Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Niliweka shada za maua kwenye makaburi matano ya watu wangu wa karibu

Mmemu outshine na konki zenu kaona aage mashindano mdogo wetu nyie wabaya sana
Sio kweli mkuu, jamaa atakuwa busy na personal issues tu. Akikaa sawa atarudi kuendelea. Kwani hajatoa taarifa zozote?
 
Sana yani
Soma hii hapa n nzuri sana huyu anatuma kila siku na imefika mbali
Noted
 
Sehemu ya Kumi na nane:


Hamna alichosema mtoto nikaelewa kwanini ana jeraha lile mguuni.

Kila alichoongea na kila alichonijibu sikuona kama vina mahusiano na kuumia kwake basi nikajikuta nasisitiza tu aache utundu na kuhangaika, atulie ndani na kusikiliza yale anayoambiwa na watu wazima.

Sasa ningefanya nini kingine?

Niliendelea na shughuli zangu za pale ndani, japo kwa uchovu mkubwa wa ujauzito.

Nilishika hiki na kile kadiri nilivyoweza na baada ya muda mfupi nilijilaza kwenye kochi nikiwa hoi, kabla sijapitiwa na usingizi nilipiga simu nyumbani kuongea na mama na kisha mdogo wangu Sarah kuhusu pesa ile nilowatumia.

Najua ilikuwa ni ndogo, haikidhi mahitaji, lakini ni kheri kuliko kukosekana kabisa, waswahili husema heri nusu shari kuliko shari kamili.

Nilimwahidi mama punde tu mshahara wangu utakapotoka nitamtumia balansi nzuri kwani najua ana mambo muhimu sana yanamngoja huko shambani.

Nilimwambia pia mdogo wangu anivumilie, mwisho wa mwezi haukuwa mbali, kama juma hivi lilikuwa limebakia, punde tarehe itakapowasili basi na yeye atapata chochote kitu, asichoke kungoja.

Baada ya simu hiyo usingizi ukaninyakua kama mwewe.

Nililala hapo nisisikie chochote mpaka pale mtoto alipokuja kuniamsha akisema baba amekuja.

Niliamka nikasilimiana na bwana Mgaya, hali ya kazi na huko atokako kisha nikampatia chai kutimiza wajibu wa mke baada ya hapo bwana huyo akaenda zake kupumzika, alisema amechoka sana, nimwache alale aamke na akili mpya.

Kabla hajaenda, aliacha pesa kidogo ya 'meza', pesa hiyo nikaihifadhi upesi maana nalikuwa na uhitaji nao sana, akiba yangu yote ilishakwanguliwa na mama kule kijijini, sasa nilikuwa nahitaji kuanza upya kwa kubabiababia pesa ya Mgaya huku nikingojea pesa yangu ya mshahara.

Baadae, majira ya jioni, baada ya kupumzika, bwana Mgaya alinambia kuwa kule kazini kwake kuna tafarani, hali haiko shwari, kuna baadhi ya watu wenye husda wanamwaribia kwa wakuu wa kazi na kama asipopambana basi anaweza kurejeshwa kwenye majukumu ya barabarani, kule alipotoka kabla hajakaimu kiti cha ofisi.

Alinambia sasa inabidi afanye namna kuongeza jitihada yake ya kazi hivyo basi katika kila juma moja, atakuwa anashinda kazini siku mbili, siku hizo zitakuwa mahususi kwaajili ya kufuatilia madereva nyakati za usiku katika kutimiza majukumu yao.

Nikapokea taarifa hiyo kwa mikono miwili.

Nilimsihi afanyie kazi hayo alosema maana kati yangu na yeye hakuna alokuwa anataka bwana huyo atoke katika kiti alichokuwa amekalia kwani malipo yake ni mazuri na pia haikuwa kazi ya kuchosha kama ile ya kushinda barabarani mlimojaa hatari za kila namna.

Hicho ndo' kilikuwa kisanga cha bwana Mgaya na kazi yake.

Lakini,

Wakati huo moshi unafuka kwa jirani yangu, kumbe na huku kwangu palikuwa panateketea...

Siku naenda kazini, mapema kabisa kabla sijaingia darasani, nilipata wito wa kufika katika ofisi ya mkuu wa shule.

Niliitikia wito huo bila hiyana, kufika nikapewa taarifa kuwa niko hatarini kusimamishwa kazi muda wowote ule kwasababu ya kushuka kwa ufanisi wa kazi yangu.

Mwalimu mkuu alinambia amepokea malalamiko kadhaa kutoka kwa mtaaluma ya kwamba sihudhurii vipindi vyangu kama inavyotakiwa na pia kazi yangu ina mapungufu mengi, mathalani sitoi kazi za watoto kufanyia majumbani, sifanyi ukaguzi wa kazi za wanafunzi, sishiriki kwenye 'playful learning' na ninachelewa kufika kazini.

Kwa maelezo ya mwalimu mkuu, ile ilikuwa ni nafasi ya mwisho, baada ya hapo nitalimwa barua nikakae nyumbani maana kazi imenishinda.

Alipomaliza kuyasema hayo, alinitaka nitoke ofisini mwake kwani ana shughuli nyingi za kufanya, yeye sio kama mimi ambaye nashinda kulala juu ya meza kwenye majira ya kazi.

Nikawa sina budi nyingine bali kwenda zangu.

Sikupewa muda wa kujieleza wala kujitetea kwa lolote, nilirudi ofisini na mzigo huo wa vitisho nikaendelea na majukumu yangu ya kila siku.

Siku hiyo, kwasababu nilitoka kupewa karipio, sikuacha hata tone moja la kazi, kila nilichopaswa kufanya nilifanya kiasi nikawa hoi sana wakati natoka shuleni.

Niliapa nikifika nyumbani, nitalala kabla ya yote maana nilihisi nashindwa kabisa kuumudu mwili wangu.

Nilifika lakini kinyume kabisa na nilivyopanga, nilianza kuhaha maana mtoto alipandwa na homa sana, kichwa chake kilikuwa cha moto mithili ya jiko la gesi.

Tangu nilipofika nyumbani, hali yake ilikuwa inazorota kadiri muda unavyoenda.

Nilimpigia bwana Mgaya kumtaarifu, uzuri akaja nyumbani upesi tukampeleka mtoto hospitali, huko alipimwa akabainika ana maambukizi kwenye damu, akapatiwa dawa tukarejea nyumbani.

Yalikuwa ni majira ya saa moja jioni.

Kufika tulikuta nyumba iko kwenye kiza totoro, hamna taa hata moja ilowashwa, tukastaajabu Amiri atakuwa wapi?

Niliingia ndani nikawasha taa, bwana Mgaya alinyookea kule mabandani kutazama, baada ya muda mchache bwana huyo alikuja ndani akasema kila kitu kilikuwa sawa kule bandani, nami nikamwambia kila kitu kipo sawa kule ndani, lakini hamna kati yetu aliyefanikiwa kumwona Amiri.

Tuliendelea na mambo mengine mimi nikiwa nimechoka sana kwani sikupumzika kule kazini na pia kufika nyumbani nilikutana na dhahma ya mtoto.

Mpaka kufikia muda naenda kulala, sikumtia Amiri machoni, ilikuwa ni kama saa tatu ama nne hivi ya usiku, nilijilaza kando ya mwanangu anayeumwa kwaajili ya kumjulia hali lakini sidhani kama nilisikia kitu mpaka kuja kukurupuka majira ya saa kumi hivi usiku.

Niliamka baada ya kubanwa na haja ndogo.

Nilienda bafuni nikiwa nimefumba macho kwa usingizi, natambaa na ukuta nikifuata hisia kama mdudu jongoo.

Wakati najihudumia maliwatoni, ni kama nilisikia kitu nje, sikuwa na uhakika na masikio yangu, lakini nilipotoka maliwato kuelekea kitandani nilisikia tena kitu hiko na sasa nikawa na uhakika,

Uhakika kuwa kile nilichosikia kilikuwa ni sahihi, nje kulikuwa na shughuli inaendelea, sikujua ni nini lakini nilihisi kabisa kuna uwepo wa mtu anayefanya jambo kule nje maana haikuacha kusikika sauti hii na sauti ile.

Nilichungulia dirishani, nikazungusha macho kule na kule, sikuona kitu.

Nilivuta subra niendelee kuangaza, kukawa kimya tuli.

Kidogo nikasikia sauti tena, kutazama nikamwona paka akitokea upande wa kule bandani, alikuwa ni paka mweupe mwenye madoa meusi, taa ya nje ilimdaka vema.

Paka huyo altembea taratibu akienda upande mwingine.

Nilimshtua kumfukuzia mbali, akasimama na kutazama sauti inatokea wapi, nikarudia kumfukuza, hapo ndo' akaona sauti inatokea dirishani pangu, akaangaza na macho makali.

Macho yake yalihakisi mwanga wa taa hivyo yakawa kama yanamulika.

Alitazama dirishani kwa kitambo kidogo kisha akaenda zake, taratibu pasipo kujali nalikuwa namfukuza au lah.

Nilimtazama mpaka anaishia, akili yangu yote ikiwa inahangaika naye, kidogo nikasikia sauti nyuma yangu, nikakurupuka kwa woga kweli!

"Mbona dirishani muda huu?"

Alikuwa ni bwana Mgaya, ameketi kitandani akinitazama.

Nilishusha pumzi ndefu kuondoa hofu kifuani mwangu kisha nikasogea kitandani na kumweleza nilichokuwa nakifanya pale dirishani.

Aliniuliza kuhusu paka yule kisha tukahamishia mazungumzo yetu kwa kijana Amiri.

Nilimuuliza kama alipata kumwona Amiri baada ya mimi kwenda kulala, akanambia hapana, alikaa sana kumngojea kama atakuja lakini hakumwona.

Kabla ya kwenda kulala, akakata shauri kwenda kutazama chumbani kwa kijana huyo ili ajihakikishie, ajabu akamkuta akiwa ndani, amejilaza kwenye godoro.

Kumbe muda wote huo tunahaha na kujiuliza juu ya uwepo wake, yeye alikuwa yuko zake ndani chumbani!

Bwana Mgaya alijaribu kumwamsha ili kumjulia hali, kwamba huenda anaumwa ndo' maana amejilaza kama mfu, lakini hakufanikiwa abadan, kijana alilala mithili ya gogo, hajigusi wala hatikisiki.

Bwana Mgaya alinambia kama isingekuwa kijana yule alikuwa anahema, basi angelidhania amefariki.

Mpaka anaondoka kuja chumbani, Amiri hakupata kuamka.

Jua lilipokuchwa shughuli ziliendelea kama kawaida, pale nyumbani na hata huko makazini.

Siku hiyo nilienda kazini mwenyewe maana mtoto alikuwa anaumwa, hivyo nilimwacha pale nyumbani pamoja na Amiri ili mimi nipate kufika kazini kivyovyote vile maana sikutaka zogo na mkuu wa shule wala mtaaluma wake.

Baadae niliporejea nyumbani nilionana na Amiri, tulisalimiana nikamjulia hali mwanangu, baada ya hapo nikapata muda mchache wa kuzungumza na kijana yule.

Nilimuuliza kuhusu siku ya jana yake, ilikuaje akawa amejilaza kitandani mapema sana tena akiwa ameacha nyumba kizani, akanambia alikuwa amechoka sana na hivyo alipojilaza baada ya kumaliza kazi zake alipitiwa na usingizi mkali.

Nilimuuliza kuhusu paka yule wa usiku kama atakuwa alimsikia vurugu zake, akanambia hakusikia kitu, usingizi alokuwa nao ulipumbaza kweli masikio yake.

Kisha aliniuliza kuhusu mtoto na lile jeraha lake la mguuni.

Alitaka kujua mtoto alilipatia wapi jeraha lile na mimi nilifanya nini baada ya kugundua.

Nilimweleza ninayoyajua kisha tukahitimisha maongezi yetu yeye akienda kule bandani.

Baadae, kama baada ya lisaa limoja hivi, bwana Mgaya alirejea nyumbani.

Ajabu siku hiyo, tofauti na siku zingine nilivyozoea, bwana huyo alikuja kwa miguu, jambo ambalo lilinishtua kwa kiasi chake.

Uso wake ulikuwa umeparwa na hasira, na alipoingia tu ndani alishusha pumzi akiegamiza kichwa kwenye kochi.

Ni dhahiri huko alikotoka hakukuwa na jema.

Nilipomuuliza alinambia amesimamishwa kazi kwa muda usojulikana, kwa muda wote huo ameambiwa arejeshe vitu vya ofisi mpaka pale atakapopewa taarifa zaidi.

Bwana huyo alikuwa amechanganyikiwa na nilelewa kwanini alikuwa vile, kupoteza kazi sio kitu chepesi kabisa haswa ukizingatia una majukumu ya familia mabegani mwako.

Alilalamika namna alivyokuwa anajitoa na kupambania kampuni lakini mwisho wa siku watu wengine ndo' wanaonekana na kupewa thamani.

Lakini bwana yule aliapa kwamba hatokubali kushindwa, ataamka na kupambania haki yake kwa namna yoyote ile.

Kweli siku ile iligeuka kuwa miongoni mwa siku mbaya sana.

Furaha ilizima kukawa kama kuna msiba vile, msiba wa mtu asofahamika.


Sasa tangu hapo, mimi ndo' nikawa mlishaji mkuu wa familia, mlishaji ninayetegemea ujira usiozidi laki tatu kwa mwezi! Ebu fikiria.

Tulipitia wakati mgumu kiasi kwamba bwana Mgaya alilazimika kuuza baadhi ya mifugo ili angalau apate 'pocket money' na pesa ya kusafiria kwenda nyumbani.

Alinambia anataka kwenda nyumbani kwa hali na mali, kule ataonana na baadhi ya watu na kila kitu kitakuwa sawa.

Alisihi sana safari hiyo ni muhimu.

Japo hakusema anaenda kukutana na nani lakini ilikuwa bayana anaenda kuonana na 'mtaalam'.

Sikuweza kufanya lolote kubadili mawazo yake, na wala sikujisumbua japo awali niliona anapoteza muda na pesa yake.

Nilimwacha afanye vile anavyoona ni sahihi kujitibu nafsi yake.

Haikupita muda, mwisho wa mwezi nilokuwa naungoja kwa hamu ukawadia.

Nilikuwa nimepanga kwenye pesa hiyo, mbali na ile mipango ya awali, nimpatie bwana Mgaya hata kiasi kidogo kitakachomuunga mkono huko safarini na kijijini.

Yani pesa ile ilikuwa ni kama lulu, nalala naiwazia naamka naiwazia.

Ajabu nilipoenda kutoa pesa hiyo, nilikuta kitu ambacho sikutarajia kabisa, kitu ambacho kilininyong'onyesha mno.

Huwezi amini, nusu nzima ya mshahara wangu ilikuwa imekatwa!

Nikatingwa na mawazo kweli, sasa nafanyaje na yale yote yalokuwa yananingoja? Nilihisi kichwa kimenielemea.

Nilimwambia bwana Mgaya habari hiyo mbaya naye akahuzunika kweli, pesa ilokuwapo haitoshi tena kugawana.

Alinambia hamna namna, atasafiri vivyo hivyo, mengine yataenda kujulikana huko mbele ya safari.

Kweli baada ya siku chache, bwana yule alifunga safari kwenda nyumbani kwao.

Safari ile sitokuja kuisahau, na kama ningelijua matokeo ya safari ile, basi ningefanya kila namna kuizuia isipate kujiri.

Kwani,

Baada ya bwana Mgaya kutoka kule Iringa, ndoa yangu haikuwapo tena, na haikukaa ikarudi katika hali yake kamwe.

Sijui ni kitu gani yule mtaalam alimwambia bwana Mgaya.

Kweli sifahamu.

***
Nimekipenda zaidi kipande hiki kwakua kinaongelea zaidi maisha halisia tunayopitia watu ,panda shuka,maanguko ya kiuchumi na etc.unakuja nagari maisha bwerere mara unakuja kwa mguu nyumbani,nabarua ya kuachishwa kazi juu.usiombe yakukute haya.
 
Hivi Chizi Maarifa upo kweli??mbona kuna vijana wana leta dhereu afu umekaa kimya tu
Huwa nafika wadau wanapoleta malalamiko mezani kwangu kama hivi. Mimi ni mtetezi wa walaji aka wasomaji. Pale inapotikea mwandishi anaandika uongo halafu anataka waaminisha watu ni kweli naingilia kati. Pia anapotaka kuanza kuwaibia wasomaji au kama pia anaanza kulega lega kuwasilisha story kwa wakati.
 
SteveMollel nimesikia kilio cha wasomaji. Nakupa masaa hayo ... Uwe umeweka kisa kingine au ujieleze kwa nini umekuwa na delay kuwatungia visa vingine wasomaji. Kumbuka kuwa hawakukuomba ulete hii story. Ni kiherehere chako mwenyewe. Sasa wameanza kufuatilia usianze kuleta madeko na mapozi.

Nakupa order tunga visa vingine ulete. Na kama umejichanganya sana sasa unakosa mwendelezo sema tu maana najua changamoto za utungaji sometimes kisa kinakosa mwendelezo sababu ulijichanganya sehemu.

Lakini kama sivyo utaniambia kwa nini usichukuliwe hatua kali kwa kuchezea hisia za wasomaji wengi ambao hawana cha kufanya hii story ndo ilikuwa inawasukumia siku zao.
 
SteveMollel nimesikia kilio cha wasomaji. Nakupa masaa hayo ... Uwe umeweka kisa kingine au ujieleze kwa nini umekuwa na delay kuwatungia visa vingine wasomaji. Kumbuka kuwa hawakukuomba ulete hii story. Ni kiherehere chako mwenyewe. Sasa wameanza kufuatilia usianze kuleta madeko na mapozi.

Nakupa order tunga visa vingine ulete. Na kama umejichanganya sana sasa unakosa mwendelezo sema tu maana najua changamoto za utungaji sometimes kisa kinakosa mwendelezo sababu ulijichanganya sehemu.

Lakini kama sivyo utaniambia kwa nini usichukuliwe hatua kali kwa kuchezea hisia za wasomaji wengi ambao hawana cha kufanya hii story ndo ilikuwa inawasukumia siku zao.
ha haaaa jamani mbona ndo atafuta na bandiko lenyewe
 
Hizi story za kutunga ambazo huwa mnalazimisha kusema ni kweli ukifikia hatua flani zinakuwa ngumu sana kuendeleza. Hapo mtunzi huanza kukimbia kimbia na kutoa udhuru. Unamwona kabisa yumo humu anasoma tu comments ila anakuambia hivi na vile. Yaani ili mradi tu.
Mara mwingine anasema nilifiwa wkt anaonekana kwenye majukwa ya michezo
 
Back
Top Bottom