Nilivyopelekwa milembe wakidhani mi kichaa kumbe ni mzima

Nilivyopelekwa milembe wakidhani mi kichaa kumbe ni mzima

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Kuna miaka nilikuwa mkoa fulani katika kupambana na maisha, nikapanga room mi na mwamba mmoja tuliyetoka nae mjini, huyu mwamba ikifika usiku mnene ananiamsha nakunionyesha watu au mtu ambaye simuoni, nikadhani anakuwa anaota, tukiamka ndio ananiambia kuwa jana usiku huyu mama wa nyumba ya jirani alikuja kutuwangia uchi, nikimuuliza kajuaje akadai ana dawa za kupaka machoni.

Siku moja nikamuomba kupaka zile dawa jioni halafu tukaenda kwenye harusi moja huko kijijini, nilichokiona sitasahau, watu walikuwa wanacheza ngoma uchi, mara wanatumia mafuvu kunywa pombe, kumbe zile dawa zinafanya kazi, kilichonifanya nikamatwe na kupelekwa milembe ni baada ya kuona kundi la fisi linakuja kila nikipiga kelele watu wanashangaa hao fisi wako wapi?

Jamaa mmoja akasema funga kamba pekeka Milembe, njiani wale fisi wakadandia pick up nikazidisha kelele, kilichoniokoa ni yule mwamba kuja kufuta zile dawa machoni mwangu.
 
Uzima ni kulingana na jamii husika..., kwa jamii iliyokuzunguka wewe sio mzima huwezi kuona fisi alafu ukajiita mzima ingawa huenda wewe ndio mzima lakini wengine wagonjwa ila ndio hivyo sababu upo peke yako inabidi upelekwe kwa wenzako mnaoona vitu ambavyo havionekani
 
Uzima ni kulingana na jamii husika..., kwa jamii iliyokuzunguka wewe sio mzima huwezi kuona fisi alafu ukajiita mzima ingawa huenda wewe ndio mzima lakini wengine wagonjwa ila ndio hivyo sababu upo peke yako inabidi upelekwe kwa wenzako mnaoona vitu ambavyo havionekani
Uko sahihi
 
Back
Top Bottom