Nilivyoweza kujinasua kwenye gharika la ndugu omba omba, Nilionekana mbahili lakini wanaanza kunielewa, pesa yangu siwezi kuitoa bila uwajibikaji

Nilivyoweza kujinasua kwenye gharika la ndugu omba omba, Nilionekana mbahili lakini wanaanza kunielewa, pesa yangu siwezi kuitoa bila uwajibikaji

Nilichofurahia kutoka kwako, wewe siyo wale matajiri kuvizia, yaani ndugu mmoja akiharibu utasikia, yaani sisaidii ndugu tena. Kwani ndugu mmoja akiharibu, si unaachana naye, akijitokeza mwingine mwenye kiu ya kupambana si unamsaidia tu! Mana ndugu wanatofautiana. Tupeane support tu!
Sina utajiri wowote, hali ya kiuchumi ya kawaida, ni kwamba kwa tamaduni zetu ni ngumu kukwepa black tax, Nilichoongeza ni uwajibikaji.
 
Wasaideni watu kama Mungu kakupa fursa ya kufanya hivo...

Katika vitu najivunia ni kua na moyo wa kutoa sana msaada kwa watu hata nisiowajua... Hata humu JF nimeshasaidia watu wengi tu kupata vibarua na hata watujuani na sijataka tujuane wengine hadi hulazimisha kunipa zawadi ila hua mara nyingi nakataa ni mmoja tu niwewahi kuchukua shukurani yake..

Kuna kipindi nilikua nimepigika sana Mungu akanifungulia milango nikapata mchongo.. kama kawaida simu kutoka kwa ndugu na jamaa zilikua nyingi na Mimi nilikua nawasaidia bila kujiuliza mara mbili...

Nakumbuka wakati wa changamoto baada ya kupoteza kazi mke wangu alikua anakaribia kuzaa Sina hili wa lile nikampigia rafiki mmoja ambaye niliwahi kumpa chaka mahala.. huwezi amini jamaa baada ya kumweleza shida zangu alinitumia milioni Moja na nusu sio mkopo.!

Kwahiyo usifikiri wewe umeyamaliza maisha na kuwaona wengine wajinga kwenye maisha Kuna kupanda na kushuka...

BEN MWAITEGE - SAFARI BADO
 
Wasaidien ndugu zenu acheni roho mbaya

Unakuta mtu mmoja umejilimbikizia uchumi mwingi sana alafu ndugu zako wote masikin mafukara wa kutupwa

Hata ikitokea umekufa hakuna hata ndugu yako mmoja mwenye uwezo wa kununulia hata jeneza la laki mbili
This is a strawman argument fallacy.

Jifunze kusoma kwa ufahamu na kujadili kimantiki si kubishana kwa ushabiki kihisia.

Mtoa mada hajapinga kusaidia ndugu, ameongelea misingi ya kuongeza ufanisi na kupunguza kusaidiana kusiko na tija ambako kutamfunga katika umasikini msaidia na msaidiwa.

Huelewi wapi?
 
This is a strawman argument fallacy.

Jifunze kusoma kwa ufahamu na kujadili kimantiki si kubishana kwa ushabiki kihisia.

Mtoa mada hajapinga kusaidia ndugu, ameongelea misingi ya kuongeza ufanisi na kupunguza kusaidiana kusiko na tija ambako kutamfunga katika umasikini msaidia na msaidiwa.

Huelewi wapi?
Bhebhe nzunya kinehe

Christmas 🎄 elelo
 
Katika jamii nyingi za kiafrika kuna kodi inaitwa Black Tax, Ukisha onekana una kipato simu zinaanza kuita, yaani tayari ushavikwa jukumu la kusaidia ndugu wa familia, ndugu wa baba, ndugu wa mama hadi wa mke.

Katika vitu ambavyo ningependa kuvijua tangu mwanzoni ni hivi
  • Usije kutaja kipato chako halisi, pendelea kutaja kipato kinachobaki baada ya kodi, matumizi, shughuli za uwekezaji, n.k. wengi ukiwaambia unapata kiasi flani, huchukulia ni kiasi kitachoweza kumudu misaada.
  • Kupaumbele cha misaada kiwe kusaidia watu wajifunze kujitegemea mfano kutoa mtaji, kukodi shamba, kulipia ada, peleka veta, n.k. Saidia kufundisha kuvua samaki sio kuwapa samaki
  • Hakikisha pesa unayotoa kuna UWAJIBIKAJI NA UWAZI WA MATOKEO

Nitazungumzia zaidi point ya tatu UWAJIBIKAJI NA UWAZI WA MATOKEO

Tatizo sio kutoa msaada bali ni kwamba waafrika wengi tunasahau kitu muhimu sana kinachoitwa UWAJIBIKAJI.

Asili ya binadamu inaonyesha kuwa kila inapokosekana uwajibikaji, unyonyaji huwa mkubwa. Na ndivyo ilivyo hata kwa watanzania wanaoishi Marekani na Ulaya wanapotuma pesa nyumbani, Wanarudi likizo hakuna kilichoendelea, Ncho yetu inapewa misaada mingi kwa miaka mingi lakini inaishia kuchezewa na viongozi kwasababu hakuna UWAJIBIKAJI.

Mara nyingi, nimewaambia wanafamilia na Ndugu wa baba / mama / mke kwamba wanaponiomba msaada wasinipe tu makadirio ya matumizi yao bali kuwe na uwajibikaji na matokeo nayoweza kuyafuatilia au kuyaona,

Mwanzoni waliniita mbahili / Kauzu, Nami nilikaza sikutoa chochote nilipoona msaada wa mwisho hauna uwajibikaji wala matokeo.

Nilikuwa nalipia ada za shule lakini ndugu hawakuwahi kunipa matokeo ya masomo, nakuja kugundua baadae kwamba mtu haendi hata shuleni, matokeo ni mabovu, n.k.

Baada ya visa vingi nimekuwa nikisema wazi kabisa kuwa ikiwa sitapata matokeo ya pesa zangu, sitatoa pesa. Nafanya kazi kwa bidii sana, siwezi kutoa pesa kwa watu ambao ni wazima wenye afya lakini hawapo tayari kuwajibika na kunipa access ya matokeo ya pesa niliyowapa, yaani kwao kupokea pesa inakuwa kama njia ya kuishi.

Haijalishi hali ya umasikini, ikiwa uwajibikaji na matokeo havipo, kuna uwezekano mkubwa sana pesa zitatumika vibaya. Siwezi tena kutoa pesa kwa ajili ya mtaji wa biashara bila masharti ya uwajibikaji na kweli kwa msimamo niliojenga watu huwa wanajua namaanisha nachosema.

Unataka pesa kwa ajili ya biashara? Nipe business plan, Nionyeshe umedhamiria kuwajibika, furaha yangu nione unajitegemea, sihitahi hata senti yako.

Unataka Nikusomeshe ? Nionyeshe una uhitaji wa elimu, niwe updated na matokeo yako hata kama sio mazuri tujue namna ya kuyaboresha.

Unataka kulima ? Niambie shamba lipo wapi nikakukodie, nishirikishe kwenye matokeo.

Misimamo yangu leo hii haijaleta matokeo makubwa sana ila naweza kujivunia

Kuna ndugu alikuwa kahitimu chuo hana kazi, nilimsaidia mtaji kidogo mwanzoni na kunionesha ana kiu, nikamuongezea zaidi, kwa sasa nafurahi kumuona tunawashiana taa barabarani

Ndugu wa mke waliokuja kumsalimia na kuishia kukaa miezi niliwatafutia sehemu ya kujifunzia kazi, mwanzoni nilipingwa nanyanyasa wageni lakini leo hii wana shughuli zao zinazowaingizia vipato na moja kaoa tayari

Mwengine kamaliza chuo kwa gpa bomba, kwa sasa kajishikiza kwenye uteller wa benki, nafurahi namna anavyopambana

Pesa siyo za bure; kila wakati zina gharama kwa mtu. Kwa hivyo, kabla ya kumsaidia mtu yeyote, daima nasisitiza nia yao ya kuwajibika na kuwepo kwa uwazi wa matokeo. Ikiwa baada ya muda sioni sifa hizi, pesa zangu hukauka na hazirudi tena.

Ninatoa msamaha tu kwa masuala yanayohusiana na afya, isipokuwa yale yanayosababishwa na mtu mwenyewe, kama vile wajomba walevi wanaojiletea matatizo ya kiafya kwa kunywa kupita kiasi bila nia ya kuacha
Wewe una sifa? YEye hana yes wewe vipi?
 
Nendeni PM wakuu, naona uzi ushabadilika kuwa wa kilugha 😂
Mkuu,

Kama Muislamu akipewa "Asalaam Aleikum" ilivyokuwa vibaya sana kukataa kuirudishia "Aleikum Salaam" na sisi Wasukuma mtu akikusalimia au kukuongelesha Kisukuma kama unakijua ni kitu kibaya sana kutomrudishia Kisukuma.

Nimeelewa hilo unalolisema ndiyo maana sijaendeleza mazungumzo.

Wewe ndiye unayaendeleza sasa.
 
Wasaideni watu kama Mungu kakupa fursa ya kufanya hivo...

Katika vitu najivunia ni kua na moyo wa kutoa sana msaada kwa watu hata nisiowajua... Hata humu JF nimeshasaidia watu wengi tu kupata vibarua na hata watujuani na sijataka tujuane wengine hadi hulazimisha kunipa zawadi ila hua mara nyingi nakataa ni mmoja tu niwewahi kuchukua shukurani yake..

Kuna kipindi nilikua nimepigika sana Mungu akanifungulia milango nikapata mchongo.. kama kawaida simu kutoka kwa ndugu na jamaa zilikua nyingi na Mimi nilikua nawasaidia bila kujiuliza mara mbili...

Nakumbuka wakati wa changamoto baada ya kupoteza kazi mke wangu alikua anakaribia kuzaa Sina hili wa lile nikampigia rafiki mmoja ambaye niliwahi kumpa chaka mahala.. huwezi amini jamaa baada ya kumweleza shida zangu alinitumia milioni Moja na nusu sio mkopo.!

Kwahiyo usifikiri wewe umeyamaliza maisha na kuwaona wengine wajinga kwenye maisha Kuna kupanda na kushuka...

BEN MWAITEGE - SAFARI BADO
🤝
 
Wasaidien ndugu zenu acheni roho mbaya

Unakuta mtu mmoja umejilimbikizia uchumi mwingi sana alafu ndugu zako wote masikin mafukara wa kutupwa

Hata ikitokea umekufa hakuna hata ndugu yako mmoja mwenye uwezo wa kununulia hata jeneza la laki mbili
Mkuu sio rahisi. Mimi naweza kukwambia asilimia 80% ya mapayo yangu huishia kwa ndugu lakini hakuna ambaye hata amepiga hatua ya kujitegemea kasoro mmoja tu.
Ni jambo linaniap stress sana and almost wote ni over 28
 
NINYI VIUMBE BINADAMU MNA MAPUNGUFU MAKUBWA SANA

MMEPEWA HEWA YA BURE NA BABA YENU WALA HAMLIPII LAKINI NINYI KUWASAIDIA NDUGU ZENU MNAWAPIGIA MAHESABU

HAKIKA MNA LAANA NDANI YENU, ITAWATESA SANA

HAKUNA BINADAMU MKAMILIFU PASIPO WENZAKE, KWENYE HALI YA MATATIZO WATAKAOWASAIDIA NI WATU WENGINE KWAMAANA KUWA WAKATI HUO NINYI HAMTAWEZA KUJISAIDIA WENYEWE
 
Mkuu sio rahisi. Mimi naweza kukwambia asilimia 80% ya mapayo yangu huishia kwa ndugu lakini hakuna ambaye hata amepiga hatua ya kujitegemea kasoro mmoja tu.
Ni jambo linaniap stress sana and almost wote ni over 28

Yes , watu hawaelewi hili jambo .

Ndo maana ni vizuri MTU ukampatia mbinu za kujimpambania yeye Kama yeye . mfano kumtafutia kibarua , n.k

Maana hamna hela ambayo utampatia MTU na akapiga hatua . wachache ndo wanaweza .
 
Back
Top Bottom