Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Sehemu ya Tisa:


Anwari aliniambia anafahamu ya kwamba nina mtoto, mtoto wa kiume, na mtoto huyo umri wake unawiana sawa na muda tulokutana mimi na yeye.

Hapo nikamgomea, si kwamba hatukukutana, lah, bali nilimwambia muda huo nilishiriki tendo pia na mume wangu, hivyo yeye ana uhakika gani kama kweli mtoto yule ni wake?

Nilimuuliza nikiwa nayajenga yangu kichwani, bwana yule hajui ninapoishi wala wapi ninapofanya kazi, alitambuaje kama nina mtoto? Alitambuaje kama nilipata mimba?

Akili yangu ikanambia ni Zai. Hamna mtu mwingine isipokuwa yeye. Zai alimwambia Anwari kuwa mimi nina mimba na akamwambia nimepata mtoto.

Zai alimwambia kila kitu isipokuwa mahali ninapoishi na mahali ninapofanya kazi. Bila shaka angefanya hivyo, tayari Anwari angelifika getini kunigongea.

Lakini kwanini Zai aliyasema yale? ... Sikukaa nikajua.

Tuliendelea kuzozana na Anwari tusipate muafaka, na kwasababu muda ulinitupa mkono, nikamwambia nataka kwenda zangu nyumbani, siku nyingine tukionana panapo majaliwa basi tutaongea.

Bwana huyo akakataa.

Alinambia haniamini maana sikawii kum-block akahangaika tena kama hapo awali, kuhangaika mpaka kumhusisha Zai.

Na mimi kwasababu sikutaka aendelee kuwasiliana na Zai kuhusiana na lile jambo letu, nikaona ni vema nimpatie Anwari uhakika wa kunipata muda wowote atakaonitafuta.

Yale alokuwa anayajua Zai yanatosha, sikutaka azidishe tena hata punje.

Basi nikamwambia namba yangu nilompigia ndo' hiyohiyo itakayokuwa hewani milele. Akinihitaji anitafute aidha kwa kupiga ama kutume ujumbe, lakini nilimpa onyo asinitafute majira ya usiku, mimi ni mke wa mtu na sikuwa radhi kuivunja familia yangu kwa muda huo.

Baada ya hapo nikaondoka kurejea shuleni, nikamchukua mwanangu na kwenda naye moja kwa moja nyumbani.

Sikufahamu, kumbe Anwari alikuwa ananifuatilia nyendo zangu mpaka mwisho.

Kwasababu ya kujificha nisimwone na kumtambua, Anwari aliacha gari lake mahali fulani akanifuata kwa kutumia usafiri wa kukodi.

Hiyo ndo' sababu pekee sikufanikiwa kumwona siku ile, laiti angelitumia gari lake ambalo nalifahamu vema kama kiganja cha mkono wangu, isingenichukua macho mawili kumbaini.

Hata kama gari hilo lingekuwa limebadili rangi yake ya muda mrefu.

Nakumbuka gari lile lililombeba Anwari kunifuatilia, nilipata kulishuhudia kwa macho yangu kabisa lakini sikufikiria kwa muda huo kama gari lile lipo kwenye misheni maalum, nilidhani ni gari tu lenye shughuli zake, limembeba mtu ama watu wanaokaa katika mandhari yale, kuja kubaini nilikuwa nimeshachelewa.

Siku Anwari ananambia baada ya kumuuliza amepajuaje kwangu , maelezo anayonipa ndo' yananirejeshea kwenye fikra ya gari lile.

Gari dogo rangi ya fedha nililoliona kwa umbali wa mita kadhaa, muda mfupi tangu niliposhuka toka kwenye gari lile la shule linalonichukua na kunirejesha.

Basi siku ile niliyoonana na Anwari, nilifika nyumbani, kama ada, nikafanya kazi zangu na kuweka kila kitu sawa.

Nakumbuka siku hiyo nilimkuta mume wangu kesharudi nyumbani, yu pamoja na Amiri wakishughulikia mifugo.

Bwana huyo alinambia siku hiyo alirejea mapema nyumbani, majira ya mchana, maana alikuwa amechoka sana kwasababu ya ule ulevi wa jana yake usiku, alilalamika kichwa kilimsumbua kweli kazini achilia mbali uchovu hivyo akaona ni vema kurejea mapema.

Lakini mbali na hayo, alinambia habari mbaya alokuta pale nyumbani, matetea mawili ya kuku yalokuwa yanatamia mayai yamekutwa yamekauka huko bandani majira ya asubuhi.

Na chanzo cha matetea hayo kufa, hamna alokuwa anajua.

Habari hiyo ikanikumbusha upesi usiku ule wa jana, usiku ule niliposikia kuku wanalia na kuparura kule bandani.

Kumbe yale nilokuwa nawaza yalikuwa ni sahihi - ya kwamba kuna mdudu ama mnyama aliingia mule bandani?

Mume wangu alinambia wamekagua banda zima pamoja na Amiri lakini hawajaona sehemu yenye uwazi wa kuingiza hata nyoka, hawajui imekuaje kuku wale wakafa kwahiyo basi walihitimisha huenda ni ugonjwa hivyo kuku wapatiwe chanjo upesi.

Niliwatazama kuku wale walokufa, kweli walikuwa wamekauka kana kwamba mti mkavu, viungo vyao vimekakamaa mno, si mbawa wala miguu yao ilokuwa inajikunja, nikahamaki ule ni ugonjwa gani ulowapata?

Kwasababu sikuwa na ufahamu wowote na mambo ya mifugo, nilinyamaza kimya maisha yakaendelea.

Kesho yake, mapema asubuhi, niliwasiliana na rafiki yangu Zai kumjulia hali.

Alinambia ameshatoka hospitali, sasa yuko kwa ndugu yake kwasababu ya uangalizi mpaka pale atakapojihisi yuko sawa.

Nilimuuliza Zai kama alimwambia chochote Anwari kuhusu mimi, Zai akakataa katakata. Nilimweleza Anwari alikuwa anajua kuhusu ujauzito wangu na sasa anajua kama nina mtoto, habari hizo kazitoa kwa nani? Zai akasema hajui kitu.

Hajawahi kuongea jambo lolote na Anwari.

Basi nikampatia ujumbe kuwa kuanzia muda huo sitaki amwambie Anwari kitu chochote kile kunihusu mimi. Sitaki kabisa wanizungumzie huko watakapokutana ama kuongea.

Niliongea kwa kufoka na swala hilo likamkwaza Zai. Alinyamaza kunisikiliza nikiropoka mpaka mwisho wake pasipo kutia neno alafu akamalizia kwa ufupi, "sawa." Kisha akaniuliza, "umemaliza?"

Nikamwambia nimemaliza, hayo yamekwisha.

Akaniuliza, "naweza kukata simu?"

Kabla hajakata, nikamgusia kuhusu lile swala lake la kuonana na yule mama kwaajili ya tatizo lake la kupandwa na kusumbuka na maruwani.

Nilimwambia nimewasiliana na mama Miraji na tayari ameshanipatia muda na siku ya kuonana naye basi tufanye hima tukatimize wajibu wa kutafuta tiba, ajabu mwanamke huyo akanigomea katu, alinambia hana shida, na kama akiwa nayo basi atajua mwenyewe namna ya kuhangaika nayo.

Baada ya kusema hayo, alinikatia simu nikabaki na butwaa.

Zai alikuwa ameghafirika.

Sikuhangaika naye siku hiyo, nikamwacha na mimi nikandelea na mambo yangu. Baada ya kama siku mbili hivi, nilipigiwa simu na Anwari.

Sikutaka kupokea simu hiyo lakini sikuwa na budi kwasababu ya maagano niliyoyaweka. Nilipokea moja kwa moja nikamuuliza bwana huyo anataka nini, hapo akaniuliza mara yangu ya mwisho ni lini kuwasiliana na Zai, nikamweleza ni juzi, basi akanambia Zai amezidiwa sana, na hapo anapoongea na mimi yupo na Zai hospitalini!

Kutazama saa, ni jioni ya saa kumi na moja, tayari nisharudi nyumbani nipo kwenye maandalizi ya chakula cha jioni.

Sasa nafanyaje?

Niliharikisha mambo yangu kisha nikamwita Amiri na kumwambia aketi na mtoto pale nyumbani, mimi natoka kidogo ila nitarudi muda si mrefu.

Niliondoka na mwendo wa dharura, sikupata hata kugusa kile nilichokipika, niliona ni vema nikawahi kwanzan hospitali alafu nitarejea kuendelea na mambo yangu.

Nilikodisha bajaji mpaka huko ambako nilielekezwa, kufika nikamkuta Anwari pamoja na dada ambaye nilimtambua kama ndugu yake na Zai, yule ndugu ambaye kwake ndipo Zai alikuwa akiishi baada ya kutoka hospitali.

Dada yule aliniambia hali ya Zai ilibadilika majira ya jioni, akisema na kubwata maneno yasoeleweka, akipasua na kubamiza vitu alafu ghafla akaanguka chini na kupoteza fahamu!

Hapo ndo' akafanya jitihada za kumleta mwanamke huyo hospitali, moja kwa moja akaingizwa kwenye chumba cha dharura na hata sasa akiwa chini ya uangalizi wa madaktari.

Walipopata wasaa wa kusema na daktari waliambiwa mwanamke huyo anasumbuliwa na presha kali ya kupanda, moyo wake umetanuka, hivyo kwa muda kidogo watabaki naye mpaka pale watakapoona ni muda sahihi kumruhusu.

Gharama za siku hiyo, zote kuanzia usafiri mpaka vipimo vya Zai, bwana Anwari alivifunika kwa kuvilipia 'cash', pesa kutoka mfukoni mwake.

Bwana huyo alitoa pesa pasipo kugugumia wala kunung'una. Nilimtazama usoni akiwa anatoa pesa kweli nikaguswa na tukio lile.

Moyo wa kipekee kabisa.

Lakini jambo lile lilinipa mwanga ni kiasi gani Zai na Anwari walivyokuwa wameshibana. Nikajiaminisha moyoni mwangu kuwa kweli Zai alimpa maneno yale bwana Anwari. Maneno kunihusu mimi.

Baada ya kukaa hapo hospitali kwa takribani masaa mawili, niliona niage niende nyumbani maana muda ulishanitupa mkono.

Bahati haikuwa na mimi, muda wote n'lokaa hapo sikufanikiwa kumwona rafiki yangu Zainabu zaidi ya kuambiwa tu hali yake na vinywa vya watu wengine.

Niliahidi nitarejea tena kesho asubuhi, kwa muda huo waniache tu niende maana nimeacha mtoto mpweke na mume atakuwa yu njiani kurudi nyumbani.

Baada ya kueleza hayo, Anwari alisema;

"Naomba nikupeleke kama hutojali."

Sikukubali.

Nilimsihi abakie hapo pamoja na yule dada, ndugu yake na Zai, mimi nitaenda mwenyewe.

Lakini bwana yule hakukoma, aliendelea kusisitiza ya kwamba muda umepita na hivyo ni vema tukaenda wote ili anisogeze.

Kweli kutazama muda nikaona nimechelewa mno, nikamwambia bwana yule anisogeze mpaka mahali fulani, si mbali sana na nyumbani kwangu, hapo nitajua cha kufanya kufika ninapoishi.

Akaridhia.

Alinibeba na gari yake, na pasipo hata kumwelekeza makazi yangu yalipo, akanyoosha na njia kwenda mwelekeo sahihi.

Tulienda kilomita kadhaa, sikujua nini kilitokea, lakini nilianza kuhisi kichwa changu kizito, sioni vizuri na siwezi kuongea.

Nilijipapatua nikauliza; "Anwari, nini kina ..." Sikumalizia kauli yangu nikabebwa na usingizi mzito mno mno, nilikuja kupata ufahamu kesho yake nipo juu ya kitanda cha Anwari, sina nguo yoyote mwilini mwangu!

Shuka limenifunika upande mmoja tu, huko kwingine ni Mungu nisadie.

Kutazama saa ya simu yangu ni saa tatu ya asubuhi! 'Missed calls' kumi na tatu za bwana Mgaya, ujumbe ndo' usiseme, kweli nikajikuta napagawa na roho yangu.

Mungu wangu! Mungu wangu! Nini hiki?

Nilikurupuka pale kitandani nikaangaza huku na kule, sikuona nguo zangu, nilimtafuta Anwari naye sikumuona, niliita jina lake mara tatu lakini hakuna aliyenijibu, kimya nyumba nzima.

Sijakaa vema, simu ya Mgaya ikaita tena, sikuelewa nipokee ama niache.

Nikipokea nasema nini?

Nikiacha nitaenda kusema nini?

Sikuelewa nataka nini, sikuelewa nafanya nini?

Nikiwa nimeshikilia shuka langu kunisitiri, mara nikaona mlango wa chumba nilichomo unafunguliwa, kutazama ni Anwari.

Bwana huyo aliingia akiniuliza, "umeamkaje, mpenzi?"

Nikajikuta najisema mwenyewe rohoni...

Maneno ya ghadhabu,

K*mmmmmmk zako Anwari!


***
Anwari mbwa wewe,utakufa vibaya
 
Sehemu ya Pili:


Binafsi sijawahi kukaa kuwa mama wa nyumbani, hata mume wangu yule, bwana Mgaya, niliyeishi naye miaka kadhaa na kupata naye mtoto wa kiume, nilimpatia katika eneo langu la kazi; shule yangu ya kwanza kufundisha kabla ya kuja kuhama kutafuta shule nyingine.

Nikiwa huko, nilimwona bwana huyu, siku ya kwanza kabisa, akiwa amekuja na bajaji kumchukua mwanafunzi wa darasa langu. Bwana huyo alinisalimu kisha akaniulizia mtoto huyo alokuja kumfuata, baada ya hapo akaondoka zake, yeye pamoja na mtoto.

Kuja kwake hapo shuleni mara kwa mara ndo' kukanifanya nizoane naye kiasi kwamba nilichukua namba yake nikawa nautumia usafiri wake pale nilipokuwa na mahitaji.

Nilizoeana naye, nikazoeana naye tena, hatimaye akaja kuwa mpenzi wangu baada ya miezi kadhaa, miezi michache tu tangu nilipoachana na mpenzi wangu wa nyuma, bwana Anwari, baada ya kumfumania na mwanamke mwingine nyumbani kwake, mwanamke ambaye hakuweza kunipa maelezo ya kueleweka alikuwa ni nani yake na pale nyumbani kwake alikuwa anafanya nini.

Kama waswahuli wasemavyo; vita ya panzi furaha kwa kunguru, ndivyo kunguru huyu, yaani bwana Mgaya, alivyofaidika na kadhia ile ya mimi na Anwari, akajiweka katikati yetu.

Sikupata hata muda wa kuwaza, muda wa kujitafakari na kujipanga, hasira na maumivu yangu yalinitia upofu nikatafuta afueni ya harakaharaka kuponyesha majeraha yangu, afueni huyo ndo' ikawa kuangukia kwenye mikono ya dereva yule wa bajaji.

Naye dereva huyo, asifanye ajizi, akayapeleka mambo upesiupesi nikajikuta kwenye ndoa, yani kama kufumba na kufumbua, yani kama hadithi fulani yenye mtiririko wa upesi sana, nami nikienda nayo tu kama mlemavu, nashuka nayo mithili ya gari bovu kwenye korongo kali.

Nami sikujali,

Kitu pekee nilichokuwa nacho moyoni, ni kumwonyesha Anwari kuwa embe aliloona lina funza akalitupa, mwingine kaliokota akaliweka kapuni.

Nini raha kama kumrusha roho 'ex' wako? Tena sio kwa tambo za mpenzi mpya, la hasha, bali tambo za mume kabisa wa ndoa, na picha nikiwa ndani ya gauni jeupe linalometameta na pete ya ndoa ipo kidoleni?

Hakuna!

Kweli nilihisi raha sana, tena raha iliyokufuru pale shoga yangu, Zai, alipokuwa ananipa taarifa za Anwari. Nami nilikuwa nikifanya hila kumwambia Zai kila jambo lililokuwa linaendelea kwani nilijua fika atayafikisha kama yalivyo kwenye masikio ama macho ya Anwari maana alikuwa amezoeana naye sana na pia anawasiliana naye huko mitandaoni.

Nami nilitaka Anwari ajue. Nilimtaka aumie kama mimi nilivyoumia au kama inawezekana basi iwe maradufu ya yale maumivu yangu.

Basi furaha yangu ya kwanza nikaja kuipata pale Zai aliponambia namna Anwari alivyoupokea ujumbe ya kwamba mimi nipo kwenye mikakati ya kuolewa.

Kwa maneno ya Zai, Anwari alilalamika sana kunipoteza. Alijilaumu na kujitusi. Alimwambia Zai namna mimi nilivyompenda lakini hatimaye akanilipa maumivu. Lakini zaidi lililonifanya nikaamini Anwari alikuwa ameumia, ni namna alivyoapa kwa Zai kuwa mimi sitakuja kuolewa na mwanamume mwingine isipokuwa yeye. Hapa nikacheka mpaka gego la mwisho.

Moyoni mwangu nikisema "huo ndo' kwanza mwanzo, funga mkanda, Anwari. Mengi yanakuja."

Furaha ya pili, ikawa ni pale nilipofikisha kadi ya mwaliko kwenye mikono ya Zai, kadi mbili kwa idadi, moja nikiandika jina la rafiki yangu huyo na pili nikiandika jina la Anwari, tena majina yake yote matatu.

Nikamwambia Zai, sikutaka bwana huyu anichangie harusi yangu lakini hili la kuhudhuria halina tabu, anakaribishwa kuniona katika siku ya furaha yangu, Zai akanambia si vizuri vile nilivyokuwa nafanya lakini mimi hakuna nilichokuwa najali isipokuwa jambo moja tu, nalo ni kumuumiza Anwari pekee!

Niliamini kadi ile itakuwa ni ujumbe tosha kuwa kweli nilimaanisha. Na kweli Zai alipompatia taarifa ile alipapatika, hakuamini macho yake, alidhania utani lakini ilikuwa kweli mimi nilikuwa naolewa.

Mara kadhaa ningekuta ujumbe wake katika simu yangu ama 'missed calls' wala nisihangaike kujibu. Mwisho wa siku nilimtumie ujumbe:

"Usije ukaniharibia ndoa yangu." Alafu nikam-block asinipate kabisa hewani. Kama haitoshi, nilibadili kabisa namba yangu tena nikimwonya Zai asije akampatia, yeye kazi yake awe ananisikia kwa mbali maisha yangu yakipepea bila yeye.

Furaha yangu ya tatu ikawa ni siku ile ya harusi, nilipopepeza macho kuangaza ukumbini kama nitamwona Anwari. Sikumwona. Nikatabasamu na moyo wangu nikijua kabisa huko aliko, hata kama hajaja pale, atakuwa anajua fika kuwa siku hiyo nafunga pingu za maisha na mwanaume mwingine, mwanaume aliyethamini pendo langu akanisitiri.

Hilo kwangu lilikuwa ni faraja tosha, achilia mbali kujumuika pamoja na familia, marafiki, ndugu na jamaa zangu katika ukumbi ule kwasababu ya sherehe yangu. Niliamini picha ya yale yote yalojiri ingemfikia Anwari, na kweli sikukosea hata chembe, nilikuja kubaini hilo baadae hapo mbeleni.

Lakini furaha yangu hiyo, nasikitika, ilikuwa ni mbio za sakafuni, haikupata kudumu bali kuja kuishia ukingoni muda si mrefu tangu nilipoingia ndani ya ndoa na kuishi na bwana Mgaya.

'Hangover' yangu ya maumivu yaliyosababishwa na Anwari ilikuja kukoma na sasa nikaanza kuuonja uhalisia mchungu ambao niliupika kwa mikono yangu mwenyewe, uhalisia ya kwamba bwana yule hakuwa moyoni mwangu kabisa bali ni maamuzi yangu ya pupa nilofanya baada ya kuumizwa.

Lakini sikuwa na budi tena, nilimwonyesha mapenzi yangu bwana Mgaya kwa kadiri nilivyoweza, naigiza na kutenda, nikiamini hapo mbeleni nitakuja kuyasahau ya nyuma na yeye ataniingia moyoni mwangu mzima mzima.

Hatimaye siku, miezi na mwaka ukapita.

Mimi na bwana Mgaya tukaona sasa ni muda muafaka wa kupata mtoto baada ya mipango yetu kadhaa ya maisha kwenda sawa.

Bwana huyo aliachana na kuendesha bajaji, sasa akawa anaendesha gari za kampuni zinazopokea wageni pale uwanja wa ndege, kwa kipato chake pamoja na changu, tukapandisha jengo katika 'site' fulani, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam, tukahamia huko pasi na kujali ujenzi haukuwa umekamilika.

Kwani

Tulijiskia fahari kuishi mahali tulipopaita nyumbani kwetu, hayo mengine yalikuwa ni ziada tu.

Eneo lile lilikuwa ni kubwa na tulivu, lina nyasi na miti mingi. Mume wangu, bwana Mgaya, aliniambia alilipata eneo lile zamani kidogo kwa pesa ya kutupa, na alivutiwa na eneo hilo kwasababu ya ndoto yake ya mbeleni ni kuja kuwa na mifugo kadhaa.

Tulikaa hapo huku ujenzi ukiwa unaendelea taratibu taratibu mpaka nyumba kukamilika kabisa: nyumba ya vyumba vinne na uzio wetu wa michongoma.

Maisha ya huko, changamoto yake ikawa ni umbali wa mimi kufika kazini, mara kadhaa mume wangu angenipeleka na gari yake ya kazi lakini mara nyingi pia asingeweza kwasababu alikuwa anashinda usiku huko kwa kazi zake za kule kiwanjani.

Hapa sasa ndo' nikaona kuna haja ya kuhama mazingira ya kazi, taratibu nikaanza kutafuta shule mbadala huku na kule katika maeno ya karibu, nikaja kupata mahali fulani, karibu kweli, lakini maslahi yake hayakuwa mazuri, nikaendelea kutafuta huku napambana na kule nilipo, bahati nikaja kupata shule, japo haikuwa karibu kama nilivyokuwa nimepanga mimi ila ilikuwa angalau ukilinganisha na ile ya mwanzo.

Nikiwa katika shule hiyo sasa, ndo' nikapata ujauzito wangu wa kwanza, ujauzito wa mtoto yule wa kiume. Ujauzito huo ukanikutanisha uso kwa uso na mama yake Mgaya, yaani mama mkwe wangu, kwa ukaribu wa zaidi, sio ule wa kupigiana simu kujuliana hali bali sasa wa kuishi nyumba moja, tunakaa sebuleni na tunapishana koridoni.

Mama huyo alikuja nyumbani kunihudumia kwasababu ya ujauzito nilokuwa nao ulikuwa unaelekea ukingoni, muda si mrefu ningejifungua, na hakukuwa na mtu wa karibu kuniangaliza.

Lakini maisha yale na mwanamke yule, chini ya paa moja, yalikuwa magumu sana. Maisha ya kikoloni na kusontwa kila mara, aidha kwa hiki ama kile. Yalikuwa ni maisha ya maigizo mbele ya mume wangu lakini nyuma ya mlango nalia na ya kwangu. Niliogopa kama ningemshirikisha mume wangu kwenye visa vile, angedhania simpemdi mama yake na mimi sikutaka niwe nyundo ya kuvunjia familia yao.

Nilikaa nikaamini labda ile ni mimba tu, Zai pia alikuwa akinishauri hivyo, punde nitakapojifungua naweza nikayaona mambo kwa namna tofauti.

Basi nikayabeba.

Nikaja kujifungua salama, nashukuru Mungu, lakini ajabu chuki yangu kwa yule mama haikwenda popote pale, iliendelea kuniganda kama nzi anayemendea kidonda kichafu, lakini nikapiga moyo konde, mathalan nimejifungua, mama yule asingekaa muda mrefu pale atarudi nyumbani kwake.

Nikavumilia amri na shurba zake, nkihesabu siku na majuma. Nayo nayaona hayasogei, yanajivuta mno. Mpaka mtoto wangu kuja kufikia hatua ya kumsimamia mimi mwenyewe kiukamilifu, hakuna rangi niliyoacha kuona. Hamna jambo lilikuwa jema kwake akaniacha nikahema.

Nilishawaza hata mara mbili, kama ningekuwa na uwezo, ningemtokomeza mama yule nirejee kwenye amani.

Amani ya moyo.

Nilimwona ananikosea sana na anastahili adhabu. Si bure, alikuja kuwa mtu wa kwanza kumzika na kuweka shada langu juu ya kifusi cha kaburi lake. Uso wangu ukiigiza huzuni mbele za watu, huku moyo unapondeka kwa furaha.

Furaha kuu.



**
Ndo naiona leo hii, ngoja nisonge nayo[emoji119]
 
Sehemu ya 11:


Nilifanya namna ya usafiri mpaka kufika kwenye makazi ya Anwari, huko nilikuta geti lake limefungwa na hata nilipobisha hodi kiasi chote kile, hadi kuokota jiwe na kugonga chuma la geti, hakuna mtu aliyekuja kunifungulia kamwe, sasa nikawa nimekwama hapo, sina la kufanya.

Nilichungulia getini kwenye mpenyo mdogo, nilichungulia kuona kama ndani kutakuwa kuna usafiri wa Anwari ule n'louzoea, kweli pale mbele ya nyumba yake nikaliona gari hilo, hapo nikapata uhakika Anwari atakuwamo ndani, shida ikabakia naingiaje humo?

Siku ile ndo' ile niliona umuhimu wa kuwa na mlinzi, hata kama ni mzee tu aiyejiweza kwani laiti angalikuwapo basi angalikuwa msaada mkubwa sana kwetu.

Nilijiuliza sana siku hiyo, hivi Anwari na nyumba yote ile anakosaje kuwa na mlinzi? Ni kwamba anajiamini sana ama ni kitu gani?

Niliongea mwenyewe, nililaani mwenyewe, nililaumu mwenyewe. Hamna kilichosaidia.

Ni baadae ndipo akili ilinijia nikatazama simu yangu kwenye majina nilohifadhi, humo nikampata bwana mmoja anaitwa Adrian, bwana huyo niliwahi kupata namba yake kipindi cha nyuma sana ingali nikiwa kwenye mahusiano na Anwari.

Kipindi hiko nilitambulishwa kwa Adrian kama rafiki wa mpenzi wangu, naye nikamjua na kuishi naye vema, lakini urafiki ule baina ya mabwana hao wawili haukudumu sana tangu mimi kutambulishwa kwao, wakatengana.

Anwari alinambia, kwa maelezo ya juu juu tu, kwamba Adrian hakuwa rafiki wa kweli wa maisha na hivyo wametengana, mimi sikupeleleza wala kusumbuka sana, niliamini wanaume hao wanajuana wenyewe kuliko mimi ninavyowajua kwahiyo maisha yakaendelea kama kawaida.

Lakini leo hii, katika simu yangu nzima, sina mtu yeyote ninayemjua kama mtu wa karibu wa Anwari isipokuwa Adrian, rafiki wake wa zamani, angalau nikaona hapo ndo' sehemu ya kuanzia.

Nilimpigia bwana huyo nikiomba awe anapatikana, bahati kwangu akapatikana na simu akapokea.

Nilimweleza kila kitu, hali niliyomo na namna ninavyomhitaji anisaidie, akanisikiliza na bahati tena akasema anakuja muda si mrefu pale nilipo.

Kweli, kama baada ya robo saa hivi, bwana huyo akafika hapo, tuliongea kidogo akakata shauri ya kukwea kuingia ndani akitumia mgongo wa gari yake.

Alipoingia alinifungulia geti kisha tukazama ndani ya jengo la Anwari tukiwa tunaita, uzuri milango ya ndani haikuwa imefungwa hata mmoja kwahiyo hatukupata tabu kuingia ndani.

Kule chumbani, tukamkuta Anwari akiwa amelala chini, hajitambui, ametokwa na mate sijui povu mdomoni mwake, kwenye kiganja cha mkono wake wa kuume kuna sindano, sindano ambayo Adrian aliichukua akaishika na kuitazama.

Aliitazama sindano hiyo akaguna kisha akanambia habari ambayo kwangu ilikuwa ngeni na ya kushtua, ati ya kwamba sindano ile ilikuwa ni ya madawa.

Madawa aina ya heroin.

Kwasababu hiyo, tulimkimbiza Anwari hospitalini, anahema kwa tabu, njiani tukawa tunaomba tufike naye salama ili wataalamu wamsaidie.

Siku hiyo ndo' nikajua kwanini urafiki wa Adrian na Anwari ulivunjika, Adrian alinambia punde Anwari alipoanza kutumia madawa ya kulevya walikosana kila mtu akashika njia yake.

Wala hakukuwa na sababu nyingine isipokuwa hiyo.

Jambo hilo kweli likanishangaza, yani muda wote huo nlokuwa kwenye mahusiano na Anwari sikuwahi kuhisi kitu chochote kuhusu matumizi yake ya madawa?

Aliwezaje kujihifadhi kiasi hiko? Sikupata majibu.

Niliwaza pia na mimi nilivyoleweshwa siku ile mpaka akanipeleka kwake na kuamka asubuhi, nikajiuliza ina maana alin'tilia madawa haya ya kulevya? Napo sikupata majibu.

Tulimfikisha bwana huyo hospitali, ileile ambayo Zai alikuwapo, akapatiwa huduma ya upesi na ya dharura.

Daktari alisema ilikuwa ni 'heroin overdose', tumpatie muda kidogo atarejea katika hali yake.

Tulirejea kule kwa Zai, Adrian akanisaidia kiasi fulani cha pesa, nilipojumuisha na cha kwangu na cha Zai pesa ikatoshea kulipia bili, uzuri kumbe Zai alishawasiliana na ndugu zake kadhaa wakamwezesha kwa kadiri walivyojiweza hivyo zoezi lake likawa limetamatika kwa mafanikio.

Kesho yake, Anwari aliamka akiwa na unafuu, dawa za kumwondolea sumu mwilini zilimsaidia sana angalau akarejea katika ubinadamu wake, japo bado alikuwa anasema anahisi kizunguzungu kwa mbali na kichefuchefu vilevile.

Baada ya siku tatu, Anwari alipona kabisa, hata Zai naye alikuwa anaendelea vema hivyo ikawa ni heri maana kila mtu aliendelea na shughuli zake kama kawaida.

Baada ya siku kama mbili hivi, Zai alinipatia taarifa ambayo haikuwa nzuri kiasi kuhusu kule kazini kwao, Zai alisema menejimenti ya shule ilikaa ikafikia maamuzi ya kumfukuza kazi, hivyo ndo' namna mkuu wa shule alivyomwambia.

Na sababu yake kufukuzwa kazi ni mbili; moja ameonekana ni hatari kuwa katika mazingira yake ya kazi lakini pia kushindwa kumudu majukumu yake kwasababu ya kukosekana eneo lake la kazi mara kadha wa kadha.

Kwakweli swala lile lilimgusa sana Zai, aliniambia kwa sauti ya kulia na mimi nikaguswa sana ukizingatia mwanamke yule alikuwa ametoka kwenye majanga muda si mrefu.

Kwaajili ya kumfariji, nikamwambia tuonane kesho yake tupate kuzungumza, na hapo ndo' ukawa mwisho wa maongezi yetu tuliyoyahitimisha kwa kuonana lakini pia kwa kutafuta tiba ya tatizo letu kule kwa mama Miraji.

Lakini cha ajabu, siku hiyohiyo, nikiwa nimerejea nyumbani, sina hili wala lile, nafanya shughuli zangu za nyumbani, mara Amiri ananifuata jikoni na kunambia nina mgeni.

Hapo nikastaajabu kidogo maana sikuwa na miadi na mtu yeyote yule, nikamuuliza Amiri mgeni huyo ni nani, naye akaniambia hamjui, lakini aliponishtua ni kuniambia mgeni huyo ni mwanaume.

Kweli hapo moyo wangu ukapiga fundo kubwa.

Nilitoka upesi kwenda kutazama, hamaki kule njenya geti nikaliona gari la Anwari! Hapo nikahisi miguu yangu inatetemeka kwa woga na hasira, huyu bwana ananitaka nini?

Sasa ameona aje kwangu kabisa?

Kabla sijamfuata kumbe naye alikuwa tayari ashatoka kwenye gari lile, nahamaki mtu huyu hapa pembeni yangu ananisalimu na kuniomba aingie ndani tukaongee.

Nikamtazama bwana huyo, sikuamini kama kweli yuko sawa kichwani, mtu mzima hawezi fanya vitu kama vile wallahi!

Nilimwambia Anwari aondoke upesi kabla sijamuitia mwizi, ajabu bwana huyo hakuogopa, akasema ita tu, na alisema hivyo maana anajua nisingeweza kufanya hiko kitu.

Mwishowe sasa ati akanipa sharti, kuondoka kwake pale ni mpaka atakapomuona mtoto wake.

Kweli kitendo kile cha kusema mtoto kikanipasua moyo na kichwa kwa mkupuo!

Nilitazama kando zangu kama kuna ambaye amesikia kauli ile, nikaona hamna, nikamrudia Anwari kwa jicho langu lote la ukali, nikamwambia kwanguvu sana, ondoka ondoka! Ondoka kwangu upesi.

Bado akasema haendi. Hatoki hapo labda amwone mwanaye au aongozane na mimi.

Nikiwa nazoza hapo, nabweka tu lakini cha kufanya sina, ndipo akatokea Amiri nyuma yangu.

Kijana huyo alisimama kando yangu akaniuliza kuna tatizo? Nikamwambia si huyu bwana hapa, amenisimamia mbele ya nyumba yangu ananifanyia vurugu.

Basi Amiri hakuuliza tena, alimjongea bwana Anwari mpaka mbele kabisa ya uso wake, akamwambia: "Tokomea hapa upesi!"

Anwari akatabasamu, kweli hata ingekuwa mimi ningelitabasamu maana kwa umbo la Amiri ukiliwanisha na Anwari ni kama vile kuku na kinda lake, nilishangaa kujiamini kule alikutolea wapi?

Tena mbele ya mbaba mpana kama yule.

Anwari aliuliza kwa kebehi, "ala! Na huyu kunguru ndo' nani?"

Amiri akamjibu ...

Akamjibu jibu ambalo mpaka leo hii nalikumbuka vema sana, alimwambia; "kunguru huyu ni Amiri, Amiri asokuwa na baba wala mama, kwahiyo unaweza ukaniita Amiri wa Amiri wa Amiri."

Kisha akamuuliza Anwari, "utaondoka hapa ama lah?"

Nikamwona Anwari kama amepigwa na bumbuwazi hivi, bumbuwazi la kumtazama Amiri, hakubisha tena bali akanitazama kwa macho ya ahadi kisha akalifuaga gari lake, hapo ndo' na mimi nikamsindikizia na maneno: "madawa yanakupelekesha wewe. Yatakuua usipate wa kukusaidia tena!"

Niliposema maneno hayo aligeuka akaniambia wewe si upo, hofu ya nini? Sikusema tena kitu, akawasha gari lake na kutokomea.

Nilimshukuru Amiri kwa kunisaidia, naye akaniahidi bwana yule hatokuja kunisumbua tena, wala nisijali. Basi nikamshukuru zaidi na zaidi.

Kama bahati, hatujakaa vema wala bado hatujarejea ndani ya uzio, gari la bwana Mgaya linatokea kwenye kona.

Bwana huyo anatusalimu na kisha anauliza mbona ameliona gari fulani hapo nyuma ya njia? Alikuwa ni nani yule?

Kwakweli mimi sikuwa nimejipanga na wongo wowote ule, pale nilikuwa nimeshtukizwa, ajabu nikiwa najitafuta Amiri anaingia na kusema bwana yule ni mteja maziwa, amekuja kuulizia bei zetu ili zitakapompendeza basi tufanye biashara.

Mgaya akafurahi sana.

Alimpongeza Amiri na hata mimi pia, hapo mambo yakageuka, tulitoka ndani kwa taharuki lakini sasa tunarejea kwa mbiu ya ushindi.

Ushindi wa kishindo.

Ushindi wangu na Amiri.

Lakini niliwaza ushindi ule ungedumu kweli? Nilisema na sauti zangu kichwani.

Hamna anayejua siku wala saa ya bwana Anwari kuibuka tena getini mwangu kugonga. Laiti ningelijua kuhamisha makazi yangu nikayapeleka mahali salama basi ningelifanya hivyo.

Hofu yangu hiyo ikaninyima raha.

Nilisahau kijana Amiri aliniahidi jambo lile halitatokea tena, na pengine hata ningelikumbuka nisingelitilia maanani, ningelidhani ni maneno tu ya kamusi, maneno yasoweza hata kutikisa jani la mtini, lakini kumbe nilikuwa nimekosea.

Amiri hakuwa mtu wa kupuuza yale yamtokayo kinywani. Nilikuja kujifunza hili baadae sana.

Ningalijua mapema huenda ningelichunga ndimi yangu kuwa mbali na maafa.

Kesho yake, nilidamka mapema kama ilivyo kawaida nikaongozana na mtoto kwenda shule, majira ya mchana nikiendelea na majukumu yangu yanayoelekea ukingoni, mara napokea simu ya bwana Adrian, rafiki yake na Anwari.

Bwana huyo alinisalimu vema kisha akaniuliza kama nimeongea na Anwari siku hiyo, nikamjibu hapana, kwanza nilikuwa nimem-block palepale jana yake alivyokuja kunisumbua nyumbani maana alienda kinyume na makubaliano yetu, hayo niliyasemea moyoni mwangu, yeye nikamwambia tu kuwa sijawasiliana na huyo bwana.

Basi nilivyompa hayo majibu akakata simu na mimi nikaendelea na shughuli zangu, baadae kidogo natoka shuleni, sasa nielekee kule kwa Zai kama nilivyopanga, simu yangu inaita tena na mpigaji akiwa ni yuleyule, yaani bwana Adrian.

Bwama huyo mara hii haulizi tena kama niliongea na Anwari bali ananipa taarifa ya msiba.

Msibwa wa Anwari.

Amemkuta bwana huyo kama kawaida chumbani mwake akiwa amejidunga na kujizidishia dozi. Mara hii hajanusurika tena, ameenda njia moja isiyokuwa na pa kutokea!

Amekufa kama vile n'livosema.

Amekufa kwa madawa.

Sasa ni kweli hatonisumbua tena kama alivyosema Amiri.

Sasa hamna atakayejua kuwa nimezaa naye. Hamna atayejua mtoto yule ni wa kwake, ameenda na jambo lake kifuani, hapana, hapo nilikumbuka kitu, Anwari hajaenda na jambo lake, Zai anafahamu siri hii.

Siri ya nguoni.

Lakini hakuna mtu yeyote aliyekuwa anafahamu, hata mimi mwenyewe vilevile, ya kwamba muda huo nilikuwa tayari nina kiumbe kingine tumboni.

Kiumbe cha marehemu.

Na hapa ndipo mkasa wa Zai na kifo chake unapoanzia...
Dah ama kweli [emoji22]
 
Hamieni kule kuna chuma cha moto kinaitwa babu yangu kama mshikaji wangu: true story
 
Back
Top Bottom