Niliwaambia wazazi wasubiri niweke mambo yakae sawa wakanigomea, sasa naona yakitimia

Niliwaambia wazazi wasubiri niweke mambo yakae sawa wakanigomea, sasa naona yakitimia

T-Bagwell

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2017
Posts
1,243
Reaction score
2,378
Habarini wana jukwaa.


Mwanzoni mwa mwaka jana (December 2024) wazazi wangu walinishauri tutume wawakilishi waende nyumbani kwa wazazi wa mchumba wangu kwaajili ya utambulisho.

Japokua Binti nilishaanza kuishi naye kwa zaidi ya miezi mitatu, ilihali tulishakaa kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka minne.

Niliwataarifu wazazi kwamba wasubirie kwanza mpaka nitakapoweka mambo sawa ndipo nitawaambia ili tuanze taratibu zote mpaka NDOA.

Binafsi mimi sio mfuasi wa DINI kwahiyo swala la ndoa nilipanga kufunga naye ndoa ya KIMAHAKAMA (Japokua hili sikuwashirikisha wazazi kwasababu ni wafuasi sana wa Dini) na pia sikupanga tarehe, mwezi au mwaka (Nilitegemea akishajifungua ndipo nitaanza kuweka taratibu za tarehe na mwezi wa tukio hilo)

Wazazi walikazania sana hilo swala pasipo kunisikiliza, ikafika mpaka hatua wakasema kama unahofia gharama basi sisi tutagharamia…. Ikabidi niwe mpole.

Wakapanga tarehe, wakapanga watu wa kwenda kisha wakanitaarifu nikatoa baadhi ya fedha kwaajili ya ku sapoti shughuli kisha watu wakaenda.

Walipewa tarehe ya mwisho wa mwaka ndipo wapeleke baadhi ya mahitaji mengine/fedha kiandaliwe chakula kwa pamoja ili ndugu zake na wakwangu waweze kufahamiana.

(KULIKUA NA CHANGAMOTO ZA HAPA NA PALE KUTOKANA NA KUTOKUFIKA KWA TAARIFA KUTOKANA NA CHANGAMOTO YA FAMILIA YAO)

Tulijadiliana na wazazi na mwisho wa mwaka ulishindikana kutokana na ratiba zilizokuwepo kwa upande wa ukoo wangu mwisho wa mwaka.

Juzi kabla ya Christmas aliniambia ameitwa kwao na baba yake kwaajili ya kikao, nikamkatalia akalalamika mpaka kufikia stage ya kulia.

Tarehe 28 walipiga simu kwetu kudai kwamba wanamhitaji binti yao kwaajili ya mazungumzo, wazazi wakanipigia nikawambia hawezi safiri mwenyewe kwasababu pia ni MJAMZITO na kama week mbili zilizopita aliumwa na kulazwa mpaka mimba ikatishia kutosha, akahudumiwa na kushauriwa apate muda wa kutosha wa kupumzika.

Baba yake akataka namba yangu azungumze na mimi nikamwambia binti asimpe, baadae nikawasiliana na wazazi wangu nikaona isiwe shida, jioni yake nilimwambia awasiliane na rafiki yake kisha nitawapeleka… kweli alifanya hivyo na rafiki yake alikubali.

Jioni ilifika nikawapeleka japokua sikuwafikisha nyumbani kwao kabisa, nikawakodishia usafiri mwingine then mimi nikaendelea na safari ya kuelekea migombani. (KILIMANJARO)

(HII SAFARI YA KWENDA KWETU ILIKUA NIMEPENGA KWENDA NAE ILI PIA AKAJUMUIKE NA NDUGU ZANGU)

Mwaka mpya ukafika na safari yangu ya kurudi ilikaribia, nikampigia simu usiku wa tarehe moja kumuuliza kama kesho yake tarehe mbili asubuhi atakua tayari ili nimpitie turudi wote nyumbani akaniambia kuna maongezi wanamalizia then yeye atakuja jioni yake/kesho yake asubuhi tarehe 2 nikaona sio shida kwasababu bado kuna ndugu zangu bado walikuwepo migombani so ingekua rahisi kumpa lift kupunguza changamoto za public transport lakini haikua hivyo kutokana na sababu alizoleta za hapa na pale

Leo asubuhi nimeamka najiandaa na harakati za siku napokea simu nyumbani kwamba upande wa mwanamke wamekaa na wametupa tarehe 15/01 kwamba ndio tarehe ya hilo tukio kwahiyo tunapaswa tutume kiasi cha fedha kwaajili ya maandalizi ya hiyo siku.

Kila nikiangalia nafasi ya hiyo tarehe kwa upande wangu na wazazi wangu inakosekana, lakini pia January ni mwezi mgumu karibia kwa kila mtu.

Nawaza ku abort mission lakini in a good way, nachomokaje kwenye hili wakuu… kwasababu tokea mwanzo nilikua namkataza mwenzangu asiende nikitegemea yote haya lazima yatatokea.

Lakini pia wazazi wangu wamechangia yote haya kwasababu nilishawaonya tokea mwanzo lakini walikataa kunisikiliza.
 
Fuata busara za wazee wako boss.

Binti hukuwa umemuoa ila ukajipa umuhimu mpaka unamgomea mzee wake binti ni lini aende kwao.
Hauna discpline kabisa mkuu, 0nadhani ni kwasababu ya kutokuwa na hofu ya MUNGU hivyo hata wazazi unawachukulia poa. Kuna koo huwezi fanya hichi kitu, wazee wanakwambia hatumtambui huyo binti ni wako.
 
Fuata busara za wazee wako boss.

Binti hukuwa umemuoa ila ukajipa umuhimu mpaka unamgomea mzee wake binti ni lini aende kwao.
Hauna discpline kabisa mkuu, 0nadhani ni kwasababu ya kutokuwa na hofu ya MUNGU hivyo hata wazazi unawachukulia poa. Kuna koo huwezi fanya hichi kitu, wazee wanakwambia hatumtambui huyo binti ni wako.
Kumuogopa Mungu kuna uhusiano gani na niliyoyaandika hapo, wazazi wangu wenyewe wameshangaa kwanini imekua ghafla hivyo na sasa wapo upande wangu.

Je nikimiuacha akaendelea kukaa kwao huoni kama ndio nitaonekana nina madharau??
 
Habarini wana jukwaa.


Mwanzoni mwa mwaka jana (December 2024) wazazi wangu walinishauri tutume wawakilishi waende nyumbani kwa wazazi wa mchumba wangu kwaajili ya utambulisho.

Japokua Binti nilishaanza kuishi naye kwa zaidi ya miezi mitatu, ilihali tulishakaa kwenye mahusiano kwa zaidi ya miaka minne.

Niliwataarifu wazazi kwamba wasubirie kwanza mpaka nitakapoweka mambo sawa ndipo nitawaambia ili tuanze taratibu zote mpaka NDOA.

Binafsi mimi sio mfuasi wa DINI kwahiyo swala la ndoa nilipanga kufunga naye ndoa ya KIMAHAKAMA (Japokua hili sikuwashirikisha wazazi kwasababu ni wafuasi sana wa Dini) na pia sikupanga tarehe, mwezi au mwaka (Nilitegemea akishajifungua ndipo nitaanza kuweka taratibu za tarehe na mwezi wa tukio hilo)

Wazazi walikazania sana hilo swala pasipo kunisikiliza, ikafika mpaka hatua wakasema kama unahofia gharama basi sisi tutagharamia…. Ikabidi niwe mpole.

Wakapanga tarehe, wakapanga watu wa kwenda kisha wakanitaarifu nikatoa baadhi ya fedha kwaajili ya ku sapoti shughuli kisha watu wakaenda.

Walipewa tarehe ya mwisho wa mwaka ndipo wapeleke baadhi ya mahitaji mengine/fedha kiandaliwe chakula kwa pamoja ili ndugu zake na wakwangu waweze kufahamiana.

(KULIKUA NA CHANGAMOTO ZA HAPA NA PALE KUTOKANA NA KUTOKUFIKA KWA TAARIFA KUTOKANA NA CHANGAMOTO YA FAMILIA YAO)

Tulijadiliana na wazazi na mwisho wa mwaka ulishindikana kutokana na ratiba zilizokuwepo kwa upande wa ukoo wangu mwisho wa mwaka.

Juzi kabla ya Christmas aliniambia ameitwa kwao na baba yake kwaajili ya kikao, nikamkatalia akalalamika mpaka kufikia stage ya kulia.

Tarehe 28 walipiga simu kwetu kudai kwamba wanamhitaji binti yao kwaajili ya mazungumzo, wazazi wakanipigia nikawambia hawezi safiri mwenyewe kwasababu pia ni MJAMZITO na kama week mbili zilizopita aliumwa na kulazwa mpaka mimba ikatishia kutosha, akahudumiwa na kushauriwa apate muda wa kutosha wa kupumzika.

Baba yake akataka namba yangu azungumze na mimi nikamwambia binti asimpe, baadae nikawasiliana na wazazi wangu nikaona isiwe shida, jioni yake nilimwambia awasiliane na rafiki yake kisha nitawapeleka… kweli alifanya hivyo na rafiki yake alikubali.

Jioni ilifika nikawapeleka japokua sikuwafikisha nyumbani kwao kabisa, nikawakodishia usafiri mwingine then mimi nikaendelea na safari ya kuelekea migombani. (KILIMANJARO)

(HII SAFARI YA KWENDA KWETU ILIKUA NIMEPENGA KWENDA NAE ILI PIA AKAJUMUIKE NA NDUGU ZANGU)

Mwaka mpya ukafika na safari yangu ya kurudi ilikaribia, nikampigia simu usiku wa tarehe moja kumuuliza kama kesho yake tarehe mbili asubuhi atakua tayari ili nimpitie turudi wote nyumbani akaniambia kuna maongezi wanamalizia then yeye atakuja jioni yake/kesho yake asubuhi tarehe 2 nikaona sio shida kwasababu bado kuna ndugu zangu bado walikuwepo migombani so ingekua rahisi kumpa lift kupunguza changamoto za public transport lakini haikua hivyo kutokana na sababu alizoleta za hapa na pale

Leo asubuhi nimeamka najiandaa na harakati za siku napokea simu nyumbani kwamba upande wa mwanamke wamekaa na wametupa tarehe 15/01 kwamba ndio tarehe ya hilo tukio kwahiyo tunapaswa tutume kiasi cha fedha kwaajili ya maandalizi ya hiyo siku.

Kila nikiangalia nafasi ya hiyo tarehe kwa upande wangu na wazazi wangu inakosekana, lakini pia January ni mwezi mgumu karibia kwa kila mtu.

Nawaza ku abort mission lakini in a good way, nachomokaje kwenye hili wakuu… kwasababu tokea mwanzo nilikua namkataza mwenzangu asiende nikitegemea yote haya lazima yatatokea.

Lakini pia wazazi wangu wamechangia yote haya kwasababu nilishawaonya tokea mwanzo lakini walikataa kunisikiliza.
Jilipue tu. Utaendelea kupostpone mpaka lini?? Ukiingalia kwa mtizamo wa kwamba sina hela ya kutosha, utaendelea kupostpone wakati wote.
 
Jilipue tu. Utaendelea kupostpone mpaka lini?? Ukiingalia kwa mtizamo wa kwamba sina hela ya kutosha, utaendelea kupostpone wakati wote.
Nilijipanga kwa mwezi wa 3/4 itakapoangukia pasaka kwasababu january hii hela hamna lakini pia ni ngumu hata kumualika mtu akakuelewa.
 
Ulizingua ulivyomgomea binti kwenda kwao na hutambuliki kitaratibu, hayo mengineyo waachie wazee na mshenga watayaweka sawa ila jiandae mfuko usiwe mtupu.
Mfuko ni mtupu
Ulizingua ulivyomgomea binti kwenda kwao na hutambuliki kitaratibu, hayo mengineyo waachie wazee na mshenga watayaweka sawa ila jiandae mfuko usiwe mtupu.
Sababu za kumgomea nilishaziweka hapo juu lakini pia sikumgomea directly.. nilimwambia awaambie kwamba hali yake si sawa na ameshauriwa apumzike.

Nilianza kuishi naye kwasababu ya hali yake si sawa ujauzito na isionekane Kama nakwepa majukumu na hata wakati wazee watoa wazo la kwenda huko kwao hawakujua kuhusu hali yake.
 
Mfuko ni mtupu

Sababu za kumgomea nilishaziweka hapo juu lakini pia sikumgomea directly.. nilimwambia awaambie kwamba hali yake si sawa na ameshauriwa apumzike.

Nilianza kuishi naye kwasababu ya hali yake si sawa ujauzito na isionekane Kama nakwepa majukumu na hata wakati wazee watoa wazo la kwenda huko kwao hawakujua kuhusu hali yake.
Waambie wazee wako uhalisia wa hali yako ili kama wataweza kukusaidia gharama wafanye hivyo au waongee na wazee upande wa pili.
 
Kwasababu Gani? Unajua hatuelewi unachotaka kujitetea. mahali si ipo?
Issue sio Mahari pekee.

Mahari inaweza isiwe shida japokua bado hawajatutajia lakini wako na expectations kubwa tofauti na mimi.

Wakati naongea na wazee nyumbani ni kwamba wamepanga baada ya hapo watoe tarehe ya pete, sijui sendoff kisha harusi pasipo kujua kwamba mimi sina mpango na hizo sherehe wanazoziwaza.
 
Issue sio Mahari pekee.

Mahari inaweza isiwe shida japokua bado hawajatutajia lakini wako na expectations kubwa tofauti na mimi.

Wakati naongea na wazee nyumbani ni kwamba wamepanga baada ya hapo watoe tarehe ya pete, sijui sendoff kisha harusi pasipo kujua kwamba mimi sina mpango na hizo sherehe wanazoziwaza.
Okk Sawa nimekuelewa, sasa hivi ulivyoniambia nakushauri kamwambie mkwe na kikao Cha wote hivi hivi watakuelewa. Utoe tu mahali Yao ndoa mtafunga popote
 
Back
Top Bottom