Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Yaani unaamini humu ndo utaondolewa stress zako? Maana umekuja nazo.mhusika hajalalamika na ameonesha kujiamini hadi anaahidi kunitag. Wewe kajamba nani unaleta makasiriko. Hii inatokana na nini?kushindwa kwako unataka kuwahamishia wengine lawama. Why cant you just shove it in your as* and run away😂😂😂😂. Mwenye uzi hana neno. Wewe tu unayaleta hapa makalio yako na kuyapigiza pwaaaah.... Huoni kuwa nimekaa hapa. Hujali na huogopi.

Siwezi jadiliana na wewe, peharps upeo wako ni mdogo hutaelewa, upo sahihi

Ushauri :

Ukiona mtu anafanya jambo lake likakubalika usimharibie bila sababu...
 
Sadist, una fikra za kupambana tu na kukosoa watu, huo ni ugonjwa, tafuta msaada, kwa watu kama sisi tuna thamani tu mda anaoutumia huyu ndugu kuhadithia kitu cha kuvuta hisia wakati tupo on transit/lay over....
Hajui tu vile tunapata burudan mkuu...ndio maana anaropokaa
 
Yaani unaamini humu ndo utaondolewa stress zako? Maana umekuja nazo.mhusika hajalalamika na ameonesha kujiamini hadi anaahidi kunitag. Wewe kajamba nani unaleta makasiriko. Hii inatokana na nini?kushindwa kwako unataka kuwahamishia wengine lawama. Why cant you just shove it in your as* and run away[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Mwenye uzi hana neno. Wewe tu unayaleta hapa makalio yako na kuyapigiza pwaaaah.... Huoni kuwa nimekaa hapa. Hujali na huogopi.
Mtoto wakiumee ww acha shobo c u kaushee Kwan Kila mada lmz uchangiée,,,,,
 
Nimekaa hapa kuangalia uongo upo wapi katika story hii. Unapotunga uzingatie sana vigezo vya utungaji. Yaani usidanganye sana utaniudh. Mugaka anafahamu habari yangu vizuri na moderators. So nakutahadhalisha uwe makini na utulie sana.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sehemu ya Nne:


Amiri aliingia ndani, begi lake liko mkononi mwangu, mume wangu akamwonyesha sehemu ya kufikia, kilikuwa ni chumba cha kwanza kabisa katika korido, baada ya hapo Amiri akashukuru kisha akaingia humo.

Mimi na mume wangu tukaingia chumbani, na si muda bwana huyo akaingia kwenda kuoga, mimi hapo ndo' nikapata wasaa wa kukagua simu yake.

Nilitazama kwenye 'call logs' na pia kwenye 'messages', kwenye call logs nikakuta rekodi za yeye kuongea na mama yake, kama mara nne hivi, na pia kule kwenye ujumbe vilevile. Moja ya ujumbe ulisema: 'nakuja leo kukuona,' na ujumbe mwingine ukasema: 'nakutumia pesa kabla ya jioni kufika'.

Mbali na hizo, hakukuwa na ujumbe mwingine lakini pia hakukuwa na majibu yoyote kutoka upande wa pili. Hili likanifanya niwaze hivi kweli hamna kilichofutwa hapa? Roho yangu ilikataa.

Lakini, hapa ndo' paliniumiza kichwa zaidi, mama yule na mambo ya kusoma na kuchati huku wapi na wapi? Nakumbuka nilipopata kukaa naye nyumbani kwa miezi na miezi, nilikuwa namsaidia kutazama majina kwenye simu yake na nilikuwa namsaidia kutuma ujumbe au kupigia walengwa wake, leo hii imekuaje? Leo hii wa kutumiwa ujumbe na mwanae?

Hapa kweli nachezewa shere.

Nilitunza namba ile ya mama mkwe kichwani, nikatazama 'gallery' picha kadhaa kisha nikarejesha simu ya mwenye nayo pale alipoiacha, namna ileile alivyoacha, alafu nikatulia tuli kwani alikuwa ametoka bafuni, yaani bwana yule alikuwa anaoga kama mkimbizi, kwahiyo ilinilazimu nisitishe oparesheni yangu kwa muda kungoja muda sahihi kwani sikutaka ahisi chochote.

Lakini sijui kama niliweza. Nilihisi kubanwa na donge kubwa kooni, alafu donge hilo halitulii, linanisuguasugua kwa uchungu nashindwa hata kumeza mate, damu yangu inachemka, kifuani nimejawa na bughudha.

Nilimtazama bwana yule akiwa anajifutafuta maji, nikawa namwona kama kiboko hivi na lile tumbo lake. Nilimtazama nikikamgua na kumkosoa, nikimsema na kumnanga humo kifuani mwangu.

Laiti angesikia hata lepe tu la yale yalokuwa yananisibu asingethubutu kulala na mimi kwa amani. Angeenda kulala chumba kingine tena alale na Amiri kabisa.

Alimaliza shughuli yake, akalala fofofo, hata kula hakula, alisema ameshakula njiani, yuko sawa, basi alipojiweka hapo kitandani, hakuchukua kitambo, akaanza kukoroma kama nguruwe mwenye mafua. Hapo ndo' mimi kuchukua simu yangu na yake kumalizia adhma yangu.

Nilitazama na kuwianisha namba ile ya mama kama kweli ni ya mama, nikabaini ni kweli ndiyo. Hakukuwa na kosa lolote lile. Sasa nikabaki na maswali mwenyewe kichwani, inawezekanaje?

Yani inawezekanaje?

Nilitafuta ujumbe wa miamala ili nione kama kweli alituma pesa na alimtumia nani, nikakuta ametuma laki mbili kwenye namba ileile ya mama yake. Siku hiyo nikalala na mawazo nikijitahidi kutegua kitendawili.

Usingizi ulinikomba nikiwa nayajenga maghorofa kichwani.

Kesho yake bwana huyo hakwenda kazini, alibakia nyumbani akirandaranda na kijana Amiri huku na kule akimwonyesha mazingira lakini pia akimpatia maelekezo ya hapa na pale juu ya kitu cha kufanya kwa mifugo ile.

Amiri alikuwa amevalia nguo zilizochoka; kama kawaida shati na suruali ya kitambaa, nguo hazitamaniki na chini ndala zake ni zilezile, zile alizokuja nazo jana yake.

Kijana huyo alikuwa akimsikiza 'boss' wake kwa umakini na adabu zote, alionekana mnyenyekevu sana, angeitikia kwenye kila alichoambiwa kwa sauti ama kutikisa kichwa. Walipomalizana huko nje walikuja ndani kupata chakula, baada ya kumaliza kula kijana yule aliwahi kuvitoa vyombo vyake akaomba asafishe meza.

Nilimwambia: "usijali, Amiri. Hizi kazi za ndani ni za kwangu, wewe uwanja wako ni kule nje, nisikuchoshe sana."

Jambo hilo likaungwa mkono na mume wangu, naye aliongezea akimtaka Amiri afanye kazi kwa nguvu zote, ikimpendeza basi atamwongezea mshahara wake, mshahara wenyewe anaouongelea ni alfu thelathini, fikiria mtu anaacha familia yake kuja kufanya kazi ya alfu thelathini huku mjini, tena anaambiwa akifanya jitihada ataongezewa alfu ishirini iwe hamsini!

Kweli dunia tambala bovu. Nilimwonea huruma kijana yule, na nilimwonea huruma zaidi alipoanza kazi yake, kazi ile haikuwa nyepesi kabisa haswa kwenda kusaka majani ya ng'ombe na toroli ama kwenda kuwachunga, lakini kijana yule hakuonekana kutia huruma, na wala hakua analalamikia majukumu yake, kila mkitazamana ungemwona anatabasamu na kukusalimu kwa kupunga mkono, ungesema huyu ni mtu, huyu ni binadamu wa mfano, lakini kiuhalisia Amiri hakuwa mtu wa kawaida ...

Amiri alikuwa shetani katika mawindo yake!

Basi hazikupita siku nyingi, kule kazini, meneja, bwana Salum, aliniita ofisini mwake, wito nikipewa na mwalimu ninayefundisha naye darasa moja, mwalimu Beatha.

Mwalimu huyo alinifuata nikiwa nipo darasani, akanipa ujumbe huo pasipo hata kunitazama.

"Meneja anakuita." Alisema kwa sauti ya puani kisha akabinua 'lips' na kuyazungusha macho yake, kitendo ambacho nilikifasiri kama dharau, lakini sikujali nikaondoka zangu kuitikia wito, japo niliona jambo lile bwana meneja alikosea, angenijuza tu kwa simu kama ananihitaji na sio kuwapa maneno hawa makurumbembe ambao najua kabisa walikuwa wanaumizwa nalo, walishatoka kuzungumzia yale ya likizo yangu, sasa kinachofuata kitakuwa ni hiki, nilikuwa naufahamu vema mdomo wa mwalimu yule.

Nilifika ofisini nikaonana na meneja, nikamsikiliza maneno yake yote kisha nikarejea kuendelea na majukumu yangu, nilipofika tu mwalimu Beatha alinidaka na kuniuliza ni nini meneja ameniambia, aliniuliza kana kwamba yanamhusu, na nilipomkatalia kusema jambo alisonya akazungusha tena 'mimacho' yake.

Pale nilibaini swala la 'afya ya akili' ni kubwa mno kuliko tunavyoliwazia. Kuna watu unaweza dhani ni wazima kabisa, kwa muonekano wao, lakini kumbe wana viashiria vya utaahira ndani yao.

Nilimchukulia mwanamke yule kama mgonjwa ili niendelee na mambo yangu vema, hapo mbeleni, kwa kupitia walimu wengine, ndipo nilikuja kubaini ya kwamba Beatha alikuwa na mahusiano na meneja Salum. Hivyo kipindi kile alikuwa ananiona kama tishio kwenye mahusiano yake hayo.

Angejua ...

Basi kama nakumbuka vema, katika wiki hiyohiyo ndo' nilikuja kumshika mume wangu na misheni yake alokuwa anafanya nyuma ya mgongo wangu.

Sijui nilipata wapi wazo lile, lakini siku hiyo nilipofika nyumbani na kuonana mume wangu wazo hilo lilinijia na nikajuta hata kwanini hata halikunijia mapema.

Bwana huyo aliingia ndani kubadili kisha akaenda zake nje kukutana na Amiri, alikuwa ameenda huko kutazama mifugo yake akaacha simu yake ndani.

Nilipojihakikishia kuna usalama, nikaichukua simu hiyo na kupiga namba ile ya 'Mama'. Simu ikaita kidogo na kupokelewa;

halo .... halo.

Mimi nimenyamaza kimya.

Halo ... halo ....

Mimi sijaongea kitu.

Halooo ....

Sauti ile haikuwa ya mama ninayemjua mimi, ilikuwa ni sauti ngeni ya mwanamke nisomfahamu. Nilitafakari kama nishawahi kuisikia popote pale, sikufanikiwa.

Nikiwa nimekaa kimya hivyo, mara mwanamke huyo akaropoka:

"Mume wangu, mbona huongei?"

Hapo ndo' moyo wangu ukalipuka. Mume wangu? Sasa nikawa nimethibitisha yale nilokuwa nayawaza kuwa bwana Mgaya ana jambo lake nyuma yangu.

Nilikata simu kisha nikatulia hapo sebuleni kama vile hamna kilichotokea. Kifua kinanibana kana kwamba kinataka kupasuka. Natamani kutabasamu, natamani kulia, yani sijui kipi ni kipi, lipi ni lipi.

Nikawaza, lakini mbona namba zile ni za mama mkwe kabisa? Sasa imekuaje anapokea mwanamke yule tena akimwita bwana Mgaya mume wake?

Kuna mahusiano gani hapo? Kwakweli sikuelewa. Nilitamani nimpigie yule mama lakini ningefanyaje na namba enyewe nlonayo ndo' ile anayopokea yule mwanamke nisomjua?

Sikufanya jambo lolote siku hiyo, nikayabeba kifuani mwangu, lakini nisikudanganye usiku ule nilitamani nimkabe bwana yule usingizini nikamuua.

Kila nilipomtazama akiwa anakoroma, nilipatwa na hasira kali, nilimwona kama ndama kitandani, nilimwomba Mungu usiku ule uishe salama, kweli ukapita, kesho yake mapema nikampigia Zai kumwomba aje nyumbani.

Nilihisi napasuka na yale nilobeba kifuani, nilihitaji mtu wa kumshushia angalau nipate kuhema. Kweli Zai akaja na kuniona tu akabaini siko vema. Nilimwambia yale yote yalonisibu akanionea huruma kweli kweli, lakini alichoniuliza kiliniumiza zaidi, na kilikua kweli kabisa.

Aliniuliza, "lakini, Mage, wewe si humpendi yule bwana? Mbona unaumia hivyo?"

Kwa muda nikajihisi mjinga, nini kinaniliza? Yule bwana mwenye tumbo kama kiboko ama kuna kitu kingine?

Lakini ....

Niliwaza.

Lakini yule ni mume wangu, nilisema pekee na nafsi yangu, yule ndo' alonioa na siwezi nikabadili hilo, ndoa yenyewe ni ya kikristo, sasa nifanye nini kumtia adabu?

Hawezi nifanya kanjere kiasi hiko alafu nami nitulie kama mjinga. Nilingoja Zai aondoke ili nipate kusema na nafsi yangu mwenyewe, nipange mikakati yangu ya ushindi, lakini wakati nayangoja hayo mara kikatokea kioja.

Ghafla nilimwona Zai akibadilika na kubadilika mbele ya macho yangu. Mara anazungusha shingo yake, mara anatoa sauti nisizozielewa, mara anapayuka na kukoroma, mara anayabidua macho kama jini, yani alimradi tafarani tafarani!

Kumbe bibie yule alikuwa amepandwa na mashetani. Aisee. Kaa tu kuyasikia haya mambo. Nilichanganyikiwa nisijue cha kufanya. Nilipagawa na kila jambo, kile hakishikiki na wala hiki hakikamatiki.

Ni hapo baadae ndo' nilikuja kukumbuka kuna mtu anaitwa Amiri, basi nikaona nifanye upesi kumwita aje kunisaidia na sakata lile. Lakini nilipopaza tu sauti kuita ikawa ndo' kama nimeyatibua mambo.

Zai alianza kupiga kelele akisema mtoe huyo jini ... mtoe huyo jini ... Mtoe nitammaliza ... Mtoe nitamuua ... Mtoe anakunywa damu ... Mtoe! Mtoe! Mtoe! ... Mtoeee! Kisha akaunguruma kama simba, alooh!

Jasho lilinichuruza kila kona ya mwili. Nilikimbia kule nje nikaangaza kila kona, Amiri hakuwepo. Niliita lakini sikuitikiwa, kote kimya nimeachwa nihanye na majanga yangu mwenyewe.

Sijakaa sawa, nikasikia mtu kule ndani akipondaponda mlango kwanguvu. Upesi nikakimbia kwenda kutazama, hamaki nikamkuta Zai amesimama koridoni, anaupiga mlango wa Amiri kana kwamba anataka kuusaga apate unga.

Anaupiga mlango huo pasi na huruma. Anaupiga akisema nitakuua ... Nitakuuua ... Nitakumaliza .....








***
Basi haya......tuendelee please [emoji120]
 
,Moderator mnaona huyu jamaa anadhalilisha watu pasi na sababu?
Tokaa peleka unafiki kule eti unawaita moderator wakt wew ndio unanitumiaga vibendera vyenu hvyo automatically nikajuwa wew ni upinde official

Bisha kama ujawai nitumia vibendera vyenu hvyo [emoji2380][emoji2380][emoji2380][emoji2380][emoji2380][emoji2380]

Kwenda uko pinde wew
 
Ndugu hv unajisikiaje kutengeneza ugomvi? Nashukuru kwa maneno yako na acha tu nikuepuke nadhani upeo wako umefikia hapo
Wew ndio unanitumiaga vibendera vyenu hvyo sas ulikuwa ulikuwa na maana gani kunitumia[emoji2380]

Muite na mwezako yule mambo sasa
 
Yaani unaamini humu ndo utaondolewa stress zako? Maana umekuja nazo.mhusika hajalalamika na ameonesha kujiamini hadi anaahidi kunitag. Wewe kajamba nani unaleta makasiriko. Hii inatokana na nini?kushindwa kwako unataka kuwahamishia wengine lawama. Why cant you just shove it in your as* and run away[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Mwenye uzi hana neno. Wewe tu unayaleta hapa makalio yako na kuyapigiza pwaaaah.... Huoni kuwa nimekaa hapa. Hujali na huogopi.
Very good ,majibu mujarabu kbsa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu - 05


Niliita Zai! Zai! Lakini hakunisikia wala hakunijali, aliendelea kubamiza mlango akiropoka na kunguruma. Niliogopa hata kumsogelea maana nilihisi angenivamia na kunijeruhi hivyo nikawa namtazama kwa mbali, namtazama huku nikipaza sauti kama itasaidia.

Kidogo nikapatwa na ufahamu, ufahamu wa kupiga simu kuomba msaada wa nini cha kufanya katika janga lile. Nliperuzi katika simu yangu nikaibuka na namba ya mama mmoja hivi ambaye alikuwa ni jirani yangu kule nilipokuwa ninaishi kabla ya kuhamia kwangu, mama huyo tulizoea kumwita Mama Miraji, alikuwa mama mwenye kushika dini sana, masaa ishirini na manne amejisitiri, hakosi ibada, swala tano kama chakula.

Nikamweleza mama huyo shida yangu naye akaniambia yuko mbali lakini ningoje aone kipi cha kufanya. Basi baada ya muda mdogo, mama huyo akanipa maelekezo, alinitaka niweke 'loudspeaker' simu yangu kisha niwe karibu na mhanga wangu, nikafanya hivyo, mara mama yule akaanza kuongea kwa lugha ya kiarabu, lugha nisiyoielewa, aliyasema na kuyasema mambo ambayo kwangu yalikuwa mageni, aliyatamka kana kwamba anayasoma mahali, kidogo kama utani, nikaanza kumwona Zai analegea na kulegea.

Hapo nikapata nguvu ya kumsogelea. Nilimsogelea nikiwa namwelekezea simu yangu kana kwamba simu ile ni silaha, si punde Zai akaanguka chini na kuwa kimya, kimya kama amekufa, nikaogopa tena!

Haraka nilimsogelea nikamtikisa, simu nimeiweka kando, bado inaendelea kusema maneno nisoyaelewa, nikamwita Zai, Zai, kimya. Ila alikuwa anahema, hilo angalau likanipa nguvu.

Baadae, kama baada ya robo saa hivi, Amiri alirejea nyumbani. Nilisikia mtu akisemezana na ng'ombe huko nje, kutoka nikamwona kijana huyo akiwa anawaswaga ng'ombe kwenda zizini, upesi nikamwita, naye upesi akaja.

Nilimuuliza alikuwa wapi namtafuta kiasi hiko? Kabla hajajibu nikamtaka aingie ndani haraka kunisaidia, akafanya hivyo mpaka kwenye mwili wa Zai, alimnyanyua mwanamke huyo kama ubua akamweka kwenye kochi. Kweli nilistaajabu. Sikutegemea kijana yule kama angeweza kumnyanyua Zai namna ile. Kama ungewahi kumwona Amiri nadhani ungenielewa kwanini nilistaajabu kiasi hicho. Mwili wake ulionekana goigoi kinyume kabisa na matendo yake.

Baada ya kumweka Zai kwenye kochi, aliniaga akafungie ng'ombe, basi akaondoka akiniacha mimi namtazama Zai. Si muda, Zai akaamka akiwa analalamika kichwa kinamuuma.

Aliponyanyua mkono wake kujishika kichwa akahisi pia maumivu. Alitazama mikono yake akaiona mekundu kwa kuvilia damu, inamwaka moto, akabubujisha machozi kama mito, tayari alishajua nini kilitokea.

Alinambia, "nimechoka hii hali! Nitaishi hivi mpaka lini?" Kweli nikamwonea huruma sana. Alinambia namna gani hali ile inavyomtesa, haikuwa habari mpya kwangu maana nilikuwa nafahamu, lakini siku ile nilihisi kila alichonieleza ni kipya, pengine sababu nilimshuhudia kwa macho yangu na si kuhadithiwa kama hapo awali.

Alilalamika, "kila mwanaume ninayepata, akishajua nina mambo haya basi ananikimbia. Nitakuja kuishi na nani mimi?"

Nilimpa pole nikamshauri tuonane na yule mama Miraji kwani kwa yale aliyoyafanya siku ile kwa simu pekee niliamini angeweza kutusaidia kukabili lile janga, hata kama hatoweza basi anaweza kutushauri pa kwenda au kipi cha kufanya.

Haikupita muda, Zai aliaga akaenda zake. Niliona hiyo ni kheri maana hakuonekana na raha tena pale. Nilijaribu kumwongelesha na kumfurahisha lakini sikufua dafu. Alipopotea, hata nami nikapata afueni. Nilijumuika na Amiri kutazama mifugo, huko tukaongea mambo machache.

Kwasababu Amiri hakuwa mtu wa kuongea sana, ni mimi ndo' nilikuwa namchokonoa kwa maswali ya hapa na pale. Kitu peke ambacho Amiri alikianzisha katika maongezi lilikuwa ni swali moja tu, aliniuliza;

"Yule ni rafiki yako?" Akimaanisha Zai, nikamjibu ndio, naye hakuongeza tena neno. Alikaa kimya mpaka mimi nilipoondoka, nilimwona akinitazama nikienda zangu mpaka kuudaka mlango na kuzama ndani.

Baada ya tukio hilo la Zai, zilipita kama siku mbili hivi bila kumwona mume wangu, kama kawaida akisema ni majukumu mapya ya kazi. Siku ya tatu, alirejea nyumbani na mimi siku hiyo nikaazimia kuendelea na zoezi langu la kukagua simu yake.

Lakini simu hiyo nilipoishika, katu sikufanikiwa, nilikuta amebadili nywila za kufungulia simu yake akiweka mpya ambazo mimi sizifahamu. Nilijaribu kila nilichowaza lakini wapi! Mwishowe nikaachana nayo nikiwaza kwanini bwana yule ameamua kufanya mabadiliko yale.

Ina maana amenishtukia au?

Au alipata kuongea na yule mwanamke kuhusu simu niliyopiga siku ile? Simu ile ambayo sikusema kitu hivyo mwishowe akagutuka? Sikupata majibu sahihi lakini niliamini mawazo yangu, bwana yule atakuwa ameshtuka.

Kesho yake majira ya mchana nikiwa kazini, nilimpigia simu mama mkwe wangu, lengo kujua atapokea nani na kama ninaweza pata chochote kwake kuhusu yanayoendelea, simu ikaita pasipo kupokelewa, kimya.

Nilijaribu kupiga tena lakini napo sikuambulia kitu, simu ilikuwa inaita mpaka kukata kwake, basi nikaachana nayo niendelee na mambo mengine, baadae majira ya jioni, nikajaribu tena, simu ikaita na mara hii ikapokelewa na sauti ya mwanamke, si sauti ya mama mkwe wangu lakini pia sio ngeni masikioni mwangu, sikuwaza sana nikaikumbuka sauti hiyo barabara, nilikuwa sahihi, ilikuwa ni sauti ya mwanamke wa siku ile, mwanamke aliyemwita bwana Mgaya mume wangu!

Mwanamke huyo alinisalimu kisha akasema mwenye simu hayupo, nikamuuliza kaenda wapi, akakaa kimya kidogo, nikarudia swali kaenda wapi? Akanijibu anaumwa yu hospitali, hawezi kutumia simu majira hayo.

Nikamuuliza, "wewe ni nani yake mama?" Hakujibu, kama kawaida nikarudia tena swali, nikalirudia kwa mkazo, akanijibu yeye ni mwangalizi wa mama wakati huu akiwa anaumwa.

Mwangalizi? Nikagunia kifuani.

Mwangalizi kama nani yani? ... Kabla sijatema kauli, akawa amekata simu. Tangu hapo nilipiga kadiri ya nilivyoweza, hakupokea tena, zaidi nilipoongeza usumbufu akani-block kabisa. Niligundua hilo maana nilipojaribu kupiga simu hazikuwa zinatoka tena, wala ujumbe haukuwa unafika.

Sasa nikaona nitulie. Nitulie nione huu mchezo unapoelekea.

Keshokutwa yake, bwana mkubwa alirejea nyumbani na kitu cha kwanza kunambia punde tu baada ya kupeana salamu ilikuwa ni hali ya mama yake. Aliniambia mama yake anaumwa, hali yake si nzuri, na vile tuongeapo, yuko hospitalini anauguzwa.

Moja kwa moja nikajua maongezi yale ni sababu ya mazungumzo nilofanya siku ile na yule mwanamke kwani mama mkwe hakuanza kuumwa siku hiyo, kwa namna nilivyoongea na mwanamke yule siku ile tayari yule mama alishatumia siku kadhaa hospitali, sasa mbona Mgaya hakuniambia?

Nilijikuta natabasamu nikimskiza Mgaya. Muda mwingine kuna raha yake mtu kukuona zuzu huku wewe unamsanifu, lakini Mgaya alihisi kabisa kuna jambo lipo kombo, kila alichosema mimi nilimkubalia na wala sikuuliza swali, mwishowe akaniuliza; "uko sawa kweli?"

Mimi nikamjibu niko sawa, hamna shaka, basi maisha yakaendelea, kichwani mwangu nikipanga vyangu na namna ya kufanya. Ilipofika mwisho wa juma, pasipo kumwambia mtu yeyote, nlijiandaa nikafunga safari kwenda Iringa, nyumbani kwa wakina Mgaya, huko ndo' nikaenda kujua mbivu na mbichi ...

Kumbe Mgaya alikuwa ameoa kimila, na mwanamke yupo huko kwao, kwenye 'kamji' kake ndani ya kaya yao, ndugu zake wote wanafahamu kinachoendelea na wanamtambua mwanamke huyo kama mke wa Mgaya!

Walishtuka kuniona nimefika hapo, na si muda mrefu Mgaya akawa amearifiwa kuhusu ujio wangu wa kushtukiza. Alipiga simu mno lakini hamna hata moja nilopokea, mwishowe nikazima simu kukwepa usumbufu.

Nilichokuja kubaini kule Iringa ni kwamba, mama yake na Mgaya, yaani mama mkwe wangu, ndiye alimshinikiza Mgaya kuwa na mwanamke mwingine wa kibena ambaye atakuwa anamtazama na kumuagua pale nyumbani.

Sawa, nalifahamu mwanamke yule hakuwa ananipenda, hata mimi sikuwa nampenda vilevile, lakini kile alichonifanyia kilivuka mipaka. Niliona amenikosea mno mno, na ajabu ni kwamba hakuonekana kujutia nalo, zaidi nilipomwona kule hospitali aliniuliza akinikenulia meno yake, umemwona mke mwenzio?

Nilitamani nimkabie hapo kitandani mpaka afe!

Baadae nilikuja kupata taarifa kuwa mume wangu yuko njiani anakuja akitokea Dar, maneno hayo niliyasikia toka kwa shemeji zangu walokuwa wakiishi hapo, nami sikutaka kuonana naye, nikafanya upesi kupanda zangu basi kurejea huko yeye alipotoka, hivyo tukapishana njiani.

Simu yake sikupokea, wala ujumbe wake sikuujibu.

Sasa nieleze, mtu huyu hakustahili kifo? Sijui kwako, lakini kwangu alistahili mno mno. Si yeye tu, pia na mama yake. Kama waliyajua haya, kwanini walikubali nikaolewa katika familia yao na desturi ile ya kipuuzi? Kwanini wasingemtafutia mtoto wao mwanamke wa huko kwao yote yakaisha?

Niliongea mwenyewe njia nzima. Nang'ata meno na kufuta machozi yanayonilenga. Naumwa na uchungu lakini nikimtazama mwanangu napambana kutabasamu, nilikuwa nafanya hivyo mpaka kufika Dar. Safari ndefu ya kuchosha. Safari ambayo mume wangu alikuwa akiifanya alipokuwa akipotea juma zima kule nyumbani.

Kuja kumwona mkewe mwingine.

Basi nilifika nyumbani nikashinda siku mbili, siku ya tatu yake majira ya usiku namwona mume wangu akiingia ndani pamoja na mama yake mzazi. Mama huyo anatembea kwa kuchechemea. Amevalia gauni na kujitanda khanga.

Bwana Mgaya akaniambia, "mke wangu, najua kuna mambo mengi yalitokea hapa katikati. Usijali, nitakueleza kila kitu pasipo kuficha. Nimeona ni stara nikamleta mama hapa nyumbani tukamuuguza, kwanza naomba tumpokee alafu yetu binafsi tutayaongea na kuyamaliza."

Mgaya ....

Maskini Mgaya,

Hakujua alikuwa amemleta mama yake kwenye kifo. Hakufahamu kuwa pale mama hakuja kuuguzwa bali alikuja kuuawa.

Mama yule hakuliona jua mara tatu katika nyumba ile, tukatangaza msiba. Yeye akiwa ndo' mtu aliyefungua dimba la umauti pale nyumbani....


***
 
Back
Top Bottom