Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani unaweza kusema walituvua nguo kabisaTukumbuke kwamba Tanzania wana historia nayo mbaya katika masuala ya ugaidi. Ubalozi wao ulishawahi kukumbwa na tukio.
Kituko zaidi walikiona watumishi wa airport kule, kwani wao waligeuzwa kuwa kama abiria tu, shughuli zote walihodhi USA, hadi uwanja wa jeshi ulikuwa chini yao. Chochote walichokiona ni tishio kiliondolewa hata kama kilikuwa kwenye eneo la jeshi, Ile miti ilipunguzwa matawi yaani wakazi wa eneo lile hakuna rangi walikosa kuiona.
Marais wa africa walipakizwa kwenye basi kwenye msiba wa malkia,Maraisi wa African wakienda huko hamna lolote linalotokea. Mimi nakumbuka nilikua mataa ya mwenge natokea mikocheni, halafu tumbo linakata balaa huku gari haziendi. Sitasahau ile siku 🤨
Labda jamaa walipuliza hewa ya kufubaza ubongokuna wanafunzi wa azania walikuepo kwenye kumpokea obama
alikuwepo uncle wangu hapo.. aliniambia hivi
uncle alipokuwa akitusogelea obama kutupungia mkono wanafunzi wote tulihisi kama mazonge hivi,
kama wamekula madawa kiasi kwamba huwezi fanya chochote kupiga kelele wala sijui kama unataka kuleta fujo
aliniambia alizani ni yeye tu sasa kwenye kushare na wanae wakamwambia sisi pia tulijisikia hivyo hivyo
mpaka leo nashindwa kuelewa ilikuwa ni issue gani hapo
Ile mvua, shikamoo …(…..)Niliyoyashuhudia ziara ya Rais Obama 2013 sitayasahau.
Kwa mara ya kwanza nilishuhudia barabara za jiji la Dar zikipigwa deki.
Siku Obama anatua jijini ilikuwa kama siku ya kiyama, mji ulisimama, nakumbuka tulikuwa tunaenda kulipa mahari ya rafiki yetu maeneo ya Msasani, tulitumia masaa kama nane kutoka Tabata mpaka Msasani, kufika ukweni saa nne usiku.
B
aba mkwe akasema wajinga ninyi wapare mna dharau rudini hatupokei mahari yenu, tukamuelewesha akatuelewa, mahari ikapokelewa.
Miezi miwili kabla Hotel ya Kilimanjaro ilishafanyiwa booking hakuna mtu aliruhusiwa kuingia, watumishi wote wakifanyiwa vetting upya, wengine walipewa likizo fupi mpaka Obama alivyoondoka.
Ikulu yetu haikubaki salama ikafanyiwa scanning sitazielezea kulinda heshima ya nchi ila kituko kimoja sitakisahau.
Kuna press conference iliandaliwa nje ya viwanja vya Ikulu ambapo Rais Kikwete na mgeni wake wangeongea na waandishi.
Ikulu ikatoa ratiba ya muda wa hiyo press, na ofisa wa Obama wakaichana chana wakisema muda huo si rafiki maana kutakuwa na mvua viunga vya Ikulu wakaomba ratiba isogezwe mbele masaa mawili.
Mzungu ni hatari muda uleule uliokuwa umepangwa na maofisa wa Ikulu lilitanda wingu mvua ikapiga kwa muda wa lisaa limoja na nusu, ilikatika nusu saa kabla ya muda waliopendekeza wasaidizi wa Rais Obama, kumbe mvua walishaiona kitambo kwenye mitambo yao.
Wewe ungekuwa baba mkwe ungefanyaje watu wameambiwa wafike saa kumi jioni wakafika saa nne usiku na mmeshaoika misosi,mitandao ya simu yote imefungwa,hakuna simu inaingia waka kutokaMkuu unataka tukubali hata hilo la baba mkwe kukataa mahari? Hatukuwepo
Pamoja na yote hayo kufanyika, hakuna kiongozi aliyehoji hali hiyo kutokea, kisababishi pamoja na impact yake.Yaani unaweza kusema walituvua nguo kabisa
Hii kali aiseeMzungu ni hatari muda uleule uliokuwa umepangwa na maofisa wa Ikulu lilitanda wingu mvua ikapiga kwa muda wa lisaa limoja na nusu, ilikatika nusu saa kabla ya muda waliopendekeza wasaidizi wa Rais Obama, kumbe mvua walishaiona kitambo kwenye mitambo yao.
Teh teh 😃 😃 😃 dah!...maisha haya..nakumbuka kuna mtu fulani mchizi alikuwa analala chini ya daraja la reli karibu pale majani ya Chai, kuingia barabara ilipokuwa zamani Tigo makao makuu.. Sasa kumbe FBI washamfuatilia yule msela zaidi ya mwezi, anaenda kariokoo anachukua mabox matupu anakuja anatandika hapo analala chini ya kidaraja fulani kilikuwa pale...Jamaa wanazoom kama mwezi hivi, wakajua hana issue.. Basi ilivyokaribia ujio wa Obama, FBI wakawambia polisi wetu, kuna mtu analala pale kwenye daraja.. Tumemchunguza hana madhara, ila kamtoeni pale ... Polisi, unavyojua walimshukia kama mwewe, hinginja hingija, tupa kule, mtama , tanganyika jeshi.... Wale FBI wanawashangaa hawa polisi, wakawambia huyo hana madhara ...
Yaani hiyo kitu ilikuwa hatari tupu..
Haiwezekani!Hawakwenda na misafara(caravans)yao wawakoge wazungu?Marais wa africa walipakizwa kwenye basi kwenye msiba wa malkia,
Dah!Ila waliwa-degrade sana.InshaAllah!Na wao tutawalipizia tu.Yaani umkonge mzungu na magari wakati kayatengeneza yeye,kaa huko kwenye kimbinyiko bus express
Mkuu mbona unataka kulisahau tukio la karibuni sana hilo?Haiwezekani!Hawakwenda na misafara(caravans)yao wawakoge wazungu?
Usiogope mkuu.Uchokozi upo kwenye DNA yangu mkuu.Mkuu mbona unataka kulisahau tukio la karibuni sana hilo?
JENGO ZIMA la Quality Center tuliambiwa tukasimame barabarani tushangilie gari za msafara wa Obama zikiwa zinapita kutoka Airport🤣🤣🤣
Thubutu!! Ile kauli ya "wasitupangie" huoni inavyotupa hekaheka. Mara urusi mara wapi huko ilimradi tafrani pakushikaDah!Ila waliwa-degrade sana.InshaAllah!Na wao tutawalipizia tu.
Walidhngiwa uwanja wa mkapa kwa siku mbili😀😀Hakuna watu niliwaonea huruma kama mateja, siku 2 kabla wote walishikwa sijui hata walipelekwa wapi mpaka siku Obama anaondoka wakaja tena kumwagwa barabarani