Niliyoyaona kwa Mkapa (Lupaso) Stadium leo ambayo kama yasipofanyiwa Kazi basi yanaenda Kujirudia tena Lake Tanganyika 25 July, 2021 ni haya

Niliyoyaona kwa Mkapa (Lupaso) Stadium leo ambayo kama yasipofanyiwa Kazi basi yanaenda Kujirudia tena Lake Tanganyika 25 July, 2021 ni haya

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
1. Kuwaanzisha Erasto Nyoni na Bernard Morrison ambao leo ndiyo Wachezaji wa Simba SC waliocheza vibaya na Kuharibu zaidi badala ya Kuwaanzisha Muzamiru Yasini na Rally Bwalya Kiufundi kumeigharimu Simba SC.

2. Kumuanzisha Clatous Chama ambaye bado Kichwa chake kimetawaliwa na Kumpoteza Mke huku ikijulikana Kiufundi kabisa Saikolojia ina nafasi yake katika Ufanisi wa Mchezaji Mpirani.

3. Kutangulia Kumuingiza Meddie Kagere ambaye kwa sasa hana tena Madhara yote na ameshuka mno Kiuchezaji na Kuchelewa Kumuingiza Mshambuliaji makini Chris Mugalu Kiufundi Kumeigharimu Simba SC.

4. Ama Kocha Mkuu na Msaidizi wake au Wachezaji wa Simba SC kwa sasa wamezidi Kujiamini na kuwa na Dharau wakisahau kuwa Mechi ya Derby'na Yanga SC ni zaidi ya Kucheza na akina AS Vita Club, Al Ahly na Kaizer Chiefs FC.

5. Simba SC kutokuheshimu Utamaduni wa Derby ambapo Kambi ya Simba SC kule Bunju ilikuwa ni ya wazi na kila Mtu hata Adui aliruhusiwa kwenda na Kuhudhuria tofauti na iliyokuwa Kambi ya Yanga SC ambayo ilitawaliwa na Umakini, Tahadhari na Ulinzi mkubwa sana.

6. Ndani ya Klabu ya Simba kuna Usaliti mkubwa sana na kuna Watu wanaodhaniwa ni Simba SC kweli kumbe ni Mapandikizi ya Yanga SC na ndiyo kwa miaka hii Minne wamechangia Yanga SC kuwa na Kiburi dhidi ya Simba SC japo Kiuwezo hata Wenyewe wanakiri Kuzidiwa na Simba SC.

7. Wachezaji wa Simba SC kutokuwa na Moyo wa Uchungu na wa Kujitolea Kuifia Timu / Klabu kama alionao Jose Miquissone ambaye huhitaji Akili Kubwa kujua kuwa ndiyo mwenye Uchungu hasa na Mafanikio ya Simba SC kuliko wengine ambao Uchungu walionao ni Kutongoza hovyo Wahudumu wa katika Ndege, Kutoroka Kambini kwenda Klabu na kufanya Uzinzi, Kujipodoa na Kutwa kuwa tu Mitandaoni kituringishia Gari zao, Nguo zao na Wake / Mademu zao.

Nitakuwa siyo Mwanamichezo, Mpuuzi na Mnafiki pia kama baada ya kusema yote haya nisiipongeze Klabu ya Yanga SC kwa Kushinda Mchezo wa leo kwa Goli la Kimchezo ambalo kamwe ukiwa Mtu wa Mpira huwezi Kumlaumu Kipa Aishi Manula na Beki Shomary Kapombe.

Kwa wale wanaomlaumu Mwamuzi Mwandembwa kuwa ameiumiza mno Simba SC je, tumeshajiuliza kuwa Timu inayoumizwa na Mwamuzi Wachezaji wake kwa Statistics wanaweza kuwa ndiyo wanaongoza kwa Kucheza Faulo / Rafu nyingi zile?

Ushauri wangu wa bure tu kwa Wana Simba SC ni kwamba badala ya Kumlaumu Mwamuzi tumeshukuru kwa Kuwavumilia sana Wachezaji wa Simba SC kwani nina uhakika angeamua Kuchezewa Kiukauzu na inavyotakiwa basi John Boko, Thadeo Lwanga, Joash Onyango, Bernard Morrison, Mohammed Hussein Tshabalala na Pascal Serge Wawa wangetolewa kwa Kadi Nyekundu.

Simba SC ikubali Matokeo ijipange mno.
 
Mkude nakiri ni Mlevi, Mvuta Bangi na Mpenda Misambwanda, ila bado ana Umuhimu mkubwa sana Kikosini Simba SC kuliko vile ambavyo Watu tuliomchoka kwa Vitimbi vyake tunavyodhani.
Akacheze timu za walevi....
Ni bora tugongwe kila siku, ila sio kumkumbatia mchezaji anayeona timu ni kama ya kwake.
 
Sasa kama mna majibu haya ya Jeuri mbona kila akitishia Kuhamia Yanga SC haraka sana huwa tunamsainisha Mkataba tena kwa Kumbembeleza abakie Msimbazi?
Safari hii imekula kwake....
Vijana lazima wajifunze, mtu miaka 10 kwenye timu yet anabehave kama mtoto mdogo.
Aende tu huko yanga, ambako labda wataruhusu mchezaji anayejipangia ratiba,
 
Anaelekea Kigoma now(joke)....
... .......anyway anayesema refa kawabeba Yanga, muulize imekuwaje leo Boko kamaliza dakika 90? Japo angepata hata yellow card......japo hakutakiwa kuwepo dimbani
bf111110376340dab724b709cae1109b.jpg
 
Jenta hapa umeandika kweli tupu ila kuna muda nawe unakuwa kama msemaji wenu mnatabia ya kupanic hovyo, utopolo aka chura kapata matokeo kutokana na alivyocheza,
 
Mkude nakiri ni Mlevi, Mvuta Bangi na Mpenda Misambwanda, ila bado ana Umuhimu mkubwa sana Kikosini Simba SC kuliko vile ambavyo Watu tuliomchoka kwa Vitimbi vyake tunavyodhani.
Mkude abadilike muda wake wa kupiga hela ndio huu
 
Mimi nimekuwa sikubaliani na upangaji wa timu wa huyu kocha kwa muda sasa. Kule south na KC alipanga list ya hovyo. Leo tena kapanga list ya hovyo. Lwanga angeenda na Muzamiru na Morrison angeanzia bench.

Ukicheza ki-Yanga Yanga huwezi kuwafunga Yanga. Mpira wa pasi nyingi huwafanya Yanga kuchanganyikiwa siku zote. Alikuja kuharibu game alipoongeza sriker wa tatu. Mfumo gani huu wa kipumbavu!!!

Alikuwa na option ya Ndemla baada kutoka Chama ambaye namsamehe kutokana na maswahiba yaliyomkuta. Kitendo cha kuchezesha wachezaji hao hao kila siku mimi binafsi sikipendi. Kweli kocha hapangiwi timu lakini kwa leo ametuangusha. Na maana hiyo ninam-miss sana Sven ambaye asingepanga magorofa matatu pale mbele ambayo hayana mbinu za kiufungaji.

Tatizo la kupoteza nafasi za wazi limekuwa ni tatizo sugu katika safu ya ushambuliaji ya Simba. Katika kila mechi atayocheza Simba iwe ya ndani au ya kimataifa, Simba hupoteza nafasi si chini ya nne katika kila mchezo. Kuna game inahitaji upate nafasi moja na uitumie. Sasa hata kama tunafunga tatu bila na kupoteza saba za wazi, ipo siku uta pay the price na hicho ndicho kilichotokea kwenye game ya leo.

Trust me, mechi ya Kigoma itakuwa ni ngumu zaidi ya hii leo na kama Simba itaanza na mtindo wake wa slow start na kuamka baada ya kufungwa goli, tutegemee matokeo kama haya kwani kwa maoni yangu naona Yanga wako vizuri kwenye viwanja vibovu kuliko sisi kutokana na nature ya mpira wao. Kwa hiyo inabidi tujipange kweli kweli huko Kigoma.
 
Katika point zako zote point ya maana sana ni ya kupoteza nafasi na ni wazi Simba ilipata nafasi za wazi nyingi zaidi kuliko hata hao Yanga lakini matumizi ya nafasi hizo ndiyo yalinishangaza.

Haya twende kwa Yanga , unaweza kuniambia ikiwa Yanga walicheza vizuri zaidi walipata clear chances ngapi na walikosa ngapi na kwa nini?

Maana kuna shida naiona katika uchambuzi wa kibongo yaani timu ikiconced goli tu anaanza kulaumiwa kocha ohh angempanga huyu au yule hapa tu unaongea eti Nyoni ni mbovu mara angeanza mzamiru ila umesahau mzamiru ana udhaifu wake ambao mechi kadhaa anauonesha nao ni kupoteza pasi nyingi japo ana ubora wake mkubwa kwenye ukabaji (kupora mipira haraka) at the end game imeisha Morison akiwemo na alicheza alivyoweza.Kumbuka Simba wanacheza mpira endelevu yaani wa kitabuni Yanga wanakamia tu cos wanatambua wana madhaifu mengi tu.

Kuhusu Sven , ndo huyo huyo mliyemlaumu daily ohh anapanga mshambuliaji mmoja , mara timu haifungi magoli mengi yaani sijui tunapenda nini kwa kweli ,hivi unaweza kwenda kuwaambia watu eti Yanga walikuwa bora zaidi ya Simba uwanjani kisa wamefunga tena a deflection ball goal yaani hicho ndicho kipimo kweli? [emoji23] unadhani watapata hizo deflection goals siku zote brother sahau hilo.

Mazoezi kuwa wazi sio sababu kama ingekuwa Sababu basi Yanga alipaswa ashinde goal 5 alipe kisasi cha miaka ile basi.Chambueni kiutu uzima sio blahblah nyingi kama hizi mnaharibu uhalisia ndiyo maana Yanga huko CAF kaenda mara nyingi than simba ila ana mafanikio kiduchu ukilinganisha na Simba kwa kuwa tu many times wanacheza kumkamia Simba while Simba ashavuka steji hiyo.

Ngoja tuone hizi next two games nani atakuwa mbabe huenda kila siku watapata deflection ball jambo ambalo kamwe siliamini
 
Katika point zako zote point ya maana sana ni ya kupoteza nafasi na ni wazi Simba ilipata nafasi za wazi nyingi zaidi kuliko hata hao Yanga lakini matumizi ya nafasi hizo ndiyo yalinishangaza...
Mkuu umecheki game?? Hebu comment kiwango cha simba.

Kwa comment hii unataka kusema simba imecheza vyema jana?? Wachezaji wake wengi walikua chini ya kiwangi sijui kwanini. Kiukweli hawakua normal leo tifauti na ile mechi ya 1-1.

Ile mechi walipofungwa goli moja tuliona kabisa uhitaji wa kusawazisha mpaka wakapata goli tofauti na hii ya jana.

Haya tusubiri kigoma.
 
Katika point zako zote point ya maana sana ni ya kupoteza nafasi na ni wazi Simba ilipata nafasi za wazi nyingi zaidi kuliko hata hao Yanga lakini matumizi ya nafasi hizo ndiyo yalinishangaza...
Wewe hapa umechambua au umelalamika?

Kinachokufanya usikubali ubora wa mpinzani wako ni nini wakati kila mtu anayechambua hapa kaiona Yanga ilivyocheza kipandi cha kwanza na Simba kupotea kwa takribani DK 30 za kwanza? Ukiamua kuchambua chambua ukija kishabiki sema wewe ni shabiki.

Kitendo cha mechi kuisha bila Mzamiru huku kocha akichezesha 3 strikers ni kubet kusiko na mpangilio. Ukiangalia Sub alizofanya Nabil utakubaliana na mleta Uzi, ni kocha kichaa tu angekubali Kaseke acheze DK 70 uwanjani,

Feitoto amecheza kwa nguvu muda mrefu na alikokuwa anaelekea ni kwenye kadi nyekundu ukikumbuka foul dhidi ya Engineer. Tuisila kuanzia DK ya 70 alikuwa likizo ya bila malipo kwa hiyo kupumzishwa ilikuwa haina mjadala.

Rudi kwenye Sub za Simba sasa.
 
Mkuu umecheki game?? Hebu comment kiwango cha simba.
Kwa comment hii unataka kusema simba imecheza vyema jana?? Wachezaji wake wengi walikua chini ya kiwangi sijui kwanini. Kiukweli hawakua normal leo tifauti na ile mechi ya 1-1.
Ile mechi walipofungwa goli moja tuliona kabisa uhitaji wa kusawazisha mpaka wakapata goli tofauti na hii ya jana.

Haya tusubiri kigoma.
Game nimeicheck vizuri kabisa ndiyo maana nimesema wazi shida ilikuwa kutumia nafasi tu upande wa Simba

Mfano Boko alikosa goli ambalo kwa mchezaji ambaye ni makini hakupaswa kukosa , Morisson alikosa goli hivyo hivyo , kwa kifupi game ilikuwa mikononi mwa Simba hasa second half ila nafasi hazikutumiwa vizuri na wachezaji wetu.Ukitazama vizuri utagundua kuwa tumeingia kwenye box ya Yanga mara nyingi zaidi , naamini huwezi kufanikiwa kuingia kwenye box ya mpinzani zaidi afu tuseme hamkucheza vizuri katikati ya uwanja au mpira kwa ujumla unless kucheza mpira vizuri kuwa kuna maana nyingine.

Goli la Yanga la deflection ni maamuzi ya mtu kupiga shuti kuelekea golini na likamgonga mtu likajaa wavuni at the end unakuwa umeshinda ila hata Kocha makini hawezi kujivunia hilo ,kocha makini atajiuliza kama ule mpira usingedeflect kwa beki wao Je,timu yangu ilikuwa na uwezo wa kutengeneza nafasi za wazi na kuzitumia? Kama hakuna nafasi zinazotengenezwa na timu kocha mzuri anajua hii sio class ni bahati tu.

Ninachokikubali kwa sehemu pia ni hili la kujitoa kufa kupona kwa Yanga (hii ni nature ya timu inayohisi ni dhaifu ila inajaribu kuonesha ina ubora mkubwa ) wachezaji katika game hizi wanacheza kwa umakini hata kama viwango vyao kesho hutoviona hivyo jambo linaloitofautisha na Simba na haya hujidhihirisha kwa namna ambavyo timu inaperform kwenye mashindano marefu hasa ya Ligi za mzunguko.

Jaribu kufikiri upya , ikiwa refa angetoa penalty ile Simba wakafunga then wakashinda tungekuja hapa kusema wachezaji wa Simba hawajitumi kama wa Yanga? Vipi kama nafasi za wazi za Morison na Boko zingekuwa magoli tungekuja na stori hiyohiyo? Kwangu ni hapana

So kama Yanga watashinda games tatu zijazo mwaka huu mbele ya Simba tutakuwa na cha kuhoji zaidi kwa nini ,ila kwa jana mi naona bahati tu maana mimi sijui ishu za uchawi naamini tu uchawi upo ila ulikuwa applied au la jana mie sijui.
 
Mkuu umecheki game?? Hebu comment kiwango cha simba.

Kwa comment hii unataka kusema simba imecheza vyema jana?? Wachezaji wake wengi walikua chini ya kiwangi sijui kwanini. Kiukweli hawakua normal leo tifauti na ile mechi ya 1-1.

Ile mechi walipofungwa goli moja tuliona kabisa uhitaji wa kusawazisha mpaka wakapata goli tofauti na hii ya jana.

Haya tusubiri kigoma.
Simba aliupiga mwingi second half
 
Back
Top Bottom