Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

Habari!

Nilipomaliza form 6 zikatoka nafasi za kwenda jeshi wanaita "kwa mujibu" basi nikaangaza macho yangu kwenye orodha nikaona "Ephen - Rukwa"

Basi nikafurahi sana, furaha haikua kwasababu naenda jeshi hapana! Hata mpango nayo nilikua sina ila tu niliona ni bahati jina langu kua kwenye list sababu sio wote uchaguliwa.

Nikawasiliana na marafiki zangu kuna baadhi walichaguliwa pia lkn hakuna niliyechaguliwaa nae kambi moja, nikaanza kusikia story plus video za status, instagram watu wanaeka makuruta wanavyogaragara kwenye matope, mazoezi magumu hadi wanalia, nikapata uoga hapo ikawa mzozo nikasema mimi jeshi siendi kwanza kunyoa kipara hapana.

Mzee akaniambia lazima uende, huko Rukwa mkuu wa kambi ni rafiki yangu hivyo wewe mateso hutoyapata nikafikiria nikaona huyu mzee ananipiga fix ili nijae mimi jeshi siendi.

Ila nikawa nataka sitaki na kilichokua kinanitatiza kwenda ni yale mateso tu niliyokua naona kwenye video.

Kuna siku rafiki yangu akanipigia simu kunishawishi twende ila akaniambia "Ephen twende kambi ya mkoa X achana na Rukwa huko wana mazoezi makali sana" nikamwambia kama hivyo fresh acha nijiandae tutaenda next week sababu deadline ilikua bado. Rafiki yangu nampa jina Anna.

Anna ana kaka ake ni mjeda sasa akawa anatupa tips muhimu za kuzingatia mojawapo alisema tranka tutakalobeba tusijaze vitu vingi tuweke vitu vyepesi ikiwezekana vitu tukanunue kambini hukohuko.

Mimi niliona usumbufu yaani nitoke na tranka tupu vitu nikanunulie kambini? nikanunua vitu vyote nikajaza kwenye tranka. Kumbe yule mjeda alikua na maana yake Aisee bora ningemsikiliza.[emoji23]

SIKU YA SAFARI
Tukatoka zetu na Anna tukapanda gari tunaenda kambi ya mkoa X japokua tumepangiwa kambi tofauti kila mtu.

Tupo kwenye gari nina furaha naenda kupata experience mpya pia nilifurahi kwenda mkoa mwingine sababu nimezoea dar tu, safari ilichukua almost masaa 7 tukafika huo mkoa X mjini, gari ndo mwisho.

Sasa wote hatujui nini kinafata hapo Anna yeye tranka lake niseme lipo tupu kabeba vitu muhimu tu, mimi nimejaza hadi kubeba linanishinda.

Tukamfata konda kumuuliza, "Sisi tunaenda kambi X tunaomba utupe muongozo" akatuambia pandeni bajaji hadi kituo flani mkifika kuna hiance zinaenda huko jina la kambi ndo jina la kituo cha kushuka.

Tukafanya kama alivyotuambia, tumeingia kwenye hiance asilimia kubwa wana vipara hivyo nikajua wote tunaenda kambini.

Kule tuliposhuka na gari nilipapenda sana ni kuzuri panavutia hamna pilikapilika nyingi nakumbuka nilimpigia simu mama, akaniuliza umepaonaje nikamjibu kwa furaha ni pazuri nimepapenda akaniambia "ukifika kambini nijulishe lkn ukiona huko mateso yamezidi nipe taarifa nikufate urudi nyumbani"

Basi tulivyokua kwenye Hiance tunaenda huko wilaya yenye kambi mwanzoni nasmile na Anna wangu ghafla akili yangu ikavurugika tuliingia barabara ya vumbi sijawahi ona, gari zima hatuonani, kila mtu kwenye gari katapakaa vumbi hadi kope zote nyeupe ndani ya pua nywele vumbi hapo nikapata sign ninapoenda sio pazuri.

Safari ilichukua kama masaa 3 tukaambiwa wale wa kambini mmefika.

Katika maisha yangu bad moment niliyowahi kuexperience ni hii siku, Tumeshuka tu nikaona njia ya vumbi imekata kulia ni ndefu kama 2km nikasikia sauti "Hapohapo wote chuchumaa tranka kichwani ruka kichurachura uelekeo huu hapa kwenda kambini"
Kudadeq ndo nikajua kwanini niliambiwa niende na tranka tupu

Anna yeye chap kachuchumaa tranka kichwani, mimi machozi yashaanza kunitoka nikamwambia Anna mimi nimeghairi siendi narudi nyumbani, hata sijamaliza sentensi nishakula bao la mgongo kutoka kwa mjeda akaanza kufoka wewe bila shaka umetoka Dar naongea tii Amri kwanini umesimama ? Aya tranka kichwani kuruka uelekeo huu.

Akaja mjeda mwingine akanitwika tranka kichwani hapo nishachuchumaa sikuweza kuimili kuruka na tranka.

Anna akaniambia lete nikusaidie chukua langu, yule mjeda aliona tu hata akinipiga ule mzigo siuwezi na Anna pia hauwezi akamwita mjeda anayejitolea chukua hili tranka wasaidie, basi nikapona hivyo.

Kimbembe kikawa hiyo kichurachura nikiangalia mbele sioni geti, ni mbali almost 2km ndo niruke kichurachura? Hapo machozi yananitoka nalia nkamwambia Anna "mimi namwambia mama anifate siwezi hizi mambo" Anna nae analia Ephen usiondoke ukaniacha mwenyewe bora hivi tupo wote Afadhali.

Nilihisi miguu inawaka moto inataka kupasuka, msafara tupo wengi hadi wanaume wanalia, sasa tulivyoloa vumbi hadi kope mtu ukimuangalia mwenzako unatamani kucheka ukisikilizia maumivu ya miguu unatamani kulia.

Itaendelea......
Pumbafuvu mtoto wakiume ulia lia heti kuluka kichula
 
SEHEMU YA 6

NIKAFUNGUA MOYO

Nilifungua moyo niliona sina jinsi pale siwezi kutoka, mateso upande wangu yalipungua kuna ratiba za jeshi nikaanza kuzipenda hivyo sikuons mambo tena kama mateso ila njia ya kujifunza.

Kwanza, saa 10 alfajiri filimbi ikilia nawahi kombania inapigwa rokoo.
Baada ya pale wanaita wagonjwa njoeni upande wa huku, wazima pangeni mistari mabio yanaanza uelekeo road kuu. (Mabio- Jogging)

Nilikua nakimbilia mabio bila kulazimishwa nilikua naenjoy zile chenja sababu zinaongeza morale na My favourite ni hii; (Nimesahau maneno ila anayekumbuka naomba aniandikie)
[emoji445]Kimbwekombweko cheza!
Kimbekele cheza....[emoji445]


WEEK 6
Nakumbuka tulikua kombania usiku tumekaa chini kwenye vumbi bakabaka ana dumu na fimbo akipiga 1 tunasimama akipiga 2 tunachuchumaa akipiga 3 tunalala chini zoezi, push up za kutosha ila hapa girls tulikua tunachekesha sana hizo pushup zetu! Tulikaa mpaka saa 5 tukaenda kulala

Mimi nilikua nikirudi Angani naenda kuoga, kupiga mswaki na marafiki zangu tukirudi tunavaa nguo kabisa ndo tunalala ili filimbi ikipigwa hiyo saa 10 alfajiri ngoma uelekeo kombania.
Basi alfajiri ikafika kila mtu kafunga kikombe chake kwenye pitshort sababu tuliambiwa kuna dharula hivyo kila mtu aende na kikombe kakifunga kwenye pitshort angani kutafungwa hivyo hakuna atakayeweza kuingia.

Kama kawaida mabio umbali kutoka Gongo la Mboto hadi Airport nilikua naenjoy mabio.

Tumerudi kushakucha! tukaambiwa tupange foleni kazi imeanza.

Nilijuta upya kwenda jeshi, Bakabaka wakaanza kurutaaaa fungua moyo kazi imeanza! wote kichurachura uelekeo huu hapa basi tunawafata kwa kichurachura huku wanatuonyesha maeneo ya jeshi kama nyumba zao, jikoni, utawala, mazingira yote. Vuta picha kambi za jeshi zilivyo kubwa sasa tunazunguka kwa kichurachura, mkichoka mnaroll.

Tukachukuliwa hadi kwenye bonde tukaambiwa aya lala chini roll mpaka darajani! Huwa nahisi kambi nyingi zina madaraja chini mteremko wa maji.

Tulikua kimafungu hivyo ni rahisi kusimamiwa na kila mtu anafanya kwa uangalizi mkubwa.
Wazee nikaanza kuroll mpaka darajani nilihisi dunia chungu, kilio sio cha nchi hii njia yenyewe ina kokoto, vumbi.

Tumefika darajani kuna mteremko wa maji yanapita njia bakabaka akasema aya tumbukieni humo ndani ya daraja, muoge sababu tokea mnekuja hamjaoga Sawa kuruti?? Tunaitikia "Ndio sawa afande"

Aisee tukatumbukia fasta sababu ukiremba cha moto utakiona
Wakatuambia hakikisha umejipakaza poda ya kutosha mwili mzima umekua mrembo ndo utoke (poda- vumbi, matope).

Sasa katika harakati za kujipaka matope kuna kitu kikanichimba gotini sijui mpaka leo ni nini damu zikaanza kumwagika kama zote goti linauma
Ikabidi wanitoe nikapelekwa zahanati kufungwa bandage hiyo siku ikawa ponea yangu
Ila wenzangu walisota sana.

Mchana sasa muda wa kula tukaambiwa kila mtu akachukue tofali kituoni dakika 5 uwe usharudi kuchukua msosi.
Mimi nina kidonda nikajua nitaonewa huruma kumbe holaa nikaenda kubeba tofali tunabeba kwenye kipara, wengine wakaeka ngata ya box!

Tulivyofika jikoni wakaanza kukagua walioeka ngata wakakusanywa wakapewa trip zingine wabebe matofali ndo wachukua msosi.
kuruta wengi tulikua tushafungua moyo, vilio malalamishi yalipungua sana.
Baada ya msosi kuruta wote uelekeo shambani hamna kupumzika.

Mjeda namesake akamfata bakabaka "Naomba mabinti wachache wakasafishe maeneo ya mkuu wa kambi
Basi na mimi nikachukuliwa ikawa ponea yangu, mkuu wa kambi alikua anaishi pale.

Jioni tukaenda kula after filimbi uelekeo kombania uwe umemaliza kula ama lah, nikaenda
Tukaanza kufundishwa kwata hapo usiku tunafundishwa zile nyepesi za mwanzo
Hapa nilipata mtihani mpya![emoji23] nilikua Nanga hatarii mkono siwezi kutupa ipasavyo usiku ule nilichezea mapanzi ya kutosha.

Kwanini wanaojitolea ni wakatili vileee?

Itaendelea.....
Hongera kwa story nzuri mtoto mzuri
 
SEHEMU YA 9
Tukaitwa kombania "Hongereni kwa kuweza kuvumilia wiki nzima bila kulala, hakika mmeiva kuruti. Ilitakiwa mkae wiki 6 bila kulala lakini tumewaonea huruma mtatufia wiki moja kwenu inatosha"

"Tii amri fungua moyo pandisha morali, jeshi ni zuri sana mlikuja mnalia ila sasa hivi mnafurahi na wiki hii ni ya kula utawala leo kwa mara ya kwanza tutawapa nafasi mkaoge, mfue nguo, mnyoe tutakutana na nyie baada ya chakula cha mchana"
Tulifurahi tukaenda angani kufanya kama tulivyoagizwa.

Nikiri jeshi kuna raha yake
Ratiba ilibadilika mateso yalipungua, kuna kazi haziepukiki kwenda shamba kung'oa visiki, kupukuchua mahindi, kubeba matofali, kubeba michanga, kumwagilizia bustani, kusafisha mazingira.

Ukiangalia ni kazi za kawaida na nzuri pia kama utafanya kwa moyo mmoja.

KUJIFUNZA KULENGA SHABAHA
Ratiba mpya ikaja baada ya chai tunaenda kombania kujifunza kulenga shabaha.
Wakati ule niliona kero na nilikua sisikilizi kwa makini nasinzia ila nilifanya jambo baya.

Somo lilikua zuri kwa waliokua makini aina za silaha, sehemu za silaha hapa nachokumbuka ni magazine kama sehemu ya kuhifadhia risasi, kitako cha bunduki na risasi zenyewe basi.
Sikumbuki kingine, Sinilijifanya Nanga acha nivune mabua.

Somo liliendelea mpaka wiki ikaisha ikabaki kwenda range kulenga shabaha.
Kumbuka mimi sikua nasikiliza darasani, hiyo siku tumeamka alfajiri kwenda huko range. Safari ilikua ndefu tunaenda kwa kukimbia ila sio kesi tukafika.

Tunasimama kimafungu kulenga shabaha wengi walikua nanga kama mimi hawakulenga lkn kufyatua risasi waliweza.

Zamu yangu ikafika nikalala chini service man akaniambia "vuta focus koki bunduki"
Nimeshika bunduki kukoki najua basi!? Nabung'aa macho

"Kuruta koki bunduki haraka"
"Afande nakoki haitaki" nikamjibu
"Wewe hujaiva! Si hivi nimeweza kukoki wewe unashindwa nini? Aya nishakoki fyatua risasi"

Nifyatue risasi! Nikavuta picha nikaona hichi kidude kinachocheza kwenye movie huwa wanakibinya... kumbuka kitako cha bunduki nimekiweka kwenye kwapa.
Basi nikakibinya! Weeee nilitoka ndukiii nalia...
Mimi nilijua ukipiga inakua kawaida tu kumbe nilivyofyatua bunduki ikanitetemesha mwili nikahisi kuzimia.

Nilichezea mabanzi! nikaambiwa naleta masihara ningejipiga risasi je?

Kuna kuruta alipewa zawadi alilenga shabaha 3 halafu anapiga risasi kwa ufasaha.

Ratiba tuliizoea kuamka alfajiri kurudi angani saa 6 usiku
Muda mwingine tukirudi tunajikuta tunapiga stori hadi kunakucha, wenyewe tunaamùa kukesha na kesho tunapiga mzigo fresh.

Nilipata wasaa wa kuongea na mama!
"Unaendeleaje"
Vizuri mama..
"Vipi bado unataka kurudi nyumbani"
Hapana! Nitakaa hadi nimalize course...
Akacheka sana.

Jeshi lilikua raha hadi wenzangu wakinikumbusha nilivyokua nalia najicheka.

Yule bakabaka mchumba ake namesake akiniona ananitania "Ephen naona umeiva!!"

Itaendelea.....

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
 
SEHEMU YA 9
Tukaitwa kombania "Hongereni kwa kuweza kuvumilia wiki nzima bila kulala, hakika mmeiva kuruti. Ilitakiwa mkae wiki 6 bila kulala lakini tumewaonea huruma mtatufia wiki moja kwenu inatosha"

"Tii amri fungua moyo pandisha morali, jeshi ni zuri sana mlikuja mnalia ila sasa hivi mnafurahi na wiki hii ni ya kula utawala leo kwa mara ya kwanza tutawapa nafasi mkaoge, mfue nguo, mnyoe tutakutana na nyie baada ya chakula cha mchana"
Tulifurahi tukaenda angani kufanya kama tulivyoagizwa.

Nikiri jeshi kuna raha yake😄
Ratiba ilibadilika mateso yalipungua, kuna kazi haziepukiki kwenda shamba kung'oa visiki, kupukuchua mahindi, kubeba matofali, kubeba michanga, kumwagilizia bustani, kusafisha mazingira.

Ukiangalia ni kazi za kawaida na nzuri pia kama utafanya kwa moyo mmoja.

KUJIFUNZA KULENGA SHABAHA
Ratiba mpya ikaja baada ya chai tunaenda kombania kujifunza kulenga shabaha.
Wakati ule niliona kero na nilikua sisikilizi kwa makini nasinzia ila nilifanya jambo baya.

Somo lilikua zuri kwa waliokua makini aina za silaha, sehemu za silaha hapa nachokumbuka ni magazine kama sehemu ya kuhifadhia risasi, kitako cha bunduki na risasi zenyewe basi.
Sikumbuki kingine, Sinilijifanya Nanga acha nivune mabua.

Somo liliendelea mpaka wiki ikaisha ikabaki kwenda range kulenga shabaha.
Kumbuka mimi sikua nasikiliza darasani, hiyo siku tumeamka alfajiri kwenda huko range. Safari ilikua ndefu tunaenda kwa kukimbia ila sio kesi tukafika.

Tunasimama kimafungu kulenga shabaha wengi walikua nanga kama mimi hawakulenga lkn kufyatua risasi waliweza.

Zamu yangu ikafika nikalala chini service man akaniambia "vuta focus koki bunduki"
Nimeshika bunduki kukoki najua basi!? Nabung'aa macho

"Kuruta koki bunduki haraka"
"Afande nakoki haitaki"😄 nikamjibu
"Wewe hujaiva! Si hivi nimeweza kukoki wewe unashindwa nini? Aya nishakoki fyatua risasi"

Nifyatue risasi! Nikavuta picha nikaona hichi kidude kinachocheza kwenye movie huwa wanakibinya... kumbuka kitako cha bunduki nimekiweka kwenye kwapa.
Basi nikakibinya! Weeee nilitoka ndukiii nalia...
Mimi nilijua ukipiga inakua kawaida tu kumbe nilivyofyatua bunduki ikanitetemesha mwili nikahisi kuzimia.

Nilichezea mabanzi! nikaambiwa naleta masihara ningejipiga risasi je?

Kuna kuruta alipewa zawadi alilenga shabaha 3 halafu anapiga risasi kwa ufasaha.

Ratiba tuliizoea kuamka alfajiri kurudi angani saa 6 usiku
Muda mwingine tukirudi tunajikuta tunapiga stori hadi kunakucha, wenyewe tunaamùa kukesha na kesho tunapiga mzigo fresh.

Nilipata wasaa wa kuongea na mama!
"Unaendeleaje"
Vizuri mama..
"Vipi bado unataka kurudi nyumbani"
Hapana! Nitakaa hadi nimalize course...
Akacheka sana.

Jeshi lilikua raha hadi wenzangu wakinikumbusha nilivyokua nalia najicheka.

Yule bakabaka mchumba ake namesake akiniona ananitania "Ephen naona umeiva!!"

Itaendelea.....
Ila naona kadri ulivtoenda rafiki yako ushamsahau kabisa au hakukuwa na jambo la maana kati yenu.

Nimeishia hapa nitarejea ukiendelea
 
SEHEMU YA 9
Tukaitwa kombania "Hongereni kwa kuweza kuvumilia wiki nzima bila kulala, hakika mmeiva kuruti. Ilitakiwa mkae wiki 6 bila kulala lakini tumewaonea huruma mtatufia wiki moja kwenu inatosha"

"Tii amri fungua moyo pandisha morali, jeshi ni zuri sana mlikuja mnalia ila sasa hivi mnafurahi na wiki hii ni ya kula utawala leo kwa mara ya kwanza tutawapa nafasi mkaoge, mfue nguo, mnyoe tutakutana na nyie baada ya chakula cha mchana"
Tulifurahi tukaenda angani kufanya kama tulivyoagizwa.

Nikiri jeshi kuna raha yake😄
Ratiba ilibadilika mateso yalipungua, kuna kazi haziepukiki kwenda shamba kung'oa visiki, kupukuchua mahindi, kubeba matofali, kubeba michanga, kumwagilizia bustani, kusafisha mazingira.

Ukiangalia ni kazi za kawaida na nzuri pia kama utafanya kwa moyo mmoja.

KUJIFUNZA KULENGA SHABAHA
Ratiba mpya ikaja baada ya chai tunaenda kombania kujifunza kulenga shabaha.
Wakati ule niliona kero na nilikua sisikilizi kwa makini nasinzia ila nilifanya jambo baya.

Somo lilikua zuri kwa waliokua makini aina za silaha, sehemu za silaha hapa nachokumbuka ni magazine kama sehemu ya kuhifadhia risasi, kitako cha bunduki na risasi zenyewe basi.
Sikumbuki kingine, Sinilijifanya Nanga acha nivune mabua.

Somo liliendelea mpaka wiki ikaisha ikabaki kwenda range kulenga shabaha.
Kumbuka mimi sikua nasikiliza darasani, hiyo siku tumeamka alfajiri kwenda huko range. Safari ilikua ndefu tunaenda kwa kukimbia ila sio kesi tukafika.

Tunasimama kimafungu kulenga shabaha wengi walikua nanga kama mimi hawakulenga lkn kufyatua risasi waliweza.

Zamu yangu ikafika nikalala chini service man akaniambia "vuta focus koki bunduki"
Nimeshika bunduki kukoki najua basi!? Nabung'aa macho

"Kuruta koki bunduki haraka"
"Afande nakoki haitaki"😄 nikamjibu
"Wewe hujaiva! Si hivi nimeweza kukoki wewe unashindwa nini? Aya nishakoki fyatua risasi"

Nifyatue risasi! Nikavuta picha nikaona hichi kidude kinachocheza kwenye movie huwa wanakibinya... kumbuka kitako cha bunduki nimekiweka kwenye kwapa.
Basi nikakibinya! Weeee nilitoka ndukiii nalia...
Mimi nilijua ukipiga inakua kawaida tu kumbe nilivyofyatua bunduki ikanitetemesha mwili nikahisi kuzimia.

Nilichezea mabanzi! nikaambiwa naleta masihara ningejipiga risasi je?

Kuna kuruta alipewa zawadi alilenga shabaha 3 halafu anapiga risasi kwa ufasaha.

Ratiba tuliizoea kuamka alfajiri kurudi angani saa 6 usiku
Muda mwingine tukirudi tunajikuta tunapiga stori hadi kunakucha, wenyewe tunaamùa kukesha na kesho tunapiga mzigo fresh.

Nilipata wasaa wa kuongea na mama!
"Unaendeleaje"
Vizuri mama..
"Vipi bado unataka kurudi nyumbani"
Hapana! Nitakaa hadi nimalize course...
Akacheka sana.

Jeshi lilikua raha hadi wenzangu wakinikumbusha nilivyokua nalia najicheka.

Yule bakabaka mchumba ake namesake akiniona ananitania "Ephen naona umeiva!!"

Itaendelea.....
karena
 
vipi umepangiwa kwa kuku...? jifunze kula mayai mabichi utakuja kunishukuru...🤣🤣🤣
Kule kwenye kuku nlikuwa naenda mara Moja Moja, ile mwanzoni nlizozana na serviceman Moja aisee nkapangwaga kwenye ujenzi uwanjani hlo tofali kulinyanyua😁siku kama hakuna ujenzi tunaenda kuangalia ruvu shooting wakifanya mazoezi
 
Back
Top Bottom