Nimeacha Rasmi Kutazama Mechi za Yanga NBC PL

Nimeacha Rasmi Kutazama Mechi za Yanga NBC PL

Best Daddy

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2019
Posts
950
Reaction score
1,672
Happy Holiday! Natumaini mnaendelea vizuri wana-Jamiiforums. Msukumo wa kuandika andiko hili umetokana kuangalia mechi tatu, pale ambapo Yanga amekutana na Mashujaa, Tanzania Prisons na hii mechi yake ya mwisho dhidi ya Dodoma Jiji.

Nimekua shabiki kindaki ndaki wa mpira wa Tanzania, nimeudhuria mechi nyingi sana hasa za Yanga katika msimu uliopita. Nimefurahi sana kwa wakati ule, lakini wakati naandika andiko hili nikiri kusema sitakuja kutazama tena mechi za Yanga isipokuwa zile mechi za kimataifa, au watakapo kutana Yanga vs Simba/Azam.

Kupitia mechi hizo hapo juu, sijui niseme ni uwezo mkubwa wa Yanga, au uwezo mdogo wa timu pinzani au kuna sababu nje ya uwanja au vyote kwa pamoja . Ila hizo mechi zilikua kama futuhi, ni maigizo yaani ni kichekesho. Kuna wakati unajiuliza inakuwaje hizi timu zinashiriki ligi kuu. Wachezaji wa timu pinzani wanashindana kufanya makosa, wachezaji wanashindana kutoa zawadi, labda kwa kuwa ni msimu wa Christmas.

Sizungumzi haya sababu za kuwa Yanga hapaswi kushinda, Hapana. Ila nazungumzia ushindani umepotea kabisa. Tofauti na miaka ya nyuma. Hizi mechi zote tajwa Yanga ameshinda sio sababu ya ubora wake, ila sababu ya udhaifu wa mpinzani. Ni ushindi mwepesi sana.

Mechi zote Yanga angekua makini hata kidogo tu, alikuwa na uwezo wa kupata hata magoli zaidi ya 10 maana ilikuwa ni washindwe wao tu. Hapo hapo ukitazama timu hizo tajwa zinapokutana na vilabu vya Simba na Azam basi ushindani unakua ni mkubwa sana.

Kuokoa soka letu, tulitazame hili kwa undani, tupate tatuzi za kinadharia na kivitendo ndani na nje ya uwanja. Either kuna baadhi ya vilabu vina influence katika timu hizi ndogo au gap kati ya Yanga na hivi vilabu vingine ni kubwa sana kusema kwamba inawathiri wachezaji kisaikolojia hata kabla hawajakutana nao.

Natambua kuwa tuna tamani vilabu vyetu vishinde kwa namna yeyote, lakini katika hili haihitaji uwe shabiki wa Yanga au Simba au hata mpira kuliona hili. Athari yake ni kuwa hii ligi itaenda kuwa dhaifu au kwa lugha ya kisoka kujulikana kama Farmers League.

Mdau wa soka mtazamo wako ni upi?
 
Unapataje mashaka na Yanga iliyo na quality kuzidi timu zote kwenye ligi
Yanga ni bingwa mara ya 3 mfululizo
Yanga amecheza final ya mashindano ya CAF
Yanga amecheza robo final na Mamelod
Yanga yupo CAFCL
Yanga amemfunga Simba mara nne mfululizo
Ni mwehu tu atapata mashaka juu ya ushindi wa Yanga
 
Kwangu ni tofauti, timu yoyote inastahili kushindwa katika ushindani wowote ila kwa njia ya halali
Ila Uto wakizulumiwa goli ule ustahili unakuwa stahili zaidi ya ustahili. Hahaha. Na wanajua kulia hao.
 
yaani upate mashaka na mechi za yanga uache kupata mashaka na mechi za simba

sema yanga akianza fanya vizuri maneno ya namna hii yanakuwa mengi mno

ukatizame mechi za yanga na simba, huyu huyu kachapwa mara 4 mfululizo

mechi ya yanga na azam huyu huyu alipigwa 4 kama dodoma jiji

we kuwa mkweli presha imekupanda baada ya yanga kuanza kushinda usijifiche kwenye kichaka cha mechi za yanga zikoje
 
Happy Holiday! Natumaini mnaendelea vizuri wana-Jamiiforums. Msukumo wa kuandika andiko hili umetokana kuangalia mechi tatu, pale ambapo Yanga amekutana na Mashujaa, Tanzania Prisons na hii mechi yake ya mwisho dhidi ya Dodoma Jiji.

Nimekua shabiki kindaki ndaki wa mpira wa Tanzania, nimeudhuria mechi nyingi sana hasa za Yanga katika msimu uliopita. Nimefurahi sana kwa wakati ule, lakini wakati naandika andiko hili nikiri kusema sitakuja kutazama tena mechi za Yanga isipokuwa zile mechi za kimataifa, au watakapo kutana Yanga vs Simba/Azam.

Kupitia mechi hizo hapo juu, sijui niseme ni uwezo mkubwa wa Yanga, au uwezo mdogo wa timu pinzani au kuna sababu nje ya uwanja au vyote kwa pamoja . Ila hizo mechi zilikua kama futuhi, ni maigizo yaani ni kichekesho. Kuna wakati unajiuliza inakuwaje hizi timu zinashiriki ligi kuu. Wachezaji wa timu pinzani wanashindana kufanya makosa, wachezaji wanashindana kutoa zawadi, labda kwa kuwa ni msimu wa Christmas.

Sizungumzi haya sababu za kuwa Yanga hapaswi kushinda, Hapana. Ila nazungumzia ushindani umepotea kabisa. Tofauti na miaka ya nyuma. Hizi mechi zote tajwa Yanga ameshinda sio sababu ya ubora wake, ila sababu ya udhaifu wa mpinzani. Ni ushindi mwepesi sana.

Mechi zote Yanga angekua makini hata kidogo tu, alikuwa na uwezo wa kupata hata magoli zaidi ya 10 maana ilikuwa ni washindwe wao tu. Hapo hapo ukitazama timu hizo tajwa zinapokutana na vilabu vya Simba na Azam basi ushindani unakua ni mkubwa sana.

Kuokoa soka letu, tulitazame hili kwa undani, tupate tatuzi za kinadharia na kivitendo ndani na nje ya uwanja. Either kuna baadhi ya vilabu vina influence katika timu hizi ndogo au gap kati ya Yanga na hivi vilabu vingine ni kubwa sana kusema kwamba inawathiri wachezaji kisaikolojia hata kabla hawajakutana nao.

Natambua kuwa tuna tamani vilabu vyetu vishinde kwa namna yeyote, lakini katika hili haihitaji uwe shabiki wa Yanga au Simba au hata mpira kuliona hili. Athari yake ni kuwa hii ligi itaenda kuwa dhaifu au kwa lugha ya kisoka kujulikana kama Farmers League.

Mdau wa soka mtazamo wako ni upi?
sasa mpinzani akiwa dhaifu si ndio unatumia udhaifu huo huo kushinda game, mpinzani akifanya makosa unatumia makosa hayo hayo kushinda game, yaani ukiona mpinzani amefungwa ujue alifanya makosa na mwenzake akatumia hiyo nafasi, hata man yu amefungwa kwa sababu alifanya makosa, ila ukiangalia ubora wa kikosi cha mbwa mwitu na man yuu huwez kudhani man yuu atafungwa
 
yaani upate mashaka na mechi za yanga uache kupata mashaka na mechi za simba

sema yanga akianza fanya vizuri maneno ya namna hii yanakuwa mengi mno

ukatizame mechi za yanga na simba, huyu huyu kachapwa mara 4 mfululizo

mechi ya yanga na azam huyu huyu alipigwa 4 kama dodoma jiji

we kuwa mkweli presha imekupanda baada ya yanga kuanza kushinda usijifiche kwenye kichaka cha mechi za yanga zikoje
Kolo mmoja mmoja atachomoka kutoka mafichoni
 
Kuna wachezaji hasa wazawa na viongozi wa hizi timu,wakicheza na Simba na Yanga...wanatamani wafungwe hata kwa kuforce! Yani Wana mapenzi nazo mno...
Ni changamoto kubwa sana kama watashindwa kutofautisha kati ya mapenzi na kazi. Hii inapelekea bias na kuua falsafa yetu ya fairness katika mchezo wetu pendwa.
Unapataje mashaka na Yanga iliyo na quality kuzidi timu zote kwenye ligi
Yanga ni bingwa mara ya 3 mfululizo
Yanga amecheza final ya mashindano ya CAF
Yanga amecheza robo final na Mamelod
Yanga yupo CAFCL
Yanga amemfunga Simba mara nne mfululizo
Ni mwehu tu atapata mashaka juu ya ushindi wa Yanga
Maybe ni quality, maybe not. Umeangalia vizuri mechi tajwa hapo juu?
 
Happy Holiday! Natumaini mnaendelea vizuri wana-Jamiiforums. Msukumo wa kuandika andiko hili umetokana kuangalia mechi tatu, pale ambapo Yanga amekutana na Mashujaa, Tanzania Prisons na hii mechi yake ya mwisho dhidi ya Dodoma Jiji.

Nimekua shabiki kindaki ndaki wa mpira wa Tanzania, nimeudhuria mechi nyingi sana hasa za Yanga katika msimu uliopita. Nimefurahi sana kwa wakati ule, lakini wakati naandika andiko hili nikiri kusema sitakuja kutazama tena mechi za Yanga isipokuwa zile mechi za kimataifa, au watakapo kutana Yanga vs Simba/Azam.

Kupitia mechi hizo hapo juu, sijui niseme ni uwezo mkubwa wa Yanga, au uwezo mdogo wa timu pinzani au kuna sababu nje ya uwanja au vyote kwa pamoja . Ila hizo mechi zilikua kama futuhi, ni maigizo yaani ni kichekesho. Kuna wakati unajiuliza inakuwaje hizi timu zinashiriki ligi kuu. Wachezaji wa timu pinzani wanashindana kufanya makosa, wachezaji wanashindana kutoa zawadi, labda kwa kuwa ni msimu wa Christmas.

Sizungumzi haya sababu za kuwa Yanga hapaswi kushinda, Hapana. Ila nazungumzia ushindani umepotea kabisa. Tofauti na miaka ya nyuma. Hizi mechi zote tajwa Yanga ameshinda sio sababu ya ubora wake, ila sababu ya udhaifu wa mpinzani. Ni ushindi mwepesi sana.

Mechi zote Yanga angekua makini hata kidogo tu, alikuwa na uwezo wa kupata hata magoli zaidi ya 10 maana ilikuwa ni washindwe wao tu. Hapo hapo ukitazama timu hizo tajwa zinapokutana na vilabu vya Simba na Azam basi ushindani unakua ni mkubwa sana.

Kuokoa soka letu, tulitazame hili kwa undani, tupate tatuzi za kinadharia na kivitendo ndani na nje ya uwanja. Either kuna baadhi ya vilabu vina influence katika timu hizi ndogo au gap kati ya Yanga na hivi vilabu vingine ni kubwa sana kusema kwamba inawathiri wachezaji kisaikolojia hata kabla hawajakutana nao.

Natambua kuwa tuna tamani vilabu vyetu vishinde kwa namna yeyote, lakini katika hili haihitaji uwe shabiki wa Yanga au Simba au hata mpira kuliona hili. Athari yake ni kuwa hii ligi itaenda kuwa dhaifu au kwa lugha ya kisoka kujulikana kama Farmers League.

Mdau wa soka mtazamo wako ni upi?
Uko sahihi kabisa. Niliwahi pia kusema hili nadhani msimu uliopita, ukiangalia mechi za Yanga unaweza kudhani wachezaji wa timu pinzani wamehongwa, yaani wanajichezea pasi zisizo na maana pale nyuma hadi wanafungwa magoli ya ajabu. Nikaja na uzi mmoja wa jinsi ya kuifunga Yanga ya Gamondi.

Kama unavyosema, inawezekana kabisa timu au wachezaji hawahongwi ila labda ni woga tu walionao kwa Yanga, wanacheza wakiwa na wenge. Ni ngumu kujua.
 
Kimsingi kinachowauma makolo ni recovery ya haraka ya yanga na namna yanga wanavyopanda kwa speed pale juu.

Mpira wa Yanga ni mtam sana mpenda soka yoyote angependa kuiangalia Yanga hii ya GUSA ACHIA twende kwao

Na niwaambie makolo wenda mkafungwa goli nyingi sana na yanga derby ijayo
 
Ni changamoto kubwa sana kama watashindwa kutofautisha kati ya mapenzi na kazi. Hii inapelekea bias na kuua falsafa yetu ya fairness katika mchezo wetu pendwa.

Maybe ni quality, maybe not. Umeangalia vizuri mechi tajwa hapo juu?
Kipindi Cha njombe mji ipo ligi juu,nimeenda kucheki game yao nikiwa pale,mechi imeisha nikawa pale wanapopita wachezaji kwenda room,mchezaji Mmoja tunafahamiana nikamshtua akaja nimsalimu,akaniuliza Matokeo ya Yanga vipi huko,maana Yanga alikua na mechi Taifa at the same time,kumwambia kadroo alisikitika Sana.
 
Back
Top Bottom