Niliyoyabaini katika Operesheni ya Polisi dhidi ya watuhumiwa wa Panya Road - Dar es salaam

Uko sahihi sana, kama kweli wanachokifanya polisi cha kuua wezi ni sahihi, kuna mtu alikamatwa kwa kujiunganishia bomba la mafuta hapo nyumbani kwake. Mbona mtu huyu hatujasikia kapigwa risasi maana yeye kaiba kikubwa kuliko panya road?
Mkuu , hata hao panya road wangekuwa wanaiba bila kudhuru mwili wa mtu kelele zisingekuwa nyingi.

Shida wao wanajeruhi na kuua na mali wanachukua pia. Hivyo haifanani na huyu aliyejiunganishia bomba bila kuingilia usalama WA watu wengine.
 
Mkuu , hata hao panya road wangekuwa wanaiba bila kudhuru mwili wa mtu kelele zisingekuwa nyingi.

Shida wao wanajeruhi na kuua na mali wanachukua pia. Hivyo haifanani na huyu aliyejiunganishia bomba bila kuingilia usalama WA watu wengine.

Ni sawa, lakini polisi hawaaminiki wanapomtuhumu mtu, ndio maana tunataka hao wauaji wakadhitishwe mahakamani.
 
Sasa wewe katika kufanya uchunguzi wako huo ulitegemea familia za hao panyaroad wakwambie walikuwa ni wezi? Acha kwanza polisi wafanye kazi yao la sivyo hao vibaka mtawapa nguvu ya kurudi upya maana wanatetewa, huu sio muda muafaka wa kuongea haya.
 
THREAD YA KUPUUZA HII.
POLISI NAO WANACHOKA JAMANI ACHA WAWAFYEKE,KUMBUKENI POLISI WETU KABLA YA KUFANYA LOLOTE HUWA WANAKUWA WAMESHACHUNGUZA KWA KINA,KABLA YA UTEKELEZAJI.
Rubbish! Polis wetu ni dhaifu sana kuchunguza ndo maana hutumia short cut kwani mahakamani watashindwa.
 
Maandamano ya POLISI kujikaimisha mamlaka ya Mahakama kuhukumu wananchi adhabu ya kifo bila kufikishwa MAHAKAMANI.

Kwani hii ni POLICE STATE???🙃🙃🙃
Yaani polis wetu wanatoa judgement za capital punishment? Khaa!!! Under what law?
 
Hujaelewa nilichokisema. Mwanao hajafanya uhalifu lakini anapigwa rusasi. Mahakama za nini Sasa?
Mnasahau ya akina Zombie?
 
Police puuzeni kelele hizi za wachache endeleeni na zoezi la kuua hawa viroboto na mapanya, tena msirudi nyuma wala msipoe mmezoeleka mno hadi raia hawana uwoga teketeza hao vibwengo panya buku wote
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam na kamanda wa kanda maalum ya Dar Es Salaa kuna siku lazima washitakiwe kwa makusudi kuvunja katiba ya nchi na kuvunja haki za binadamu. Kuna tofauti gani kati ya wananchi wenye hasira kali na polisi wenye wajibu wa kulinda raia na mali zake? Panga na mshale inaweza ikajibiwa kwa risasi ya moto?

1. Mkuu wa mkoa Dar
Kamanda kanda maalum ya Dar
3. Kamanda wa upelelezi kanda maalu ya Dar
4. Waziri wa mambo ya ndani

Hao watajwa hapo juu hata ikichukua miaka kumi mbele watakuja kushitakiwa kujibu ni nani aliwapa mamlaka ya kuua raia aisye na silaha inayozidi bunduki. Hata huko Serengeti haiwezekani raia akamiliki silaha ya G3, hiyo ipo jeshi ya ulinzi na JKT pekee. Kila silaha huwa ina namba tambuzi je, silaha hiyo ni ya Tanzania au imepatikana kwa wakimbizi na ilifikaje Mara, Serengeti wakati haina mgogoro wa kivita na mipaka ya Kenya?

Yanayosemwa na wananchi yapuuzeni tu majuto ni mjukuu.
 
Uko sahihi sana, kama kweli wanachokifanya polisi cha kuua wezi ni sahihi, kuna mtu alikamatwa kwa kujiunganishia bomba la mafuta hapo nyumbani kwake. Mbona mtu huyu hatujasikia kapigwa risasi maana yeye kaiba kikubwa kuliko panya road?
Huyu hajamtoboa mtu na bisibisi mkuu
 
Abduli Nondo a.k.a Mwalimu na wakili wa Panya Road na wewe ni lofa .
Unacheza na amani ya nchi.
Halafu uko kwenye Chama Cha kijamaa. Unawezaje kujenga ujamaa na Wahalifu.

Polisi Kwa raia wema ni wastarabu sana. Tena siku hizi wanakupigia simu au kukupelekea barua kupitia mtendaji. Unaenda Kistarabu mwenyewe kituoni.

Kwa hiyo ukiona Polisi wametoka kituoni na kukufuata ujue wanataarifa zote za uhalifu. Kwa hiyo wanakuja Kwa tahadhari zote ulijaribu kuzingua wanakuzingua.


Lakini pia wewe ni mtanzania asiyefaa kabisa yaani ni Msaliti. Na dawa ya Msaliti ni Moja TU. Wanaokua kwenye vita dhidi ya panya road wanajua dawa ya Msaliti hivyo Huyo Nondo sijui Nunda anapaswa kupewa dawa yake.
Hawa akina Nondo wakiachwa ndio watakaoleta uhalifu na mauaji ya wafanyakazi wa mabenki , Wasafiri kama kule kwao Burundi wanavyopora wasafiri kwenye mabasi. Huyu Nunda na ndugu zake Kule Burundi waliwaua sana watanzania miaka ya 2000 mpaka 2010 Kwa kuvamia mabasi kule Kagera na Kigoma . Kwao huyo mpuuzi uporaji ni kazi halali hivyo hatuna haja ya kumsikiza.

Wewe na wanaharakati washenzi kama wewe kama wanaweza kufanya uchunguzi Kwa Polisi basi ni wahuni mana wanashindwa kuchunguza Wahalifu halafu wanaweza kuchunguza Polisi. Wachunguzeni Wahalifu ili muwabaini Kisha Polisi watawakamata na kuwapeleka mahakamani . Lakini wewe na wahuni wengine mnashindwa kutumia ujuzi wako wa uchunguzi kuwabaini Wahalifu halafu inakuja kulia lia hapa.

Panya road wasipoacha uhalifu wataendelea kuliwa kichwa TU na mwishowe wakili wao Nondo naye naye atakula chuma TU mana hakuna namna nyengine
 
Rubbish! Polis wetu ni dhaifu sana kuchunguza ndo maana hutumia short cut kwani mahakamani watashindwa.
Upelelezi ni pamoja na Jina LA muhalifu kuwa na kesi au mashauri mengi ya kihalifu katika vituo mbalimbali na kufungwa jela zaidi ya Mara 3-4,bila mtuhumiwa kukoma KUFANYA uhalifu.,ndio maana nikasema probably wengi hao huwa ni wahalifu sugu,wasiotaka kubadilika hata baada ya kufunzwa na serekali.
KUYAFUGA MAJITU SUGU NI HATARI KUBWA NA USUMBUFU MKUBWA KWA SIKU ZA USONI.
N.b,-Acha kutukana bila hawa ndugu zetu hata usingizi wako pengine ungekuwa mashakani.
 
Nina mashaka humu kuna majambazi.
Au kuna watu hawajawahi kukutwa na dhahma za vitendo vya kihalifu wakawaona jinsi madogo wakishavuta mabangi na ugoro jinsi wasivyo na huruma,huku tabata kuna mama mjamzito aliwahi kufyekwa mimba kwa upanga,dada wa watu akajifia bila sababu.
 
Umeandika yote Ila sijaona sehemu umesema kuwa umewahoji Majirani na wanasemaje kuhusu Hao waliouawa!

Lete interview ya Majirani tuone wanasemaje!

Unadhani mzazi anaweza kukiri mwanae ni panya road ?

Halafu mbona majuzi kuna Panya road kauawa na raia Manzese hujaifuata familia yake kuwahoji na uanze kukemea raia kuchukua hatua za kisheria mkononi.


Tunajua police Wana mapungufu Yao, tuwakemee. Ila Kwa hili la Panya road hapana kabisa Acha hawa vijana walambwe Shaba!
 
Mkuu , hata hao panya road wangekuwa wanaiba bila kudhuru mwili wa mtu kelele zisingekuwa nyingi.

Shida wao wanajeruhi na kuua na mali wanachukua pia. Hivyo haifanani na huyu aliyejiunganishia bomba bila kuingilia usalama WA watu wengine.
Issue kubwa hapa ni kwamba polis wana uhakika gani waliomuuwa ndiye alifanya uhalifu huo wa kuiba, kujeruhi na hata kuua.
Yaani polis nao wanauwa tu kitu ambacho hawaruhusiwi kwani wanalazimika kisheria kuwapeleka mahakamani.

Inavyoonekana wengi humu moja kwa moja akamatwaye na polis tayari ana makosa.

Mbona watuhumiwa wengine huwapeleka mahakamani? Siwangekuwa wanawahukumu wao tu na kuwapeleka jela kama wanao uwezo huo kisheria?

Watz hebu tujaribu kufikiri masuala haya kwa kufuata misingi ya Sheria.
 
Ndiyo maama watu walilalmikia teuzi za Wambura na Kingai kuwa IGP na DCI. Historia zao toka wakati wa JPM si nzuri.

Mikono ya SSH imeshachafuka kwa damu za watu wasio na hatia.

Hii damu itamlilia, sidhani kama damu hii itamuacha salama!.Mikono yake imeshaloa damu!
 
Haidhuru basi polis wanapowauwa washukiwa wa panya road wangekuwa wanataja vifungu vya Sheria vinavyowapa uwezo kufanya hivyo.
Najua Kuna watu watakuja hapa na hoja ya kijinga kama: 'Kwani wao panya road wanatumia vifungu gani vya Sheria kuua'.
Hoja za kijinga sana hizi kwani wahalifu huwa hawafuati Sheria yoyote lakini polis analazimika kufuata Sheria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…