Vionjo vya Arsis - Majini ya Kojani- Pemba 1.
nilivyokutanishwa na majini ya Kingazija (Comoros) na Kipemba Kojani.
Baada ya kuongea na mshikjai nikampigia Babu. Baada ya kusalimiana.
Mimi; Babu umesikia kilichokuepo?
Babu; Kuhusu nini Simba nifahamishe.
Nikamuelez kama alivonambia Dokta.
Babu; Hilo nakifahamu, Sheikh...wa Unguja kanipigia jana, akanambia nikujulishe, nikaona saa hizi upo kazini, nilikua nangojabaada ya dhuhuri niku[igoie, Najua hua mnapumzika kidogo.
Mimi; kwa mwanao hapa kuna kupumzika, kama hujajiongeza mwenyewe, hata siku moja hasemi ka[pimzikeni.
Baba; Simba huyo, simba hawapumziki wawe wameshiba.
Mimi; Mwanao huyu saa zote ana njaa?
Babu: Muulize, mtajuana nae wenyewe, mbona mimi unanuliza?
Mimi; Mwanao huyu si unajua haongei ongei sana?
Babu; Simba, huyo achana nae wewe nenda ukapaone Pemba na Kojani ukaone huo mwaka koga wao wa Kojani, nasikia wanatoka dunia nzima siku hio, ha[patoshi. Kajonee huko, umekosa kuoa Unguja labda huko utapata, usinisahau lakini.
Mimi; Babu tunangea vitu serious wewe unaleta mambo ya kuoa?
Babu; hakuna itu seripous duniani kama kuoa, asikudanganye mtu, huyo wako mke ndagu, sasa tafuta asie ndugu. Pemba kuna mitotoya Kimanga huko, Wewe nenda tu babu...
Babu: Sikiliza Simba, wewe ukiweza leo hii nenda kwa Mzee Ali ukamsikilize, maana kishaambiwa bila wewe Dokta haendi, nenda ukamuone, kisha leo usiku nambie. Tena usimpigoie simu kama unakwenda, wewe mstukize tu. Si ulinambia pete uliitumia kujificha kwa mara ya kwanza Unguja?
Mimi; Ndio babu.
Babu; Sasa leo nenda kwake kama ulivyoingia kwa Bi S. Unguja akustukize upo ndani. Haya kwaheri Simba, usiache kwenda.
Akakata simu, nikawa nafanya kazi zangu lakini sina raha kabisa, baada ya kusa alasiri tu nikwamuaga Mzee.
Mzee; Babu yako kakwambia nini, umeongea nae?
Nikamweleza Mzee yote.
Mzee; Sawa, wewe nedna mradi babu yako kakwambia hivyo usitie shaka, na mimi nikitika hapa 11 nakuja huko moja kwa moja, Wewe fanaya mambo yako lakini usiningoje mimi.
Mimi; Nikatoka nikaomba dua ya safari nikaanza.
Njiani nikawa nafikiria ntaiweka wapi gari pale na parking mpaka lifunguliwe geti, likanijia wazo, kuna Kituo cha mafuta pale Buguruni naweza kuweka gari, kuna jamaa fundi pale, gari zake zote hizi za za kisasa tunamtengenezea kwetu.
Kufika, kweli nikamkuta, nikamwambia mimi naingia Buguruni pale nikamwelekeza hakuna parking mtaa ule, akanambia mitaa nuksi kweli ile chukua boda mwanagu, wacha gari yako hapa au nikupe pikipiki utaendesha mwenyewe? Nikamwambia hapana boda tu anatosha.
Nikaenda na boda mpaka karibu ya kufika nikamwambia hapahapa, nimefika. Ngapi mshikaji? Akanambia fundi pale kanambia nisichukue pesa kwako, nikampa buku mbili, nikamwabia basi hii kunywa soda mwanangu. Akanambia hapa Buku tu. Nikamwabia ubani wako huo mwana, usiwe na shaka. Akaondoka zake.
Kufika nyumba moja kabla ya Mzee Ali sikutazama hata kama kuna watu au hakuna, nikaigeuza pete nikaiminya, nikaingilia mlango wa uani kama tulivyoingizwa siku ile noikauta kina mama na kina dada wamekaa hawana habari kabisa, nikaenda moja kwa moja chumba chake cha kutibu watu, kuna watu wa pale pale kwake walikua wamekaa nje mlangoni kama kawaida.
Nikakaa kama dakika tatu nikaona hakuna anaekuja, nikatoka nikatazama tazama uani, wapo watu na shughuli zao kama mwanzo, hakuna hata anaeniona. Nikaingia mlango wa uani wa kuingilia nyumba kubwa, nikasikia Mzee Ali anaongea na mtu zaidi ya mmoja lakini kwenye chumba sio kule ukumbini kwake.
Nikatime mlango nikaona umefungwa, nikiufungua itakua noma.
Nikaenda ukumbini kwake nikakaa peke yangu mara nikasikia mlango umefunguliwa nikasoge wakawa wanatoka ndani, kumbe walikua watu watatu na yeye Mzee Ali, wawili wanaume mmoja mwanamke.
Mzee Ali; Sasa wewe mama na mumeo subirini kule ukumbini tulipokaa kwanza mke wangu lazima akupe nguo za mapambano mupe kama nusu saa mjje. Mimi na huyu bwana tunakwenda, kazi yake huyu ndogo tu. Nikawapita nikaenda chumba chake cha uganga nikawapita wale qa mlangoni, hakuna alieniona wala kustuka kabisa, nikaingia ndani nikakaa nikaiachia pete. Nikamsikia mzee Ali uwani anampa maelekezo mkewe kuhusu yule mwanamke na huku chumbani kwake aletewe ndoo za maji.
Nilikua nimekaa kiti anachokaa yeye, sijui kwanini niliamua hivyo. Cha ajabu nilikua sina uoga wala kuwaza matokeo ya kitendo changu. Mara namsikia mzee Ali mlangoni anamkaribisha mgeni wake karibu bwana karibu.
Akatangulia Mzee Ali kuingia hakuniona au hakutengenmea sielewi, ghafla aageukia mlangoni, karibu, karibu bwana yule mgeni alioingi tu macho yake na yangu, akapiga Salamu alekum, nikaitika Alekum Salam, na mzee Ali ndio anageuka ananiona, nikamuona kama kanitole macho, mdomo kawacha wazi, akapiga kelele kama yowe hivi halafu akaruka juu mara ya kwanza, karuka mara ya pili akapiga samasolti kwa mbele, mpaka nikashangaa, mtu mzima na ana mwili kidogo lakini kapiga samasalti, alipofikia akakaa chini, akatoa macho, akaanza kutazama chumba kizima akawa kama kapigwa ganzi, yule jamaa aliekuja naenkasimama karibu ya ukuta macho na kijasho chembembamba kina mtoka, hajui kinachoendelea.
Mzee Ali; Salaam, salaam salaam. Nimekuja kwa amani, nilikua nategemea utakuja lakini sio kimya kimya. Akamgeukia mgeni wake, kaa chini, huyu mhgeni wangu pia.
Mgeni; Au niwapishe?
Mimi; Kaa chini, hakuna siri inayotoka nje ya chumba hiki.
Mzee Ali; kaa bwana kaa.
Nakajua alikuwa sio yeye kwanza anaepiga samasamasolti, sasa ni yeye anaongea.
Mzee Ali; Bwan Simba, hali yako bwana?
Mimi; Sisi salama, wewe tu?
Mzee Ali; Nyie watotohapoo nje, hebu njooni haraka.
Hosi hodi. Mzee Ali piteni, ile kuingia tu.
Mzee Ali; kwanini anakuja mgeni hamnambii mnamkaribisha humu ndani peke yake?
Mabinti: Hakuna megni aliyekuja Baba.
Mimi; Mzee Ali, hawakuniona hao, hii habari yetu haiwahusu hao, waache wakafanye yao.
Mzee Ali; haya nendeni. Bwana Simba mbina umenistuwa, leo mpaka kaja mwenyewe hapa. Habari kubwa hii. Haya nambie bwana Simba.
Mimi: Mzee Ali unasema ulikua uanjua kua nitakuja, haya nambie wewe.
Mzee Ali; Bwana mgeni tafadhali katungoje pale ukumbini tuna mazungumzo ya faragha kidogo na bwana Simba hapa. Samahani sana.
Nikaona yule mgeni kama kashukuru kutoka nje. Akatoka nje.
Mzzee Ali alikua kasimama.
Mzee Ali; Nikae chini mkuu?
Mimi; kaa tu, usiwe na hofu, wala usiwalumu wanao au yeyote yule hakuna alieniona nikiingia, mimi nilikua na nyinyi toka kule mlipokaa na wale wengine, si umewaambia atakwenda mkeo kumpa yule dada nguo za mampano? Nakueleza hayo ili ujue kua nilikua na nyinyi. Sasa sema ukweli wako, uwe ukweli mtupu.
Mzee Ali; kama kashikwa kigugumizi cha mbali, Sikiliza Simba, mimi niliambiwa utakuja lakini sikujua kama utakuja ghafla hivi, nilijua utakuja Dokta akiwepo hapa ili tuongee na wewe habari ya safari.
Mimi: Ongea yote, Mzee Aliaua nikuulize ujibu maswali?
Mzee SAli; Itakua vozuri maana sijui yepi ya kuongea yepi sio ya kuongea.
Mimi: Hii safari ilikua ya Dokta tu, kwanini sasa iwe na yangu?
Mzee Ali; Nilipata maelekezo kwa huyu Mkuu aliekuja hapa sasa hivi, hakukaa lakini kaondoka haraka, kanambia niyamalize haraka na niseme ukweli mtupu, kama ulivyonambia wewe.
Mimi; Nataka kujua kama nilivyokuuliza, tafadhali kila unavyochelewa unazidi kuwachelewesha wageni zako.
Mzee Ali; Mimi ndio mkubwa wa shughuli inayofanyika nyumbani, ilikua niende na dokta poeke yake, lakini nimeletewa habari kua kuna watu wetu aliokua nao Dokta tunamtazama hali yake, wameshikwa wote na hakuna njia ya kuwawachiwa walioshikwa mpaka tukamuombe msamaha mbele ya wakubwa kojani na wewe tukuombe usaidie ili watu wetu wapoatikane.
Mimi; Wangaoi watu wenu?
Walioshikwa ni site lakini na wanaopokezana nao kumi na mbili nao hawajashikwa wapo nyumbani lakini wamezuliwa kufanya kazi yoyote si kwa Dokta si kwengine. Wakubwa wakajua kwanza ni Vibuki, vibuki sisi tunaviweza, lakini imeonekana hii nguvu kubwa inatokea kwako na haiwezekani kuwakatali, tutasambaratishwa Kojani nzima. Huo ndio ujumbe nilioletewa, kwa hio ilikua ukija nikuombe twende wote Kpojani.
Mimi; Bado hujasema ukweli, wakubw azako wamekwambia uniombe mimi twende kojani?
Mzee Ali; Hapoana Bwana Simba, hilo nasema mimi, wao wamenambia utakuwepo Kojani nikukaribishe kwa salama na amani na wamenambia ukija hapa nikukaribishw kwa salama na amani.
Mimi; Sasa kwanini wewe umetaka nifatane na wewe Kojani?
Mzee Ali; Nimewaz hio ndio itakuwa wepesi maana nimesisitizwa asikose Dokta kwenda, hivi kabla ya hao wageni kuja nilikua naongea Dokta namsisitiza kuja, lakini Sheikh kamwambia asije huku kwangu bila wewe, ndio nikajua mtakuja niwaombe twende sote.
Mzee Ali; Wanataka ukaombe msamaha wa nini kwa Dokgta huko Kojani?
Mzee Ali; Yamenikuta, hayasemeki lakini nabidi niyatapike.
Mimi: kama unavyotapisha kiuongo? Hapa ukisema uongo Dokta haji na unajua ndio utakua mwisho wako wa kukaa Dar?
Mzee Ali: Simba, nisamehe sana, ngoja nikwambi ukweli Mkuu. Mimi natafuta rizki tu, yale mambo ya kuwatapisha watu ni kujongezea kipato tu.
Mimi; Sikukuuliza hayo yote, jibu nililokuuliza, nilikupa fursa ya kuongea mwenyewe ukawa huongei, sasa nakwambia, kama hujajibu swali ninalokuuliza, urafiki wetu unaishia hapa na ujua hato jini yeyote kukusaidia utapeli wako, na wala hakua takaepandisha jini hapa kwako.
Mee Ali; Hilo nimeliona, hata yule mwanamke ilikua apandishe hukohuko tulikokua nae nikaona ajabu leo hajapandisha, ndio nikasema nimuhamishie huku.
Mimi: kama hujajibu swali, hatopandisha na utakua huna ujanja, si unaona hata huyo mkuu wenu kaja kakimbia kuniona mimi hapa?
Mzee Ali; Nisamehe, naanza kukujibu. Mi nilikua nakwenda kumuomba msamaha kwa uongoniliomfanyia. Na nimemrishewa nipiga hesabu ya pesa zote nilizochukua akarudishiwe mbele ya wakuu huko na wewe niliambiwa utakuwepo huko, nikuobe msamaha pia kwa kufanay uongo mbele yako na babako.
Mimi; Kwanini unamtaka Dokta aje hapa?
Mzee Ali; Ili nihakikishe anakuja Kojani, tukawatoe hai wanaonisaidia kazi niwarudishe kwao nipewe wengine.
Mimi; Kwanini hujawarudisha hapa ulipompachika nao?
Mzee Ali; Imeshindikana bwana Simba, mpoakawakubwa wamejaribu kuwarudisha kule imeshindaka, hata hawaonekani kabis, hatujui walipo lakini tunajua nguvu sako ndio zimewazuia.
Mimi; Nani kakwambia hivyo?
Mzee Ali; Huyu aliekuja akaondoka hapa, na yeye anaambiwa na wakubwa ake.
Mimi; Mwambia aje.
Mzee Ali; Huyu bwana akija anapirika nyingi sana, si umeona alivyokuja kwanza?
Mimi; Usiogope, mwambie aje, au nimwambie mimi?
Nikamngoja kama dakika tatu.
mzee Ali; Namwabia lakinihaji kabisa, sio kawaida yake. hua nikimwita tu anakuja, hachukui hata nusu dakika.
Mimi; haya tulia, mimi nimeshamwita anakuja, na hafanyi fujo yoyote leo.
Mzee kama akatingishika kidogo tu.
Mzee Ali Salaam, Salaam Salaam, nimekuja mkuu kama ulivyoniita niko chini ya amri yako.
Mimi; Anakusikia huyu?
Mzee Ali; Ndiyo ananisikia.
Mimi: Haya mwambie kinachoendelea na nini kinatakiwa kifanyike haraka sana, au wewe na yeye unajua kitakachowapata. Ilikua kama sauti ya Jini 2 inanambia niseme nini.
Mzee Ali; Sikiliza kiti, huyu Simba ni mkubwa wa wakubwa zetu sisi na wote wanamuheshimu sana na hawataki hata kuwaza vita na ukoo wake na marafiki zake. Kw ahio Ali, umkatie tiketi ya ndege huyu na Daktari ya kwenda na kurudi Pemba, wiku moja kabla ys shughuli kubwa na siku moja baada ya shughuli kubwa, bila hivyo itakua fedheha kubwa Kojani, sherhr haitofanyika kabisa.
Mpigie yule mteja wako anafanyua kiwanja ya ndeh)ge, anajua namna ya kutaka tiketi na namna atavyowapa hawa. Wewe kama utamlipa yule au humlipi mtajuana nae yule. Hii haina mjadala. Wamesema wnajua wenyewe pakufikia na wanajua wenyewe watfika vipi Kojani, wewe wape tiketi zao tu leo hii, zowe na tarehe ya kwenda na kuondoka, ukikosea shauri lako.
Mzee Ali; Kunalingine Mkuu Simba?
Mimi' Ndio, nataka heshima na adabau kuanzia leo, wewe na wakubwa zako na huyu mjinga wenu mfahamisheni. Akikuita tena uje kama kawaida yako usichelewe. Mengine, sisis gtunajua tuongee vipi na wakubwa zako bila kupitia kwa huyu mwizi mwenzako.
Mzee Ali; Nimekuelewa mkuu, naomba niondoke.
Mimi ; Haya kwaheri.
Hakuna cha samasolti wala nini.
Mzee Ali; Samahani Simba, naomba niagize naji a kunywa.
Mimi; Agiza, harakanataka kuondoka.
Mzee Ali; Nyiiie Mabinti leyteni maji chupa mbili haraka.
Mabingti wakaleta maji Mzed Ali wakanywa na mimi nikafungua nikanywa, kuonesha ustaarabu. Mzee akayagida chupa nzima.
Mzee Ali; Nashukuru yameisha salama, Sasa bwana simba kwanza naanza kukuomba msmaha hapahapa mradi mmeongea na hawa wakuu, mimi nikutimiza tu, sasa hizi napigia simu yule binti afanye tiketi, naoimba nimpe namba yako akitaka majina au maelezo mengine. Wewe mpe maelezo yote, leo huyajui majina ta Dokta? yake nayajua yote mpaka la mamake. Yako bwana Simba ndio sina. Nikamwabia haya andika jina langu kamili, Wee binti njoo uandike haraka, akaja binti mmoja mkubwa mkubwa hivi Haya andik, nikampa tena majina, yule binti akawa anayaandika kwenye simu yake.
Mimi; Haya mimi naondoka akiwa gtayari na tiketi ndio anijulishe, leo hii hii baada ya lisaa limoja asinitafute kabla.
Mzee Ali; Sawa bwana Simba, ahsante sana tutawasiliana.
Mimi; Usiwasiliane na mimi wala Dokta kuanzia leo, wasiliana na yule mwizi mmwenzio, nimeshamwambi aje ukimwita. Huamini?
Mzee Ali; hapana, Bwana Simba nimesema kimazowea tu.
Nikanyayuka huyo nikatoka, nikajua wambea walikua wansikiliza mlangoni, na mkewe kakaa nao. Nikatoa Salaam nikaitikiwa na wote mbio mbio. Nikatoka langi uani, kutoka tu nje nikatazama kushoto nikaona Gari ya Mzee, nikawa sina haja ya kuminya pete nikaifata gari, nikaona yupo ndani na mshikaji.
Majini ya Kojani, Pemba 2
Majini ya Kojani, Pemba 3
Majini ya Kojani, Pemba 4
Majini ya Kojani, Pemba 5
Majini ya Kojani, Pemba 6
Majini ya Kojani, Pemba 7
Majini ya Kojani, Pemba 8
Majini ya Kojani, Pemba 9
Majini ya Kojani, Pemba 10
Majini ya Kojani, Pemba 11
Majini ya Kojani, Pemba 12