Ways back miaka ya elf 2 nakumbuka nilikula training moja kali Sana viwanja vya mwamposa kawe jkt wakasome yule Mkenya retired army alitupigisha training hatari utadhani unaajiriwa na Wagner Group kumbe KK security aisee.
Pana siku nilizidiwa nikatoka nduki Cha kufia nini nilipofika home nikikumbuka msoto wa mtaa kesho yake nikawahi kwenda kuomba msamaha nikatoa sababu,wakaniambia awaajiri vichaa toka hapa.
Nikabembeleza sana aisee life msoto wakanikubalia.Nikamaliza training ya wiki mbili.
Wajinga wale mnalishwa wali maharage saa Saba baada ya kula mnaenda kuulipa uwanjani.
Nikapiga kazi mwaka mmoja huku napiga mishe zingine.
Supervisor alinielewa nikawa naingia usiku tu asubuhi naulamba kutembeza kaki maofisini jioni naingia Lindon, home narudi weekend.
Hakika safari ya maisha ni simulizi tosha.
Pana siku likapigwa Dili la kuingiza wezi waibe mafuta Depot za matenk ya mafuta kurasini.
Kazi ikapigwa tukapewa pesa mbuzi wajinga wanazijua koki zote kulingana na aina ya mafuta dizeli, petrol,taa.
Kumbe security manager nyuma ya geti Kuna nyumba ya Mzee mmoja informer wao akamnyoshea mchezo wote mzima asubuhi tukaitwa tukawekwa mtu kati.
"Niambieni ukwel au muende jela ikabidi tufunguke ni kweli mchezo tunaijua ikaripotiwa ofisin kwetu,wakatufukuza kazi.
Nikashukuru maana jela miaka 7 walitusaidia sana.
Baada ya kazi kuisha nikazama BOT kuendesha crane za ukutani za kupandisha mafundi juu enzi zile za ujenzi wa majengo pacha ya BOT, Nikiwa kwenye mchakato wa kuchukua Hela yangu nssf nifanye nauli ya kuchomoka south Africa.Nikapata kazi panono bongo.
Mlinzi mwenzangu niliyekuwa nae tukilinda akapata kazi panono tukaja kutana nae CBE tukapiga bachelor siku hizi anaporomosha vituo vya mafuta tu.
Maisha ni safari kutoka kulinda hadi Leo nalala nimelindwa.
Usikate tamaa,usichague kazi.