Nimeacha kudharau wanaosoma vyuo tofauti na UDSM

Kama mi nilivyofurahi??? Kwa sababu nilisoma diploma Muccobs enzi zile! Ila mambo yananiendeaje kazini!! Malizeni Vyuo mje mtaani vijana! Tulioko makazini hatuachi kazi ng'oo labda tufe! Teh teh

ebola ipo njiani! Angalizo tu kwa mfano vile...utang'atuka tu hata kama we binti kiziwi et
 
Wewe mtoto ungekuwa na akili ungekuwa ukikesha unaomba bodi wakupe mkopo.

Maana inaonekana unaotaka kila siku kwenda chuo.

Hahahaha ona sasa ulivyo punguani, nimeshakwambia acha kufikiri kwa kutumia saburi, unaongozwa kwa hisia sana inabidi ujihadhari kwani ipo siku utajikuta unamwambia mama yako naye akaombe mkopo HESLB.kwi kwi kwi kwi

CC Kamanda MpingaUKAWA njoo uone jinga huku linavyokurupuka eti mkopo hahaha
 
Last edited by a moderator:
ebola ipo njiani! Angalizo tu kwa mfano vile...utang'atuka tu hata kama we binti kiziwi et

Hahaah nimekuelewa mkuu, mtaani pagumu nilipo pata kazi nilivaaje ID ya kazini! Hahaah hadi restaurant siku moja thread moja ya wavaa vitambulisho ilinitachije? Sema nishaga acha!
 

Don't take real member wa JF aisee!
 
Last edited by a moderator:
Hahaah nimekuelewa mkuu, mtaani pagumu nilipo pata kazi nilivaaje ID ya kazini! Hahaah hadi restaurant siku moja thread moja ya wavaa vitambulisho ilinitachije? Sema nishaga acha!
Unatembea na vitambulisho mpaka kwenye restaurant haha unatuaibisha wasomi
 
jina la chuo halikupi ajira bali jitihada zako ktk kile unachokisoma
how competent you are? +gpa nzuri! ndo mpango mtaa
 
Kwani huwez kudanganya juu ya hili?tutaamini vipi kua ni kweli hakuna wa UDSM?

ofisini kuna taarifa za kila staff za elimu yaan level ya elimu yake, kozi na chuo alichosoma na mwaka aliomaliza.
 
Meanwhile bakhresa....LA SABA DROP OUT!
 
Nshawahi kusema ukiona mtu anavimba kichwa kisa chuo fulani jua ni mburura.Chuo ni wewe mwenyewe,mimi nimesoma ualimu Udom na nimepiga interview za tume ya ajira na nkapata job nafundisha Kibaha girls hapa Shirika la Elimu Kibaha.

Na interview tulofaulu wapo mchanganyiko wa udom.udsm.mum.suz.sua n.k.Nikimaanisha uone sasa kwenye field ya kazi waajiri hawaangalii eti chuo fulani bali wewe upoje kiuwezo.

Kupanga ni kuchagua wewe kula bata kisa upo udsm.ardhi.sua.udom.nk then kichwa kirudi kitupu uone kama kazini utapewa kwa jina la chuo.Maana hata ajira za moja kwa moja kama ualimu mkishakuja ingawa hakuna usaili mashuleni tunawaona hadi lesson plan kuandaa shida.
Mimi juzi nimewapokea wa field na wapo ambao ni majanga na wengine safi na sijaona eti chuo fulani wapo sawa zaidi ya wengine.
Sasa nyie kalia sifa za vyuo wenzenu na udom zetu tupo mashirika ya umma tunapiga PTSS 11,
 
Tatizo watoto wa udsm mnajikuta nyie ndio wasomi apa bongo.mim nasoma Ruco law nilifanya fild advocate's chamber 1 apa mjin na mwanafunz wa udsm hamna kitu procedures kibao hajui.then uki muelekeza analeta dharau
 

Ninachojua ww ulieandika huu uzi siyo mwana udsm ingawa umejaribu kueleza kama mwana udsm,lakini hukuwahi kujiuliza kwann udsm ni chuo cha Tanganyika!
 

kijana itabidi ujitume zaidi. Hiyo PTSS 11 ni ya kununulia nyanya chungu. Kama unahitaji kujenga nyumba, kusomesha watoto n.k, basi unatakiwa uanzishe biashara au uachane na hiyo kazi yako na utafute ajira nyingine inayolipa zaidi.
 

Perry, ulisifika kwa kua mtetezi wa UDSM hapo zamani, lakini leo umesaliti. Nawasiwasi na uwepo wako pale UDSM, huenda umedisco ndio maana umeamua kuanzisha chuki ndogondogo.
Pamoja na kuonyesha chuki kwa MLEZI, ila umeongea mambo mazuri sana. Jamii inakushukuru kwa mawazo yako mazuri kwa vijana wetu, kua wasiende chuo fulani kwa kufuata jina la chuo, bali wafuate ubora wa kile wanachokifuata. Niushauri mzuri kwa vijana wakiufuata!
 
Hata wanaoponda wenzao waliosoma vyuo tofauti na wao bila kujua walikua na div ngapi, nao ma.punga tu.
 
Jadilini mambo ya kitaaluma tutapima uwezo wenu. Hapa mwaonyesha udhaifu tu wa mtiririko wa ujinga. Tafuteni dhana, theme nk mtoe ushauri kitaaluma. Hoja zs kusoma chuo fulan ni porojo za time wasters.
 
kijana itabidi ujitume zaidi. Hiyo PTSS 11 ni ya kununulia nyanya chungu. Kama unahitaji kujenga nyumba, kusomesha watoto n.k, basi unatakiwa uanzishe biashara au uachane na hiyo kazi yako na utafute ajira nyingine inayolipa zaidi.

Ndo walewale wa wanaosujudia vyuo na ni wazi bado upo chuo na unavimbishwa kichwa kwa kozi unayosoma.Mimi sibishani na Mulugo product.Mtu anayejua mishahara ya mashirika ya umma na Tanzania ilivyo hawezi kuandika upuuzi kama huu,isitoshe mada haijahusu mishahara mikubwa au midogo.
 

Perry ushauri wako mzuri hasa mzuri hasa hapo kwenye Tabia ya watu kukimbilia tu kozi Fulani ili a some UDSM....but angalizo fulani, chuo kama UDSM ki ukweli kipo more organized hasa jinsi ya taaluma yao wanavyoitoa pia facilities zao ni kubwa which means kwa mwanafunzi anayejielewa,upataji wake wa elimu hasa kwenye kozi ambazo bahati mbaya wewe hujazigusia kama engineering ina-matter.
Mfano mwingine ni kwamba, hivi Vyuo vi kubwa,kwanza walimu wengi wana elimu ya juu (ma-dokta na maprofesa) na vina network kubwa hasa globally issue za scholarship za exchange studies au kujishirijisha na organization mbali mbali za kimataifa wamepiga hatua,mimi binafsi ni shuhuda wa hilo hasa baada ya kuja kusoma nje ya nchi. Ila ukweli utabaki pale pale, jitihada binafsi zinahusika sana,uwe bcom au engineering....
 
si amekiri kosa..na yeye amegundua kua jina la chuo sio inshu..
 
Teacher wetu wa economics always anawaambia wanafunzi waandike UDSM kwenye madaftari yao ili wasome kwa bidii kufikia chuo hiko....Kila akifundisha aishi kuongelea UDSM...mara viongozi wote wa taifa utaonana nao UDSM...mara wanafunzi walioongoza kitaifa utawakuta UDSM...mara watunzi wa vitabu kama akina ambilikile nilikua naonana nao UDSM...anadai wakati yeye anasoma madaftari yote aliandika UDSM ili afike huko....
Basi mpaka watu wamembatiza hilo Jina....nilipomfatilia vizuri kumbe amesomea chekechea mpaka form six mikoani..sasa alikua bado ana ushamba wa magorofa na kuiona dar..ndivyo ilivyo kwa wengi wanaodharau vyuo vingine...kila mtu na malengo yake..mimi nasoma advance nikijua nitaingia ARDHI au SUA basiiiii...
 
jina la chuo halikupi ajira bali jitihada zako ktk kile unachokisoma
how competent you are? +gpa nzuri! ndo mpango mtaa

usiamin sana katika GPA,akili za darasana ni tofaut na za mtaani(angalizo) tu mdau
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…