].
Mimi kazi yangu ni udereva wa chap tuu, jamaa kazi yake kupokea tu pesa na mali tofauti usiku kwa usiku, Maana asubuhi inatakiwa tuwe mbeya, hakuna anayetakiwa kujua tulikua wapi usiku.
Na kwa kazi yangu ya bodaboda hata nikirudi saa7 usiku majirani wanajua kawaida tu, mana bodaboda wanakesha mpaka asubuhi, ndio maana hawa jamaa wanapenda kutumia madereva bodaboda.
Ila usiku plate number inabadilishwa, tunaweka fake.
Wahenga walisema za mwizi arobaini, Siku hiyo tukaingia porini bhana kama kawaida, tukafika mpaka chimbo la kupangia mikakati.
Wakati nakaribia nikawasha taa mara4 kama kawaida, ajabu Ile cruiser ikawasha mara3 badala ya mara5 tuliyoizoea.
Jamaa akasema kimenuka, wawashie tena, nikawasha tena mara4, , round hii akajibu vilevile tena mara3, Jamaa akaniambia tumejaa, Akili ikacheza, nikageuza chuma U-turn haraka, yani almanusra tuanguke.
Nilichomoka na Accelelator mtoni mpaka tairi ya mbele ikataka kuinuka.
PAAAH!! PAAH!!
Sikuwahi kusikia mlio wa risasi kwa ukaribu vilee, Niliishiwa nguvu, nikapoteza Controll, mimi na yule jamaa tukaenda chini na pikipiki yetu 😭.
Nitakuja kuimalizia hapa hapa wakuu, Tutafute pesa za halali, Lakini pia Hawa polisi tusiwachukulie poaa mazee, Nilinyooshwa.
Imeendelea post no323.