Niliyoyaona baada ya kuita roho za giza kwa kutumia OUJIA board (don't try this at home)

Niliyoyaona baada ya kuita roho za giza kwa kutumia OUJIA board (don't try this at home)

Unataka kutoa boriti ya jicho langu wakati ww jicho lako hutaki Kanisani kila jumapili mnafundishwa uongo mbona usemi ukiwa ww unapenda kusema kweli biblia imejaa uongo kila mahali mbona hujawahi kusema
Naona unataka kuhalalisha uongo wako kwa vile wengine wanadanganya. Kwa hio umekubali wewe ni muongo?!
 
Hahaha!

Kuna channel moja niliifuata You Tube wanajihusisha na paranormal activity.

Wana session yao kuomba kutumiwa vitu ambavyo vina aminika vina vina laana au vinaleta majanga mfano kama mdoli wa Annabelle.

Alitumiwa mzigo mmoja kutoka Haiti baada ya siku mbili aliutupa.
Nipe link mkuu nicheke
 
Naona unataka kuhalalisha uongo wako kwa vile wengine wanadanganya. Kwa hio umekubali wewe ni muongo?!
Biblia imejaa uwongo kama ww msema kweli mbona hujawahi kuwaambia kanisani kuwa kuna uwongo au uwongo wako upo kwa upande upande na kila jumapili unaenda kanisani kusikiliza habari za kutunga na hujawahi ongea
 
Biblia imejaa uwongo kama ww msema kweli mbona hujawahi kuwaambia kanisani kuwa kuna uwongo au uwongo wako upo kwa upande upande na kila jumapili unaenda kanisani kusikiliza habari za kutunga na hujawahi ongea
Itakuwaje umefanya occult na useme bibilia ina uwongo, hujui consecration ya vitu na huyo beelzebub au amaymon zinafanywa na bibilia bila hyo hupati usaidizi wa kumsubdue any of the principal kings wa kuzimu.
Nikiwa muislamu hivi hilo najua itakuwaje hujui ???
 
Itakuwaje umefanya occult na useme bibilia ina uwongo, hujui consecration ya vitu na huyo beelzebub au amaymon zinafanywa na bibilia bila hyo hupati usaidizi wa kumsubdue any of the principal kings wa kuzimu.
Nikiwa muislamu hivi hilo najua itakuwaje hujui ???
Habari nyingine za uwongo hata akili ya kawaida haikubali mfano Yesu kuzaliwa bila ya baba hii ni hadithi ya kutunga hakuna mtu anaeweza kuzaliwa bila ya baba hayupo kwa vyovyote vile Yesu atakuwa ana baba ake wa kibanadamu
 
Nielekeze sasa niwaone mimi hao ndio nawataka 😹😹😹
Aah! Wewe!
Binafsi sifahamu namna gani ya kukutana nao isipokuwa ni matatizo tu yakanikutanisha nao!

Ila hutoweza kulala! Na utashikwa na kiwewe! Kuna vitu kwa maelezo havitoshelezi ila ukiviona kwa macho vinatisha.

Wale viumbe (majini) Mungu kuwaficha kwetu ana maana kubwa.

Mosi, maumbile yao yanatisha.

Pili, wanatoa harufu.
 
Habari za wakati huu wana jukwaa

Duniani hatupo peke yetu, vipo viumbe au roho ambazo kwa macho hatuwezi kuziona, zipo katika dimension nyingine, lakini ipo namna tunaweza kuwasiliana au kutengeneza ukaribu nao.

Swala hili halina uhusiano wowote na imani yangu bali ni jambo ambalo niliona katika baadhi ya harakati na tafiti zangu binafsi, kujaribu na kudadisi mambo mapya ni moja ya hulka na tabia yangu.

OUJIA board ni nini?

View attachment 3045441

Ni kipande au ubao ulioundwa kwa mbao na kuandikwa kwa mpangilio wa herufi na namba ambazo hutumika kuita au kufanya mawasiliano na roho za giza. Upande wa kushoto kuna neno YES na upande wa kulia NO, upande wa chini lipo neno linalo someka GOOD BYE.

Ubao huu huambatana na kitufe au kipande kidogo cha mbao ambacho huitwa planchettes, hii hutumika kama pointer, kimbao hicho huwa na umbo la kopa na kishimo kidogo katikati yake.

Matumizi ya vitu hivi viwili yana lengo la kutafuta au kuita roho ambazo zipo karibu yetu katika mazingira tuliyopo kwa wakati huo kwa kuzungusha kipande kidogo juu ya ubao wa OUJiA board.

Baada ya kufuatilia kwa ukaribu mchezo huu na kugundua una uhalisia na kuleta matokeo, ndipo na mimi nikaona ni vyema kujaribu na kujua ni nini hasa hutokea au huonekana.

Nilikuwa na rafiki ambaye anajihusisha na uagizaji wa bidhaa katika soko la Amazon, ndipo nikamuomba tufanye order ya OUJIA board, nilifanikiwa kuipata bidhaa ikiwa katika hali nzuri kama yalivyokuwa matarajio yangu.

Nilikaa nayo kwa muda mrefu pasipo kujaribu kuitumia, sababu ni bado nilikuwa najifunza kwa kutazama videos ili nijue njia sahihi ya kutumia ubao huo. Japo katika video hizo niliona matukio ya kutisha lakini bado niliamini naweza kufanya kwa usahihi bila kupata au kuona madhara yoyote.

Mnamo tarehe 24/ 11/2022, baada ya kurejea nyumbani Mida ya saa tatu usiku, ndipo nikatoa ubao ule na kuutazama kwa dakika kadhaa, nikaona hii ndyo siku sahihi ya kufanya majaribio.

Nikauchukua ubao na kuuweka chini, nikawasha mishumaa mitatu na kuiweka pande tofauti yani mbele, nyuma na pembezoni mwa ubao. Nikatia nia na kufungua zoezi kwa kutamka maneno maalum. Hofu ilinijaa lakini sikusita kwani tayari nilikuwa na kusudi la kujaribu.

Nilianza kuzungusha kipande kidogo cha mbao katika herufi na namba zilizoandikwa katika OUJIA board, sikuona wala kusika chochote. Nikajaribu tena kwa mara nyingine huku nikiuliza kwa sauti "Is there any presence of spirits? " Am I alone? "

Nilichagua kutumia Lugha ya kingereza kwa kuhofia labda kiswahili kinaweza sababisha nikaita vigagura au vibwengo vya kiswahili. Wakati bado nazungusha kipande cha mbao (pointer) juu ya ubao, ndipo nikahisi kuna sauti nasikia bila kujua zinatoka wapi.

Nilihisi labda ni woga tu niliokuwa nao, niligeuka nyuma na sikuona kitu, lakini bado nilihisi sauti na upepo kutokea upande wa nyuma. mkono wangu uliokua juu ya ubao ukaanza kusogea bila idhini yangu, hapo nikajua tayari nimepata ugeni.

Nikauliza "what is your name"? Mkono ukasogeza ile pointer mpaka kwenye herufi "J", nikauliza "how old are you" pointer ikajisogeza yenyewe wakati nimeishika mpaka kwenye namba 34.

Nikauliza "do you wish to harm or attack me" pointer ikasogea Mpaka upande ulio andikwa NO. Bado nikawa nahisi upepo au hewa kali inatokea upande wa nyuma nilipokuwa nimekaa, lakini nikigeuka sioni kitu.

Uoga ulinizidi kwani ilikuwa ni usiku sana na nilikuwa pekeyangu, nikaamua nisitishe zoezi na kumalizia mchezo.

Kwa utaratibu wa mchezo huu, baada ya kutosheka na maongezi na Spirit husika, unapaswa kusogeza pointer katika maneno yaliyo andikwa Good bye ili kuruhusu roho hiyo kuondoka na kumaliza game, lakini nilishindwa kufanya hivyo kwani mkono ulikuwa hauwezi kabisa kusogeza kile kibao.

Nikatoa mkono na kuacha ile pointer, ajabu ni kwamba ilianza kuzunguka yenyewe na kurejea kwenye herufi 'J' kisha namba 34. Ubao niliuweka chini kabisa hivyo usidhani kwamba labda ulikuwa kwenye meza na chini kuna sumaku au kitu kingine. Ni kweli kabisa niliona pointer inazunguka yenyewe juu ya ubao pasipo kuguswa na mtu.

Niliogopa sana na nilifanikiwa kutoka nje haraka. Siku ile sijarudi nyumbani kabisa na nikaenda kulala kwa rafiki. Nilipo rejea asubuhi nikachukua ubao ule na nikautupa, ila badae niliurejea na kuuchoma moto kabisa.

Nadhani nilikosea sheria au taratibu za mchezo, pia niligundua sio jambo sahihi kutafuta mawasiliano au ukaribu na roho za giza. Kuanzia siku hiyo mpaka leo, nikilala kwenye chumba changu naota lakini sikumbuki ndoto yoyote, tofauti na sehemu nyingine. Nahisi bado kuna tatzo ndani ya chumba changu, itabidi nihame nijaribu sehemu nyingine.

Hili tukio ni la kweli na nilikutana nalo wala sio hadithi au story ya kutunga, kama yupo atakaye hitaji kujaribu, nipo tayari kumpa maelekezo lakini atambue kwamba ni mchezo hatari sana na sio vyema kuufanya ukiwa pekeyako.

Shukran kwa kusoma andiko hili, karibu share maoni au experience yako kuhusu OUJIA board.

View attachment 3045421


______________________



#BM
Hongera
 
Aah! Wewe!
Binafsi sifahamu namna gani ya kukutana nao isipokuwa ni matatizo tu yakanikutanisha nao!

Ila hutoweza kulala! Na utashikwa na kiwewe! Kuna vitu kwa maelezo havitoshelezi ila ukiviona kwa macho vinatisha.

Wale viumbe (majini) Mungu kuwaficha kwetu ana maana kubwa.

Mosi, maumbile yao yanatisha.

Pili, wanatoa harufu.
Km wanatoa harufu basi mkuu 😹😹😹
 
😹😹😹 Nipe namba zao mkuu, tena itapendeza km ukinipa za chairman wao nimrukie hewani..!!
Hahaha! Una masihara wewe unanifurahisha sana!

Ngoja nizungumze na jamaa yangu amwambie kuna mtu anataka kujenga na wewe urafiki. Akikubali nitakufahamisha.
 
Hahaha! Una masihara wewe unanifurahisha sana!

Ngoja nizungumze na jamaa yangu amwambie kuna mtu anataka kujenga na wewe urafiki. Akikubali nitakufahamisha.
Liwe linanipa michongo ya pesa sasa.!!
Sio urafiki wa kutishana tyuu.!! 😹😹😹
 
Aah! Wewe!
Binafsi sifahamu namna gani ya kukutana nao isipokuwa ni matatizo tu yakanikutanisha nao!

Ila hutoweza kulala! Na utashikwa na kiwewe! Kuna vitu kwa maelezo havitoshelezi ila ukiviona kwa macho vinatisha.

Wale viumbe (majini) Mungu kuwaficha kwetu ana maana kubwa.

Mosi, maumbile yao yanatisha.

Pili, wanatoa harufu.
[emoji81] kwaiyo hawa nukii marashi mazuri tena .
 
Km wanatoa harufu basi mkuu 😹😹😹
Vumilia tu!

Kwa mara moja inakuwa!

Halafu wanapenda kutokea kwa mazingira ya kutisha.

Kama kawaida yako ni kutoka asubuhi sana unaweza ukashangaa siku umekutana na mtu ghafla kasimama barabarani. Sasa itategemea mwenyewe atataka akujie kwa umbile gani!
 
Vumilia tu!

Kwa mara moja inakuwa!

Halafu wanapenda kutokea kwa mazingira ya kutisha.

Kama kawaida yako ni kutoka asubuhi sana unaweza ukashangaa siku umekutana na mtu ghafla kasimama barabarani. Sasa itategemea mwenyewe atataka akujie kwa umbile gani!
Sio wabakaji?? 😹😹😹
Nijiandae kabisa usiniletee midude ikanipelekea moto bure..!!
 
Liwe linanipa michongo ya pesa sasa.!!
Sio urafiki wa kutishana tyuu.!! 😹😹😹
Achana nao wale viumbe pesa zao zina masharti sana!

Chochote utakachoingia nao mkataba lazima ukilipie gharama.
 
Back
Top Bottom